Usimamizi wa Facebook ulisema utalipa Dola4 bilioni pesa taslimu na Dola
13 bilioni kupitia ubadilishanaji wa hisa.PICHA|MAKTABA
Na Mwandishi wetu, Mwananchi
Posted Ijumaa,Februari21 2014 saa 24:0 AM
Posted Ijumaa,Februari21 2014 saa 24:0 AM
Kwa ufupi
WhatsApp ni maarufu miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma ya kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS).
Marekani. Kampuni ya Mtandao wa
Jamii ya Facebook imesema itanunua mtandao wa mawasiliano wa ujumbe
mfupi wa WhatsApp kwa Dola 19 bilioni za Marekani (Sh30.9 trilioni), ili
kuimarisha umaarufu wake hasa miongoni mwa vijana.
Pia, wasimamizi wa Facebook walitangaza nyongeza
zaidi ya Dola 3 bilioni zitalipwa waanzilishi wa Mtandao wa WhatsApp na
wafanyakazi wake.
Hiyo ndiyo biashara kubwa zaidi ya ununuzi ambayo iliwahi kutekelezwa na Facebook kufikia sasa.
WhatsApp ni maarufu miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma ya kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS).
WhatsApp iliweza kuwasajili zaidi ya watumiaji
milioni 450. Katika taarifa yake, Mwanzilishi wa Facebook, Mark
Zuckerberg alisema mtandao huo upo kwenye harakati ya kuwaunganisha watu
bilioni moja, jambo litakalofanya Facebook kuwa na thamani kubwa zaidi.
Zuckerberg alisema idadi kubwa ya watumiaji wa
Facebook wanatumia simu za mkononi, hivyo mtandao wa WhatsApp ambao
hutumiwa kwa simu utasaidia kuimarisha mawasiliano kwa gharama ya chini.
Mitandao hiyo imekuwa na watumiaji wengi duniani.
Jan Koum alitangazwa kujiunga na bodi ya usimamizi wa mtandao wa Facebook.
Usimamizi wa Facebook ulisema utalipa Dola4 bilioni pesa taslimu na Dola 13 bilioni kupitia ubadilishanaji wa hisa.
Masharti
Watumiaji wa WhatsApp na Facebook ambao ni wengi katika mataifa ya Amerika na Canada walisifu hatua hiyo.
Mamlaka ya Facebook iliahidi kudumisha masharti ya WhatsApp na kutoa kitita cha 1milioni kulipa iwapo masharti hayo yatakiukwa.
Mapema mwezi huu Facebook ilisherehekea miaka 10 tangu kubuniwa na kufikia sasa ina watumiaji zaidi ya bilioni moja.
Soma zaidi http://www.mwananchi.co.tz/kitaifa/Facebook-kununua-WhatsApp-kwa-Sh1-36-trilioni/-/1597568/2215618/-/item/1/-/fqr6tj/-/index.html
Soma zaidi http://www.mwananchi.co.tz/kitaifa/Facebook-kununua-WhatsApp-kwa-Sh1-36-trilioni/-/1597568/2215618/-/item/1/-/fqr6tj/-/index.html