m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Friday, 22 November 2013

Prof. Mwaluko Atakumbukwa

Photo: Prof. Mwaluko Atakumbukwa
===================
Kwa niaba ya KII na kwa niaba yangu mimi mwenyewe nimepokea taarifa za kifo cha Prof. Gabriel Mwaluko kwa majonzi makubwa. Prof Mwaluko mwanataaluma nguli katika fani ya udaktari na ambaye alikuwa mkuu wa chuo kikuu cha mt. Yohana (St. John's) amefariki dunia akiwa nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu ya Saratani ya koo katika Hospital ya Appolo. Prof Mwaluko ambaye wakati wote alijawa na tabasamu na asiye na makuu ndani ya miaka miwili ya uwepo wake SJUT alikuwa na jitihada kubwa ya ya kukiendeleza chuo. Katiba hotuba ya alipotutembelea Kituo cha Mt. marko Dar Es Salaam aliahidi kukifanya kuwa cho kikuu kishiriki jambo ambalo ingekuwa hatua kubwa ya maendeleo ya chuo, Kwa kuanzia akakubali mahafali ya St. marks kwa mara ya kwanza kufanyika Dar es Salaam.
Binafsi nitamkumbuka sana lakini chuo cha Mt. Yohana kinapaswa kumbkumbuka kwa vitendo  kwa kuondoa urasimu katika utendaji na pili kufanikisha kukifanya kituo cha Dar es Salaam kuwa Chuo Kikuu Kishiriki ili kukipa nguvu zaidi jambo ambalo Prof Mwaluko alitamani litokee kabla mwaka huu haujaisha.
Bwana alitoa na Bwana Ametwaa... Jina la Bwana lihimidiwe. Kwa niaba ya KII na kwa niaba yangu mimi mwenyewe nimepokea taarifa za kifo cha Prof. Gabriel Mwaluko kwa majonzi makubwa. Prof Mwaluko mwanataaluma nguli katika fani ya udaktari na ambaye alikuwa mkuu wa chuo kikuu cha mt. Yohana (St. John's) amefariki dunia akiwa nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu ya Saratani ya koo katika Hospital ya Appolo. Prof Mwaluko ambaye wakati wote alijawa na tabasamu na asiye na makuu ndani ya miaka miwili ya uwepo wake SJUT alikuwa na jitihada kubwa ya ya kukiendeleza chuo. Katiba hotuba ya alipotutembelea Kituo cha Mt. marko Dar Es Salaam aliahidi kukifanya kuwa cho kikuu kishiriki jambo ambalo ingekuwa hatua kubwa ya maendeleo ya chuo, Kwa kuanzia akakubali mahafali ya St. marks kwa mara ya kwanza kufanyika Dar es Salaam.
Binafsi nitamkumbuka sana lakini chuo cha Mt. Yohana kinapaswa kumbkumbuka kwa vitendo kwa kuondoa urasimu katika utendaji na pili kufanikisha kukifanya kituo cha Dar es Salaam kuwa Chuo Kikuu Kishiriki ili kukipa nguvu zaidi jambo ambalo Prof Mwaluko alitamani litokee kabla mwaka huu haujaisha.
Bwana alitoa na Bwana Ametwaa... Jina la Bwana lihimidiwe.