m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Friday, 12 April 2013

We offer best services, read

KII offered services are available for you, Karibu sana

MAAJABU, MAKANISA NDANI YA MAPANGO

Mapango yana mchango mkubwa katika historia ya Uyahudi na Ukristo kwa ujumla. Daudi alijificha kwenye pango wakati akimtoroka mfalme Sauli, nyaraka muhimu za 'bahari ya shamu'pia zilipatikana kwenye pango, na wakristo pia wamekuwa wakikutana kwenye mapango kwa ajili ya kuabudu.
Huko Bulgaria, katika mji wa Mihalich - kuna pango ambalo kanisa lilikuwa likikutana. Wanahistoria na wataalamu wa mambo ya kale wanaamini kuwa kanisa hilo la pango limetumika mnamo karne ya 10.

 Flickr/Klearchos Kapoutsis - Creative Commons
Kwa mujibu wa tovuti ya a view on cities, Kanisa la pango la Mtakatifu Stefano mjini Budapest, Romania, lilifungwa na wakomunisti mwaka 1951, na kisha kufunguliwa tena mwaka 1989. Kanisa hilo lilikamilishwa ujenzi wake mwaka 1931.
© Flickr/Robot B - Creative Commons
Pengine kanisa la pango ambalo linafahamika sana duniani ni lile la Misri, ambapo wa'Zabbaleen', watu wanaokusanya taka jijini Cairo wanaabudu.
Kwa mujibu wa mtandao wa wikipedia, kuna makanisa ya pango saba yaliyojificha kwenye mapango ya mlima Mokattam. Kanisa la Mtakatifu Simon the Tanner ndilo kanisa kubwa mashariki ya kati, likiwa na uwezo wa kuchukua watu waliokaa 20,000.

© Flickr/Roaring Jellyfish - Creative Commons



Kanisa hilo limechuka jina la Mtakatifu Simon the Tanner ili kumuenzi, mkristo wa dini ya Coptic kutoka karne ya kumi.
Urithi ambao umeachwa na makanisa ya handaki ni mkubwa na wa kipekee.
Mtume Paulo anaandika kwenye waraka wa Waebrania sura ya 11 kuhusu waamini waaminifu ambao wameonesha imani ya kipekee.
"(Watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi" Waebrania 11:38
Mpaka hivi sasa, kuna wakristo ambao huabudu kwenye makanisa yaliyo kwenye mapango.