Hata hivyo furaha yangu ina wasiwasi mwingi kutokana na ajenda ya Muungano kuonekana ndio muhimu zaidi kwani kila mtu na kila chama kabla bunge halijaanza wamekuwa wakizungumza muundo wa Muungano.
Nina shaka kubwa kwamba inawekezekana Bunge hili likakubwa na minyukano juu ya muungano na kusahau kwamba Muungano ni suala la Kisiasa lakini bado yapo masuala muhimu wanayohitaji watanzania.
Tunaweza kupata katiba nzuri ya Muungano ni kuwa na muungano safi kama wanasiasa watakavyo lakini kama haitazingatia masuala ya kijamii, kiuchumi na elimu itakuwa sawa na nyumba iliyosakafiwa nje ndani vumbi tupu.
Nchi yetu haisongi mbele kwa sababu ya masuala ya utendaji hivyo lazima ipatikane katiba itakayoweka misingi bora ya utendaji, utawala na uwajibikaji.
