Siku ya Ijumaa tar 24.05.2013 ilikuwa njema sana hasa pale ilipotimu muda wa kawaida wa ibada wa saa 6:00 CASFETA TAYOMI tawi la Chuo Kikuu St. John's. Siku ilikuwa ya pekee kwa kuwa ilikuwa ibada ya kwanza kuruhusu maswali na majibu ya kiroho.
Maswali makuu yaliyoulizwa na kujadiliwa ni;
1. Nini maana ya Mkristo, anapatikanaje na nini uthibitisho wake?
2. Ni kwanini tunakataza kunywa pombe wakati yesu alitengeneza divai? Na je nimsaidiaje mtu anayeohoji uhalali wa kukataza pombe kwa mkristo?
3. Kijana wa kiume anapotaka mchumba afanyaje? Makanisa mengine yana hatua tatu za urafiki, uchumba mpaka ndoa, Je nini msimamo wa kipentekoste?
4. Nini tofauti ya divai na mvinyo?
5. Fafanua tofauti ya Sala, Maombezi, Shukrani na Dua?
Spika wa mjadala Peter kapagi ndo anaruhusu maswali
Mwenyekiti Hamphrey Mhuville akiongoza shangwe za ibada hiyo
Mwl Luka akitoa ufafanuzi
Katibu mkuu mstaafu akiulizwa Swali
Aquilina Charles akikoleza kipindi kwa swali mwanana
Jacob Msokwa akiulizwa swali nini maana ya mkristo?
Majibu ya kiroho ni Biblia bwana, ona Mwenyekiti wa wakaka mstaafu akijibu kwa ufafanuzi makini
Ibada ilikuwa tulivu wakati wa maswali japo ilikuwa na shangwe kuu ilipoanza
Usajili pia ulikuwepo ili kubaini wangapi wamehudhuria