m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Wednesday, 29 May 2013

IBADA YA MASWALI NA MAJIBU YA KIROHO CASFETA SJUT-DSM

Bwana asifiwe wapendwa.
Siku ya Ijumaa tar 24.05.2013 ilikuwa njema sana hasa pale ilipotimu muda wa kawaida wa ibada wa saa 6:00 CASFETA TAYOMI tawi la Chuo Kikuu St. John's. Siku ilikuwa ya pekee kwa kuwa ilikuwa ibada ya kwanza kuruhusu maswali na majibu ya kiroho.
Maswali makuu yaliyoulizwa na kujadiliwa ni;
1. Nini maana ya Mkristo, anapatikanaje na nini uthibitisho wake?
2. Ni kwanini tunakataza kunywa pombe wakati yesu alitengeneza divai? Na je nimsaidiaje mtu anayeohoji uhalali wa kukataza pombe kwa mkristo?
3. Kijana wa kiume anapotaka mchumba afanyaje? Makanisa mengine yana hatua tatu za urafiki, uchumba mpaka ndoa, Je nini msimamo wa kipentekoste?
4. Nini tofauti ya divai na mvinyo?
5. Fafanua tofauti ya Sala, Maombezi, Shukrani na Dua?
 Spika wa mjadala Peter kapagi  ndo anaruhusu maswali
 Mwenyekiti Hamphrey Mhuville akiongoza shangwe za ibada hiyo
 Mwl Luka akitoa ufafanuzi
 Katibu mkuu mstaafu akiulizwa Swali
 Aquilina Charles akikoleza kipindi kwa swali mwanana
 Jacob Msokwa akiulizwa swali nini maana ya mkristo?
 Majibu ya kiroho ni Biblia bwana, ona Mwenyekiti wa wakaka mstaafu akijibu kwa ufafanuzi makini

Ibada ilikuwa tulivu wakati wa maswali japo ilikuwa na shangwe kuu ilipoanza
 Usajili pia ulikuwepo ili kubaini wangapi wamehudhuria