Tumeanza!!!
Ninayo furaha kubwa kwamba Ofisi yetu kuu ya Kapagi Information Institute -KII imefunguliwa rasmi hapo jana Jumamosi ya tar 25oct, 2013. Kila kitu kimeenda sawa kama nilivyokuwa nikitaarifu awali. Kwa niaba ya KII na mimi mwenyewe ninazo shukrani za pekee kwa Bwana Yesu Kristo na kwa wote walioshiriki kuniunga mkono na kuniamini hata kunichochea sana niweze kufungu ofisi japo wengi walipenda iwe Dar es Salaam.
Natamani kuwaorodhesha wote waliniunga mkono kwa hali, mawazo na mali hakika si wachache ni wengi lkn kwa neema nitaorodhesha japo wachache kwa niaba ya wengi.
Acha niwaorodheshe ijulikane kwamba wapo walio nyuma yangu na taasisi, wapo wanaoitakia mema, kuimbea, kushauri hata kuwa radhi kufadhili
Nianze kwa familia, dada John Janet Merinyo, Mauki, Furaha Samwel na Mr Chipanda, Sunny, Xaveria, Neema Michael, Abel Mwakyandwike, Uncle Mwasomola, Oswin Joctan, Rehema Chillery, Sia na Neem Stationery, Shangarai, Papalika, Mary Simon, Uncle Dickson (Computer Doctor), Teddy na Yamsebo Stationary, Bineth Printing bila Kumsahau Mama G wa ukweli (rehema Sanga) na Gladiness Stationery, Sae internet Cafe kwa Software, Mzee Chale na Marge (St. Marks Library), Janus Bernard,
Aaah, ni wengi na hili linanipa nguvu kwamba nimeanza na kuna watu wapo nyuma kwa ajili ya Taasisi hii Muhimu. Nisamehe ikiwa sikukuorodhesha na hiyo siyo maana kwamba sijaheshimu mchango wako. Una maana kwangu na kwa KII, na ikiwa una maana kwangu una kubwa kwa jamii nitakayoihudumia.
Niwe na tamko moja tu sasa kwamba nimeanza na sitorudi nyumba, nitaficha wapi sura yangu kwa kundi hili kubwa linaloniunga mkono usiku na mchana.
Niwe na Ahadi moja kwamba nilipofundisha ujasiriamali mara zote nimezungumzia kuwa "kwa wafanyakazi wenye mshahara wa msingi ujasiriamali ni njia ya kujipatia kipato cha ziada" LAKINI MIMI NITAENDA MBALI NATAKA KUFANYA UJASIRIAMALI KUWA JIPATO CHA MSINGI na mshahara kiduchu wa serikali na mashirika dhalimu kuwa kipato cha ziada. hili halitafanyika kwa njia nyingione isipokuwa kutumia kila furasa kuwahudumia watu na kuondoa matatizo ya msingi kwa jamii na taaluma.
Kwa kuwa ndo kama naanza nisiwe na mengi, Wakati ujao nitakuja na makala yenye Dira, Malengo na Wito wa Kapagi Information Institute-KII.
Tumeanza tukiwa dhaifu, tujipange kufanya Makubwa. Tanzania yenye huzuni inatusubiri ifanye sherehe ya kuzaliwa kwetu kama wakombozi.
m
"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "
-- Dale Carnegie, motivational expert
Sunday, 27 October 2013
Thursday, 24 October 2013
KII HEAD OFFICE IN MBEYA
KII Head Office going to be opened soon in Mbeya.
Am very happy to write these because i was waiting it for a long time
as my supporters demand. Our head office will open on Saturday at Zambia
rd/ Ituha st, Mbeya city.
The functions of office will be Ultimate
Secretarial services, Entrepreneurship training, Computer software and
maintainance as well as to search and provide information basing on
religion, economics and politics.
KII NEED TO GO BIG NOW
Join and Support it
Habari ni Maisha
kapagiii.blogspot.com
FULL PROFILE ON KII IS COMING on Blog and our Facebook page...be patient
Wednesday, 2 October 2013
Mashine za TRA zazua tafrani jijini Mbeya
Suala la ununuzi wa mashine za TRA za kieletroni za risiti kwabei ya sh. 800,000/= limezua Tafrani kubwa jijini Mbeya. tfrani hiyo imesababishwa na bei ya mashine hiyo ambayo inauzwa kuanzia sh.800,000/- kiasi ambacho wafanyabioashara wanapinga kwa kigezo kuwa bei hiyo ni zaidi ya mtaji wa biashara. katika mahojiano baadhi ya wafanyabiasha eneo la Mwanjelwa na Sae wamezungumzia bei ya mashine hizo kuwa na uwizi mkubwa kwani wenyewe hawapinmgi matumizi yake isipokuwa wanahoji kwanini ziuzwe kwa gharama kubwa kiasi hicho.
Wengine wameenda mbali zaidi wakikosoa mchakato huo kwamba utawakwamisha wafanyabiashara wengi na kwamba kwa kuwa mashine hizo zitawafaidisha TRA kwa suala ulipaji kodi zingepaswa kutolea bure sawa na mita za maji na umeme kwani zitakuwa mali ya TRA. Baadhi ya watu wakahoji kwanini mashine hizo ndogo ziwe ghali kiasi hicho kuzidi gharama ya mashine kubwa za photocopy ambazo huuzwa kwa sh.600,000, Kompyuta na hata Printer ambazo gharama zake si zaidi ya 500,000/=
Kufuatia tamko hilo la TRA kuwataka wafanyabiashara wote wanaouza zaidi ya sh.45,000/= kwa siku kuhakikisha wananunua mashine hizo likasababisha mgomo wa wafanyabiasha wa Mwanjelwa ambao wakaandaa mkutano uliokua ufanyike Viwanja vya S/M Ruanda Nzovywe ambao hata hivyo ukazuia na polisi kwa ulipuaji wa mabomu ya machozi.
Hapa ni baadhi ya picha za matukio ya vurugu hizo;
Polisi
wakiwa wanasindikiza gari la matangazo kutangaza
kuomba Vurugu hizo na maandamano yasiyo na kibali yasitishwe
Polisi wakiwa wameimarisha ulinzi mkali
Wafanya biashara wakiwa viwanjwa vya Shule ya Msingi Ruanda Nzovwe kungoja kusikiliza nini hatma yao
Baadhi ya watu wakikimbia Mabomu ya machozi yalipoanza kurushwa ili kuepusha vurugu
Mawe yakiwa yamepangwa kuzuia magari yasiende kokote
Maduka yote yakiwa yamefungwa eneo la mwanjelwa kupinga ununuzi wa mashine hizo za TRA
Vijana hawa wakiwa wana nawa uso baada ya Bomu la machozi kuwapitia
Jiwe kubwa likiwa limewekwa katika Barabara magari yasipite
Matairi yakiwa yamewashwa barabarani kuanza vurugu kupinga mashine hizo
Tuesday, 1 October 2013
TOZO LA SIMU
==========
Natamani mjadala uanze wa tozo la simu, kufungiwa kwa mwananchi na Mtanzania isiwe hoja ya kuzuia mjadala wa tozo la simu maana Naona magazeti yote yamegeukia mzozo wa kufungiwa Mwananchi na Mtanzania.
Nchi hii inachosha kwani wawekezaji wakubwa wa madini tunawaachia kodi wanatupa mrabaha wa 3% wakati madini ni ya kwetu wakati huo huo wanataka kumchangisha mwananchi 1000 kila mwezi kwa ajili ya simu ambayo mawasiliano yake ya mchango mkubwa kwa maendeleo ya Taifa. Nchi hii inaacha pesa nyingi za madili zinaliwa na mabeberu wajiitao wawekezaji huku ikitaka kuwakandamizi wananchi katika ardi yao wenyewe..inashangaza sana, inatia uchungu. Ona nchi za uarabuni zina vita kila siku lakini bado zina jeuri ya uchumi imara kwa sababu moja tu kuwa na utajiri wa Mafuta. ni kweli bado hatuchimbi mafuta lakini ni nani asiyejua madini ghali duniani kuwa ni Dhahabu, Almasi na Tanzanite? Je si ndo yametapaka Shinyanga, Geita, Mara, Arusha ukiachana na mikoa inayozalisha kidogo kama Chunya-Mbeya n.k? je madini hayo hayatoshi kujenga barabara, huduma za afya, maji na shule?
Tunapaswa kujifunza namna ya kuwanyonya wawekezaji na si kuwanyonya watanzania katika ardhi yao...hiyo haitakuwa demkrasia tena, itakuwa udikteta na unyonyaji mbaya zaidi kuliko ukoloni.
==========================
Kwa kweli tozo hilo halikubaliki kama vile Kodi za Kikoloni za Kichwa, Matiti tax na Kipande system.
Ikipitishwa kabisa tozo la simu basi ni Bora Tumrudishe Richard Turnbull, gavana Mwingereza aje atutawale hata akituchaapa tutamwelewa kwa kuwa ni Mzungu.
Subscribe to:
Posts (Atom)