Shalom Mpendwa.
Mwanzo: 37
Ninaendelea kujifunza kutoka kwa Mbeba maono Yusufu. Watu wengi tunamtazama Yusufu kam ambeba maono tu, lakini kumbe hatupaswi kuishia hapo tunatakiwa kuangalia namna alivyoyabeba maono na nguvu iliyomwezesha kubeba maono yake.
Maono ni jambo la kwanza, kubeba ni jambo la pili na nguvu ni jambo la tatu. Unaweza ukawa na maono lakini maono yako yakafa kwa sababu umeshindwa kubeba, wakati mwingine unaweza ukayabeba maono lakini ukashindwa kuendelea nayo kwa. Mpenzi kuinua mzigo ni jambo rahisi lakini kuendelea nao ama kupiga hatua nao ni jambo lingine gumu sana kwani inategemea nguvu ya misuli uliyonayo.
Binafsi naamini hakuna kijana aliyekosa maono ikiwa ana imani thabiti kwani Yoeli 2:28 inatamka wazi kuwa vijana wataona maono. Vijana wengi wanalo jambo la kufanya lakini hawajatambua na waliotambua wameshindwa kubeba. Lazima kuwa mwanagalifu unapokuwa na maono.
Kubeba maono ni kama kubeba YAI, yai si kiumbe chenyewe bali kasha lililobeba kiumbe kumbe kulivunja ni kuvunja kiumbe na kulitunza vizuri ni kutunza kiumbe kijacho. Kwa mfano kufikiri kuanzisha shule ni sawa na yai kwani mawazo yamebeba shule lakini si shule yenyewe.
Unapobeba maono kunakuwa na changamoto nyingi ambazo zinaweza kuharibu au kuua kabisa maono yako.
Kwa leo hebu tujifunze kwa Yusufu nguvu iliyomsaidia kubeba maono. YUSUFU ALIKUWA MTII NA MWENYE KUFUATA MAELEKEZO katika safari yake ya maono. Ndugu unapobeba maono umeanza safari ni kama kuku anapoatamamia yai, kutotoa kwa vifaranga kutategemea namna ambavyo atadhamiria kuatamia mayai yake.
AMUA KUATAMIA MAONO YAKO
Yusufu alikuwa mtii kweli kwani tunamtazama akiwa na umri wa miaka 17 tu tayari ameanz kuota ndozo zinazotoa maelekezo ya maono yake...nini atafanya kwa wakati gani na kwa nani.
Utii unaonekana kwa Yusufu kwanza kila alipoota kamsimulia baba yake na familia yake mst. 2, 5 na 9. Pili Yusufu alipotumwa kwenda kuwaona nduguze bado anaendelea na desturi ya utii kwani inaoneka anaenda mahali asipojua vizuri ndio maana anapofika anauliza wapo wapi ndugu zake na hapo tena utaona namna Yusufu anavyopenda kufuata maelekezo kwani anauliza. Hizi ni tabia za kawaida kwa mtu lakini zina maana sana kwa ajili ya kutunza maono. Mst 15
Utii wa Yusufu ndio uliopelekea kuweza kubeba maono yake, Kwani Ysufu unafiak wakati nduguze wanamkamata wanamvua kanzu bao hatuambiwi kama alileta matata bali alitii, wanamtumbukiza kisimani bado hakuleta matata akatii, wanamuuza bado akatulia akatii, Wamidiani wanamchukua hadi Misri bado anatii na tena wamidiani wanamuuza kwa Potifa bado anatii (kama angeleta matata ingeandikwa).
Kumbe kama umebeba maono ni lazima uwe mtii, unaweza kukumbana na mugumu wakati wa maono lakini yakupasa uchukulia kama changamoto tu, Yusufu aliandaliwa kuwa mtawala lakini tunaona natawaliwa na ndugu zake na hata utumwani jambo ambalo ni kinyume na alivyoona. Yeye anaona kutawala lakini yanayotokea ni kutaliwa na hata kutaka kuuawa. mst 23, 24, 27, 28, 36.
Maisha ya ushindi ni pamoja na kuwa na maono, wengine waimngia dhambini kwa sababu hawana maono, hawajui nafasi yao na wanapoelekea.
Ikiwa umebeba maono kubali kuwa mtii kwa Mungu mwenyewe, viongozi wa Imani na wakati mwingine hata watawala kwani hujua ni nani atakayeweza maono yako, maono yatatekelezeka kutia nani. Yusufu ilikuwa kupitia nduguze na hatimaye Farao
Katika kuonyesha nia ya kulinda utamaduni wa kiafrika Uganda imeonyesha njia licha vitisho kutoka Marekani. Rais wa Uganda, Yoweri Museveni,
ametia saini sheria mpya inayotoa adhabu kali kwa wanaopatikana na
hatia ya kutembea nusu uchi au kuhusika na vitendo vinavyohusisha picha
zenye watu uchi.
Wanawake pia wamezuiwa kabisa kuvalia sketi fupi
sana au 'Mini Skirt' kama zinavyojulikana au blausi ambazo zinaonyesha
kifua chao hadharani na kusababisha hisia za kingono .Akihutubia waandishi wa habari, mjini Kapmala, waziri wa maadili na utawala bora, Reverend Simon Lokodo alisema kuwa Rais Museveni alipitisha sheria hiyo tarehe 6 mwezi huu, miezi mwili bada ya bunge kuipitisha.
Kwa mujibu wa sheria hiyo kamati dhidi ya vitendo hivyo itabuniwa ili iweze kutekeleza sheria hiyo kwa kuhakikisha kuwa picha, au video zenye watu uchi zinanaswa na kuharibiwa.
Kamati hiyo, itajumuisha watu kutoka katika sekta mbali mbali ikiwemo ya habari na utumbuizaji.
Sheria hiyo inasema kuwa mtu yeyote atakayepatikana akijihusisha na vitendo cya watu kuwa uchi, kuvalia nusu uchi , kuona sinema za watu wakiwa uchi au kuchapisha picha za watu walio uchi kwa lengo la kuleta hisia tofauti utachukuliwa hatua kali za kisheria.
Waziri alisema kuwa serikali haitaki watu kuvalia nguo zisizo na heshima na kuzua hisia zisizofaa miongoni mwa watu.
Watakaopatikana wakivunja sheria na kuvalia visivyo watafungwa hadi miak 10 na wale watakaopatiokana na hatia ya kuhusisha watoto katika biashara ya ngono watafungwa hadi miaka 15.
chanzo: bbcswahili.com