m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Monday, 29 April 2013

Wafu wanavyofukuliwa, kisha kuzikwa wapya

Makaburi yaliyopo jijini Dar es Salaam 
Na Florence Majani  (email the author)

Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.

Siku zote tunaamini kuwa mtu anapofariki hupumzika kwa amani, lakini siku hizi wafu hao hawapumziki tena kwa amani, bali huamshwa, kisha, wafu wengine kushika nafasi zao.
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.
Maeneo mengi ya kuzikia katika Jiji la Dar es Salaam, hasa yale maarufu kama Kinondoni, Sinza, Temeke na Kisutu yanapendwa zaidi na watu na sasa yamefurika.
Kujaa kwa maeneo haya ya kuzikia kumesababisha makaburi ya watu wengine, kufukuliwa kisha kutumika kuzikia miili mingine.
Hata hivyo, makaburi ambayo hufukuliwa ni yale ambayo hayajajengewa, yametelekezwa, hayana kitu chochote cha kuonyesha kuwa kuna kaburi pale au mengine hayana alama kama misalaba au imeondolewa.
Msemaji wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian Kaiohela anasema kuwa anafahamu kwamba makaburi hayo yamejaa, lakini hakutaka kuzungumza zaidi akitoa ahadi kuwa siku ya Jumatatu atalifikisha suala hilo kwa wahusika wakuu.
Katika makaburi ya Temeke Chang’ombe, Mwananchi Jumapili lilishuhudia makaburi yakiwa yamesongamana kiasi ambacho ni vigumu mtu kupata nafasi ya kuweka mguu.
Mlinzi wa makaburi hayo, Athuman Mtembwe anasema kutokana na ufinyu wa nafasi katika makaburi hayo, makaburi ambayo hayana alama yoyote ni rahisi kufukuliwa na kuzikiwa kwa mara nyingine.
“Mimi kama mlinzi wa eneo hili ninaweza kukutafutia sehemu ambayo unaweza kuchimba kaburi, lakini kama hufahamu utafukua tu maiti nyingine,” anasema
Anasema kuwa mara kwa mara watu wanaokuja kuchimba makaburi ili kuzika ndugu zao, wamekuwa wakifukua miili ya watu wengine ambayo makaburi yao hayakuwa na alama yoyote.
“Ni kawaida, mchimba kaburi anafukua, anakuta mifupa, anaiweka pembeni au anaizika katika shimo dogo…kisha anaendelea na taratibu za kuzika mwili mwingine,” anaeleza.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760490/-/12b2t5y/-/index.html 

Kiongozi wa Kanisa azikwa akiwa hai mkoani Mbeya

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani 


Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Mbeya. Msaidizi wa zamani wa Padri (Katekisita) katika Kigango cha Kanisa Katoliki Kijiji cha Mkwajuni, Florian Mwamosi (70) amekufa baada ya kuzikwa akiwa hai katika kaburi moja na mtu anayedaiwa kumuua kwa njia ya kishirikina.
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani  alikiri kutokea  kwa tukio hilo akieleza kuwa lilitokea  saa 9:00 mchana katika kijiji hicho cha Maweni Mkwajuni wilayani Chunya.
“Marehemu aliuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na mawe kwa tuhuma za kuhusika na uchawi na kusababisha kifo cha Peter Robert,” alisema.
Kamanda Athumani alisema kuwa uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea na kwamba wahusika wote wa tukio hilo wamekimbia na kuzihama nyumba zao, hivyo polisi wanaendelea na msako wa kuwatia mbaroni watuhumiwa na kwamba tayari  kaburi hilo limefukuliwa jana kutenganisha maiti hizo.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa  marehemu huyo ambaye alikuwa akituhumiwa kwa ushirikina aliwahi kuwa Katekista wa kigango hicho hadi mwaka 2007.
Wameeleza kuwa Mwamosi alikwenda kuhudhuria mazishi ya Peter  Robert (28) katika kitongoji hicho cha Maweni, baada ya kufuatwa nyumbani kwake na watu wakitaka aende kwa sababu yeye ni mmoja wa wazee wa mila katika kitongoji hicho.
“Bwana Mwamosi alikuwa akituhumiwa kwa uchawi kwa muda mrefu na wenzie wawili, hivyo alipofika makaburini ilianza minong`ono ya watu na huku wengine wakiguna na ndipo alipoombwa aingie kaburini kwa ajili ya kupokea jeneza lililobeba mwili wa marehemu Peter Robert,” alisema mkazi mmoja wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Joseph.
Alisema kuwa baada ya kuingia kaburini akiwa na watu wengine watatu wenzake walitoka kwa haraka na kumwacha Mwamosi peke yake ndipo kundi la watu waliokuwa eneo hilo la makaburi walianza kumshambulia kwa kumpiga mawe huku wakimwamuru akae chini.
Shuhuda huyo alisema kuwa baada ya kukubali kukaa chini akiwa ndani ya kaburi hilo, walianza kumfukia na alipofukiwa nusu ya mwili wake waliingiza jeneza la marehemu Peter na kuliweka juu yake na kuanza kulifukia kaburi hilo.
“Baada ya kukaa chini ndani ya kaburi hilo ndipo walianza kumfukia kwa udongo na baadaye wakachukua jeneza la marehemu na kuliweka juu yake, kisha kumfukia na udongo na taratibu za mazishi ziliendelea kwa ajili ya marehemu  Peter,”alisema.
 http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760482/-/12b2t55/-/index.html