m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Friday, 21 June 2013

Kesi dhidi ya Rais Kenyatta yaakhirishwa


Rais Uhuru Kenyatta
Mahama ya kimataifa ya ICC imeakhirisha siku ya kuanza kusikilizwa kwa kesi dhidi ya rais Uhuru Kenyatta hadi tarehe 12 mwezi Novemba mwaka huu.
Hii ni kufuatia ombi la mawakili wa Rais Kenyatta kutaka kesi yao kuahirishwa hadi mwezi Januari mwaka ujao.
Mahakama iliamua kuwa upande wa Kenyatta unahitaji muda wa ziada ili kujiandaa ipasavyo kwa kesi, kwa sababu viongozi wa mashtaka walichelewa kufichua ushahidi walio nao dhidi ya rais Kenyatta.
Kenyatta anakabiliwa na tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadmau wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya miaka sita iliyopita, akisemekana kuunga mkono mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya watu wa kabila moja.
Naibu Rais wa Kenya William Ruto naye pia anakabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC kuhusu tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kupanga mashambulizi dhidi ya jamii hasimu.
Majaji waliwaalika mawakili wa Uhuru Kenyatta kutoa maoni yao kuhusu muda wanaotaka ili kujiandaa kwa kesi dhidi ya mteja wao.
Baada ya kupokea maoni kutoka kwa upande wa utetezi, upande wa mashtaka, pamoja na waakilishi wa kisheria, majaji waliamua kuakhirisha kesi hiyo kutoka tarehe 9 Julai mwaka huu hadi Novemba.
Tarahe hiyo mpya ilifikiwa baada ya kuzingatia maswala mbali mbali ikiwemo haja ya upande wa mashtaka kujiandaa vyema kwa utetezi wao na mipango ya usafiri.
Rais Kenyatta ameshtakiwa kwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya , makosa ya jinai ikiwemo, mauaji, kuwahamisha watu kinyume na sheria, ubakaji , mateso na vitendi vingine vya kinyama vinavyodaiwa kufanywa wakati wa ghasia hizo mwaka 2007/2008

Mazingira mabaya shuleni hukimbiza walimu

MWALIMU ni mtu wa muhimu katika jamii yoyote kwa kuwa anabadilisha maisha ya kila mtu kutoka hatua moja kwenda nyingine. Cha kushanganza maisha yake ni tofauti na kazi kubwa anayoifanya. Pia wanapata changamoto nyingi katika utendaji kazi wao… wengine wanajikuta wakivikimbia vituo vyao vya kazi kutokana na mazingira magumu wanayofanyia kazi.

Jambo la kusikitisha walimu wanafikia hatua ya kutembea kilomita kubwa kutoka majumbani kwao kwenda kwenye vituo vyao vya kazi hali ambayo haiwezi kuleta matokeo mazuri ya elimu nchini.

Mwalimu anatembea kila siku kilometa 10 kwenda na kurudi kutoka shuleni, anafika amechoka na hana hamu ya kufundisha hivyo anafundisha chini ya kiwango kinachotakiwa.

Licha ya Serikali kujitahidi kuajiri walimu wengi kwenye vituo mbalimbali karibu mikoa yote ya Tanzania, bado imesahau kuwa baada ya kutoa ajira walimu wanaenda kukaa katika mazingira gani.

Idadi kubwa ya walimu wanapelekwa maeneo ya vijijini kutokana na uhaba wa walimu katika maeneo hayo, lakini huduma za kukidhi mahitaji yao bado ni hafifu.

Inasikitisha kuwaona walimu ambao ni mhimili mkubwa katika jamii wanalala jikoni kwa miaka mitatu huku wafanyakazi wengine wakiwa wanatembea zaidi ya kilomita kumi, jambo hili linasikitisha na linatia aibu kwa Serikali yetu.

Kuhusu walimu wanaotoroka kazini na kujiunga na vyuo vya elimu ya juu pasipo ridhaa ya mwajiri, tatizo hili linaathiri zaidi mikoa iliyopo Kanda ya Ziwa na Kaskazini, ambayo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu ambapo chanzo kikubwa ni mazingira mabaya ya kufanyia kazi.

Taratibu za kuyarekebisha maisha ya walimu yatasaidia kupunguza utorokaji wa walimu katika maeneo mbalimbali hapa ikiwemo vijijini ambapo matatizo yanakuwa mengi kuliko wale wa mjini.

Walimu wengi hukimbilia mjini ili kukwepa matatizo ya vijijini ambapo baadhi yao wanajikuta wakiishi kwenye nyumba za udongo na kuamua kuachana na kazi ya ualimu na kujihusisha na biashara nyingine.

Kutokana na hali kuwa tete Serikali ilipanga kuwachukulia hatua watumishi wake zaidi 800 waliotoroka kazini na kujiunga na vyuo vya elimu ya juu bila idhini ya mwajiri.

Jumla ya walimu 26,537 wameajiriwa serikalini kwa mwaka wa fedha 2012/2013, walimu wa ngazi ya cheti walioajiriwa ni 13,568.

Kati yao walimu 13,527 wamepangwa kufanya kazi katika shule za msingi zilizopo kwenye halmashauri na walimu 41 wamepangwa katika shule za msingi za mazoezi zilizo chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Jumla ya walimu wa sekondari na vyuo vya ualimu walioajiriwa ni 12,973 wakiwemo walimu wa Shahada 8,887 na Stashahada 4,086, lakini swali la kujuuliza maeneo waliyopangiwa yanakidhi viwango?

Idadi ya walimu walioajiriwa mwaka 2012/2013 imeongezeka kwa asilimia 11 sawa na walimu 2,630 ikilinganishwa na walimu 23,907 walioajiriwa mwaka uliopita 2011.

Walimu wapya wanakuwa na shauku kubwa ya kuanza kazi, lakini baada ya kuripoti kwenye vituo vyao vya kufanyia kazi na kukuta mazingira si mazuri baadhi yao wanaamua kuondoka baada ya wiki tatu au mwezi mmoja.

Baada ya Serikali kutilia shaka matokeo hayo Baraza la Mitihani Tanzania (BAMITA) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wameamua kurudia kusahihisha lakini matokeo hayajabadilika kwa asilimia kubwa sio siri ufaulu si nzuri kama inavyotakiwa.

Licha ya Serikali kujitahidi kuwaajiri walimu kwa wingi kila mwaka lakini hali bado ni mbaya hasa maeneo ya vijijini ambapo unaweza kuikuta shule ina jumla ya wanafunzi mia 400 lakini wanafundishwa na walimu wawili au watatu hali ambayo haiwezi kuleta matokeo mazuri.

Walimu hawawezi kufanya kazi zao kwa ufanisi ulio juu huku wakiwa wanalala jikoni kwa miaka mitatu na wengine kutembea kwa kilomita kumi,kitu ambacho hakiwezekani.

Wanafunzi wa sasa wanamaliza darasa la saba hawajui kusoma wala kuandika lakini mwanafunzi huyo anafaulu kwenda kidato cha kwanza,kwa hali hii tusitegemee kupata matokeo mazuri na viongozi wazuri wa baadaye.
Chanzo; Mtanzania.co.tz

Mizengo Pinda: Nasema wapigwe tu

Share bookmark Print Email Rating
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda 
Na Waandishi Wetu  (email the author)

Posted  Alhamisi,Juni20  2013  saa 20:57 PM
Kwa ufupi
Lazima tuwakamate na kama katika kuwakamata watafanya jeuri, jeuri, watapigwa tu kabla ya kupelekwa tunapotakiwa kuwapeleka, kwa sababu hatuwezi kuendelea na hali hii, mkadhani kwamba tutafika tunapokwenda.

Dodoma/Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameagiza vyombo vya dola kuwashughulikia kwa kuwapiga wale watakaokataa kutii amri wakati wakifanya vitendo vya uvunjifu wa amani.
Akizungumza katika Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu, bungeni Dodoma jana, Pinda alisema watu wanapokaidi wanajitakia matatizo na vyombo vya dola.
Alisema hayo alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu aliyeuliza: “Serikali ipo tayari kiasi gani kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”
Waziri Mkuu alijibu: “Ni lilelile nililosema... mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria.
“Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.”
Pinda alisema Serikali imedhamiria kurejesha amani nchini ikiwamo mkoani Mtwara na kuwataka Watanzania waiache Serikali ifanye kazi hiyo. Alisema Serikali ina orodha ya watu wanaosemekana kuwa ni vyanzo vya vurugu na matatizo yaliyotokea Mtwara na kushangaa wale wanaopinga kukamatwa kwao.
“Lazima tuwakamate na kama katika kuwakamata watafanya jeuri, jeuri, watapigwa tu kabla ya kupelekwa tunapotakiwa kuwapeleka, kwa sababu hatuwezi kuendelea na hali hii, mkadhani kwamba tutafika tunapokwenda. Nami nasema vyombo vya dola vijipange imara vihakikishe vinadhibiti hali hii,” alisema.
Hata hivyo, jibu hilo lilipata upinzani wakati Mbunge wa Konde (CUF), Khatibu Said Haji alipomwuliza Waziri Mkuu: “Hapo awali umetoa kauli nzito ya kuliambia taifa hili kwamba wale raia wote, ambao watakaokuwa wakaidi wapigwe tu na watapigwa tu; naomba ninukuu Katika Ibara ya 13 na Kifungu cha 6B cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
“Ni marufuku kwa mtu yeyote aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kuteswa kama mtu mwenye kosa, mpaka itakapothibitika anayo hatia kwa kutenda kosa hilo.
“Pia ibara hiyohiyo Kifungu cha 6 E; kinasema ni marufuku kwa mtu yoyote, kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazoweza kumdhalilisha. Kwa kauli yako uliyoitoa huoni kwamba umevunja Katiba?” Akijibu swali hilo, Pinda alisema ni lazima kutofautisha kati ya mtu aliyekwishakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria... “Mimi ninayemzungumza hapa ni mtu yule ambaye ameamua kufanya vitendo hajakamatwa na ndiyo maana nilikwambia usiandamane... hapa mahali hutakiwi kwenda wewe ukaamua kutumia mabavu kwa sababu mko wengi, ndiyo maana nikasema, hawa watu tutashughulika nao hivyohivyo.”
Mbunge huyo hakuridhishwa na majibu hayo na kumtaka Waziri Mkuu kuyafuta.
Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda aliingilia katika na kumweleza mbunge huyo kuwa kila mtu alikuwa amemwelewa Waziri Mkuu na hakukuwa na haja ya kuendelea na hoja hiyo.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Mizengo-Pinda--Nasema-wapigwe-tu/-/1597296/1889674/-/xk60drz/-/index.html