m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Wednesday, 5 September 2012

Nguvu ya Neno

SOMO:   NGUVU YA NENO
MUWASILISHAJI:     Peter Kapagi
Tukisoma waebrania 4:12 isemayo
Utagundua mambo yafuatayo juu ya neno la kristo;
1.    Lina nguvu, nguvu huwezesha jambo litendeka au kazi yote ifanyike. Neno lipo kuwezesha mambo ya mwammini yafanyike hata kama haikuwezekana mbele ya neno lazima yawezekane na yatendeke tu.
2.    Neno li hai- maana yake lipo katia utendaji wakati wote masaa yote bila kupumzika.
3.    Neno lina ukali, lina magumu yote unayoweza kukumbwa nayo.
4.   Lina choma, linaweza kutenganisha vidhaifu na vyenye nguvu na mkristo haimpasi kuwa na mambo dhaifu na yenye nguvu kwani imempasa kuwa na vyenye nguvu tu.
5.    Linatambua mawazo ya moyo, yaani linaweza linaweza kukuonya na kukuongoza kila linapotambua mawazo ya moyo wako.
Neno linaweza kuyatenda hayo kwa sababu neno ni Kristo mwenyewe kama Yohana 1:1-4 isemavyo
KAZI KUU ZA NENO
Maombi pasipo neno ni bure kwa sababu maombi ni utekelezaji wa neno na ni lazima kwanza ujifunze neno au uitwe kwa neno au uisikie sauti ya bwana Yesu ikibisha ndani yako kwa neno ndipo uombe.
Injili na huduma yoyote yenye kuhitaji mafanikio katika mambo yote inahitaji neno lenye nguvu maana hapo ndipo zile kazi/ sifa tano tajwa hapo juu zinaweza kufanya kazi na kuthibitisha utukufu/ uwezo wa Bwana Yesu.
Neno linalaani na neno linabariki neno linajenga na kuumba na neno linabomoa