
Na Kelvin Matandiko, Mwananchi
Posted Jumatano,Decemba18 2013 saa 13:10 PM
Posted Jumatano,Decemba18 2013 saa 13:10 PM
Kwa ufupi
- Fursa iliyoipata Tanzania ya kuhutubia
na aina ya hotuba iliyotolewa na Rais Kikwete kwenye mazishi ya Mandela
imeipaisha nchi kidiplomasia na kufanya historia yake ijulikane dunia
nzima.
Matukio mbalimbali yaliyotokea Jumapili kwenye
mazishi ya Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela
yamenikumbusha yaliyotokea katika sherehe za miaka 50 tangu kuanzishwa
OAU, sasa Umoja wa Afrika (AU).
Katika maadhimisho hayo, Tanzania ilimwagiwa sifa
kedekede kutoka kwa wakuu wa nchi mbalimbali walioshiriki, wakiwamo Rais
wa Senegal, Mark Sall, Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Dessalegne
na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
Rais Zuma alitoa hisia zake kwa Tanzania, akisema
wazi kuwa wananchi wa nchi Afrika Kusini hawatausahau mchango wa
Tanzania katika kuwakomboa na kuwafikisha walipo sasa. “Tulisaidiwa na
nchi nyingi, lakini Tanzania ilitusaidia kwa namna ya kipekee.”
Sifa hizo ziliwekewa uzito katika hotuba ya Rais
Jakaya Kikwete kwenye mazishi, alipoamua kueleza kwa uwazi historia ya
Tanzania katika ukombozi wa Afrika Kusini na Afrika kwa jumla.
Awali, ilipofanyika ibada ya kumbukumbu ya Mandela
ambapo viongozi mbalimbali zaidi ya 100 kutoka maeneo mbalimbali
duniani walishiriki, Watanzania hawakuelewa kuona mchango wa Tanzania
hauelezwi wazi katika tukio hilo muhimu wala kupewa fursa ya kuhutubia,
lakini bila shaka nyoyo zao zilisuuzika baadaye Jumapili, fursa hiyo
ilipopatikana siku ya mazishi.
Kauli ya Prof Mpangala
Miongoni mwa walioweka wazi dukuduku lao ni
Profesa Gaudence Mpangala wa Kitengo cha Sayansi ya Jamii, Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam (UDSM), akisema Tanzania ilitakiwa kupewa nafasi ya
kuzungumza lolote kutokana na ukaribu wa nchi hizo.
Anasema Tanzania ni moja ya nchi duniani zenye historia kubwa na ujenzi wa taifa la Afrika Kusini.
“Na baada ya kutoka gerezani mwaka 1990, Tanzania
ilikuwa nchi ya kwanza Mandela kuitembelea kwa lengo la kutoa shukrani
zake, tukampatia na heshima ya jina lake kuitwa barabara muhimu, Mandela
Road,” anasema Profesa Mpangala na kuongeza;
Sasa sijui ni utaratibu gani uliotumika kuangalia
vigezo vya kuhutubia, kwa sababu siku zote rafiki yako wa karibu ndiye
anayestahili nafasi ya kuzungumza siku ya msiba wako,” anasema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania
(TGNP) Usu Mallya anasema kutokana na mazingira hayo, kuna kila sababu
ya Watanzania kujiuliza kwa sasa, iwapo thamani iliyokuwapo katika
harakati za ukombozi bado inatambuliwa.
Anaongeza kuwa ni muhimu kukumbuka kwamba Tanzania
ilikuwa kitovu cha harakati za ukombozi na kituo cha kuandaa fikra
mbadala kwa ajili ya kutumika katika harakati za kuleta mabadiliko kwa
ndani na nchi nyingine za Afrika.
Kusoma zaidi bofya hapa http://www.mwananchi.co.tz/Makala/Nafasi-ya-Tanzania-imeonekana-msiba-wa-Mandela/-/1597592/2117016/-/cnsj5cz/-/index.html
Kusoma zaidi bofya hapa http://www.mwananchi.co.tz/Makala/Nafasi-ya-Tanzania-imeonekana-msiba-wa-Mandela/-/1597592/2117016/-/cnsj5cz/-/index.html
No comments:
Post a Comment