m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Monday, 15 April 2013

Dar yarejea enzi za ujima

Abiria wakigombea basi dogo katika kituo cha mabasi ya daladala Ubungo jijini Dar es Salaam jana.
Wakati nauli mpya za daladala, mabasi na treni zikianza kutumika rasmi leo, hali ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam imezidi kuwa mbaya kutokana na mabasi kuwa machache na hivyo kusababisha abiria kulazimika kusafiri kwa malori na magari mengi madogo huku wakitozwa nauli kubwa.
 
Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE umebaini kuwa maeneo ambayo yamekumbwa zaidi na tatizo la usafiri ni kutoka Mwenge kwenda Tegeta, Mwenge-Kibaoni, Ubungo-Mbezi, Ubungo-Mbagala, Gongolamboto-Mwenge na Ubungo kwenda Mlandizi.
 
Kutokana na ukosefu wa daladala kwenye maeneo hayo, kwa takribani wiki moja sasa wananchi wamekuwa wakitumia malori, Toyota Noah, Bajaj, Pick Up, teksi pamoja na Toyota Coaster ambazo hazijasajiliwa kuchukua abiria jijini hapa.
 
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa kutokana na ukosefu wa daladala, hali hiyo imetoa fursa kwa magari yaliyoanza kutoa huduma ya usafiri kwenye maeneo hayo kutoza abiria nauli kubwa ambayo haipo katika viwango vya nauli vilivyopangwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Usafiri wa Majini na Nchi kavu (Sumatra). Nauli inayotozwa na wamiliki magari hayo mfano kutoka Mwenge hadi Tegeta, Mwenge-Bunju, Mwenge-Kibaoni ni Sh.1,000 hadi 2,000 kwa mtu mmoja badala ya Sh. 300 au 400 ya sasa.
 
Kutoka Ubungo kwenda Mbezi, Ubungo-Mbagala, nauli zinazotozwa ni kati ya Sh. 500 hadi 1,000 badala ya Sh.300 wakati kutoka Ubungo-Mlandazi ni Sh.1,000 hadi 2,500.
Magari yaliyobainika kutoza nauli kubwa ni yale ambayo hayajasajiliwa na Sumatra kutoa huduma ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam na yaliyoiba njia.
 
Aidha, daladala ambazo zimesajiliwa kutoa huduma jijini hapa, zinaongoza kukatisha ruti (kuiba njia) na zinafanya hivyo ziweze kurejea mapema vituoni kuchukua abiria wengine hali ambayo inakuwa ni faida kwao. 
 
Mathalani, katika kituo cha Mwenge inapofika jioni, gari za ruti ya Tandika-Mwenge kupitia barabara ya Ali Hassan zimekuwa zikipakia Ubungo na kisha kushusha abiria wote na kupakia tena kwenda Bugurudi na zinapofika hapo hupakia kwenda Tandika.
 
Wakati mwingine, gari hizo zinapofika Ubungo hurudi tena Mwenge kupakia abiria.
 
Wakizunguma na NIPASHE kituo cha Ubungo, abiria waliokuwa wakisafiri kwenda Mbezi Luis, walisema tatizo la usafiri limekuwa sugu na kwamba wakati mwingine wanachukua zaidi ya saa tano kupata gari.
 
Amon Kisimbo mkazi wa Mbezi Luis alisema tatizo la usafiri katika jiji la Dar es Salaam linasababishwa na msongamano wa malori na kwamba serikali inatakiwa kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyowahi kutolewa mwaka 2009.
 
Kisimbo ambaye alidai alikuwa miongoni mwa watu walioshiriki kuandaa mapendekezo hayo katika tume iliyoundwa na serikali, alisema pendekezo walilotoa ni kutaka Bandari ya Dar es Salaam ihamishwe kutoka ilipo sababu inasababisha malori kupita katikati ya jiji na hivyo kusababisha msongano usiokuwa wa lazima. Ofisa Mfawidhi wa Sumatra, Kanda ya Mashariki, Conrad Shio, akizunguza na NIPASHE jana alisema kutokana na ukiukwaji wa sheria za barabara unaofanywa na wenye magari hayo, magari 74 yamekamatwa kutokana na makosa mbalimbali.
 
Shio alisema magari 36 yamekamatwa kwa kukatisha ruti, 18 kwa kuiba ruti na magari 20 yamekamatwa kwa kutoza nauli kubwa.
 
Alisema magari ambayo yamekamatwa kwa kosa la kukatisha ruti wamiliki wake watatakiwa kwenda Sumatra na mkataba wa madereva wengine na hao waliosababisha kosa hilo hawataruhusiwa kufaya kazi ya udereva mahali popote nchini.
 
Alisema tatizo la ukosefu wa magari katika baadhi ya maeneo linatokana na kwamba Sumatra imesimamisha usajili katika ruti ya barabara ya Ali Hasani Mwinyi-Kilwa kwa sababu kuanzia Julai mwaka huu wamiliki wa daladala watatakiwa kujiunga katika kampuni ili kutoa huduma ya usafiri kwenye ruti hiyo.
 
Alisema siyo kweli kwamba daladala zimeadimika na kwamba baadhi ya wamiliki wanakwepa kusajili magari yao kwenye njia zenye foleni kubwa kama Mbezi-Kimara hadi Kivukoni au Kariakoo.
 
MWAKYEMBE ABARIKI NAULI
Serikali imebariki ongezeko jipya la nauli za mabasi yanayotoa huduma mijini, ya masafa marefu na treni hivyo kuziruhusu kuanza kutumika rasmi leo.
 
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, aliwaambia wanahabari jana mjini Dodoma kuwa nauli mpya imeongeza Sh. 50 kwa mwanafunzi na Sh. 100 kwa watu wazima; hivyo daladala zitatoza Sh. 400 badala ya 300 na wanafunzi Sh. 200 badala ya Sh. 150.
 
Alisema  serikali imeridhia ongezeko la nauli lililotangazwa na Sumatra, baada ya kuhakiki na kujiridhisha kuwa ongezeko hilo lilizingatia mchakato wa kupandisha nauli na viwango viliridhiwa na wadau wanaowakilisha maslahi ya wanaotoa na wale wanaotumia huduma hiyo.
 
“Mimi kama Waziri wa Uchukuzi sina tatizo na ongezeko hili dogo la nauli za daladala tatizo langu ni tabia ya Watanzania kukacha vikao halali vinavyojadili mambo yanayotuhusu na kusubiri kuja kulalamika baadaye,” alisema Dk. Mwakyembe.
 
Alisema hayo akiwakosoa wananchi na asasi nyingine kulalamikia nauli nje ya utaratibu licha ya vikao vya kuwataka kutoa maoni kupitia Sumatra kutangazwa na kuwataka wananchi wajitokeze wakati maombi ya wamiliki wa vyombo vya usafiri ya kupandisha nauli yalipokuwa yanajadiliwa.
 
Waziri Mwakyembe alisema maombi ya kuongezwa nauli hiyo mpya yalitolewa baada ya wadau wakiwamo Baraza la Taifa la Walaji wa Huduma zinazodhibitiwa na Sumatra, Chuo cha Usafirishaji, vikiwamo vyama vya watoa huduma vya madereva vya kutetea abiria na wanahabari, kuridhia.
 
“Kulikuwa na mvutano mkubwa wamiliki wakitaka nauli iongezeke na wawakilishi wa abiria wakitaka nauli ibakie ile ile iliyotangazwa mwaka 2011. Ndipo maamuzi  ya nyongeza ya nyongeza ndogo yakawa Sh. 100 na Sh. 50 kwa mwanafunzi yakaafikiwa,” alisema.
 
Aliongeza kuwa wawakilishi wa abiria na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji waliamriwa kuwa iwapo kuna upande usioridhia ukate rufaa kwenye Baraza la  Ushindani, lakini hakuna aliyefanya hivyo.
 
Wiki iliyopita Waziri Mwakyembe alisema wizara hiyo itapitia nauli hizo kutokana na malalamiko mengi kutolewa na wananchi wakipinga nyongeza hiyo.
Imeandikwa na Gaudensia Mngumi, Dodoma na Thobias Mwanakatwe, Dar
CHANZO: NIPASHE

Baadhi ya wadaiwa wa Bodi ya Mikopo wako taabani

http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/10881-baadhi-ya-wadaiwa-bodi-ya-mikopo-wako-taabani

Gesi ni hatari, Zimamoto wawahi kuokoa.



Gari la zimamoto likiwasili eneo la tukio
Leo asubuhi muda wa saa 3:30 kumetokea mlipuko mkubwa kwenye Glosary ya Kipingu eneo Mtaa wa Sae karibu kabisa na kituo cha Sae. Mlipuko huo wa moto umetokana na jiko la gesi lililokuwa likiwashwa ili kupasha supu na ndipo likalipuka na kuanza kuwaka moto mkali. Moto umezua balaa kubwa kwani kutokana na ukosefu wa vifaa vya tahadhari  vya zima moto na elimu ya majanga watu wakaanza kuzima kwa maji na mchaka lakini ikawa ni kama kuuchochea zaidi. Baada ya kushindika kuzima moto uliokuwa ukiwaka kwenye mtungu wa gesi na kuendelea kusambaa kwenye vyombo vingine ndipo kijana mmoja jasiri maarufu kama KP akajitosa na kuuburuzia nje mtungi uliokuwa ukiwaka moto mkali. Hapo ndipo akawa ameokoa nyumba hiyo yenye maduka manne isiwake moto.
Zimamoto wawahi kuokoa, kinyume na desturi ya zimamoto ya kuchelewa mara wanapoitwa kwenye majanga ya moto kwani waliwasiri mara moja baada ya kupigiwa simu. Zimamoto wamewapongeza wananchi kwa kuweza kuokoka jingo kuwaka moto kwa kuutoa nje mtungi unaowaka moto. Askari wa zimamoto wakauzima moto uliokuwa unaendelea kuwaka kwenye mtungi wa Gesi.
Wasisitiza kutoa taarifa mapema kila mara janga linapotokea kuwakumbusha wananchi kuw ana namba za simu ya kiganjani mbali ya ile ya mezani ili kutoa taaarifa kwa haraka zaidi. Ikumbukwe kuwa mara nyingi zima moto wamekuwa wakilalamikia baadhi ya watu wasio waaminifu wamekuwa waktoa taarifa za uongo kupitia simu ya bure ya 111.
Ushauri wa bure kwa wote wenye majiko ya gesi ni bora wakanunua kifaa cha kuzima moto (Fire Extinguisher) ili watumie kuzima moto mara moto unapolipuka.
Namba za kiganjani za Zimamoto jiji la Mbeya ni
0755 651923
Tazama Picha kutoka eneo la tukio
watu wakushuhudia uzimaji wa mtungi

mtungi umezima

Askari akizima mtungi uliolipuka

 Hata boda boda walikuwepo kujionea wenyewe




 Moto umezimwa tayari kwa safari.
Picha zote na KII

Kwisha! UFARANSA YAPITISHA MUSWADA NDOA ZA JINSIA MOJA, SWEDEN NAKO KIMBILIO LAO

Vuta nikuvute imetokea katika bunge la senate nchini Ufaransa, ambapo mwisho wa siku iliamuliwa kupitisha kwa muswada wa sheria ya kuruhusu ndoa za jinsia moja nchini humo, licha ya upinzani mkali kutoka kwa wabunge wenye msimamo mkali, ikiwamo viongozi wa dini.
Uamuzi huu ambao umepitishwa Ijumaa taehe 12 Aprili 2013 na Ufaransa , taifa lenye asili ya katoliki, umekuja baada ya muda mrefu wa majadiliano, kama ambavyo Rais François Hollande alivyoahidi kwenye uchaguzi mkuu mnamo Aprili mwaka 2012, sera ambayo ilimfanya avune kura nyingi za wafuasi wa ndoa hizo.
Waziri wa Haki, Bi Christian Taubira. © Gouvernement
Mtetezi mkubwa wa muswada huo, waziri wa haki nchini huko, Bi Christian Taubira, amesemema kuwa muswada huo unakuja kutokana na umuhimu wake, hasahasa kwa watoto wanaoishi na wazazi wa jinsia moja, ili wapate haki zao sawa na watoto wa wazazi wa kawaida. na kwa mujibu wa muswada huu, basi wenye ndoa za jinsia moja, watarushusiwa kuasili watoto kwa ajili ya kuwalea.
Tumefanya hivi kwa sababu kuna watoto hawali chakula cha afya, wanakula pipi kwa wingi, na kadha wa kadha, hao pia tunawalinda - wanahitaji hilo. Christian aliwaambia maseneta mara baada ya kupitisha muswada huo, ambao utapitiwa tena February 2014 kwa ajili ya marekebisho.
Kwa upande wake, seneta wa chama cha UMP, Jean-Pierre Raffarin, amesema kuwa bado wataendeleza mpambano kwa kuwa bunge bado lipo, na kilichopo ni kwamba watakuwa wakiongea na wananchi wataobadili mawazo ili kuhakikisha muswada huu unaondolewa na kurejea katika hali ya mwanzo, yaani mume na mke na si vinginevyo.
Mpaka sasa ufaransa imegawanyika kuhusiana na ndoa za jinsia moja, ambapo mnamo January mwaka huu, takriban watu 340,000 waliandamana kupinga ndoa za aina hii, wakisisitiza Baba na Mama kwa familia. Ambapo wiki mbili baadae, kundi la watu takriban 125,000 walijitokeza mtaani kuunga mkono ndoa za namna hiyo.
Nchi ambazo zimeridhia ndoa za jinsia moja mpaka hivi sasa. © CBC
Ulaya ni bara ambalo nchi zake kadhaa zimeruhusu ndoa za namna hii, ambapo kwa watu ambao nchi zao haziruhusu, wamekuwa wakikimbilia huko ili kuonana na kuishi kwa sheria za huko. mfano mmojawapo ni mashoga wawili Waganda, ambao walikimbia nchi yao na kuelekea Sweden ili kuonana kutokana na nchi yao kukataza vitendo vya ushoga na usagaji.
Wadau wa Gospel Kitaa walio nchini Sweden, walifanikiwa kupata tukio hilo kama lilivyofanyika mwezi wa kwanza kwa kamera, na hatimaye mdau Nahshon Kamugisha kuzirusha kwa GK.


Jimmy na Lawrence wakiwa na mashoga wenzao wakati wa sherehe ya 'kuonana'.
Gospelkitaa.com

Maajabu Geita:Aliyefariki miaka mitano iliyopita afufuka

mwanamke anayedaiwa kufariki miaka mitano iliyopita 


Posted  Jumapili,Aprili14  2013  saa 24:51 AM
Kwa ufupi
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.Share

Geita: Mji wa Geita na maeneo ya jirani juzi ulikumbwa na taharuki ya aina yake, pale mwanamke ambaye anadaiwa kwamba alifariki miaka mitano iliyopita alipoonekana akiwa hai katika eneo la Kasamwa.
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.
Aliyekuwa wa kwanza kumwona Flora ni mdogo wake aitwaye Monica Onesmo ambaye baada ya kuamka saa 11:00 alfajiri nyumbani kwa dada yake, alimwona mwanamke aliyekuwa ameketi nje ya nyumba hiyo, lakini alimfananisha mwanamama huyo na marehemu dada yake.
“Baada ya kumwona nilimwita mtoto wake tunayekaa naye na nikampigia simu dada (Monica) ambaye alikuwa amelala chumba kingine nikamwambia kwamba nimeamka na kumkuta mwanamke amekaa hapa nje, lakini kila nikimwangalia anafanana na marehemu dada yetu,”alisema Jubili na kuongeza kwamba alipowaita wote walitoka nje.
Alisema mtoto wa Flora (marehemu anayedaiwa kufufuka) anaitwa Rebeka Elisha (16) na kwamba walimchukua tangu 2008 wakati mama yake huyo alipofariki dunia katika Hospitali ya Geita ambako alikuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.
Rebeka ambaye ni mtoto wa nne wa Flora alisema: “Mama mdogo alituita sisi tulikuwa tumelala akasema kwamba nje kuna mwanamke ambaye anafanana na marehemu mama yetu, ndipo na sisi tukatoka na kweli kumwangalia alikuwa ni yeye kabisa.”
Alisema walipomuhoji mama yake huyo kwamba ametokea wapi, aliwaeleza kuwa ametoka eneo la Katoro kwa mganga na aliletwa na watu ambao hakuwatambua Alhamisi saa 1:30 usiku ndani ya gari na watu hao walimshusha kwa mtu aitwaye Juma Luchunga ambaye ni jirani na dada zake hao.
Kauli ya Flora
Akizungumza na waandishi wa habari, Flora alisema yeye ni mkazi wa Katoro na kwamba alitokea Katoro nyumbani kwa mganga wa jadi ambaye hata hivyo hakumtaja kwa maelezo kwamba wataalamu wake (majini) wamemkataza.
“Nilikuwa naishi kwa mganga wa kienyeji ila alikuja mwanaume wakati nikiwa pale akaninywesha dawa kisha tukapakizwa kwenye gari na watu wawili ambao sikuwatambua, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume mpaka hapa Kasamwa tukashushwa saa 1:00 jioni,”alisema Flora.
Alisema alipofika Kasamwa alikwenda kunywa uji kwa mama mmoja ambaye pia hakumtaja na kwamba baadaye alipelekwa nyumbani kwa mtu mwingine saa nne usiku, lakini watu wa nyumba hiyo walipomwona walimwambia: “Hapa si kwako twende tukupeleke kwa ndugu yako” na ndipo wakampeleka kwa dada yake ambako aliketi nje hadi alfajiri.
Flora alisema kabla ya kuishi kwa mganga alikuwa akiishi porini ambako alitupwa na watu asiowafahamu na baadaye aliokotwa na wasamaria wema ambao ndiyo walimpeleka kwa mganga ambako alikuwa akiishi muda wote.
Endeleahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1747968/-/129ypge/-/index.html