
Jengo la Chuo Kikuu Dodoma(Udom) moja ya vyuo vitakavyo tumika katika utaratibu huo mpya
Kwa ufupi
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14,
utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na
kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo
kikuu.
Dar es Salaam. Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU),
imepanga kuanza kuwadahili wanafunzi wa kujiunga na masomo ya vyuo vikuu
kwa kutumia uzoefu wao.
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo
2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la
saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi
ya chuo kikuu.
Kupitia utaratibu huo mpya, mtahiniwa atajiunga na
Chuo Kikuu kulingana na fani atakayoiomba na atatakiwa kufanya mitihani
mitatu na kufaulu kwa wastani wa daraja B.
Mkurugenzi wa Ithibati na Ubora wa Elimu ya Juu
kutoka TCU, Dk Savinus Maronga aliliambia gazeti hili kuwa baada ya
kuona kuna watu wengi wanaopenda kuendelea na masomo ya elimu ya juu,
lakini wameshindwa kutokana na kutokuwa na vigezo, TCU imeamua kuanzisha
mitihani hiyo maalumu.
Alisema kuwa mfumo huo unaojulikana kama
‘Recognition of Prior Learning’ (RPL), utamwezesha mwombaji kudahiliwa
vyuoni kupitia tume hiyo kama wanavyofanya watahiniwa wengine.
Sifa zinazotakiwa
Kuhusu sifa za kujiunga, Dk Maronga alisema kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba.
Kuhusu sifa za kujiunga, Dk Maronga alisema kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba.
“Mwombaji anatakiwa kuwa na nia ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu na uzoefu wa kile ambacho anakusudia kukisoma.
Awe na uwezo wa kuandika na kusoma Lugha ya
Kiingereza, ambayo ndiyo inayotumika kufundishia vyuoni,”alisema Dk
Maronga na kuongeza:
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1753450/-/12aid4m/-/index.html
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1753450/-/12aid4m/-/index.html