Bwana Yesu asifiwe…
Mpendwa leo ninayo furaha kubwa sana kurejea tena
ukurasa wetu na kichwa hapo juu.
JE WAJUA KUWA NCHI YETU TANZANIA IMETAJWA KATIKA
BIBLIA TAKATIFU?
ISAYA 18:
Mst 1. Ole wa
nchi ya uvumi wa mabawa, Iliyoko mbali kupita mito ya Kushi;
2 Ipelekayo wajumbe wake
kwa njia ya bahari, Na katika vyombo vya manyasi juu ya maji. Nendeni wajumbe wepesi, kwa watu warefu laini, watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu wakanyagao watu, ambao mito inakata nchi yao.
3 Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni.
4 Maana Bwana ameniambia hivi, Mimi nitatulia, na kuangalia katika makazi yangu, kama wakati wa mwangaza mweupe wa jua kali, mfano wa wingu la umande katika hari ya mavuno.
5 Maana kabla ya mavuno, maua yaangukapo, na maua yakawa zabibu zianzazo kuiva, ndipo atakapoyakata matawi kwa miundu, na kuviondoa vitawi vilivyopanuka na kuvikata.
6 Wote pamoja wataachiwa ndege wakali wa milimani, na hayawani wa nchi; ndege wakali watakaa juu yao wakati wa jua, na hayawani wote wa nchi watakaa juu yao wakati wa baridi.
7 Wakati huo Bwana wa majeshi ataletewa hedaya na watu warefu, laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu, wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao;
Mpendwa nilistaajabu mwaka 2011 nilipokutana na Mwl.
Brown Mwakibete pale Kijitonyama, kwa kujiamini sana akanidokeza kwamba
Tanzania imetajwa kwenye Biblia, imetabiriwa na nabii Isaya. Nami kwa
nilivyokuwa namwamini nikaungana naye kutafakari kifungu hicho mara tu
aliponitaka nifungue Biblia yangu.
Ndugu yangu ukitazama mstari wa kwanza wa Isaya 18
utaona unataja nchi ya uvumi iliyoko mbali kupita mito ya kushi. Katika Biblia
Kushi ni nchi ya Ethiopia ya leo, ukitazama ramani utabaini kuwa nchi zilizo
mbali na mito ya Ethiopia ni nchi za Afrika Mashariki na Somalia kidogo. (ukitokea
kaskazini ambako ndio inapatikana Israel) TANZANIA ni mojawapo ya nchi hizo.
Mstari wa 2 unataja kuwa nchi hiyo inapeleka wajumbe
wake kwa njia ya habari na katika vyombo vya mnyasi. Hapo utabaini kuwa nchi
zinazopakana na bahari na kutumia ngalawa ni Kenya, TANZANIA na Somalia.
Sehemu ya pili inazungumzia watu wepesi lani watishao
tangu mwanzo wao hata sasa. Hapa utaona kuna mkanganyiko kidogo kwa watu laini
tunaweza tafsiri kuwa watu wapole wasio na makuu lakini wakati huohuo watu hao
wanatisha tangu mwanzo. TANZANIA ndio nchi inayoongoza Afrika kwa ukarimu
(hospitality) lakini pia ndio nchi pekee Afrika iliyoongoza mapambano dhini ya
wakoloni kwa nchi zote za kusini mwa jangwa la Sahara, iliwatisha wakoloni
ikiwa ina ujinga, maradhi na umaskini wakati wao wana silaha, elimu, utajiri na
afya njema. TANZANIA ndio nchi pekee Afrika iliyopigana na nchi nyingine na
kuishinda iliipiga Uganda ikakanyaga watu wao hadi kaskazini ikamng’oa Dikteta
Idd Amini na kisha kuweka mtawala wao. Kabla ya Amiri Jeshi Mkuu kuruhusu vita
alianza kwa kuwatisha waganda na dunia nzima. TANZANIA inatisha kwani wakati
huo pia Malawi walitaka kunyang’anya ziwa Nyasa na Kenya wakaumendea mila
Kilimanjaro lakini Nyerere akawatisha wakashindwa. Tanzania. Hakuna aisyeijua
TANZANIA katika kusuluhisha migogoro, mfano Mauaji ya Kimbari ya Rwanda, Imedhibiti
uasi visiwa vya Comorro, imetatua mgogoro wa Kenya 2007 na hatimaye madagascar
Mstari unaomaliza kwa kutaja kuwa mito inakata nchi
yao, Afrika Mashariki ni TANZANIA pekee mbayo mito mikubwa inapita katikati,
hebu tazama Mito mikubwa ya Ruaha, Pangani, Malagarasi, Ugalla, Rufiji,
Wami bila kusahau mito ya mipakani
ambayo ni pamoja na Kagera, Mara, Ruvuma na Songwe. Bila shaka yeyote nchi
inayozungumziwa hapa ni TANZANIA kwani Kenya na Somalia hazina mito mikubwa.
Mst wa 3 unazaungumzia kuinuliwa bendera mlimani na
kupiga tarumbeta. Tanzania ndio nchi pekee barani Afrika ambayo ilipandisha
bendera yake ju ya mlima Kilimanjaro. Na ikapiga tarumbeta kwani baada tu ya
uhuru wa Tanzania ndipo nchi nyingi zikafuatia miaka ya 1962 na 1963 zikiwemo
Uganda, Kenya na makoloni mengi ya kifaransa. Yote ni kwa kuwa nchi ya Tanzania
ilisimama kidete kwa ajili ya ukombozi wa waafrika.
Mst 7 unazungumzia kwamba watu hao warefu laini
watamletea Hedaya Bwana wa majeshi, tena unasisitiza kabisa Taifa la wenye
nguvu, wakanyagao watu, amabo mito inakata nchi yao.
Ni nchi gani hiyo zaidi ya TANZANIA?
Huwezi kuombea vema kitu usichokujua, natamani unabii
huu ukupe nguvu ya kuiombea nchi yetu TANZANIA.
Mpendwa leo nimedokeza kidogo tu unabii wan chi yetu
TANZANIA kama ulivyotolewa na nabii Isaya. Nitafurahi kama utakuwa mwanzo tu wa
mjadala juu ya nchi yetu katika ulimwengu war oho, wengine husema Tanzania
ndiyo Israeli ya Afrika, je ni kweli? Kuna hoja gani?
Kama una masomo au hoja yoyote juu ya Tanzania yetu
katika ulimwengu wa roho usisite kuwasilisha kupitia mawasiliano yafuatayo;
Email: kakakapagi@gmail.com
Simu: +255 685 306666, +255 764 734620
MUNGU IBARIKI TANZANIA
Wenu katika safari
Mwl Peter Kajolo Kapagi