m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Thursday, 30 May 2013

ICC tayari kushauriana na Kenya kisheria


 30 Mei, 2013 - Saa 16:25 GMT

ICC inashikizwa iweze kuhamishia Kenya kesi za washukiwa William Ruto na Rais Uhuru Kenyatta
Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya jinai ya kimataifa- ICC, Fatou Bensouda leo amesema kwamba mahakama hiyo iko tayari kushauriana na Kenya kisheria kuhusu ombi la kutaka kesi inayowakabili rais wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto kuhamishiwa nyumbani.
Tamko hilo linatolewa wiki moja tu baada ya viongozi wa Umoja wa Afrika kutoa wito kwa ICC irejeshe kesi za Uhuru na Ruto zishughulikiwe nchini Kenya.
Akijibu maswali ya waandishi kutoka radio moja ya kibinafsi ya Nairobi, mwendesha mashtaka huyo mkuu amenukuliwa akisema hatua ya ICC kufanya mazungmzo na Kenya kuhusu kesi za Uhuru na Ruto kurejeshwa nchini Kenya ni utaratibu wa kisheria utakao amuliwa na majaji wa ICC.
Alisema kwa mujibu wa mkataba wa Roma ambao ndio msingi wa mahakama ya ICC, nchi yoyote inayotaka kesi irejeshwe yafaa itosheleze kwa majaji wa ICC kwamba itaendeleza mashtaka hayo hayo kwa watuhumiwa.
Bi Bensouda alisema ICC ni mahakama huru ambayo haiegemei misingi ya kisiasa na majaji wake hutoa uamuzi bila kushurutishwa na yeyote.Alisema ICC itaendelea kushirikiana na mataifa 34 yaliyosaini mkataba wa kujiunga na mahakama hiyo.
Wiki jana, viongozi na serikali wanachama wa Umoja wa Afrika waliafikiana mjini Addis Ababa Ethiopia kwenye kongamano lao kwamba yafaa kesi zinazowakabili rais Uhuru Kenyatta, naibu wake, William Ruto pamoja na mwanahabari Joshua arap Sang zirejeshwe na kushughulikiwa nchini Kenya.
Uhuru na Ruto wameshtakiwa kwa kupanga na kufadhili mapigano ya baada ya uchaguzi mkuu wa Kenya wa 2007, yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu na kuwaacha wengine takriban nusu milioni bila makao.
bbcswahili

Israel yapanga kujenga makaazi mapya Jerusalem

Mjumbe wa kimataifa wa Wapalestina Saeb Erakat amesema mpango wa Israel wa kujenga makaazi mengine 1000 mashariki mwa Jerusalem utazikwamisha juhudi za kuyafufua mazungumzo ya kuutatua mgogoro wa Mashariki ya Kati.
Erakat aliitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya asasi moja kuarifu kwamba Israel inapanga kujenga makaazi zaidi ya walowezi.
Erakat amesema mpango wa Israel wa kujenga makaazi zaidi katika Jerusalem ya Mashariki utazivuruga kabisa juhudi zinazofanywa na Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry za kuufufua mchakato wa kuleta amani katika Mashariki ya Kati.
Erakat ameliambia shirika la habari la AFP kwamba Israel ina mpango wa makusudi wa kuzivuruga juhudi za Waziri Kerry. Amesema inapohusu kuchagua biana ya makaazi mapya na amani, Israel wakati wote imechagua kuendelea na ujenzi wa makaazi mapya katika maeneo ya Wapalestina.
Kandarasi za ujenzi zatiwa saini:
U.S. Secretary of State John Kerry (L) meets with Israeli Prime Minster Benjamin Netanyahu in Jerusalem May 23, 2013. REUTERS/Jim Young (ISRAEL - Tags: POLITICS) Jonh Kerry und Benjamin Netanjahu wakiwa Jerusalem
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali nchini Israel bwana Danny Seidemann aliliambia shirika la habari la AFP kwamba kandarasi kwa ajili ya nyumba 300 katika kitongoji cha Ramot kaskazini mashariki mwa Jerusalem tayari zimeshatiwa saini na viwanja 797 vitauzwa kusini mwa Jerusalem katika kitongojo cha Golo kilichopo karibu na Ukingo wa Magharibi.
Vitongoji hivyo viwili vipo katika maeneo ambayo hasa ni ya Waarabu katika mji huo wa Jerusalem. Vitongoji hivyo vilitekwa na Israel katika vita vya siku sita vyamwaka wa 1967 na baadae kuwekwa chini ya himaya ya Israel, hatua ambayo mpaka leo haijatambuliwa na jumuiya ya kimataifa.
Mkurugenzi wa asasi iliyotoa taarifa juu ya ujenzi wa makaazi mapya bwana Seidemann amesema mipango ya ujenzi ilishapitishwa mwaka uliopita kabla ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuagiza kimya kimya kusimamisha kwa muda ujenzi wa makaazi. Lakini habari juu ya mipango ya ujenzi wa makaazi hayo 1000 zimepenya kwa vyombo vya habari.
Netanyahu ajaribu kuepuka lawama:
Ingawa hatua ya kusimamisha ujenzi kwa muda ,haikuthibitishwa rasmi, mashirika yasiyo ya kiserikali nchini Israel yamesema, Netanyahu hakutaka kuonekana kuwa ni pingamizi la juhudi za Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry za kuyafufua mazungumzo baina ya Israel na Wapalestina
Wapalestina wanaitaka Israel iache kabisa shughuli za ujenzi wa maakazi mapya katika maeneo yao ili mazungumzo yaweze kuanza tena.
Mwandishi:Mtullya Abdu.Aptn,afp,
Mhariri:Mohammed Abdul-rahman

Matokeo Mapya ya Kidato cha nne haya hapa!!!

MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE YAMETOKA!

Baraza la mitihani linapenda kuwataarifu kuwa matokeo mapya ya kidato cha nne yaliyopangwa upya yametoka.

Unaweza kuangalia matokeo hayo hupitia:

LINK 1: http://196.44.162.25/csee2012/Olevel.htm

LINK 2: http://196.44.162.33/csee2012/Olevel.htm

LINK 3: http://www.matokeo.necta.go.tz/matokeo_html_2013/CSEE_2012/olevel.htm

LINK 4:http://www.necta.go.tz/matokeo_html_2013/CSEE_2012/olevel.htm