Hatimaye mahafali kwanza ya CASFETA Chuo Kikuu St. John's-Dar es Salaam yamefanyika Jumamosi, tar 29.06.2013 ukumbi wa Mary Peake. Mahafali hayo yalikuwa kwa ajili kuwaaga wahitimu wa shahada ya kwanza ya sanaa na elimu, biashara, uchumi na theolojia. Mgeni rasmi katika mahafali hayo alikuwa Ndg Christopher Ngubiageya Katibu (M) Vyuo Vikuu (CCM). Mgeni rasmi pamoja na mambo mengina alisisitiza juu ya kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa lakini pia umuhimu wa vijana kushiriki katika siasa na uongozi ili kujenga taifa, kuhubiri amani na utulivu hasa ktika kipindi ambacho Taifa linapita katika misukosuko ya gesi na mabomu.
Picha katika mahafali hayo jinsi yalivyofana;
Picha zote zimepigwa na Dany kwa hisani ya Kapagi Info Institute