HOJA MPYA YA ASKOFU GAMANYWA--MAHUSIANO YA KIIMANI KATI YA MKRISTO NA TAIFA LA ISRAELI (SEHEMU YA 1)
![]() |
Askofu Sylvester Gamanywa,Rais wa WAPO MISSION INTERNATIONAL. |
Hivi karibuni nimetangaza mkakati maalum wa kuongoza
misafara ya kuzulu Israeli. Misafara hii nimeipa jina la “ziara za kinabii
katika Israeli”. Ziara ya kwanza itafanyika tarehe 9/7/2012 na itakuwa ya siku
12. Kwa kuwa ninafahamu kwamba, kuna utata wa kitheolojia uliochanganyikana na
itikadi za kisiasa, nimeona niilete mada hii ili kutoa elimu sahihi, kuhusu
“mahusiano ya kiima yaliyopo kati ya Mkristo na taifa la Israeli. Katika mada
hii nakusudia kusimulia kwa ufupi historia ya maagano ya Mungu kwa Israeli na
jinsi maaganoo hayo yanavyomgusa kiimani kila ajiitaye Mkristo, mpaka uchambuzi
wa kiini cha utata wa kitheolojia kinachosababisha baadhi ya wakristo wasijue
umuhimu wa kulinda mahusiano ya kiimani
kati ya na Israeli. Kwa leo nitaanza na historia fupi kuhusu maagano ya Mungu
kwa Israeli na utendaji wake kiimani kwa mkristo halisi:
Agano
La Mungu Kwa Ibrahimu
Japokuwa kihistoria katika Biblia
kuhusu maagano ilianza kwa Adamu na
kisha kwa Nuhu. Tunapochunguza uzito wa maagano kati ya Mungu na binadamu,
tunakuta unakuwa na uzito wa pekee kuanzia maisha ya mtu aliyeitwa Ibrahimu.
Mungu anajieleza kwa Ibrahimu akimtabiria mambo makubwa yanayomhusu yeye
binafsi na vizazi vyake vitakavyofuata baada yake. Tunapochunguza mchakato wa agano
la Mungu kwa Ibrahimu tunakuta unaanza na wito, unafuatiwa na kiapo na utabiri
wa mambo yajayo kwa uzao wa Ibrahimu:
1. Wito
wa Mungu kwa Ibrahimu
Historia ya Agano la Mungu kwa Ibrahimu
inaanza ni wito maalum wa kutoka katika nchi yake, katika jamaa zake, na
kuhamia katika nchi mpya ambayo angeoneshwa na Mungu mwenyewe. Mungu anatoa ahadi maalum kwa Ibrahimu
zitakazotokana na utii na uaminifu wake mbele za Mungu.
“Bwana akamwambia Abramu, toka wewe
katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpka nchi
nitakayokuonyesha; name nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na
kuliza jina lako; nawe uwe Baraka; name nitawabariki wakubarikio, naye
akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.”
(Mw.12:1-3)
Ukilisoma kwa makini agano hili utagundua mambo muhimu
matatu ambayo ni ahadi maalum zisizo na masharti ambazo Mungu alizitoa kwa
Ibrahimu. La kwanza, ahadi ya nchi, pili ni ahadi ya uzao,
na tatu ahadi ya Baraka.
2. Kiapo
cha Mungu cha agano na Ibrahimu
Baada ya Ibrahimu kutii wito na
kuondoka nyumbani kwa baba yake na jamaa zake, wakati ameingia katika nchi
ambayo Mungu alikuwa amekusudia kumpa, aliwasiliana naye ili kumhakikishia
uaminifu wa ahadi zake. Ibrahimu aliomba ushahidi wa utumilifu wa ahadi za
Mungu, na ndipo Mungu akaagiza dhabibu zitolewe ili wafanye agano:
“Kisha akamwambia, Mimi ni BWANA,
niliyekuleta kutoka Uru wa Wakaldayo nikupe nchi hii ili uirithi. Akasema ee
Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi? Akamwambia, unipatie ndama wa
miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na kondoo mume wa miaka mitatu, na
hua na mwana wa njia. Akampatia hao wote, akawapasua vipande viwili, akaweka
kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuwapasua” (Mw.15:7-10)
Maandiko haya yashuhudia mchakato wa
agano ulivyokuwa na ukihusisha kutoa dhabihu ya damu ya wanyama ambayo ni
ishara kuwa ahadi zilizotolewa kulingana dhabihu lazima zitazimizwa.
Kimsingi, utaratibu wa agano hili
ulikuwa ni lazima watu wawili wanaofanya agano wapiti katikati ya vipande
viwili vilivyopasuliwa ikiwa ni ishara ya kila mmoja kujitoa mhanga wa kushika
agano husika. Lakini katika mazingira haya, Mungu akitaka kuonyesha kuwa hili
lilikuwa ni “agano lisilo na masharti” hakumruhusu Ibrahimu kupita katikati ya
dhabihu. Badala yake tunasoma kwamba Mungu peke yake kwa ishara ya moto aliamua
mwenyewe kupita katikati ya dhabihu hiyo:
“Ikawa,
jua lilipokuchwa ikawa giza, tazama, tanuru ya moshi na mwenge unaowaka ulipita kati ya vile vipande vya nyama. Siku
ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, uzao wako nimewapa nchi hii,
kutoka mto wa Misri mpaka huo mto Frati, Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni, na
Mhiti, na Mperizi, na Mrefai, na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na
Myebusi.” (Mw.15:18-21)
3. Ukomo
wa Agano la Mungu kwa Ibrahimu
Aina ya agano la Mungu linaonesha
kwamba ni la kudumu. Mungu alimhakikishia kwamba hilo litakuwa ni agano la milele, kutoka
vizazi hadi vizazi vijavyo na halitabadilika wala kufikia ukomo. Mojawapo ya
mambo ambayo ni ya kudumu ni “haki ya umilikaji” wa nchi ya Kanaani:
“Agano langu nitalifanya imara kati ya
mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele,
kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako. Nami nitakupa wewe na
uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa
miliki la milele; name nitakuwa Mungu wao” (Mw.17:7-8)
4. Mapito
yajayo ya uzao wa Ibrahimu
Pamoja na kwamba, agano la Mungu kwa
Ibrahimu halikuwa na masharti ya kumwajibisha, lakini liliweka bayana kuhusu
mapito ambayo uzao wake utapitia.
Biblia ilitabiri kabla kwamba wa
Ibrahimu ungelijikuta utumwani kwa kipindi cha miaka mia nne. Lakini baada ya
hapo Mungu angekumbuka ahadi yakwe kwa Irahimu na kwenda kuwakomboa ili
kuwaleta katika nchi aliyomwonyesha:
“BWANA akamwambia Abramu, ujue hakika
ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu
wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne. Hata na taifa lile watakaowatumikia,
nitawahukumu; baadaye watatoka na mali nyingi. Lakini wewe utakwenda
kwa baba zako kwa amani, utazikwa kwa uzee mwema. Na kizazi cha nne kitarudi
hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado.” (Mw.15:13-16)
Agano
La Mungu Kwa Isaka
Wakati Mungu alipokuwa akiweka agano na
Ibrahimu, bado alikuwa hana watoto wa kuwazaa mwenyewe. Siku moja Mungu
alimhakikisha kwamba atampa mtoto wa kurithi agano la ahadi. Katika mahangaiko
ya kibinadamu Sara alimshauri Ibrahimu amchukue Hajiri mjakazi ili ajipatie
mtoto kupitia yeye.. Katika zoezi hilo
akapatika mtoto wa kiume aliyeitwa Ishmael.
Wakati Mungu alipomtokea ili kuimarisha
agano lake, Ibrahimu alimpendekeza Ishmael kuwa apokee mbaraka wa agano la
ahadi kwa ajili ya vizazi vijavyo. Biblia imeandika msimamo wa Mungu kwa
Ibrahimu kuhusu mtoto atakayekuwa mrithi wa agano la ahadi. Mungu hakumteua
Ishmaeli akubeba wajibu huo maalum: Badala yake alipendekeza habari za urithi
huo utatwaliwa na nani:
“Ibrahimu akamwambia Mungu,, lau kwamba
Ishmaeli angeishi mbele yako. Mungu akasema sivyo, lakini Sara mkeo atakuzalia
mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake
Isaka. Nami nitafanya
agano langu imara kwake kuwa agano la milele kwa ajili ya uzao wake baada yake.
(MW.17:18-19)
Pamoja na kwamba Mungu hakumteua
Ishmael kuwa mrithi wa agano la ahadi, lakini pia hakumtelekeza kabisa. Mungu
alimpatia Ishmael mbaraka wake maalum ambao unadhihirisha kwamba yeye naye
kabarikiwa na Mungu.
“Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia,
nimembariki, nitamzidisha, nami
nitamwongeza san asana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe
taifa kuu. Bali agano langu nitalifanya imara kwa Isaka, ambaye Sara atakuzalia
majira kama haya mwaka ujao.” (Mw.17:20-21)
Kikapita kipindi cha mwaka ndipo Isaka
akazaliwa. Hapo katikati yalipita mengi
lakini Biblia imeandika kwamba ulipofika wakati Ibrahimu kugawa urithi
wake alitii agizo la Mungu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo:
“Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa
nayo. Lakini wana wa Masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi,
naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake,
waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu.” (Mw.25:5-6)
Mwisho tunashuhudia Mungu akiwasiliana
na Isaka moja kwa moja ili kulifanya imara agano lile alilolirithi kutoka kwa
Baba yake:
“Ikawa njaa katika nchi hiyo, mbali na
njaa ile ya kwanza iliyokuwa siku za Ibrahimu. Isaka akamwendea Abimeleki,
mfalme wa Wafilisti, huko Gerari. BWANA akamtokea, akasema, usishuke kwenda
Misri, kaa katika nchi nitakayokuambia. Kaa ugenini katika nchi hiyo, name
nitakuwa pamoja nawe, na kukubariki, maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi
zote. Nami nitakifanya imara kiapo nilichomwapia Ibrahimu baba yako.
Nitazidisha uzao wako nchi hizi zote, na katika uzao wako mataifa yote ya dunia
watajibarikia. Kwa sababu Ibrahimu alisikiai sauti yangu, akayahifadi maagizo
yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu.” (Mw.26:1-5)
Agano
La Mungu Kwa Yakobo
Historia ya Biblia imeandika jinsi
ambavyo, Mungu alikuwa makini sana
katika kuhakikisha anateua mtu anayestahili kurithi agano la ahadi alilofaanya
na Ibrahimu. Tumekwisha kuona jinsi alivyomteua Isaka badala ya Ishmaeli. Sasa
tunamkuta Mungu akiwa makini katika uteuzi wake.
Isaka alizaa watoto wawili wa kiume
mapacha. Esau na Yakobo. Aliyetangulia kuzaliwa ni Esau lakini akifuatiwa na
Yakobo akiwa ameshika kisigino cha Esau.
“Siku zake za kuzaa zilipotimia,
tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake. Wa kwanza akatoka, naye alikuwa
mwekundu mwili wote kama vazi la nywele.
Wakamwita jina lake
Esau. Baadaye ndugu yake
akatoka, na mkono wake umashika Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo.
Isaka alikuwa mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa.” (Mw.25:24-24)
Historia ya Biblia inaendelea kusimulia
jinsi ambavyo mapacha hawa walikuwa na mambo kibinadamu yalitafsiriwa kuwa
ujanja lakini yamadhihirisha kuwa ulikuwa ni ushindani wa kiimani, tena mabao
Mungu aliufuatilia kwa karibu mpaka mwisho.
Jambo la kwanza, Yakobo kununua haki ya
mzaliwa wa kwanza:
“Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau
akaja kutoka nyikani naye alikuwa amechoka sana. Esau akamwambia Yakobo tafadhali nipe
hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu.
Yakobo akamwambia, kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza. Esau
akasema, tazama, mimi ni karibu na kufa, itanifaa nini haki hii ya uzazi?
Yakobo akamwambia, uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake
ya mzaliwa wa kwanza. Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye
akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake
y amzaliwa wa kwanza.” (Mw.25:29-34)
Tukio la pili la aina yake ni pale ambapo Isaka alitaka kurithisha agano
la ahadi kwa mtoto wake wa kwanza mbaye ni Esau. Inavyoonesha lile tendo la
Esau kumuuzia Yakobo haki ya mzaliwa wa kwanza hazikuwahi kumfikia Isaka.
Lakini mkewe Rebeka tangu wakati akiwa mjamzito wa mapacha ya Esau na
Yakobo alipata shida mpaka mimba hiyo mpaka akamwomba Mungu kuhusu hali hiyo.
Na Mungu hakusita alimjibu kuhusu mambo yatakayowapata watoto atakaowazaa:
“Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema,
Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza BWANA. BWANA
akamwambia, Mataifa mawili yako tumboni mwako, Na kabila mbili za watu
watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili,
Na mkubwa atamtumikia mdogo. “(MWA. 25:22, 23)
Hapa tunahitaji kuzingatia mambo ya msingi yafuatayo. Kwanza,
Rebeka alijua tangu kuzaliwa kwa Esau na Yakobo ni nani atachukua nafasi ya
urithi wa Agano la ahadi. Haijulikani kama Rebeka alimwabia Yakobo siri hii au
la. Pili, tukumbuke kwamba kisheria, Esau alikwisha kuipoteza haki ya mzaliwa
wa kwanza kwa Yakobo. Lakini naye aliamua kupuuza. Yakobo aliamini kwamba
kisheria yeye ndiye mzaliwa wa kwanza badala ya Esau, japokuwa baba yake Isaka
hajui yote hayo.
Watafsiri wengine wa maandiko wanadhani kwamba Yakobo na mama yake wote
waliijua siri hii ya nani anastahili kupokea mbaraka wa mzaliwa wa kwanza.
Ndiyo maana hoja haikuwa kwa nini wanafanya hila, bali hofu ya kugundulika kwa
hila yenyewe kabla na Isaka.
Biblia haikuficha ukweli wa suala zima badala yake imeandika jinsi mbinu
ilivyofanyika baada ya Esau kwenda kuwinda mnyama wa kumwandalia Isaka chakula;
huku nyuma mama yake Yakobo akamwandalia mwanawe chakula ili awahi kumpelekea
Isaka kabla Esau hajarudi.
Zoezi hilo
lilifanikiwa. Yakobo akawasilisha chakula kwa Isaka baba yake, na baada ya
mahojiano mengi, hatimaye Isaka akaachilia mbaraka wa mzaliwa wa kwanza kwa
Yakobo badala ya Esau:
“Akakaribia akambusu. Naye akasikia harufu ya
mavazi yake, akambariki akasema, Tazama, harufu ya mwanangu. Ni kama harufu ya
shamba alilolibariki Bwana. Mungu na akupe ya umande wa mbingu, Na ya manono ya
nchi, Na wingi wa nafaka na mvinyo. Mataifa na wakutumikie, Na makabila
wakusujudie, Uwe bwana wa ndugu zako, Na wana wa mama yako na wakusujudie.
Atakayekulaani alaaniwe, Na atakayekubariki abarikiwe. (MWA. 27:27-29)
Maswali magumu yameulizwa kuhusiana na tukio hili. Je! Mungu aliridhia
mbaraka huu ambao mtoaji hakuwa anajua anambariki nani? Kama ndiyo, je! Mungu
naye ameshiriki kubariki hila ili mbaraka uende kwa asiyehusika? Kumbuka maswali haya yanamhusu Mungu moja kwa
moja, na vile ambavyo alilichukulia tukio hili.
Lakini kama tulivyokwisha kusoma huko nyuma, Biblia inaweka wazi msimamo
wa Mungu tangu mwanzo kuhusu suala hili. Pamoja na kwamba, mchakatp mzima wa
Yakobo kuupata mbaraka umejaa utata mtupu mbele za Mungu; kinachozingatiwa ni
kile kilichokwisha kutabiriwa na Mungu mwenyewe kabla ya kuzaliwa kwa wahusika.
Isitoshe, Mungu aliridhia Yakobo kupokea mbaraka huo sio kwa ujanja uliotumika,
bali kwa sababu alikwisha kustahili kwa mujibu wa sheria.
“Wala si hivyo tu, lakini Rebeka naye, akisha
kuchukua mimba kwa mume mmoja, naye ni Isaka, baba yetu, (kwa maana kabla
hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame
kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo bali kwa sababu ya nia
yake aitaye,) aliambiwa hivi mkubwa atamtumikia mdogo.” (Rum.9:10-12)
Biblia pia imeandika yote yaliyojiri baada ya Esau kurudi na kukuta
tayari Yakobo ameshateka mbaraka! Biblia
pia inasimulia jinsi Isaka alivyoshtuka baada ya kugundua aliyechukua mbaraka
ni Yakobo na si Esau aliyemkusudia tangu mwanzo. Hata hivyo, Isaka alikuja
kumsamehe Yakobo na kuamua kwa hiari kumbariki rasmi:
Hii kwa chanzo cha Gospel Kitaa.blogspot.com
No comments:
Post a Comment