m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Sunday, 30 June 2013

MAHAFALI YA KWANZA CASFETA TAYOMI CHUO KIKUU ST.JOHN'S DSM YAFANA

Hatimaye mahafali kwanza ya CASFETA Chuo Kikuu St. John's-Dar es Salaam yamefanyika Jumamosi, tar 29.06.2013 ukumbi wa Mary Peake. Mahafali hayo yalikuwa kwa ajili kuwaaga wahitimu wa shahada ya kwanza ya sanaa na elimu, biashara, uchumi na theolojia. Mgeni rasmi katika mahafali hayo alikuwa Ndg Christopher Ngubiageya Katibu (M) Vyuo Vikuu (CCM). Mgeni rasmi pamoja na mambo mengina alisisitiza juu ya kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa lakini pia umuhimu wa vijana kushiriki katika siasa na uongozi ili kujenga taifa, kuhubiri amani na utulivu hasa ktika kipindi ambacho Taifa linapita katika misukosuko ya gesi na mabomu.
Picha katika mahafali hayo jinsi yalivyofana;















Picha zote zimepigwa na Dany kwa hisani ya Kapagi Info Institute

Tuesday, 25 June 2013

Tsvangirai apingana na Mugabe kuhusu uchaguzi


Waziri mkuu Morgan Tsvangirai
Waziri mkuu nchini Zimbabwe Morgan Tsvangirai ametoa wito kwa mahakama ya kikatiba nchini humo kufutilia mbali agizo la rais wa taifa hilo Robert Mugabe kuandaa uchaguzi mwishoni mwa mwezi Julai.
Tsvangirai ameonya kuwa huenda taifa hilo likakumbwa na hali ya switofahamu iwapo uchaguzi huo utafanyika.
Katika ombi lake waziri huyo anasema kuwa mda uliotolewa kuandaa shughuli ya usajili wa wapiga kura na uteuzi wa wagombea ni mchache mno.
Hata hivyo Tsvangirai hakusema ni lini angependa uchaguzi huo ufanyike.
Tayari uamuzi huo wa Mugabe kuitisha uchaguzi mapema kuliko ilivyotarajiwa, umekashifiwa na viongozi wengine wa mataifa ya Afrika Kusini.
Rais Mugabe alikwenda mahakamani mwezi jana kufuatia shinikizo kutoka kwa muungano wa nchi za Afrika Kusini (SADC) kubana hatua ya kuakhirisha shughuli nzima ya uchaguzi.
Ikiwa Tsvangirai atashinda kesi hii, anasema mahakamana itakuwa imezuia jambo lisilo la kisheria kuweza kutumbukiza nchi katika hali ya switofahamu.
Tsvangirai anataka uchaguzi ufanyike tu baada ya mageuzi ya sheria za uchaguzi ambayo yametokana na katiba mpya.
bbcswahili.com

Sunday, 23 June 2013

Ajabu; Gari lililomsafirisha Mandela liliharibika

Mandela akiwa na Mkewe Graca
Gari la wagongwa lililokuwa likimsafirisha hospitalini rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela wiki mbili zilizopita, liliharibika likiwa njiani kwenda hospitalini.
Msemaji wa rais wa Afrika Kusini Mac Maharaj, amethibitisha kuwa gari hilo lilikumba na matatizo na kuwa ilibidi rais huyo wa zamani kuhamishwa hadi gari lingine.
Hata hivyo Bwana Maharaj, amesema tukio hilo halikuwa na tishio lolote kwa afya ya Bwana Mandela, kwa sababu alikuwa na madaktari wa kutosha.
Shirika la habari la Marekani CBS limenukuu vyanzo kadhaa vikidai kuwa Mandela alisalia katika eneo hilo kwa zaidi ya dakika arubaini kabla ya usaidizi kufika.
Shirika hilo la CBS limesema kuwa wakati Bwana Mandela alipokuwa akihamishwa hadi gari lingine viwango vya joto vilikuwa chini sana.
Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alikuwa akisafirishwa kutoka hospitali moja mjini Johannesburg hadi Pretoria, wakati wa tukio hilo lililotokea tarehe nane Juni mwaka huu.
Mandela alilazwa hospitalini huku hali yake ikiwa mbaya kutokana na maambukizi ya mapafu ya mara kwa mara na tangu wakati huo amekuwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.
Hii ni mara ya tatu kwa Bwana Mandela kulazwa hospitalini mwaka huu.
Chanzo; BBC

Rais Kagame afanya mabadiliko ya jeshi


Rais Kagame wa Rwanda
Rais Kagame wa Rwanda

Rais Kagame afanya mabadiliko kwenye uongozi mkuu wa jeshi na kumteua Jenerali Patrick Nyamvumba kuwa mkuu mpya wa majeshi.

Jenerali Patrick Nyamvumba amechukua nafasi ya jenerali Charles Kayonga aliyeshikilia nafasi hiyo tangu mwaka 2002.
Mkuu mpya wa majeshi ya Rwanda,alikuwa kamanda wa kikosi cha umoja wa mataifa cha kulinda amani UNAMID katika jimbo la Darfur nchini Sudan tangu mwaka 2009.
Mabadiliko hayo pia yameshuhudia wadhifa mpya katika uongozi wa jeshi la Rwanda, ambao ni wadhifa wa mkaguzi mkuu wa jeshi uliopewa Brigedia jenerali Jack Nziza baada ya kupandishwa cheo na kuwa meja jenerali.Jack Nziza amekuwa akihudumu kama mkurugenzi mkuu katika wizara ya ulinzi.Pia mkuu wa zamani wa idara ya upelelezi wa nje kanali Dany Munyuza ameteuliwa kuwa naibu kamishna mkuu wa polisi ya Rwanda.Sababu za mabadiliko hayo hazijawekwa wazi.
Chanzo; BBC

Jasusi Snowden atua Moscow

Edward Snowden

Ndege iliyombeba mtaalamu wa zamani wa shirika la ujasusi la Marekani, Edward Snowden imetua mjini Moscow baada ya kusafiri kutoka Hong Kong.

Chanzo kutoka ndege hiyo ya taifa la Urusi kimesema bwan snowden anayetakiwa na Marekani kwa mashtaka ya wizi wa siri za serikali,
Amepanga kuondoka hapo kesho jumatatu kuelekea nchini Cuba kabla ya kuelekea Venezuela ambako amepanga kuomba hifadhi.
Mamlaka ya Hong Kong imesema bwana Snowden aliondoka kwa hiyari yake mwenyewe na kisheria baada ya kugundua njama za kutaka kumkamata zinazofanywa na mtandao wa kijasusi wa marekani kambi ya Uchina.
Hong Kong imesema imeyakataa maombi ya marekani ya kutaka kumkamata na kumrejesha bwana Snowden nchini Marekani kwa nguvu kwa kuwa maombi hayo hayaendani na sheria za ndani za nchi hiyo.
Chanzo; bbcswahili.com

Friday, 21 June 2013

Kesi dhidi ya Rais Kenyatta yaakhirishwa


Rais Uhuru Kenyatta
Mahama ya kimataifa ya ICC imeakhirisha siku ya kuanza kusikilizwa kwa kesi dhidi ya rais Uhuru Kenyatta hadi tarehe 12 mwezi Novemba mwaka huu.
Hii ni kufuatia ombi la mawakili wa Rais Kenyatta kutaka kesi yao kuahirishwa hadi mwezi Januari mwaka ujao.
Mahakama iliamua kuwa upande wa Kenyatta unahitaji muda wa ziada ili kujiandaa ipasavyo kwa kesi, kwa sababu viongozi wa mashtaka walichelewa kufichua ushahidi walio nao dhidi ya rais Kenyatta.
Kenyatta anakabiliwa na tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadmau wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya miaka sita iliyopita, akisemekana kuunga mkono mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya watu wa kabila moja.
Naibu Rais wa Kenya William Ruto naye pia anakabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC kuhusu tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kupanga mashambulizi dhidi ya jamii hasimu.
Majaji waliwaalika mawakili wa Uhuru Kenyatta kutoa maoni yao kuhusu muda wanaotaka ili kujiandaa kwa kesi dhidi ya mteja wao.
Baada ya kupokea maoni kutoka kwa upande wa utetezi, upande wa mashtaka, pamoja na waakilishi wa kisheria, majaji waliamua kuakhirisha kesi hiyo kutoka tarehe 9 Julai mwaka huu hadi Novemba.
Tarahe hiyo mpya ilifikiwa baada ya kuzingatia maswala mbali mbali ikiwemo haja ya upande wa mashtaka kujiandaa vyema kwa utetezi wao na mipango ya usafiri.
Rais Kenyatta ameshtakiwa kwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya , makosa ya jinai ikiwemo, mauaji, kuwahamisha watu kinyume na sheria, ubakaji , mateso na vitendi vingine vya kinyama vinavyodaiwa kufanywa wakati wa ghasia hizo mwaka 2007/2008

Mazingira mabaya shuleni hukimbiza walimu

MWALIMU ni mtu wa muhimu katika jamii yoyote kwa kuwa anabadilisha maisha ya kila mtu kutoka hatua moja kwenda nyingine. Cha kushanganza maisha yake ni tofauti na kazi kubwa anayoifanya. Pia wanapata changamoto nyingi katika utendaji kazi wao… wengine wanajikuta wakivikimbia vituo vyao vya kazi kutokana na mazingira magumu wanayofanyia kazi.

Jambo la kusikitisha walimu wanafikia hatua ya kutembea kilomita kubwa kutoka majumbani kwao kwenda kwenye vituo vyao vya kazi hali ambayo haiwezi kuleta matokeo mazuri ya elimu nchini.

Mwalimu anatembea kila siku kilometa 10 kwenda na kurudi kutoka shuleni, anafika amechoka na hana hamu ya kufundisha hivyo anafundisha chini ya kiwango kinachotakiwa.

Licha ya Serikali kujitahidi kuajiri walimu wengi kwenye vituo mbalimbali karibu mikoa yote ya Tanzania, bado imesahau kuwa baada ya kutoa ajira walimu wanaenda kukaa katika mazingira gani.

Idadi kubwa ya walimu wanapelekwa maeneo ya vijijini kutokana na uhaba wa walimu katika maeneo hayo, lakini huduma za kukidhi mahitaji yao bado ni hafifu.

Inasikitisha kuwaona walimu ambao ni mhimili mkubwa katika jamii wanalala jikoni kwa miaka mitatu huku wafanyakazi wengine wakiwa wanatembea zaidi ya kilomita kumi, jambo hili linasikitisha na linatia aibu kwa Serikali yetu.

Kuhusu walimu wanaotoroka kazini na kujiunga na vyuo vya elimu ya juu pasipo ridhaa ya mwajiri, tatizo hili linaathiri zaidi mikoa iliyopo Kanda ya Ziwa na Kaskazini, ambayo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu ambapo chanzo kikubwa ni mazingira mabaya ya kufanyia kazi.

Taratibu za kuyarekebisha maisha ya walimu yatasaidia kupunguza utorokaji wa walimu katika maeneo mbalimbali hapa ikiwemo vijijini ambapo matatizo yanakuwa mengi kuliko wale wa mjini.

Walimu wengi hukimbilia mjini ili kukwepa matatizo ya vijijini ambapo baadhi yao wanajikuta wakiishi kwenye nyumba za udongo na kuamua kuachana na kazi ya ualimu na kujihusisha na biashara nyingine.

Kutokana na hali kuwa tete Serikali ilipanga kuwachukulia hatua watumishi wake zaidi 800 waliotoroka kazini na kujiunga na vyuo vya elimu ya juu bila idhini ya mwajiri.

Jumla ya walimu 26,537 wameajiriwa serikalini kwa mwaka wa fedha 2012/2013, walimu wa ngazi ya cheti walioajiriwa ni 13,568.

Kati yao walimu 13,527 wamepangwa kufanya kazi katika shule za msingi zilizopo kwenye halmashauri na walimu 41 wamepangwa katika shule za msingi za mazoezi zilizo chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Jumla ya walimu wa sekondari na vyuo vya ualimu walioajiriwa ni 12,973 wakiwemo walimu wa Shahada 8,887 na Stashahada 4,086, lakini swali la kujuuliza maeneo waliyopangiwa yanakidhi viwango?

Idadi ya walimu walioajiriwa mwaka 2012/2013 imeongezeka kwa asilimia 11 sawa na walimu 2,630 ikilinganishwa na walimu 23,907 walioajiriwa mwaka uliopita 2011.

Walimu wapya wanakuwa na shauku kubwa ya kuanza kazi, lakini baada ya kuripoti kwenye vituo vyao vya kufanyia kazi na kukuta mazingira si mazuri baadhi yao wanaamua kuondoka baada ya wiki tatu au mwezi mmoja.

Baada ya Serikali kutilia shaka matokeo hayo Baraza la Mitihani Tanzania (BAMITA) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wameamua kurudia kusahihisha lakini matokeo hayajabadilika kwa asilimia kubwa sio siri ufaulu si nzuri kama inavyotakiwa.

Licha ya Serikali kujitahidi kuwaajiri walimu kwa wingi kila mwaka lakini hali bado ni mbaya hasa maeneo ya vijijini ambapo unaweza kuikuta shule ina jumla ya wanafunzi mia 400 lakini wanafundishwa na walimu wawili au watatu hali ambayo haiwezi kuleta matokeo mazuri.

Walimu hawawezi kufanya kazi zao kwa ufanisi ulio juu huku wakiwa wanalala jikoni kwa miaka mitatu na wengine kutembea kwa kilomita kumi,kitu ambacho hakiwezekani.

Wanafunzi wa sasa wanamaliza darasa la saba hawajui kusoma wala kuandika lakini mwanafunzi huyo anafaulu kwenda kidato cha kwanza,kwa hali hii tusitegemee kupata matokeo mazuri na viongozi wazuri wa baadaye.
Chanzo; Mtanzania.co.tz

Mizengo Pinda: Nasema wapigwe tu

Share bookmark Print Email Rating
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda 
Na Waandishi Wetu  (email the author)

Posted  Alhamisi,Juni20  2013  saa 20:57 PM
Kwa ufupi
Lazima tuwakamate na kama katika kuwakamata watafanya jeuri, jeuri, watapigwa tu kabla ya kupelekwa tunapotakiwa kuwapeleka, kwa sababu hatuwezi kuendelea na hali hii, mkadhani kwamba tutafika tunapokwenda.

Dodoma/Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameagiza vyombo vya dola kuwashughulikia kwa kuwapiga wale watakaokataa kutii amri wakati wakifanya vitendo vya uvunjifu wa amani.
Akizungumza katika Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu, bungeni Dodoma jana, Pinda alisema watu wanapokaidi wanajitakia matatizo na vyombo vya dola.
Alisema hayo alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu aliyeuliza: “Serikali ipo tayari kiasi gani kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”
Waziri Mkuu alijibu: “Ni lilelile nililosema... mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria.
“Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.”
Pinda alisema Serikali imedhamiria kurejesha amani nchini ikiwamo mkoani Mtwara na kuwataka Watanzania waiache Serikali ifanye kazi hiyo. Alisema Serikali ina orodha ya watu wanaosemekana kuwa ni vyanzo vya vurugu na matatizo yaliyotokea Mtwara na kushangaa wale wanaopinga kukamatwa kwao.
“Lazima tuwakamate na kama katika kuwakamata watafanya jeuri, jeuri, watapigwa tu kabla ya kupelekwa tunapotakiwa kuwapeleka, kwa sababu hatuwezi kuendelea na hali hii, mkadhani kwamba tutafika tunapokwenda. Nami nasema vyombo vya dola vijipange imara vihakikishe vinadhibiti hali hii,” alisema.
Hata hivyo, jibu hilo lilipata upinzani wakati Mbunge wa Konde (CUF), Khatibu Said Haji alipomwuliza Waziri Mkuu: “Hapo awali umetoa kauli nzito ya kuliambia taifa hili kwamba wale raia wote, ambao watakaokuwa wakaidi wapigwe tu na watapigwa tu; naomba ninukuu Katika Ibara ya 13 na Kifungu cha 6B cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
“Ni marufuku kwa mtu yeyote aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kuteswa kama mtu mwenye kosa, mpaka itakapothibitika anayo hatia kwa kutenda kosa hilo.
“Pia ibara hiyohiyo Kifungu cha 6 E; kinasema ni marufuku kwa mtu yoyote, kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazoweza kumdhalilisha. Kwa kauli yako uliyoitoa huoni kwamba umevunja Katiba?” Akijibu swali hilo, Pinda alisema ni lazima kutofautisha kati ya mtu aliyekwishakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria... “Mimi ninayemzungumza hapa ni mtu yule ambaye ameamua kufanya vitendo hajakamatwa na ndiyo maana nilikwambia usiandamane... hapa mahali hutakiwi kwenda wewe ukaamua kutumia mabavu kwa sababu mko wengi, ndiyo maana nikasema, hawa watu tutashughulika nao hivyohivyo.”
Mbunge huyo hakuridhishwa na majibu hayo na kumtaka Waziri Mkuu kuyafuta.
Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda aliingilia katika na kumweleza mbunge huyo kuwa kila mtu alikuwa amemwelewa Waziri Mkuu na hakukuwa na haja ya kuendelea na hoja hiyo.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Mizengo-Pinda--Nasema-wapigwe-tu/-/1597296/1889674/-/xk60drz/-/index.html 

Saturday, 8 June 2013

ROHO MTAKATIFU NA KAZI ZAKE KWETU

SOMO LA 1 semina

ROHO MTAKATIFU,MTOA UTAKATIFU
Katika somo la kwanza katika mfululizo wa masomo haya yanayohusu Roho Mtakatifu,Tulijifunza kwamba Roho Mtakatifu,ni mtakatifu,hivyo anakuwepo na kudumu mahali palipo na utakatifu tu.Tukiwana maisha ya uchafu,yaani dhambi;humfanya Roho Mtakatifu akose makao kwetu,na hivyo hawezi kuwepo kwetu.Kama alikuwepo mwanzo kwetu,huondoka (1Samweli 16:14;
Zaburi 51:4,10-11).Sasa swali linakuja,tunawezaje kuwa watakatifu katika maisha yetu ili Roho Mtakatifu afanye makao
kwetu?Jibu ni kwamba,Roho Mtakatifu ,ndiye huyohuyo anayetoa utakatifu tunaouhitaji.Sasa tunamwangalia Roho
Mtakatifu kama Mtoa Utakatifu,kwa kutafakari kazi yake hiyo katika vipengere vitano:-
1. ROHO MTAKATIFU,ROHO ATUPAYE KUZALIWA MARA YA PILI
2. ROHO MTAKATIFU ROHO AWAFUFUAYE WATU WALIOKUFA KIROHO
3. ROHO MTAKATIFU, ROHO AWATIAYE UZIMA WATU WALIOZIMIA KIROHO
4. ROHO MTAKATIFU ROHO ATUPAYE UTAKASO
5. ROHO MTAKATIFU, ROHO ATUPAYE TUNDA LA ROHO

BOFYA HAPA USOME ZAIDI

http://calivarychurch.blogspot.com/2011/04/roho-mtakatifu-na-kazi-zake-kwetu.html 

Roho mtakatifu ni nani?



Swali: "Roho mtakatifu ni nani?"

Jibu:
Kuna utatanishi mwingi juu ya kumtambua Roho mtakatifu. Wengine humchukulia kama nguvu Fulani zisizoonekana. Wengine huamini kwamba ni uwezo wa Mungu ambao Mungu huuachilia maishani mwa wale ambao ni waumini wa kristo. Je, biblia inasemaje juu ya Roho mtakatifu? Kwa kifupi biblia inasema kwamba Roho mtakatifu ni Mungu. Pia biblia inasema kuwa Roho mtakatifu ni mtu, mwenye akili, hisia na mapenzi yake.

Swala la kuwa Roho mtakatifu ni Mungu limo ndani ya aya nyingi za biblia kama vile Matendo 5:3-4. Katika ayah ii petro anapambana na anania aliyemdanganya Roho mtakatifu na nasisitiza yakuwa “hukumdanya mtu bali Mungu.” Hili ni tangazo la wazi kwamba kumdanganya Roho mtakatifu ni kumdanganya Mungu. Tunaweza pia kujua Roho mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana tajwa na hali sawa na za Mungu. Roho mtakatifu yuko kila mahali katika Zaburi 139:7-8, “nitaenda wapi nijifiche na Roho? ama nitakimbilia wapi mbali na uwepo wako? Nikipanda juu mbinguni, huko uko; nikifanya malazi yangu kuzimu, tazama uko huko,” tena katika wakorintho wa Kwanza 2:10 tunaona hali yakuwepo kila mahali kwa Roho mtakatifu “Lakini Mungu ameyajulisha kwetu kupitia Roho wake mtakatifu. Kwa kuwa Roho huyachunguza mambo yote, naam, mambo ya siri ya Mungu. Kwa maana ni nani ayajuaye ya mwanadamu isipokuwa roho ya mwanadamu inayokaa ndani yake? Vivyo hivyo, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.”

Tunaweza kujua kweli kwamba Roho mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana akili, hisia na mapenzi yake. Roho mtakatifu hufikiri na hujua (Wakorintho wa kwanza 2:10). Roho mtakatifu anaweza kuugua (Waefeso 4:30). Roho hutuombea (Warumi 8:26-27). Roho mtakatifu hufanya maamuzi kutokana na mapenzi yake mwenyewe (Wakorintho wa kwanza 12:7-11). Roho mtakatifu ni Mungu, sehemu ya tatu ya utatu wa Mungu. Kama Mungu, Roho mtakatifu anaweza kufanya kazi ya msaidizi na mshauri kama vile Yesu kristo aliyevyoahidi kuwa atakuja kufanya (Yohana 14:16,26; 15:26).
Chanzo; http://www.gotquestions.org/Kiswahili/roho-mtakatifu.html

Tuesday, 4 June 2013

Tanzania mpya na Rasimu ya Katibu

Share bookmark Print Email Rating
 
Na Mwandishi Wetu  (email the author)

Posted  Jumatatu,Juni3  2013  saa 20:50 PM
Kwa ufupi
Miongoni mwa mambo ambayo hayamo kwenye Rasimu ya Katiba ni pamoja na Serikali za majimbo, Mahakama ya Kadhi.
 
Dar es Salaam. Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana ilizindua rasimu ya Katiba Mpya inayopendekeza kuwapo kwa mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa utawala, yakiwamo ya kuwa na Serikali Tatu; Shirikisho la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar.

Mabadiliko mengine yaliyosheheni kwenye rasimu hiyo ni kufutwa kwa viti maalumu vya ubunge, suala la maadili ya viongozi wa taifa, umri wa urais kubaki kama ulivyokuwa na kuruhusiwa kwa wagombea binafsi katika ngazi zote; urais, ubunge, udiwani mpaka ngazi za mitaa.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba alisema Tume pia imependekeza kuingizwa kwenye Katiba Mpya mambo kadhaa kama Tunu, Dira na Misingi ya Taifa.
“Tulitaka kuifanya rasimu hii iwe fupi kadri iwezekanavyo, lakini kutokana na wingi wa maoni tumeifanya iwe na Ibara 240. Katiba ya sasa ina Ibara 152,” alisema Jaji Warioba na kuongeza:
“Tumeendelea kuitambua misingi mikuu minne ya taifa ambayo ni Uhuru, Haki, Udugu na Amani. Lakini pia tukaongeza misingi mingine mitatu ambayo ni Usawa, Umoja na Mshikamano. Tumependekeza Katiba yetu mpya iwe na misingi saba.”
Jaji Warioba alisema Tume pia imetambua mambo kadhaa kuwa ni Tunu za Taifa: “Tunu ya kwanza ni Utu. Tunaamini kuwa watu wote ni sawa, tusiwe na ubaguzi wala tofauti zozote. Tunu nyingine ni Uzalendo, Uadilifu, Umoja, Uwazi Uwajibikaji na Lugha ya Kiswahili.”
Jaji Warioba alisema pia kuwa Tume imebainisha malengo ya Taifa ambayo yatakuwa mwongozo wa Mihimili ya Dola; Serikali, Bunge na Mahakama.
“Malengo hayo yatakuwa ya aina mbalimbali. Kuna malengo ya kisiasa, kiuchumi, kimazingira na mengine mengi yatakayofafanuliwa baadaye,” alisema.
Jaji Warioba alisema Tume pia imependekeza Katiba ijayo ionyeshe wazi maadili ya kijamii, kiutawala na kiuongozi.
“Tumependekeza kuwapo maadili ya viongozi, miiko na kiundwe chombo cha kusimamia maadili. Tunapendekeza sekretarieti ya maadili ya viongozi iliyopo, iwe tume kamili,” alisema.
Muundo wa Serikali Tatu
Jaji Warioba alisema baada ya kupitia maoni mengi, Tume imeridhika kwamba inafaa Tanzania iwe na mfumo wa Serikali tatu, yaani Serikali ya Shirikisho, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
“Tumependekeza Serikali ya Muungano iwe na mawaziri wasiozidi 15 na wabunge 75. Wabunge 50 kutoka Bara, 20 Zanzibar na wabunge watano wa kuteuliwa na Rais,” alisema wabunge wa kuteuliwa watatoka katika kundi la watu wenye ulemavu tu.
Alisema Serikali hiyo ya Muungano itakuwa inaongozwa na Rais Mtendaji. Alitaja mambo yatakayoingia kwenye Muungano kuwa ni Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ulinzi na usalama, uraia na uhamiaji, sarafu na Benki Kuu, mambo ya nje, usajili wa vyama vya siasa na ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.
Mikutano 1,942
Jaji Warioba alisema rasimu hiyo ya Katiba imekamilika baada ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba kufanya mikutano 1,942 ambayo ilihudhuriwa na watu 1,306,500.
“Watu 395,000 walitoa maoni ya ana kwa ana na makundi 160 maalumu yalitoa maoni yao. Pia tulizungumza na viongozi wa kitaifa; walioko madarakani na wastaafu. Viongozi 43 walitoa maoni,” alisema.
Jaji Warioba alisema baada ya maoni hayo, walikuwa na miezi mitatu kuyachambua na kuandaa rasimu ya Katiba, lakini wakalazimika kuongeza muda huo hadi Mei mwaka huu.
“Kutokana Sheria, Rasimu hii itachapishwa kwenye Gazeti la Serikali na baadaye kwenye magazeti kabla ya Mabaraza ya Katiba kuanza kazi,” alisema Jaji Warioba .
Alisema mchakato huo wa Mabadiliko ya Katiba ulioanza kwa Sheria iliyotungwa Novemba 2011 na baadaye kufanyiwa mabadiliko Februari 2012, umepangwa kumalizika ndani ya miezi 18... “Hivyo Tume imekusudia kumaliza mchakato huo Novemba Mosi mwaka huu,” alisema.
Chanzo; mwananchi.co.tz

Sunday, 2 June 2013

Mauaji ya kutisha yaibuka msituni

 
Na Burhani Yakub,Horohoro  (email the author)

Posted  Juni1  2013  saa 20:14 PM
Kwa ufupi
  • Kwa kipindi kirefu msitu huo umekuwa eneo la kufanyia mauaji kwa watu wasio na hatia, ambapo genge la wahalifu kutoka Kenya limedaiwa kuhusika na mauaji hayo.

Matukio ya mauaji ndani ya msitu wa Mwakijembe yameendelea kutishia usalama wa Watanzania, wanaoishi jirani na eneo la Horohoro linalopakana na nchi jirani ya Kenya.
Kwa kipindi kirefu msitu huo umekuwa eneo la kufanyia mauaji kwa watu wasio na hatia, ambapo genge la wahalifu kutoka Kenya limedaiwa kuhusika na mauaji hayo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini msitu huo wenye rasilimali nyingi unaodaiwa kutumiwa na genge hilo kwa vitendo haramu vya ujangili, uchimbaji madini na uvunaji wa miti, ikiwemo uchomaji mkaa.
Taarifa za uchunguzi ambazo zilithibitishwa na viongozi wa Serikali ya Vijiji vinavyopakana na msitu huo, zilibaini genge hilo limekuwa likiua kila linayemhisi atafichua uhalifu wao.
Inatoka UK 1
Uchapisha wa Hati za Kusafiria (Kwa mujibu wa taarifa za karibuni, kwa mwaka huu pekee, watu wawili tayari wameshauawa kwa kuchinjwa ndani ya msitu huo.
Matukio hayo ya mauaji yalithibitishwa na Diwani wa Kata ya Mwakijembe, Ramadhani Mtiota ambaye alisema kwa sasa katika eneo hilo hali imekuwa ya hofu kutokana na kuongezeka kwa makundi ya vijana wa rika la Morani wa Kimasai, wanaojiandaa kuvishambulia vijiji vya Kenya.
Diwani huyo alisema ametoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza kuhusu hali hiyo pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Andrew Ngoda.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alisema wanafahamu kuhusu mauaji yanayotokea kwenye msitu huo.
Alisema taarifa za mauaji ya hivi karibuni ya watu wawili, Ali Mohamed na msichana wa kabila la Kimasai Kendie Minja yanafahamika na yanafanyiwa uchunguzi na polisi.
”Ninachofahamu ni mauaji yaliyofanyika ya msichana Kendie kuchinjwa na kufichwa msituni upande wa Kenya, lakini upelelezi unafanywa na Jeshi la Polisi la wenzetu wa Kenya kwa hivyo sijui zaidi ya hivyo,” alisema Massawe.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza alisema anaandaa mkutano wa ujirani mwema utakaowahusisha viongozi wa Serikali Mkoa wa Tanga na Jimbo la Mombasa, Kenya.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Mauaji-ya-kutisha-yaibuka-msituni/-/1597296/1869732/-/11tcb6hz/-/index.html 

Membe: Tanzania haiwezi kuomba radhi Rwanda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akipongezwa na Mawaziri na wabunge mara baada ya kusoma makadirio ya bajeti ya wizara yake Bungeni. ameelezea  kuwa Tanzania haitaiomba Rwanda msamaha kutokana na kauli ya Rais Jakaya Kikwete 
Na Fidelis Butahe, Mwananchi  (email the author)

Posted  Juni1  2013  saa 20:22 PM
Kwa ufupi
  • Serikali ya Rwanda iliitaka Tanzania iombe radhi kwa madai kuwa kauli ya Rais Kikwete ni kama tusi kwao na kwamba wao hawawezi kukaa na kuzungumza wapinzani ambao ni wauaji

Dodoma. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amesema kamwe Tanzania haitaiomba radhi Rwanda, baada ya Rais Jakaya Kikwete kuishauri nchi hiyo kufanya mazungumzo na upinzani ili kumaliza vita katika eneo hilo la Maziwa Makuu.
Serikali ya Rwanda iliitaka Tanzania iombe radhi kwa madai kuwa kauli ya Rais Kikwete ni kama tusi kwao na kwamba wao hawawezi kukaa na kuzungumza wapinzani ambao ni wauaji.
“Kama Rwanda haitaki kufuata ushauri wa Rais Kikwete inatakiwa kuuacha na siyo kumtaka aombe radhi,” alisema.
Membe alitoa ufafanuzi huo bungeni jana wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika mjadala wa makadirio ya matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka 2013/2014.
Tamko hilo la Serikali limekuja ikiwa zimepita takriban siku sita tangu Serikali ya Rwanda kutoa tamko la kupinga ushauri huo uliotolewa na Rais Kikwete wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Akijibu pendekezo hilo la Rais Kikwete, Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Louise Mushikiwabo alisema kuwa Rwanda haiko tayari kufanya mazungumzo na watu ambao walishiriki kwenye mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, dhidi ya Watutsi na kwamba kufanya hivyo ni sawa na kuhalalisha mauaji kwa wananchi wake.
“ Wale wote wanaodhani kuwa Rwanda itaanzisha majadiliano na waasi wa FDLR nadhani kwa ukweli hawajui kile wanachozungumza. Rwanda haiwezi kujadiliana na wauaji,” alisema waziri huyo wakati akizungumza na Idhaa ya Kimataifa ya Radio Ufaransa.
Alisema kuwa wakati serikali ya Rwanda imefaulu kuzika mienendo inayopalilia mauaji ya halaiki, lakini bahati mbaya kumesalia makundi ya watu ambayo bado yanahubiri itikadi zinazokumbusha uchungu na kutonesha kidonda kilicholeta maafa makubwa kwa wananchi.
“ Kumbe kuna wasemaji wengi wa kundi la FDLR. Wengine wao wanaendelea kufungamana na itikadi za kundi hili. Rwanda ilifaulu kutokomeza mauaji ya halaiki lakini hatukutokomeza itikadi za kundi hili,” alisema waziri huyo.
Kauli ya waziri huyo imeungwa mkono na baadhi ya wasomi pamoja na wanaharakati waliosema kuwa kuiomba Rwanda ianzishe majadiliano na kundi hilo, wanapaswa kufikiri mara mbili.
Katika ufafanuzi wake Membe alimnukuu Waziri Mkuu wa zamani wa Israel, Isaack Rabin kwamba mwaka 1995 aliwahi kutoa tamko lililosema, ‘Tunajenga amani na tunajadiliana na maadui zetu na si marafiki’.
Alisema kama Serikali ya Rwanda itakuwa imesikia kauli hiyo inatakiwa kufanya mazungumzo ya amani na maadui, na wasingoje kufanya mazungumzo ya amani na Tanzania, ambayo wana uhusiano mzuri na ni nchi rafiki kwa muda mrefu.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Tanzania-haiwezi-kuomba-radhi-Rwanda/-/1597296/1869740/-/11cm237z/-/index.html 

Saturday, 1 June 2013

Zana za Hizbollah zapatikana Nigeria

  31 Mei, 2013 - Saa 08:30 GMT


Jeshi lilisema kuwa silaha hizo zilikuwa zimefichwa chini ya vumbi la mbao
Karakana ya silaha inayoaminika kumilikiwa na kundi la Hezbollah, nchini Lebanon imapatikana Kaskazini mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa za jeshi na shirika la ujasusi la Nigeria raia watatu wa Lebanon wamekamatwa. Msemaji wa jeshi, Brigedia Gen Ilyasu Isa Abba, pia amethibitisha hilo.
Silaha hizo ikiwemo, risasi, zana za kukinga magari ya kivita dhidi ya mashambulizi na RPG, zilipatikana ktika karakana mjini Kano.
Maafisa wa usalama walisema kuwa silaha hizo zilinuiwa kutumiwa dhidi ya maslahi ya Israel na nchi za Magharibi.
Hii ni kazi ya Hezbollah," katibu mkuu wa usalama mjini Kano Bassey Ettang alisema.Na unaweza hata kuwa na uhakika kuwa ikiwa hili linafanyika, inawezekana wanasaidia makundi ya kigaidi wanaoendesha harakati zao nchini humu,'' alidokeza bwana Bassey.
Brig Gen Ilyasu Isa Abba alisema kuwa zana 11 za magari ya kivita, guruneti na makombora 21 bunduki 17 aina ya Ak-47 na maguruneti 76 ni baadhi ya silaha zilizopatikana.
Mmiliki wa karakana hiyo, ambako silaha zilipatikana, zikiwa zimefichwa chini ya vumbi la mbao, hakuwa nchini humo.
Kuna jamii kubwa ya walebanese wanaofanya kazi mjini Kano, mji wa kibiashara wa Nigeria Kaskazini.
Mji wa Kano eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zimekubwa na mashambulizi ya mara kwa mara katika miaka mitatu iliyopita, tangu wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram walipoanzisha harakati zao.
Bwana Ettang aliongeza kuwa "unaweza pia kuwa na uhakika kundi kama hili likiwa lipo, inaweza hata kuwasaidia wapiganaji wengine walioko nchini humo.''
Hezbollah ni kundi la Kishia pamoja na kuwa vuguvugu la kisiasa lenye makao yake nchini Lebanon. Linatambulika na Marekani kama kundi la kigaidi.
Boko Haram, ambalo jina lake lina maanisha tamaduni za kimagharibi zinapingwa, linasema, nia yake ni kuipindua serikali sasa na kubuni serikali ya kiisilamu.
Kuna wasiwasi mkubwa kuwa kundi la Boko Haram huenda linasaidiwa na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda katika nchi zengine
bbcswahili.com

Japani kuipa Afrika msaada wa dola bilioni 32




Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe Jumamosi (01.06.2013) ameahidi kutowa msaada wa dola bilioni 32 kwa Afrika katika kipindi cha miaka mitano kusaidia ukuaji wa uchumi wa bara hilo kupitia sekta za serikali na binafsi.
Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe ametoa ahadi ya masaada huo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa siku tatu kuhusu maendeleo ya Afrika unaofanyika katika mji wa Yokohama nchini Japani.
Msaada huo unajumuisha utowaji wa yeni bilioni 650 kwa ajili ya mikopo katika ujenzi wa miundo mbinu na mpango wa mafunzo kwa ajili ya vijana wa Afrika.Mpango huo utawapa fursa vijana 1,000 wa Kiafrika kujifunza katika vyuo vikuu vya Japani na kujifunza kazi katika makampuni ya Kijapani.
Abe amesema kuendeleza rasilmali ya nguvu kazi, huduma muhimu za matibabu na kukuza sekta ya kilimo ni mambo muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa Afrika.Amesema kile inachokihitaji Afrika ni uwekezaji katika sekta ya binafsi ambapo ushirikiano kati ya sekta za umma na binafsi utatoa fursa ya kufaidikia na uwekezaji huo. #
Shauku ya Japani kuwekeza Afrika
Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Maendeleo ya Afrika (TICAD) mjini Yokohama Japani. Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Maendeleo ya Afrika (TICAD) mjini Yokohama Japani.
Tangazo lake hilo linaonyesha shauku ya Japani kuchuana na China katika masuala ya kuipatia msaada na kuwekeza Afrika bara lenye utajiri wa mali asili.
Licha ya uhusiano wa muda mrefu uliopo kati ya Japani na Afrika,umuhimu wa Japani kwa bara hilo umekuwa ukipunguwa kulinganishwa na ule wa China ambapo kiwango chake cha biashara na Afrika ikilinganishwa na Japani ni mara tano zaidi na mara nane zaidi katika uwekezaji wa moja kwa moja.
China huwa haitangazi kiwango cha msaada wake wa maendeleo lakini repoti zinadokeza kwamba hutoa hadi dola bilioni mbili kila mwaka.Kiwango ilichotangaza Japani Jumamosi kimepita sana kiwango hicho cha China.Uhusiano wa Japani kwa Afrika unatofautiana na mataifa mengine kwa bara hilo amesema Abe katika kauli inayoonekana kuikusudia China.
Serikali ya China imekuwa ikishutumiwa na baadhi ya nchi kwa kile mara nyengine kinachoonekana kuwa inachofanya barani humo ni kunyakua ardhi na kutohusisha uwekezaji na masharti ya kuboresha haki za binaadamu au kuzitaka nchi zinazopokea misaada kuwa wazi zaidi.
Waziri Mkuu huyo wa Japani amesema mali asili ya Afrika inasababisha kuwepo kwa fursa muhimu za biashara kwa nchi yenye uhaba mkubwa wa mali ghafi kama Japani lakini nchi hiyo haitotafuta na kuchimba rasilmali hizo kwa sababu tu ya kuzileta Japani.
Msaada ukuze uchumi
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn na Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa mkutano wa TICAD mjini Yokohama Japani. Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn na Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa mkutano wa TICAD mjini Yokohama Japani.
Amesema wataisaidia Afrika ili kwamba mali asili za Afrika zisababishe ukuaji wa kiuchumi wa bara hilo.Abe pia ametoa wito wa kuanzishwa kwa kanuni za uwazi katika biashara na kuimarisha usalama kwa Wajapani wanaoishi na kufanya kazi barani Afrika.Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn ameitaka Japani kuimarisha uwepo wake barani Afrika.
Akizungumza katika kikao cha ufunguzi wa mkutano huo wa Kimataita wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD), amesema ni jambo la kushangaza kwamba kuhusika kwa Japani katika fani ya uwekezaji barani humo kuko nyuma kabisa kuliko vile ingelipaswa iwe kwa hivi sasa kulinganisha na nchi mpya ambazo hivi sasa zimekuwa zikijihusisha katika harakati nyingi.
Afrika lazima ibadilike
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini. Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
Suala la uwekezaji katika sekta ya binafsi limekaribishwa na wajumbe ambapo Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amesema uchumi wa bara hilo hauna budi kuendelezwa. Amesema Afrika lazima ibadilike kutoka kuwa na uchumi unaotegemea usafirishaji nje wa bidhaa na kuwa na uchumi wenye kuongozwa na viwanda pamoja na kutanuwa njia mbali mbali za kiuchumi.Zuma amesema mambo matatu ni muhimu kufikia maendeleo nayo ni : kuunganisha masoko, kuendeleza viwanda na kuendeleza miundo mbinu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon pia amehudhuria mkutano huo ambapo amesema malengo ya mkutano huo ni malengo ya Umoja wa Mataifa.Amesema wamejizatiti kuisaidia Afrika itimize Malengo ya Maendeleo ya Milenia yakiwemo kutokomeza umaskini na njaa ifikapo mwaka 2015.
Mkutano huo wa TICAD utaendelea kufanyika hadi Jumatatu ambapo wajumbe kutoka zaidi ya nchi 50 za Afrika watakuwa wanajadili na Japani jinsi ya kuhakikisha ukuaji wa uchumi endelevu barani Afrika.Mkutano huo unaandaliwa kwa ushirikiano wa mashirika ya kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa,Benki ya Dunia na kwa mara ya kwanza Umoja wa Afrika.Mkutano huo umekuwa ukifanyika kila baada ya miaka mitano nchini Japani tokea ulipoanzishwa hapo mwaka 1993.
Mwandishi : Mohamed Dahman/AFP,dpa
Mhariri :Caro Robdw
dw.de

Ziara ya Obama nchini yazua malumbano

ZIARA ya Rais Barrack Obama wa Marekani imewagawa Watanzania huku wengi wao wakionyesha hofu kubwa ya viongozi wa mataifa makubwa kuwa wanakuja kwa nia ya kupora rasilimali za nchi. Wakati Watanzania wakiwa na hofu, Wakenya wamelalamika kupitia mitandao ya jamii kitendo cha Rais Obama kuwatenga wakati chimbuko la baba yake ni kutoka Kenya.
Wakizungumza na MTANZANIA kwa nyakati tofauti jana baadhi ya wananchi walisema wanashangazwa na ziara ya Rais Obama ikiwa ni miezi michache baada ya ziara ya Rais Xi Jimping wa China ambaye alitia saini mikataba 17 ya maendeleo.

Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro alisema kitendo cha nchi kupokea wageni wakubwa wa mataifa makubwa ni heshima kwa nchi lakini inategemea kiongozi huo amebeba ajenda gani.

Naye Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), Deogratus Munishi alisema Tanzania ni uwanja wa mapambano kwa mataifa makubwa kutokana na rasilimali zake.

Munishi alisema uchumi wa mataifa makubwa unategemea soko na rasilimali za mataifa madogo na akisisitiza kwamba madini ya uranium ndiyo chanzo cha viongozi wakubwa kukimbilia Tanzania.

Katika ziara yake ya kwanza katika Afrika, Rais Obama aliitembelea Ghana.

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YAPAA

Baraza la mitihani limetangaza matokeo ya kidato cha sita mwaka 2013. Matokeo hayo ni mazuri kulinganisha na matokeo ya kidato cha nne yalileta mtikisiko mkubwa. Kwa mujibu wa baraza la mitihani

Asilimia 93 ya waliofanya mtihani huo wa kidato cha 6 wamefaulu.

Shule ya kwanza iliyoongoza ni Marian Girls ya mkoani Pwani na ya pili ni Mzumbe ya Morogoro.

Mwanafunzi wa 1 wa kiume kwa sayansi ni Erasmi Inyase kutoka Ilboru, na kwa wasichana ni Lucylight wa Marian girls.

Upande wa masomo ya Biashara mwanafunzi wa 1 ametoka shule ya Tusiime anaitwa Erick Robert.

Wanafunzi 89 matokeo yao yamezuiliwa kwa sababu mbalimbali.

Wanafunzi watakaothibitika kuwa walikuwa na matatizo ya kiafya, watapewa nafasi ya kurudia mtihani.

Bofya hapa chini ujionee matokeo

http://www.necta.go.tz/matangazo2013/tangazo-usajili-ACSEE2014.pdf