m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Tuesday, 30 April 2013

Maajabu ya Mnali kuwachapa walimu viboko


Leo nimekumbushwa mbali kwa maajabu aliyofanya kanali Mnali aliyewachapa walimu viboko. hakika ni tukio baya kuwahi kutokea hasa kwa mtu mkubwa kama yeye, alituongoza kutokuwa na heshima na maadili. Walimu wote waungane kulaani uonevu

 Kama uliwahi kusikia mkuu wa  wilaya ya Bukoba, Bwana Albert Mnali aliyewachapa walimu viboko ni huyo mwenye miwani na koti jeusi (aliyezungushiwa duara jeusi) aliweka historia Tanzania,kipindi hicho alikuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba na
 taarifa ni kwamba aliwachapa viboko walimu wa shule tatu za Katerero, Kanazi na Kasenene katika mkoa wa Kagera.

Israeli PM admits airstrike against Gaza

04-30-2013 18:45 BJT
JERUSALEM, April 30 (Xinhua) -- Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu admitted that the Israeli Air Force launched a raid on the Gaza Strip on Tuesday morning, leaving a Salafist militiaman dead.
"Today we struck at one of those involved in the criminal firing of rockets at Eilat," Netanyahu said at the start of his meeting with Serbian President Tomislav Nikolic.
"I said that we will not ignore this. Our action is in continuation of our police. We will not accept sporadic firing of rockets from the Gaza Strip or Sinai," Netanyahu added.
"We will act, and are acting, to defend Israeli citizen," Netanyahu said.
He further offered condolences to the Israeli victim, who was stabbed by a Palestinian in the Tapuch junction in the West Bank on Tuesday morning.
"I would like to extend my condolences to his family. The terrorist who perpetrated the murder has been captured and we will continue to act on this front as well in order to defend our citizens," he added.
Earlier, the Israeli Air Force raided the Gaza enclave and killed one person, who is allegedly connected to missile launches towards southern Israel.
The target of the raid was Hitam al-Mashal, 29, who was said to be responsible for 17 missiles launches towards southern Israel in April.
Hitam al-Mashal, 29, was killed as he was riding his motorcycle near a Hamas military base.
This is the first time Israel had targeted a specific person at an air raid since operation Pillar of Defense took place in November, 2012.
The IAF attacked targets at the strip on Saturday night following a rocket launch from the strip towards an Israeli community.
According to a statement released by the Israeli Defense Forces (IDF) spokesperson unit, an Israeli aircraft shelled a terror facility and weapons cache in the southern strip.
This comes after a ceasefire agreement inked between Hamas and Israel after the November military campaign.
cctv.cn

Monday, 29 April 2013

Wafu wanavyofukuliwa, kisha kuzikwa wapya

Makaburi yaliyopo jijini Dar es Salaam 
Na Florence Majani  (email the author)

Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.

Siku zote tunaamini kuwa mtu anapofariki hupumzika kwa amani, lakini siku hizi wafu hao hawapumziki tena kwa amani, bali huamshwa, kisha, wafu wengine kushika nafasi zao.
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.
Maeneo mengi ya kuzikia katika Jiji la Dar es Salaam, hasa yale maarufu kama Kinondoni, Sinza, Temeke na Kisutu yanapendwa zaidi na watu na sasa yamefurika.
Kujaa kwa maeneo haya ya kuzikia kumesababisha makaburi ya watu wengine, kufukuliwa kisha kutumika kuzikia miili mingine.
Hata hivyo, makaburi ambayo hufukuliwa ni yale ambayo hayajajengewa, yametelekezwa, hayana kitu chochote cha kuonyesha kuwa kuna kaburi pale au mengine hayana alama kama misalaba au imeondolewa.
Msemaji wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian Kaiohela anasema kuwa anafahamu kwamba makaburi hayo yamejaa, lakini hakutaka kuzungumza zaidi akitoa ahadi kuwa siku ya Jumatatu atalifikisha suala hilo kwa wahusika wakuu.
Katika makaburi ya Temeke Chang’ombe, Mwananchi Jumapili lilishuhudia makaburi yakiwa yamesongamana kiasi ambacho ni vigumu mtu kupata nafasi ya kuweka mguu.
Mlinzi wa makaburi hayo, Athuman Mtembwe anasema kutokana na ufinyu wa nafasi katika makaburi hayo, makaburi ambayo hayana alama yoyote ni rahisi kufukuliwa na kuzikiwa kwa mara nyingine.
“Mimi kama mlinzi wa eneo hili ninaweza kukutafutia sehemu ambayo unaweza kuchimba kaburi, lakini kama hufahamu utafukua tu maiti nyingine,” anasema
Anasema kuwa mara kwa mara watu wanaokuja kuchimba makaburi ili kuzika ndugu zao, wamekuwa wakifukua miili ya watu wengine ambayo makaburi yao hayakuwa na alama yoyote.
“Ni kawaida, mchimba kaburi anafukua, anakuta mifupa, anaiweka pembeni au anaizika katika shimo dogo…kisha anaendelea na taratibu za kuzika mwili mwingine,” anaeleza.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760490/-/12b2t5y/-/index.html 

Kiongozi wa Kanisa azikwa akiwa hai mkoani Mbeya

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani 


Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Mbeya. Msaidizi wa zamani wa Padri (Katekisita) katika Kigango cha Kanisa Katoliki Kijiji cha Mkwajuni, Florian Mwamosi (70) amekufa baada ya kuzikwa akiwa hai katika kaburi moja na mtu anayedaiwa kumuua kwa njia ya kishirikina.
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani  alikiri kutokea  kwa tukio hilo akieleza kuwa lilitokea  saa 9:00 mchana katika kijiji hicho cha Maweni Mkwajuni wilayani Chunya.
“Marehemu aliuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na mawe kwa tuhuma za kuhusika na uchawi na kusababisha kifo cha Peter Robert,” alisema.
Kamanda Athumani alisema kuwa uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea na kwamba wahusika wote wa tukio hilo wamekimbia na kuzihama nyumba zao, hivyo polisi wanaendelea na msako wa kuwatia mbaroni watuhumiwa na kwamba tayari  kaburi hilo limefukuliwa jana kutenganisha maiti hizo.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa  marehemu huyo ambaye alikuwa akituhumiwa kwa ushirikina aliwahi kuwa Katekista wa kigango hicho hadi mwaka 2007.
Wameeleza kuwa Mwamosi alikwenda kuhudhuria mazishi ya Peter  Robert (28) katika kitongoji hicho cha Maweni, baada ya kufuatwa nyumbani kwake na watu wakitaka aende kwa sababu yeye ni mmoja wa wazee wa mila katika kitongoji hicho.
“Bwana Mwamosi alikuwa akituhumiwa kwa uchawi kwa muda mrefu na wenzie wawili, hivyo alipofika makaburini ilianza minong`ono ya watu na huku wengine wakiguna na ndipo alipoombwa aingie kaburini kwa ajili ya kupokea jeneza lililobeba mwili wa marehemu Peter Robert,” alisema mkazi mmoja wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Joseph.
Alisema kuwa baada ya kuingia kaburini akiwa na watu wengine watatu wenzake walitoka kwa haraka na kumwacha Mwamosi peke yake ndipo kundi la watu waliokuwa eneo hilo la makaburi walianza kumshambulia kwa kumpiga mawe huku wakimwamuru akae chini.
Shuhuda huyo alisema kuwa baada ya kukubali kukaa chini akiwa ndani ya kaburi hilo, walianza kumfukia na alipofukiwa nusu ya mwili wake waliingiza jeneza la marehemu Peter na kuliweka juu yake na kuanza kulifukia kaburi hilo.
“Baada ya kukaa chini ndani ya kaburi hilo ndipo walianza kumfukia kwa udongo na baadaye wakachukua jeneza la marehemu na kuliweka juu yake, kisha kumfukia na udongo na taratibu za mazishi ziliendelea kwa ajili ya marehemu  Peter,”alisema.
 http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760482/-/12b2t55/-/index.html

Saturday, 20 April 2013

Darasa la saba sasa kujiunga vyuo vikuu

Jengo la Chuo Kikuu Dodoma(Udom) moja ya vyuo vitakavyo tumika katika utaratibu huo mpya 
Na Ibrahim Yamola, Mwananchi  (email the author)

Posted  Aprili20  2013  saa 24:48 AM
Kwa ufupi
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.

Dar es Salaam. Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), imepanga kuanza kuwadahili wanafunzi wa kujiunga na masomo ya vyuo vikuu kwa kutumia uzoefu wao.
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.
Kupitia utaratibu huo mpya, mtahiniwa atajiunga na Chuo Kikuu kulingana na fani atakayoiomba na atatakiwa kufanya mitihani mitatu na kufaulu kwa wastani wa daraja B.
Mkurugenzi wa Ithibati na Ubora wa Elimu ya Juu kutoka TCU, Dk Savinus Maronga aliliambia gazeti hili kuwa baada ya kuona kuna watu wengi wanaopenda kuendelea na masomo ya elimu ya juu, lakini wameshindwa kutokana na kutokuwa na vigezo, TCU imeamua kuanzisha mitihani hiyo maalumu.
Alisema kuwa mfumo huo unaojulikana kama ‘Recognition of Prior Learning’ (RPL), utamwezesha mwombaji kudahiliwa vyuoni kupitia tume hiyo kama wanavyofanya watahiniwa wengine.
Sifa zinazotakiwa
Kuhusu sifa za kujiunga, Dk Maronga alisema kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba.
“Mwombaji anatakiwa kuwa na nia ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu na uzoefu wa kile ambacho anakusudia kukisoma.
Awe na uwezo wa kuandika na kusoma Lugha ya Kiingereza, ambayo ndiyo inayotumika kufundishia vyuoni,”alisema Dk Maronga na kuongeza:
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1753450/-/12aid4m/-/index.html 

Monday, 15 April 2013

Dar yarejea enzi za ujima

Abiria wakigombea basi dogo katika kituo cha mabasi ya daladala Ubungo jijini Dar es Salaam jana.
Wakati nauli mpya za daladala, mabasi na treni zikianza kutumika rasmi leo, hali ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam imezidi kuwa mbaya kutokana na mabasi kuwa machache na hivyo kusababisha abiria kulazimika kusafiri kwa malori na magari mengi madogo huku wakitozwa nauli kubwa.
 
Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE umebaini kuwa maeneo ambayo yamekumbwa zaidi na tatizo la usafiri ni kutoka Mwenge kwenda Tegeta, Mwenge-Kibaoni, Ubungo-Mbezi, Ubungo-Mbagala, Gongolamboto-Mwenge na Ubungo kwenda Mlandizi.
 
Kutokana na ukosefu wa daladala kwenye maeneo hayo, kwa takribani wiki moja sasa wananchi wamekuwa wakitumia malori, Toyota Noah, Bajaj, Pick Up, teksi pamoja na Toyota Coaster ambazo hazijasajiliwa kuchukua abiria jijini hapa.
 
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa kutokana na ukosefu wa daladala, hali hiyo imetoa fursa kwa magari yaliyoanza kutoa huduma ya usafiri kwenye maeneo hayo kutoza abiria nauli kubwa ambayo haipo katika viwango vya nauli vilivyopangwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Usafiri wa Majini na Nchi kavu (Sumatra). Nauli inayotozwa na wamiliki magari hayo mfano kutoka Mwenge hadi Tegeta, Mwenge-Bunju, Mwenge-Kibaoni ni Sh.1,000 hadi 2,000 kwa mtu mmoja badala ya Sh. 300 au 400 ya sasa.
 
Kutoka Ubungo kwenda Mbezi, Ubungo-Mbagala, nauli zinazotozwa ni kati ya Sh. 500 hadi 1,000 badala ya Sh.300 wakati kutoka Ubungo-Mlandazi ni Sh.1,000 hadi 2,500.
Magari yaliyobainika kutoza nauli kubwa ni yale ambayo hayajasajiliwa na Sumatra kutoa huduma ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam na yaliyoiba njia.
 
Aidha, daladala ambazo zimesajiliwa kutoa huduma jijini hapa, zinaongoza kukatisha ruti (kuiba njia) na zinafanya hivyo ziweze kurejea mapema vituoni kuchukua abiria wengine hali ambayo inakuwa ni faida kwao. 
 
Mathalani, katika kituo cha Mwenge inapofika jioni, gari za ruti ya Tandika-Mwenge kupitia barabara ya Ali Hassan zimekuwa zikipakia Ubungo na kisha kushusha abiria wote na kupakia tena kwenda Bugurudi na zinapofika hapo hupakia kwenda Tandika.
 
Wakati mwingine, gari hizo zinapofika Ubungo hurudi tena Mwenge kupakia abiria.
 
Wakizunguma na NIPASHE kituo cha Ubungo, abiria waliokuwa wakisafiri kwenda Mbezi Luis, walisema tatizo la usafiri limekuwa sugu na kwamba wakati mwingine wanachukua zaidi ya saa tano kupata gari.
 
Amon Kisimbo mkazi wa Mbezi Luis alisema tatizo la usafiri katika jiji la Dar es Salaam linasababishwa na msongamano wa malori na kwamba serikali inatakiwa kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyowahi kutolewa mwaka 2009.
 
Kisimbo ambaye alidai alikuwa miongoni mwa watu walioshiriki kuandaa mapendekezo hayo katika tume iliyoundwa na serikali, alisema pendekezo walilotoa ni kutaka Bandari ya Dar es Salaam ihamishwe kutoka ilipo sababu inasababisha malori kupita katikati ya jiji na hivyo kusababisha msongano usiokuwa wa lazima. Ofisa Mfawidhi wa Sumatra, Kanda ya Mashariki, Conrad Shio, akizunguza na NIPASHE jana alisema kutokana na ukiukwaji wa sheria za barabara unaofanywa na wenye magari hayo, magari 74 yamekamatwa kutokana na makosa mbalimbali.
 
Shio alisema magari 36 yamekamatwa kwa kukatisha ruti, 18 kwa kuiba ruti na magari 20 yamekamatwa kwa kutoza nauli kubwa.
 
Alisema magari ambayo yamekamatwa kwa kosa la kukatisha ruti wamiliki wake watatakiwa kwenda Sumatra na mkataba wa madereva wengine na hao waliosababisha kosa hilo hawataruhusiwa kufaya kazi ya udereva mahali popote nchini.
 
Alisema tatizo la ukosefu wa magari katika baadhi ya maeneo linatokana na kwamba Sumatra imesimamisha usajili katika ruti ya barabara ya Ali Hasani Mwinyi-Kilwa kwa sababu kuanzia Julai mwaka huu wamiliki wa daladala watatakiwa kujiunga katika kampuni ili kutoa huduma ya usafiri kwenye ruti hiyo.
 
Alisema siyo kweli kwamba daladala zimeadimika na kwamba baadhi ya wamiliki wanakwepa kusajili magari yao kwenye njia zenye foleni kubwa kama Mbezi-Kimara hadi Kivukoni au Kariakoo.
 
MWAKYEMBE ABARIKI NAULI
Serikali imebariki ongezeko jipya la nauli za mabasi yanayotoa huduma mijini, ya masafa marefu na treni hivyo kuziruhusu kuanza kutumika rasmi leo.
 
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, aliwaambia wanahabari jana mjini Dodoma kuwa nauli mpya imeongeza Sh. 50 kwa mwanafunzi na Sh. 100 kwa watu wazima; hivyo daladala zitatoza Sh. 400 badala ya 300 na wanafunzi Sh. 200 badala ya Sh. 150.
 
Alisema  serikali imeridhia ongezeko la nauli lililotangazwa na Sumatra, baada ya kuhakiki na kujiridhisha kuwa ongezeko hilo lilizingatia mchakato wa kupandisha nauli na viwango viliridhiwa na wadau wanaowakilisha maslahi ya wanaotoa na wale wanaotumia huduma hiyo.
 
“Mimi kama Waziri wa Uchukuzi sina tatizo na ongezeko hili dogo la nauli za daladala tatizo langu ni tabia ya Watanzania kukacha vikao halali vinavyojadili mambo yanayotuhusu na kusubiri kuja kulalamika baadaye,” alisema Dk. Mwakyembe.
 
Alisema hayo akiwakosoa wananchi na asasi nyingine kulalamikia nauli nje ya utaratibu licha ya vikao vya kuwataka kutoa maoni kupitia Sumatra kutangazwa na kuwataka wananchi wajitokeze wakati maombi ya wamiliki wa vyombo vya usafiri ya kupandisha nauli yalipokuwa yanajadiliwa.
 
Waziri Mwakyembe alisema maombi ya kuongezwa nauli hiyo mpya yalitolewa baada ya wadau wakiwamo Baraza la Taifa la Walaji wa Huduma zinazodhibitiwa na Sumatra, Chuo cha Usafirishaji, vikiwamo vyama vya watoa huduma vya madereva vya kutetea abiria na wanahabari, kuridhia.
 
“Kulikuwa na mvutano mkubwa wamiliki wakitaka nauli iongezeke na wawakilishi wa abiria wakitaka nauli ibakie ile ile iliyotangazwa mwaka 2011. Ndipo maamuzi  ya nyongeza ya nyongeza ndogo yakawa Sh. 100 na Sh. 50 kwa mwanafunzi yakaafikiwa,” alisema.
 
Aliongeza kuwa wawakilishi wa abiria na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji waliamriwa kuwa iwapo kuna upande usioridhia ukate rufaa kwenye Baraza la  Ushindani, lakini hakuna aliyefanya hivyo.
 
Wiki iliyopita Waziri Mwakyembe alisema wizara hiyo itapitia nauli hizo kutokana na malalamiko mengi kutolewa na wananchi wakipinga nyongeza hiyo.
Imeandikwa na Gaudensia Mngumi, Dodoma na Thobias Mwanakatwe, Dar
CHANZO: NIPASHE

Baadhi ya wadaiwa wa Bodi ya Mikopo wako taabani

http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/10881-baadhi-ya-wadaiwa-bodi-ya-mikopo-wako-taabani

Gesi ni hatari, Zimamoto wawahi kuokoa.



Gari la zimamoto likiwasili eneo la tukio
Leo asubuhi muda wa saa 3:30 kumetokea mlipuko mkubwa kwenye Glosary ya Kipingu eneo Mtaa wa Sae karibu kabisa na kituo cha Sae. Mlipuko huo wa moto umetokana na jiko la gesi lililokuwa likiwashwa ili kupasha supu na ndipo likalipuka na kuanza kuwaka moto mkali. Moto umezua balaa kubwa kwani kutokana na ukosefu wa vifaa vya tahadhari  vya zima moto na elimu ya majanga watu wakaanza kuzima kwa maji na mchaka lakini ikawa ni kama kuuchochea zaidi. Baada ya kushindika kuzima moto uliokuwa ukiwaka kwenye mtungu wa gesi na kuendelea kusambaa kwenye vyombo vingine ndipo kijana mmoja jasiri maarufu kama KP akajitosa na kuuburuzia nje mtungi uliokuwa ukiwaka moto mkali. Hapo ndipo akawa ameokoa nyumba hiyo yenye maduka manne isiwake moto.
Zimamoto wawahi kuokoa, kinyume na desturi ya zimamoto ya kuchelewa mara wanapoitwa kwenye majanga ya moto kwani waliwasiri mara moja baada ya kupigiwa simu. Zimamoto wamewapongeza wananchi kwa kuweza kuokoka jingo kuwaka moto kwa kuutoa nje mtungi unaowaka moto. Askari wa zimamoto wakauzima moto uliokuwa unaendelea kuwaka kwenye mtungi wa Gesi.
Wasisitiza kutoa taarifa mapema kila mara janga linapotokea kuwakumbusha wananchi kuw ana namba za simu ya kiganjani mbali ya ile ya mezani ili kutoa taaarifa kwa haraka zaidi. Ikumbukwe kuwa mara nyingi zima moto wamekuwa wakilalamikia baadhi ya watu wasio waaminifu wamekuwa waktoa taarifa za uongo kupitia simu ya bure ya 111.
Ushauri wa bure kwa wote wenye majiko ya gesi ni bora wakanunua kifaa cha kuzima moto (Fire Extinguisher) ili watumie kuzima moto mara moto unapolipuka.
Namba za kiganjani za Zimamoto jiji la Mbeya ni
0755 651923
Tazama Picha kutoka eneo la tukio
watu wakushuhudia uzimaji wa mtungi

mtungi umezima

Askari akizima mtungi uliolipuka

 Hata boda boda walikuwepo kujionea wenyewe




 Moto umezimwa tayari kwa safari.
Picha zote na KII

Kwisha! UFARANSA YAPITISHA MUSWADA NDOA ZA JINSIA MOJA, SWEDEN NAKO KIMBILIO LAO

Vuta nikuvute imetokea katika bunge la senate nchini Ufaransa, ambapo mwisho wa siku iliamuliwa kupitisha kwa muswada wa sheria ya kuruhusu ndoa za jinsia moja nchini humo, licha ya upinzani mkali kutoka kwa wabunge wenye msimamo mkali, ikiwamo viongozi wa dini.
Uamuzi huu ambao umepitishwa Ijumaa taehe 12 Aprili 2013 na Ufaransa , taifa lenye asili ya katoliki, umekuja baada ya muda mrefu wa majadiliano, kama ambavyo Rais François Hollande alivyoahidi kwenye uchaguzi mkuu mnamo Aprili mwaka 2012, sera ambayo ilimfanya avune kura nyingi za wafuasi wa ndoa hizo.
Waziri wa Haki, Bi Christian Taubira. © Gouvernement
Mtetezi mkubwa wa muswada huo, waziri wa haki nchini huko, Bi Christian Taubira, amesemema kuwa muswada huo unakuja kutokana na umuhimu wake, hasahasa kwa watoto wanaoishi na wazazi wa jinsia moja, ili wapate haki zao sawa na watoto wa wazazi wa kawaida. na kwa mujibu wa muswada huu, basi wenye ndoa za jinsia moja, watarushusiwa kuasili watoto kwa ajili ya kuwalea.
Tumefanya hivi kwa sababu kuna watoto hawali chakula cha afya, wanakula pipi kwa wingi, na kadha wa kadha, hao pia tunawalinda - wanahitaji hilo. Christian aliwaambia maseneta mara baada ya kupitisha muswada huo, ambao utapitiwa tena February 2014 kwa ajili ya marekebisho.
Kwa upande wake, seneta wa chama cha UMP, Jean-Pierre Raffarin, amesema kuwa bado wataendeleza mpambano kwa kuwa bunge bado lipo, na kilichopo ni kwamba watakuwa wakiongea na wananchi wataobadili mawazo ili kuhakikisha muswada huu unaondolewa na kurejea katika hali ya mwanzo, yaani mume na mke na si vinginevyo.
Mpaka sasa ufaransa imegawanyika kuhusiana na ndoa za jinsia moja, ambapo mnamo January mwaka huu, takriban watu 340,000 waliandamana kupinga ndoa za aina hii, wakisisitiza Baba na Mama kwa familia. Ambapo wiki mbili baadae, kundi la watu takriban 125,000 walijitokeza mtaani kuunga mkono ndoa za namna hiyo.
Nchi ambazo zimeridhia ndoa za jinsia moja mpaka hivi sasa. © CBC
Ulaya ni bara ambalo nchi zake kadhaa zimeruhusu ndoa za namna hii, ambapo kwa watu ambao nchi zao haziruhusu, wamekuwa wakikimbilia huko ili kuonana na kuishi kwa sheria za huko. mfano mmojawapo ni mashoga wawili Waganda, ambao walikimbia nchi yao na kuelekea Sweden ili kuonana kutokana na nchi yao kukataza vitendo vya ushoga na usagaji.
Wadau wa Gospel Kitaa walio nchini Sweden, walifanikiwa kupata tukio hilo kama lilivyofanyika mwezi wa kwanza kwa kamera, na hatimaye mdau Nahshon Kamugisha kuzirusha kwa GK.


Jimmy na Lawrence wakiwa na mashoga wenzao wakati wa sherehe ya 'kuonana'.
Gospelkitaa.com

Maajabu Geita:Aliyefariki miaka mitano iliyopita afufuka

mwanamke anayedaiwa kufariki miaka mitano iliyopita 


Posted  Jumapili,Aprili14  2013  saa 24:51 AM
Kwa ufupi
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.Share

Geita: Mji wa Geita na maeneo ya jirani juzi ulikumbwa na taharuki ya aina yake, pale mwanamke ambaye anadaiwa kwamba alifariki miaka mitano iliyopita alipoonekana akiwa hai katika eneo la Kasamwa.
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.
Aliyekuwa wa kwanza kumwona Flora ni mdogo wake aitwaye Monica Onesmo ambaye baada ya kuamka saa 11:00 alfajiri nyumbani kwa dada yake, alimwona mwanamke aliyekuwa ameketi nje ya nyumba hiyo, lakini alimfananisha mwanamama huyo na marehemu dada yake.
“Baada ya kumwona nilimwita mtoto wake tunayekaa naye na nikampigia simu dada (Monica) ambaye alikuwa amelala chumba kingine nikamwambia kwamba nimeamka na kumkuta mwanamke amekaa hapa nje, lakini kila nikimwangalia anafanana na marehemu dada yetu,”alisema Jubili na kuongeza kwamba alipowaita wote walitoka nje.
Alisema mtoto wa Flora (marehemu anayedaiwa kufufuka) anaitwa Rebeka Elisha (16) na kwamba walimchukua tangu 2008 wakati mama yake huyo alipofariki dunia katika Hospitali ya Geita ambako alikuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.
Rebeka ambaye ni mtoto wa nne wa Flora alisema: “Mama mdogo alituita sisi tulikuwa tumelala akasema kwamba nje kuna mwanamke ambaye anafanana na marehemu mama yetu, ndipo na sisi tukatoka na kweli kumwangalia alikuwa ni yeye kabisa.”
Alisema walipomuhoji mama yake huyo kwamba ametokea wapi, aliwaeleza kuwa ametoka eneo la Katoro kwa mganga na aliletwa na watu ambao hakuwatambua Alhamisi saa 1:30 usiku ndani ya gari na watu hao walimshusha kwa mtu aitwaye Juma Luchunga ambaye ni jirani na dada zake hao.
Kauli ya Flora
Akizungumza na waandishi wa habari, Flora alisema yeye ni mkazi wa Katoro na kwamba alitokea Katoro nyumbani kwa mganga wa jadi ambaye hata hivyo hakumtaja kwa maelezo kwamba wataalamu wake (majini) wamemkataza.
“Nilikuwa naishi kwa mganga wa kienyeji ila alikuja mwanaume wakati nikiwa pale akaninywesha dawa kisha tukapakizwa kwenye gari na watu wawili ambao sikuwatambua, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume mpaka hapa Kasamwa tukashushwa saa 1:00 jioni,”alisema Flora.
Alisema alipofika Kasamwa alikwenda kunywa uji kwa mama mmoja ambaye pia hakumtaja na kwamba baadaye alipelekwa nyumbani kwa mtu mwingine saa nne usiku, lakini watu wa nyumba hiyo walipomwona walimwambia: “Hapa si kwako twende tukupeleke kwa ndugu yako” na ndipo wakampeleka kwa dada yake ambako aliketi nje hadi alfajiri.
Flora alisema kabla ya kuishi kwa mganga alikuwa akiishi porini ambako alitupwa na watu asiowafahamu na baadaye aliokotwa na wasamaria wema ambao ndiyo walimpeleka kwa mganga ambako alikuwa akiishi muda wote.
Endeleahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1747968/-/129ypge/-/index.html

Sunday, 14 April 2013

Israel marks Memorial Day


Watch Video

Play Video
Israel is entering one of its most emotionally charged weeks of the year. On Sunday, the country held a Memorial Day ceremony for the Israeli Defense Forces’ Fallen Soldiers at Jerusalem’s Ammunition Hill.
Memorial Day will run from Sunday to Monday evening. It will be followed by the country’s 65th Independence Day celebration. Both holidays keep with Jewish tradition, in which sunset marks the beginning of a new day.
Israel’s Independence Day marks the end of the British Mandate. The country’s first prime minister, David Ben-Gurion, declared Israel’s independence in 1948.
CCTV

Venezuelans vote on future of "Chavista" socialism



CARACAS | Sun Apr 14, 2013 4:31pm EDT
(Reuters) - Venezuelans went to the polls on Sunday to vote whether to honor Hugo Chavez's dying wish for a longtime loyalist to continue his self-proclaimed socialist revolution or hand power to a young challenger vowing business-friendly changes.
Acting President Nicolas Maduro had a double-digit lead over opposition challenger Henrique Capriles in most polls heading into election day, buoyed by Chavez's public blessing before he died from cancer last month. But the gap narrowed in recent days, with one survey putting it at 7 percentage points.

http://www.reuters.com/article/2013/04/14/us-venezuela-election-idUSBRE93C0B120130414 

Saturday, 13 April 2013

Yes! President Uhuru meets Raila, Kalonzo


Uhuru and Ruto share a light moment with Odinga and Musyoka at State House Nairobi
By PPS
President Uhuru Kenyatta and his Deputy William Ruto Saturday at State House Nairobi met and held talks with CORD leaders Hon. Raila Odinga and Hon. Kalonzo Musyoka who paid him a courtesy call.
During the meeting, the CORD leaders conveyed their message of goodwill to the President and his deputy saying they wished them well in running the country.
In light of the recently concluded general election that was closely contested, the talks also touched on the need to bring Kenyans together and unite the country.
During the meeting, President Kenyatta expressed the willingness of the Jubilee leadership to nurture a working relationship with all Kenyans irrespective of their political affiliations in order to strengthen national unity.
The leaders called upon Kenyans to now rise above the differences that arose during the electoral period and join hands in nation building as members of the same Kenyan family.
Source; kcb.co.ke

Friday, 12 April 2013

We offer best services, read

KII offered services are available for you, Karibu sana

MAAJABU, MAKANISA NDANI YA MAPANGO

Mapango yana mchango mkubwa katika historia ya Uyahudi na Ukristo kwa ujumla. Daudi alijificha kwenye pango wakati akimtoroka mfalme Sauli, nyaraka muhimu za 'bahari ya shamu'pia zilipatikana kwenye pango, na wakristo pia wamekuwa wakikutana kwenye mapango kwa ajili ya kuabudu.
Huko Bulgaria, katika mji wa Mihalich - kuna pango ambalo kanisa lilikuwa likikutana. Wanahistoria na wataalamu wa mambo ya kale wanaamini kuwa kanisa hilo la pango limetumika mnamo karne ya 10.

 Flickr/Klearchos Kapoutsis - Creative Commons
Kwa mujibu wa tovuti ya a view on cities, Kanisa la pango la Mtakatifu Stefano mjini Budapest, Romania, lilifungwa na wakomunisti mwaka 1951, na kisha kufunguliwa tena mwaka 1989. Kanisa hilo lilikamilishwa ujenzi wake mwaka 1931.
© Flickr/Robot B - Creative Commons
Pengine kanisa la pango ambalo linafahamika sana duniani ni lile la Misri, ambapo wa'Zabbaleen', watu wanaokusanya taka jijini Cairo wanaabudu.
Kwa mujibu wa mtandao wa wikipedia, kuna makanisa ya pango saba yaliyojificha kwenye mapango ya mlima Mokattam. Kanisa la Mtakatifu Simon the Tanner ndilo kanisa kubwa mashariki ya kati, likiwa na uwezo wa kuchukua watu waliokaa 20,000.

© Flickr/Roaring Jellyfish - Creative Commons



Kanisa hilo limechuka jina la Mtakatifu Simon the Tanner ili kumuenzi, mkristo wa dini ya Coptic kutoka karne ya kumi.
Urithi ambao umeachwa na makanisa ya handaki ni mkubwa na wa kipekee.
Mtume Paulo anaandika kwenye waraka wa Waebrania sura ya 11 kuhusu waamini waaminifu ambao wameonesha imani ya kipekee.
"(Watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi" Waebrania 11:38
Mpaka hivi sasa, kuna wakristo ambao huabudu kwenye makanisa yaliyo kwenye mapango.

Thursday, 11 April 2013

G8 wailaani Korea Kaskazini

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa mataifa manane yaliyoendelea zaidi kiviwanda wameungana kuilaani Korea Kaskazini, na kuitaka nchi hiyo kukomesha mara moja kutoa vitisho vya kivita
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani, Guido Wester Welle, amesema katika siku ya pili ya mkutano wa mawaziri hao unaoendelea jijini London, Uingereza, kuwa mataifa yote ya G8 yanaaminini kuwa kuongezeka kwa matamshi hayo ya kuchochea vita kutoka kwa Korea Kaskazini lazima kusitishwe.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani, Guido Westerwelle Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani, Guido Westerwelle
"Suala la kwa nini matamshi hayo ya kuchochea vita yanaongezeka – ingawa ni muhimu, lakini halina uzito mkubwa. Muhimu zaidi ni kwamba matamshi hayo hayapelekei kuripuka kwa vita. Na ndio maana ni muhimu sasa kuona jumuiya ya kimataifa ikiwajibika na kuzungumza kwa sauti moja. Siyo pekee nchi za magharibi zinazobidi kuwa na msimamo mmoja, bali pia China na Urusi. Maoni yangu ni kwamba nchi hizi mbili pia zingependelea hivyo," alisema Wester Welle.
Korea kaskazini imetoa vitisho dhidi ya Korea Kusini, Japan na Marekani na inaonekana kujiandaa kufanya majaribio kadhaa ya makombora ambayo wadadisi wanasema huenda ikayafanya kwa wakati mmoja. Waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza, William Hague, alisema nchi iko njia panda hivi sasa, na inaweza kuishia kuwa taifa lililosambaratika na kutengwa, iwapo itashindwa kushiriki mazungumzo.
Tisho la mfululizo wa majabirio ya makombora
Jeshi la Korea Kusini limenukuliwa leo likisema kuwa Korea Kaskazini inaweza kufanya majaribio hayo ya makombora muda wowote, na kwamba mitambo ya kuvurumishia makombora hayo imekwishawekwa katika pwani ya mashariki ya nchi hiyo. Shirika la habari la Yonhap la mjini Seoul limesema kuwa mitambo karibu mitano imeonekana katika mkoa wa mashariki wa Hamkyung Kusini.
Shirika hilo likimnukuu afisa wa serikali ya Korea Kusini ambaye halikumtaja jina, limesema kuwa zipo dalili za wazi kuwa Korea Kaskazini inaweza kuvurumisha makombora aina ya Musudan, Scud na Nodong kwa wakati mmoja. Makombora ya Scud yana uwezo wa kwenda umbali wa kilomita kati ya 300 na 500, na Nodong yanaweza kwenda kati ya kilomita 1,300 hadi 1,500.
Mawaziri wa mambo ya kigeni wa mataifa yaliyoendelea zaidi kiviwanda G8 wakiwa katika mkutano wao mjini Londo Uingeraza Alhamisi 11.04.2013. Mawaziri wa mambo ya kigeni wa mataifa yaliyoendelea zaidi kiviwanda G8 wakiwa katika mkutano wao mjini Londo Uingeraza Alhamisi 11.04.2013.
Wakati wasiwasi ukizidi kutanda katika rasi ya Korea, katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami NATO, Anders Fogh Rasmussen, amewasili Korea Kusini kwa ajili ya mazungumzo, katika ziara ya kwanza kabisa ya kiongozi huyo wa jumuiya hiyo ya kijeshi.
Korea Kusini pia imeisihi Korea Kaskazini kufungua tena eneo la viwanda la Kaesong lililofungwa tangu siku ya Jumanne. Eneo hilo linaendeshwa kwa pamoja kati ya Korea mbili, na waziri wa muungano wa Kusini, Ryoo Kihl, ameitaka kaskzini irudi katika meza ya mazungumzo. Lakini afisa kutoka wizara hiyo alisema baadaye kuwa taarifa hiyo ya waziri Kihl Jae haikuwa pendekezo rasmi la kuanzisha tena mazungumzo.
Mwandishi: Iddi Ismail Ssessanga/dpae,
Mhariri: Jospehat Charo

DW

Wednesday, 10 April 2013

Uhuru aapishwa, ICC kunani?

Kenya's President elect Uhuru Kenyatta waves to guests as he arrives for his official swearing-in ceremony at Kasarani Stadium in the capital Nairobi, April 9, 2013. REUTERS-Thomas Mukoya (KENYA - Tags: SOCIETY POLITICS ELECTIONS PROFILE)Hatimaye Uhuru Kenyata ameapishwa leo kuwa raisi wa nne wa Kenya. Kuna mambo mengi ya kujifunza kutoka kwa rais huyu kijana lakini kubwa na la kihistoria ni ule msukumo wake wa kugombea urais japo ana kesi katika mahakama ya ICC. Si jambo rahisi na binafsi naweza kumuona kuwa ni mtu jasiri na mfuasi wa UKWELI yaani alitaka aone wakenya wakiamua kumkubali au kumkataa na si wale vibaraka waitwao ICC. Uhuru anaungana na Obama kuwa vijana walithubutu kufanya kitu kisichowezekana na KIMEWEZEKANA. Wote Uhuru na Ruto wameudhihirishia ulimwengu uongo na uchonganishi wa ICC kwamba wakati yenyewe inawaona ni wahalifu nyumbani wameonekana mashujaa na watu wanaohitajika kuwaongoza.
Binafsi nimekuwa na wasiwasi mkubwa juu ya the Hegue ikiwa kweli ni mahakama ya kweli na ya usawa kwa watu wote, nahisi ipo kwa ajili ya waafrika na zaidi kuwachonganisha ili kuendeleza ukoloni mamboleo. Inawezekanaje Uhuru na Ruto wakutwe na kesi lakini Odinga aliyeamuru watu na zaidi vijana waingie mtaani kupinga matokeo? si mtaani ndiko ukageuka uwanja wa mapigano?
Aaah nashikwa na kigugumizi na hivyo acha nimalizie habari kuapishwa, jambo lililonigusa kwa Uhuru ni ule msimamo na kujiamini na zaidi kusimama yeye kama yeye, ndio marais waliokosekana Afrika watu wanaoweza kuonyesha msimamo na kutoa maamuzi mazito ya kuleta mageuzi katika nchi zao. Afrika sasa inahitaji viongozi ambao hawatakuwa tayari kutishwa na vijibwa vya kizungu ambavyo kwa ajili ya kudoea maliasili zetu vinaleta uchonganishi kila kukicha. Binafsi sipingi kushtakia kwa viongozi waahalifu bali nataka nione wakishtakiwa Afrika, nataka kuona ICC ya kiafrika kama ile ya Arusha ya Mauaji ya kimbari. Mbona Mahakama ya Arusha hatujasikia ikishutumiwa na imefanya kazi zake kwa amani pasipo mgogoro wowote? Waafrika tuhukumiane wenyewe hata sisi tuna roho kama za wazungu rangi siwape shida. Sasa nafikiri ICC itabidi wafikiri upya. Uhuru kaapishwa ICC kunani? lazima wapate kigugumizi
Pia sitakuwa nimetenda vyema kwa kutomgusa Odinga yule rafiki yangu wa mwaka 2007, nasema rafiki yangu maana nilimpigia chapu katika uchaguzi ule hasa katika hadithi zetu vijiweni. Lakini Odinga huyu ambaye kwa kushindwa kwake watu elfu walikufa baadaye akapewa cheo kipya cha Waziri Mkuu badala ya kutekeleza ahadi akashughulika na cheo chake tu, na hapo akajipandishia mshahara wananchi wakibaki kuhaha tu na umaskini. Leo Odinga pasipo aibu anarudia kusema ameibiwa kura, mimi si mkenya lakini naelewa fikra za wakenya hasa linapokuja suala la utawala na ukabila. odinga kachakachuliwa kula na kutotimiza Ahadi kwake na roho ya ukabila iliyotawala kenya nas si vinginevyo. Jambo la ajabu kabisa ni vile Odinga asivyokomaa kisiasa kwa kuamua kukimbilia Afrika Kusini wakati mwenzake akiapishwa, hakika kaonyesha kutokuwa Mzalendo na zaidi kuwa kwake muhimu ni cheo na si utumishi.
Nampa Hongera Uhuru na Ruto na zaidi wapate changamoto ya kuwathibitishia wakenya na ulimwengu kuwa wanaweza kuleta maguzi kinyume na matariajio ya The Hegue.

Tuesday, 9 April 2013

Uhuru Kenyata aapishwa kuwa rais wa nne wa Kenya

Viongozi kutoka mataifa kadhaa ya Afrika wamewasili jijini Nairobi kuungana na Wakenya kwenye sherehe za kuapishwa kwa rais mpya wa Kenya, Uhuru Kenyatta, kwenye uwanja wa mpira uliojaa maelfu ya wafuasi wake.
Kenyatta mwenye umri wa miaka 51 ni mtoto wa rais wa kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta. Ushindi wake wa asilimia 50.07 katika uchaguzi wa tarehe 4 Machi ulihalalishwa na Mahakama ya Juu baada ya pingamizi lililowekwa na Waziri Mkuu anayemaliza muda wake, Raila Odinga, kutupiliwa mbali na mahakama hiyo.
Kenyatta anayekuwa rais wa nne wa taifa hilo la Afrika ya Mashariki tangu lilipopata uhuru wake kutoka Uingereza mwaka 1963, anakuwa rais wa pili barani Afrika kuwa madarakani hali anakabiliwa na mashitaka kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kwa tuhuma za kusaidia kuchochea ghasia za kikabila zilizoukumba uchaguzi wa urais wa Kenya wa mwaka 2007. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mwezi Julai, ambapo Kenyatta na naibu wake, William Ruto, wanakabiliwa na mashitaka ya aina moja.
Hata hivyo, uchaguzi wa mara hii ulikuwa wa amani na kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, Wakenya wengi wanatarajia kwamba Uhuru atatimiza ahadi yake ya kuwa kiongozi wa watu wote na hatakuwa rais wa kabila lake tu, jambo ambalo limekuwa kawaida kwa wanasiasa wa huko.
Utata unaoyakumba mataifa ya Magharibi
Kenya's President Uhuru Kenyatta (C) displays the special Rais Uhuru Kenyatta akikabidhiwa upanga wa mamlaka na rais wa zamani Mwai Kibaki Rais Uhuru Kenyatta akikabidhiwa upanga wa mamlaka na rais wa zamani Mwai Kibaki
Kwa mataifa ya Magharibi, ambao ni wafadhili wakubwa wa nchi hiyo yenye uchumi mkubwa zaidi kwenye eneo la la mashariki mwa Afrika, Kenya ni mshirika muhimu katika mapambano dhidi ya makundi ya kidini yenye siasa kali kwenye eneo hilo.
Lakini sasa mataifa hayo yanakabiliwa na uchaguzi wa ama kuendelea kuimarisha mahusiano au kujitenga na kiongozi ambaye anakabiliwa na mashitaka kwenye mahakama ya ICC mjini The Hague.
Marekani na mataifa makubwa ya Ulaya yalisema yangelituma mabalozi wao kwenye sherehe za kuapishwa kwa Kenyatta, kiwango cha uwakilishi ambacho wanasema bado kinakwenda sambamba na msimamo wao wa kuwa na mahusiano ya lazima tu na watuhumiwa hao.
Mtaalamu wa masuala ya Kenya katika Chuo Kikuu cha Warwick, Daniel Branch, ameiambia Reuters kuwa mataifa ya Magharibi yamejikuta kwenye hali ngumu sana, lakini huenda kila nchi ikatafuta njia yake yenyewe na mahusiano na Kenya.
China huenda ikapata fursa mpya
Wanajeshi wa Kenya wakati wa kuapishwa Uhuru Kenyatta. Wanajeshi wa Kenya wakati wa kuapishwa Uhuru Kenyatta.
Ikiwa mataifa ya Magharibi yatagawika kuhusu mahusiano yake na Kenya chini ya Uhuru Kenyatta, hali hiyo itafungua njia zaidi kwa China na mataifa mengine makubwa ya Asia ambayo yamekuwa yakijizolea ushawishi wa kisiasa na kibiashara barani Afrika kwa siku za hivi karibuni.
Wakati kwenye sherehe hizo, viongozi wakuu wa Afrika watajikuta wamewekwa pamoja na mabalozi tu wa nchi za Magharibi, Kenya na India - ambazo zote mbili hazijasaini Mkataba wa Rome ulioanzisha ICC - zimetuma maafisa wao wa ngazi za juu.
Hata hivyo, mabalozi wa Kimagharibi wataepuka matusi mengine, baada ya maafisa wa Kenya kusema kuwa Rais Omar Hassan al-Bashir wa Sudan asingelihudhuria sherehe hiyo.
Mwandishi: Mohammed Khelef/Reuters/AP
Mhariri: Josephat Charo

DW.DE

Serikali yarudisha viboko shuleni

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo 


Posted  Jumatatu,Aprili8  2013  saa 21:1 PM
Kwa ufupi
Kadhalika alisema Serikali imepiga marufuku matumizi ya simu za mikononi kwa sababu baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakizitumia vibaya jambo ambalo linawarudisha nyuma kimasomo. 

Mpoki Bukuku, MWananchi
Serikali imesema itarudisha adhabu ya viboko kwa wanafunzi shuleni ili kujenga nidhamu na kujituma.Akizungumza Dar es Salaam jana wakati akizindua tovuti ya www.shledirect.co.tz inayowezesha wanafunzi kujisomea kwa njia ya mtandao, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo ilisema kuondolewa kwa adhabu ya viboko shuleni kumewafanya wanafunzi wengi kukosa nidhamu na wakati mwingine kujifanyia mambo kienyeji.

“Wasipotandikwa mambo hayaendi, nilipokuwa mwalimu mkuu nilikuwa nawatandika kweli ndiyo maana shule yangu ilikuwa ikiongoza Mkoa wa Mbeya hivihivi hawaendi...” alisema huku akishangiliwa na wageni waalikwa.

Alisema watoto wa siku hizi wamekuwa wakitumia vibaya teknolojia ambayo ingeweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa katika masomo yao... “Tovuti kama hiyo ingewasaidia kwa masomo, lakini wao wanakimbilia kwenye facebook na mambo mengine yasiyofaa.”

Aliyalaumu mashirika yasiyo ya kiserikali na haki za binadamu ambayo yamekuwa yakipigania kuondolewa kwa adhabu hiyo shuleni na kusababisha kushuka kwa nidhamu kwa kiasi kikubwa.

Kadhalika alisema Serikali imepiga marufuku matumizi ya simu za mikononi kwa sababu baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakizitumia vibaya jambo ambalo linawarudisha nyuma kimasomo.
“Simu tunazipiga marufuku, mwalimu akimkuta mwanafunzi na simu amnyang’anye ndizo zinatuharibia taifa letu.”

Aliwapongeza wabunifu wa mtandao huo akisema ni wazalendo kwani wamekuwa msaada katika jitihada za Serikali kukuza elimu nchini.

“Watu wanapiga kelele Mulugo na Kawambwa wajiuzulu, hata tukijiuzulu haitasaidia, bali kila Mtanzania atoe mchango wake katika elimu ili kuweza kuiendeleza.”
Mwanzilishi wa tovuti hiyo, Faraja Nyalandu alisema itakuwa na manufaa kwa wanafunzi wa Tanzania kwani masomo yanayotolewa yanaandaliwa na walimu wazoefu wenye shahada hivyo wanafunzi watakapoitumia watapata manufaa makubwa.

Maoni ya wadau
Akizungumzia hatua hiyo ya Serikali, Waziri Kivuli wa Elimu Mafunzo ya Ufundi, Suzan Lyimo aliitaka iache kuangalia mambo madogo ambayo yanachangia kwa kiasi kidogo tu kudorora kwa elimu na kuacha mambo makubwa.

“Kuna mambo makubwa zaidi yaliyotufikisha hapa tulipo, hii ni sawa na kushughulika na matawi na kuacha mizizi. Lazima tuangalie suala hili kwa upana zaidi, kuna ripoti nyingi na nzito hazijafanyiwa kazi mpaka sasa badala yake Serikali inaibuka na kuanza kutangaza vitu vidogo kama hivyo, wafanyie kazi kwanza ripoti ambazo zilitumia pesa nyingi za walipakodi kwani nyingi zina mapendekezo mazuri.”

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mpwapwa, Rukonge Mwero alisema uzuri wa adhabu ya viboko ni kwamba haipotezi muda”

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Helen Kijo Bisimba alisema adhabu ya viboko haina maana katika kipindi hiki akisema wanafunzi wanapaswa kupewa adhabu ambazo zinawafundisha kama zile za kufanya usafi na kazi mbalimbali.

“Viboko havifundishi zaidi ya kumpatia mwanafunzi maumivu na kusababisha aichukie shule. Waelimishwe kwa kuelekezwa lakini wakiendelea kukiuka, wapewe adhabu za kufanya kazi mbalimbali.

Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba alisema walimu hawapati faida yoyote kuwachapa au kutowachapa viboko wanafunzi.“Hawa viongozi kila kukicha wanazungumza mambo yasiyo na maana, badala ya kuzungumzia masilahi ya walimu wanazungumza kuhusu viboko, hatuelewi wakiamka kesho watasema nini,” alisema Mukoba.
Chanzo; Mwananchi.co.tz

Monday, 8 April 2013

Wakristo wa Kikopti, Idadi ya waliofariki Misri yaongezeka


 8 Aprili, 2013 - Saa 11:23 GMT
 

Ni juzi tu nilipochapisha makala ya kiingereza kutoka mtandao mmoja yaliyohusu nchi kumi hatari kwa wakristo duniani yenye kichwa Top 10 Most Dangerous Countries for Christians,japo Misri haimo katika nchi kumi hataari kwa wakristo lakini dhahiri kuwa ni miongoni mwa nchi wakristo wanapata tabu, wananyanyaswa na hata kuuawa kwa sababu tu ya kuwa wakristo. Nchini Misri kumetokea mapambano baina ya wakristo wa madhehebu ya kikopti ambao ndo kanisa kubwa nchini Misri la Ki-othodox, chanzo chabari kinaendelea kueleza kuwa;

Watu wawili wameripotiwa kufariki katika makabiliano nje ya kanisa la Kikopti nchini Misri.
Duiru zinasema kuwa hali ya utulivu ilirejea katika eneo la Abbassiya ambako polisi walikuwa kwa wingi kudhibiti hali ya usalam. Eneo hilo linapakana na kanisa ambako makabiliano yalitokea.
Waandamanaji kadhaa wa ambao ni waumini wa kanisa hilo, walikusanyika katika eneo hilo mapema asubuhi ya leo
Makabiliano makali yalitokea nje ya kanisa hilo kufuatia mazishi ya wakristo wanne wa kikopti waliouawa katika ghasia za kidini siku ya Alhamisi.
Waombolezaji waliokuwa wanatoka katika kanisa hilo walikabiliana na wenyeji wa eneo hilo nje ya kanisa.
Polisi walifyatua gesi ya kutoa machozi kujaribi kuwatawanya waandamanaji. Zaidi ya watu 80 walijeruhiwa kwa mujibu wa shirika la kitaifa la habari.
Wizara ya afya ilisema kuwa mtu mmoja aliuawa katika ghasia hizo.
Waombolezaji awali walikuwa wakiimba nyimbo za kupinga serikali ya rais Mohammed Morsi.
Walioshuhudia vurugu hizo waliambia wanahabri kuwa ghasia zilianza baada ya umati wa watu kuvamia kikundi cha waombolezaji walipokuwa wanaondoka kanisani kwa kuwarushia mawe na mabomu ya petroli. Wakati huo pilisi walikuwa wachache sana katika eneo hilo.
Wakristo nao walijibu mashambulizi dhidi yao kwa kuwarushia mawe watu hao hadi polisi walipowasili katika eneo hilo na kujaribu kusitisha vurugu kwa kuwarushia watu gesi ya kutoa machozi
Duru zilisema kuwa barabara zilizoko karibu na eneo hilo zilikuwa na ghasia kati ya wakristo na watu wasiojulikana
Aidha moto uilianzishwa katika jengo lililokuwa karibu na kanisa hilo lakini moto huo ukazimwa kwa wakati.
Pia inaarifiwa kuwa Rais Morsi alilaani ghasia hizo kupitia kwa njia ya simu kwa papa Tawadros wa pili ambaye ndiye kiongozi kwa kanisa la kikopti.
''Shambulizi lolote dhidi ya kanisa hilo ni kama shambulizi dhidi yangu,'' alisema Papa Towadros ambaye pia aliwataka watu kuwa watulivu.
Kwa msaada wa BBC swahili