Maana ya Pasaka na Maombi yake.
Mpendwa watu wengi sasa
wanatamka pasaka lakini ajabu ni kwamba wanaitamka kwa desturi tu, wengine hata
ukiwahoji pasaka maana yake nini hawaelewi chochote. Hakika laiti wangelijua
maana ya pasaka wangeliomba mambo makubwa kabisa kwani ndo majira ambayo
mageuzi makubwa yanafanyika kwa mwanadamu.
Maana
ya Pasaka
Pasaka haikuanza baada ya
kuzaliwa Kristo au baada ya mateso ya Kristo bali wakati wana wa Israeli wa
lipokuwa Misri.
Kutoka 12:11 ...nanyi mtamla kwa
haraka; ni pasaka ya Bwana.
Bwana alipokuwa anataka
kuangamiza wazaliwa wa kwanza wa wana na wanyama wa wamisri akatafuta namna ya
kuwaokoa wana wa Israeli kutoka maangamizi hayo na ndipo anawaamuru wachinje
mnyama asiye na ila, damu yake wapake katika milango na wamle pasaka. Na
wakakumbushwa wafanye hivyo kama ukumbusho vizazi na vizazi.
Kwanini
Mateso ya Bwana Yesu Krito wa Nazareth yaitwe Pasaka?
Kwanza mateso yalitukia
majira ya Pasaka ile sikukuu ya mikate isiyotiwa Chachu (Pasaka ya ukumbusho wa
Bwana alivyowakoa kule Misri zidi ya maangamizi ya mzaliwa wa kwanza) Luka 22
:1-2 ikakaribia sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, iitwayo sikukuu ya pasaka.
Na wakuu wa makuhani na waandishi
walikuwa wakitafuta njia ya kumwua, maana walikuwa wakiwaogopa watu.
Kwa hiyo Mafarisayo
walipanga kumuua majira ya pasaka japo waliogopa kuiharibu pasaka kwa sababu
kuu moja kwamba kama wangemuua majira mengine nje ya pasaka basi wangesababisha
kuwepo pasaka mbili yaani ile ya mikate isiyotiwa chachu na ya mateso na kuuawa
kwa Bwana Yesu. Nasema hivi kwa sababu Pasaka ya kwanza ilikuwa taswira ya
pasaka ya pili pasaka halisi ya ukombozi wa wanadamu wote.
Je
kuna uhusiano wa Pasaka hizi mbili?
Ndio kwa sababu pasaka ya
kwanza ilihitajika ili kuwaokoa wana wa Israel na pasaka ya mateso ya Kristo
kwa ajili ya kuwaokoa wanadamu wote.
Mathayo 1:21 Naye atazaa mwana nawe
utamwita jina lake Yesu, yeye ndiye
atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.
Pasaka ya kwanza ilimhitaji mwanakondoo asiye
na ila yaaani asiye na kosa wala jeraha na ya pili inamhitaji mtu asiye na ila,
uovu wala jeraha katika maisha yake ndio Yesu Kristo wa Nazareti. Kwamba hakuwa
na uovu haikuthibitishwa na wanafunzi wake( maana wangemtetea) bali
alithibitisha Pilato mwenyewe.
Mathayo 27:24 …mimi sina hatia katika
damu ya mtu huyu mwenye haki… pia Luka 23: 22 … huyu ametenda uovu gani?....
Kwa hiyo Pasaka ni
sikukuu ya ukombozi wa wanadamu si kuwaokoa tu kutoka dhambi bali kuwakomboa
kutoka maangamizi ya Yule muovu Ibilisi pamoja na mateso yake maana Bwana Yesu
aliteswa ili wanadamu wasiteseke akawa mtu wa huzuni wanadamu wawe na furaha na
amani tele. Isaya 53 inafafanua vizuri kabisa mateso aliyopata Bwana yesu kwa
ajili ya mwanadamu.
Maombi
wakati wa Pasaka
Yamfaa mtu aombe kuokoka
yaani amkiri Bwana Yesu Kristo wa Nazareti kuwa Bwana na mwokozi wa Maisha
yake. Amtwike mizigo yake.
Mathayo 11:28. Njooni kwangu, ninyi
nyote msumbukao na kuelemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Baada ya kuokoka na kwa mwamini WAKATI WA PASAKA NDO MAJIRA MUHIMU SANA KWA MKRISTO
NA YAMPASA AOMBE MAMBO MUHIMU ZAIDI NA
SI TU YALE ANAYOAMINI BWANA ATATENDA BALI YALE ANAYOHITAJI. Aombe mambo
ambayo hayakuwezekana kwa miaka mingi lakini sasa autazame msalaba mahali
ambapo Bwana Yesu alitamka alikamilisha wokovu. Naandika hivi kwa kumaanisha kwa sababu kuna
waamini wanaomba lile waloamimini Bwana anaweza kutenda kwa hiyo kama imani
yake ni ndogo basi ataomba vitu vidogo vidogo tu, lakini aombe mambo
anayohitaji yatokee, na Bwana atayafanya kwani aliwekwa msalabani kwa ajili ya
mwanadamu siteseke tena.
Wako katika safari,
Mwl Peter Kapagi