Furaha ya Kanisa
Furaha ni hali isiyoshikika
inayomtokea mtu pale anapopata jambo nzuri, habari njema au anapokuwa na amani
moyoni, naweza kusema furaha si amani bali amani huweza kuoneshwa kwa furaha. Furaha
inaweza kuwa ya muda mfupi(temporary) au kipindi kirefu (permanent).
Isaya
35:10 … na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao..
Ukweli ni kwamba kuna kundi kubwa la
watu ambalo halina furaha katika jamii ya kikristo, kuna wapendwa bado hawana
furaha kanisani.
Hivyo ni lazima kufanyike jitihada ya
pamoja kati ya mwamini/mshirika na kiongozi ili kuleta furaha kanisani au
katika jumuiya ya kikristo.
Kwa mfano mwaka 2011 radio DW
ilitangaza kwamba kanisa la RC nchini ujerumani linapoteza umaarufu kwa 70%,
hapa suala si dhehebu bali ni ukristo. Unafikiri kwa nini ? Sababu kubwa ya
kupoteza umaarufu ni kwamba waumini hawana furaha tena kanisani na hivyo
wanaamua kutafuta furaha mahali pengine. Kama waumini wanaona kanisa(si RC bali
kanisa lolote la kikristo) limeingia udhalimu kazi yake kukusanya sadaka na
mbegu tu, kama kanisa limeingiza ndoa za jinsia moja na unajisi kwa watoto,
kanisa linaona injili ya utajirisho na miujiza ndio imani sahihi, litakuwa limewafanya waumini kuliona
kama mahali pa wahalifu na wanyang’anyi wanaamua kulikimbia maana haliwapi furaha
wanayoitaka.
Mathayo 21:13 akawaambia imeandikwa , Nyumba ya yangu haitaitwa nyumba ya sala; bali
nivyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.
Bwana Yesu mwenyewe anaona uharibifu
ndani ya kanisa na hapendi kuona hali hiyo, hapendi kuona uhalifu wa ndani ya
kanisa kama ifanyikavyo leo. Mfano mwishoni
mwa mwaka 2011 nikakutana na mwanamke ambaye Bwana ake alidhulumiwa mamimilioni
ya pesa na mtumishi mmoja huko Arusha, kwa kweli ukimuona yule mwanamke
amechoka kabisa na maisha na nilipoongea naye akaoneka ni mkristo mwenye
kulifahamu neno barabara na ndipo nikavutiwa kuzungumza naye na kunieleza jinsi
walivyofanyiwa unyang’nyi na mtumishi na hata kupelekea bwana ake kufukuzwa
kazi benki. Ipo mifano mingi ya nyang’anyi ufanyikao kanisani hata kupoteza furaha
kwa waumini. Hata hivyo nikutie moyo kwamba bado kuna kanisa la kweli na furaha
ya kweli tena iliyo thabiti.
Je furaha ya mkristo ni katika
kutajirika, kuoa, kuoa na kuolewa au mafanikio yoyote?
La hasha Matendo 8:5-8 inajibu …6na makutano kwa nia moja
wakasikiliza maneno yale yaliyosemwa na Filipo walipoyasikia na kuziona
ishara…..8ikawa furaha kubwa
katika mji ule.
Ni dhahiri kuwa furaha ya mkristo
inaanzia kusikiliza maneno na hatimae kuziona ishara za maneno hayo. Furahaa ya
mkristo ni matokeo ya kulisikiza na kulisoma neno safi
la kristo na utendaji wa neno hilo
na si propaganda nyingine.
Tena Yohana
16:24 inasema …ombeni nanyi mtapata,
furaha yenu iwe timilifu.
Kumbe kupata kwa Bwana kunaikamilisha
furaha na si kwamba ndiyo furaha yenyewe.
Kwa mfano injili ya utajirisho haina
nguvu Ulaya na Arabuni maana wana utajiri mkubwa lakini bado wapungukiwa furaha
ya kweli bado wana hofu na mambo mbalimbali. Kama
ni mafanikio ya Nyanja zote wameyapata katika elimu, uchumi, sayansi na hata
siasa lakini furaha bado ni tatizo la msingi kwao. Wao wanahitaji Yesu halisi
ahubiriwe maana wengine ni wasomi bado wana hofu juu ya hatima ya maisha yao. Ikiwa kuna jehanam
au la na nini hatima yao
baada ya kifo.
Hebu tupitie
mambo matano yanayoleta furaha kwa mkristo
1.
Kumkaribia
Mungu
Ni jambo la pekee kwa mkristo maana
wakristo wengi wapo mbali na Mungu na imekuwa chanzo cha kutoiona furaha ya
ukristo
Zaburi 73:28..
Mfalme Daudi anasema nami kumkaribia
Mungu ni kwema kwangu…
Jambo jema kabisa kwa mkristo ni
kumkaribia Mungu kwa maneno, matendo na kila jambo.
2.
Kwenda
madhabahuni.
Huku ni kupiga hatua kuzungumza na
Mungu kwa sala na maombi, kusifu, kuabudu na hata shukrani.
Zaburi 43:3-4
…4 Hivyo nitakwenda
madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu….
Kumbe ni Mungu(Yesu Kristo) ndiye
furaha ya mkristo na MUngu huyu napatikana madhabahuni, na hapa madhabahu ni
sehemu yoyote ifaayo kumsifu, kumuabudu na kumuomba Mungualiye hai.
3.
Kumwona Yesu
Baada ya kumkaribia na kwenda
madhabahuni jambo linalofuata ni kumwona Yesu.
Yohana 20:20
inasema …basi wanafunzi wakafurahi walipomwona bwana.
Hapa ni zaidi ya kuona kwa macho ya
nyama bali kushiriki na katika matendo mbalimbali, huduma na maombi na zaidi
kuomba na kujibiwa. Wakristo wengi wamepata furaha baada ya kuona matokeo ya
maombi na imani katika maisha yao.
Kujibiwa maombi si imani yenyewe tu bali kunachochea imani na furaha ya
mkristo.
4.
Kumkaribisha
Bwana.
Kumkaribisha bwana ni kule kumfanya
awe sehemu ya maisha yako, awe wa kwanza kwa kila jambo, kila mahali na wakati
wote kutembea na bwana Yesu.
Luka 19:5-6
habari ya zakayo ..6 akafanya haraka,
akashuka, akamkaribisha kwa furaha.
Ni hakika kuna wakristo wengi
hawajamkaribisha bwana Yesu katika maisha yao,
nyumba, kazi na biashara zao na hivyo siku zote zimekuwa za taabu na mashaka.
Fanya haraka kama Zakayo ambaye aliposikia
Bwana Yesu anataka kuingia nyumbani kwake na kushinda humo akamkaribisha kwa
furaha.
5.
Kujifunza kwa
Bwana Yesu
Mkristo ni lazima akubali kujifunza
kwa Bwana wakati wote na hatua kwa hatua ili aone furaha kamili ya ukristo.
Yeremia 15:16
inanena maneno yako yalionekana, nami
nikayala: na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu maana nimeitwa kwa jina
lako, Ee Bwana wa majeshi.
Mnenaji hapa si kwamba tu aliona
maneno bali aliyala, akayatendea kazi na hata kujifunza kwa maneno hayo na
ndipo akapata furaha na shangwe na hata kutambua kuwa ameitwa kwa jina
lake(Bwana) sawa kabisa na wa wakristo wa leo ambao kwa sababu wamegoma
kujifunza neno basi hata hawatambui kwamba wameitwa kwa jina la Bwana (Kristo).
Ninaweza
kumaliza maneno machache kwamba kuna kanisa la Kweli, ukristo wa kweli na ambao
umejaa furaha kwelikweli. Karibu katika furaha ya milele ya wokovu.
Filipi
4:4 inaisistiza furahini siku zote.
Katika safari
Kapagi