Tuesday, 28 May 2013

Mbunge amlipua Blandina Nyoni

*Ni Katibu Mkuu wa zamani Wizara ya Afya
*Adaiwa kuchakachua mashine ya kusafisha figo
*Aelezwa aliiitoa Muhimbili kuipeleka Aga Khan

MBUNGE mmoja amemlipua aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni akidai alishiriki kuhamisha mashine ya kusafisha figo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Akiuliza swali bungeni jana, Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya (CUF) alidai Katibu Mkuu huyo kwa kushirikiana na daktari katika hospitali hiyo walihamisha mashine hiyo na kuipeleka katika Hospitali binafsi ya Aga Khan.“

Lini Serikali itairudisha mashine ya kusafisha figo iliyohamishwa kutoka Muhimbili na aliyekuwa Katibu Mkuu kwa kushirikiana na daktari wa hospitali hiyo na kuipeleka katika Hospitali ya ‘private?’, alihoji.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid alisema asingeweza kujibu swali hilo kwa kuwa hakuwa na taarifa kamili.

No comments:

Post a Comment