Tuesday, 28 May 2013

Anguko la elimu; cha kufanya kujinasua (3)

Share bookmark Print Email Rating
 
Na John Malata  (email the author)

Posted  Jumanne,Mei28  2013  saa 14:57 PM
Kwa ufupi
  • Serikali kwa nyakati tofauti imejaribu kuweka msisitizo wa ufundishaji kwa kutumia lugha ya Kiingereza bila mafanikio. Mfano mzuri ni mradi ujulikanao kwa jina la English Language Teaching Support Project 1996-2000 (ELTSP).

Leo nahitimisha mfululizo wa makala zangu kuhusu sababu za anguko la elimu nchini na namna tunavyoweza kunusuru mustakbali wa elimu yetu. Endelea…
Serikali kwa nyakati tofauti imejaribu kuweka msisitizo wa ufundishaji kwa kutumia lugha ya Kiingereza bila mafanikio. Mfano mzuri ni mradi ujulikanao kwa jina la English Language Teaching Support Project 1996-2000 (ELTSP).
Mradi huu ni miongoni mwa mikakati iliyoshindwa kutuletea manufaa katika ufundishaji wa lugha ya Kiingereza shuleni kama lugha ya kufundishia. Ifike wakati tukubali sasa kuwa tunahitaji kufanya uamuzi mgumu na wenye gharama kwa manufaa ya taifa letu.
Idara ya Ukaguzi ndicho chombo chenye mamlaka ya kusimamia ubora wa elimu itolewayo nchini. Hata hivyo, idara hii imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi, jambo linalosababisha ishindwe kutimiza wajibu wake ipasavyo.
Kuna haja ya kudurusu upya majukumu ya idara hii ili pamoja na mambo mengine, miongozo na mipango katika ukaguzi wa shule itoe kipaumbele katika matokeo ya wanafunzi.
Ripoti ya uchunguzi uliofanywa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mwaka 2008, inaeleza wazi kuwa ukaguzi shuleni umeshindwa kusimamia utoaji wa elimu bora.
Kuna haja ya Serikali kuangalia uwezekano wa kuifanya idara ya ukaguzi wa shule kuwa taasisi inayojitegemea kama zilivyo taasisi nyingine za elimu. Aidha, muundo na utendaji wake viangaliwe upya ili kuipa nguvu idara hii.
Ninaamini idara hii ikiwezeshwa kwa kupewa hadhi ya kuwa taasisi au hata mamlaka kamili, upo uwezekano mkubwa kuwa sasa shule zetu zitakuwa na nafasi kubwa ya kukaguliwa mara kwa mara. Kwa hakika tunahitaji kuwa na shule zinazokaguliwa.
Wajibu wa wadau wa elimu
Katika muktadha wa mjadala huu, wadau wa elimu ni pamoja na waajiri, wazazi, walimu na wanafunzi. Kila mmoja kati ya hawa ana wajibu wa kujenga mustakabali wa maendeleo ya Taifa, kwa kuhakikisha anatimiza wajibu wake kikamilifu.
Mwajiri kwa mfano, anapaswa kuhakikisha kuwa mwalimu anajengewa uwezo na mazingira bora yatakayo mwezesha kutekeleza wajibu wake akiwa na moyo mkunjufu.
Aidha, wazazi na jamii kwa jumla ni kiungo muhimu sana katika kuinua kiwango cha elimu hapa nchini. Hii inatokana na ukweli kuwa mwanafunzi ni zao la jamii husika na ndiko anakotumia muda mwingi katika ukuaji wake nje ya shule.
1 | 2 Next Page»
http://www.mwananchi.co.tz/uchambuzi/Anguko-la-elimu--cha-kufanya-kujinasua--3-/-/1597604/1865152/-/lw5nhsz/-/index.html

No comments:

Post a Comment