Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe
*Asema anajipanga kwenda kortini
*Amwandikia Dk. Slaa kudai kauli ya Chadema
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, ameibuka na kutoa kauli na tamko dhidi ya tuhuma mpya dhidi yake zilizosambazwa katika mitandao ya intaneti katika siku za hivi karibuni.
Zitto, ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Kigoma Mjini, amefanya hivyo akitumia majukwaa mawili tofauti. Mwanasiasa huyo kijana ambaye amejipambanua kuwa mtetezi wa misingi ya utaifa, raslimali za nchi, uchumi na masuala ya utawala bora ndani na nje ya chama chake, alifanya hivyo kwa mara ya kwanza juzi jioni, wakati alipokuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika uwanja wa Kolimba wilayani Kariua, Mkoa wa Tabora.
http://rai.co.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=721:zitto-nimechoka-kuzushiwa-na-kuchafuliwa-&catid=1:siasa&Itemid=2
No comments:
Post a Comment