Saturday, 1 June 2013

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YAPAA

Baraza la mitihani limetangaza matokeo ya kidato cha sita mwaka 2013. Matokeo hayo ni mazuri kulinganisha na matokeo ya kidato cha nne yalileta mtikisiko mkubwa. Kwa mujibu wa baraza la mitihani

Asilimia 93 ya waliofanya mtihani huo wa kidato cha 6 wamefaulu.

Shule ya kwanza iliyoongoza ni Marian Girls ya mkoani Pwani na ya pili ni Mzumbe ya Morogoro.

Mwanafunzi wa 1 wa kiume kwa sayansi ni Erasmi Inyase kutoka Ilboru, na kwa wasichana ni Lucylight wa Marian girls.

Upande wa masomo ya Biashara mwanafunzi wa 1 ametoka shule ya Tusiime anaitwa Erick Robert.

Wanafunzi 89 matokeo yao yamezuiliwa kwa sababu mbalimbali.

Wanafunzi watakaothibitika kuwa walikuwa na matatizo ya kiafya, watapewa nafasi ya kurudia mtihani.

Bofya hapa chini ujionee matokeo

http://www.necta.go.tz/matangazo2013/tangazo-usajili-ACSEE2014.pdf 


No comments:

Post a Comment