Asilimia 93 ya waliofanya mtihani huo wa kidato cha 6 wamefaulu.
Shule ya kwanza iliyoongoza ni Marian Girls ya mkoani Pwani na ya pili ni Mzumbe ya Morogoro.
Mwanafunzi wa 1 wa kiume kwa sayansi ni Erasmi Inyase kutoka Ilboru, na kwa wasichana ni Lucylight wa Marian girls.
Upande wa masomo ya Biashara mwanafunzi wa 1 ametoka shule ya Tusiime anaitwa Erick Robert.
Wanafunzi 89 matokeo yao yamezuiliwa kwa sababu mbalimbali.
Wanafunzi watakaothibitika kuwa walikuwa na matatizo ya kiafya, watapewa nafasi ya kurudia mtihani.
No comments:
Post a Comment