Vuta nikuvute imetokea katika bunge la senate nchini Ufaransa, ambapo
mwisho wa siku iliamuliwa kupitisha kwa muswada wa sheria ya kuruhusu
ndoa za jinsia moja nchini humo, licha ya upinzani mkali kutoka kwa
wabunge wenye msimamo mkali, ikiwamo viongozi wa dini.
Uamuzi huu ambao umepitishwa Ijumaa taehe 12 Aprili 2013 na Ufaransa ,
taifa lenye asili ya katoliki, umekuja baada ya muda mrefu wa
majadiliano, kama ambavyo Rais François Hollande alivyoahidi kwenye
uchaguzi mkuu mnamo Aprili mwaka 2012, sera ambayo ilimfanya avune kura
nyingi za wafuasi wa ndoa hizo.
Waziri wa Haki, Bi Christian Taubira. © Gouvernement |
Mtetezi mkubwa wa muswada huo, waziri wa haki nchini huko, Bi Christian
Taubira, amesemema kuwa muswada huo unakuja kutokana na umuhimu wake,
hasahasa kwa watoto wanaoishi na wazazi wa jinsia moja, ili wapate haki
zao sawa na watoto wa wazazi wa kawaida. na kwa mujibu wa muswada huu,
basi wenye ndoa za jinsia moja, watarushusiwa kuasili watoto kwa ajili
ya kuwalea.
Tumefanya hivi kwa sababu kuna watoto hawali chakula cha afya, wanakula
pipi kwa wingi, na kadha wa kadha, hao pia tunawalinda - wanahitaji
hilo. Christian aliwaambia maseneta mara baada ya kupitisha muswada huo,
ambao utapitiwa tena February 2014 kwa ajili ya marekebisho.
Kwa upande wake, seneta wa chama cha UMP, Jean-Pierre Raffarin, amesema
kuwa bado wataendeleza mpambano kwa kuwa bunge bado lipo, na kilichopo
ni kwamba watakuwa wakiongea na wananchi wataobadili mawazo ili
kuhakikisha muswada huu unaondolewa na kurejea katika hali ya mwanzo,
yaani mume na mke na si vinginevyo.
Mpaka sasa ufaransa imegawanyika kuhusiana na ndoa za jinsia moja,
ambapo mnamo January mwaka huu, takriban watu 340,000 waliandamana
kupinga ndoa za aina hii, wakisisitiza Baba na Mama kwa familia. Ambapo
wiki mbili baadae, kundi la watu takriban 125,000 walijitokeza mtaani
kuunga mkono ndoa za namna hiyo.
Nchi ambazo zimeridhia ndoa za jinsia moja mpaka hivi sasa. © CBC |
Ulaya ni bara ambalo nchi zake kadhaa zimeruhusu ndoa za namna hii,
ambapo kwa watu ambao nchi zao haziruhusu, wamekuwa wakikimbilia huko
ili kuonana na kuishi kwa sheria za huko. mfano mmojawapo ni mashoga
wawili Waganda, ambao walikimbia nchi yao na kuelekea Sweden ili kuonana
kutokana na nchi yao kukataza vitendo vya ushoga na usagaji.
Wadau wa Gospel Kitaa walio nchini Sweden, walifanikiwa kupata tukio
hilo kama lilivyofanyika mwezi wa kwanza kwa kamera, na hatimaye mdau
Nahshon Kamugisha kuzirusha kwa GK.
Jimmy na Lawrence wakiwa na mashoga wenzao wakati wa sherehe ya 'kuonana'.
Gospelkitaa.com
No comments:
Post a Comment