Gari la zimamoto likiwasili eneo la tukio
Leo
asubuhi muda wa saa 3:30 kumetokea mlipuko mkubwa kwenye Glosary ya Kipingu
eneo Mtaa wa Sae karibu kabisa na kituo cha Sae. Mlipuko huo wa moto umetokana
na jiko la gesi lililokuwa likiwashwa ili kupasha supu na ndipo likalipuka na
kuanza kuwaka moto mkali. Moto umezua balaa kubwa kwani kutokana na ukosefu wa
vifaa vya tahadhari vya zima moto na
elimu ya majanga watu wakaanza kuzima kwa maji na mchaka lakini ikawa ni kama
kuuchochea zaidi. Baada ya kushindika kuzima moto uliokuwa ukiwaka kwenye
mtungu wa gesi na kuendelea kusambaa kwenye vyombo vingine ndipo kijana mmoja
jasiri maarufu kama KP akajitosa na kuuburuzia nje mtungi uliokuwa ukiwaka moto
mkali. Hapo ndipo akawa ameokoa nyumba hiyo yenye maduka manne isiwake moto.
Zimamoto
wawahi kuokoa, kinyume na desturi ya zimamoto ya kuchelewa mara wanapoitwa kwenye
majanga ya moto kwani waliwasiri mara moja baada ya kupigiwa simu. Zimamoto
wamewapongeza wananchi kwa kuweza kuokoka jingo kuwaka moto kwa kuutoa nje
mtungi unaowaka moto. Askari wa zimamoto wakauzima moto uliokuwa unaendelea
kuwaka kwenye mtungi wa Gesi.
Wasisitiza
kutoa taarifa mapema kila mara janga linapotokea kuwakumbusha wananchi kuw ana
namba za simu ya kiganjani mbali ya ile ya mezani ili kutoa taaarifa kwa haraka
zaidi. Ikumbukwe kuwa mara nyingi zima moto wamekuwa wakilalamikia baadhi ya
watu wasio waaminifu wamekuwa waktoa taarifa za uongo kupitia simu ya bure ya
111.
Ushauri
wa bure kwa wote wenye majiko ya gesi ni bora wakanunua kifaa cha kuzima moto
(Fire Extinguisher) ili watumie kuzima moto mara moto unapolipuka.
Namba za kiganjani za Zimamoto jiji la Mbeya ni
0755 651923
Tazama
Picha kutoka eneo la tukio



Hata boda boda walikuwepo kujionea wenyewe
Moto umezimwa tayari kwa safari.
Picha zote na KII
No comments:
Post a Comment