Wednesday, 7 September 2016

Kimungu mke (Goddess) achoka sauti

Hakika Mungu mkuu atabaki kuwa Mungu kwani mwimbaji Beyonce yule aliyejiita kimungu mke( goddess) kule marekani na kuanzisha kitabu chake alichofananisha na biblia kiitwacho beyble achoka sauti na kushauriwa na madaktari kupumzisha sauti. Je ni Mungu gani anayeshauriwa na wanadamu juu ya Afya yake akakubali?Habari kamili na bbcswahili;-

 

Beyonce ashauriwa kupumzisha sauti yake


Beyonce ashauriwa kupumzisha sauti yakeImage copyrightV
Image captionBeyonce ashauriwa kupumzisha sauti yake
Mwanamuziki Beyonce ameahirisha tamasha lake la New Jersey kwa jina World Tour baada ya madaktari kumshauri kupumzisha sauti yake.
Msanii huyo ambaye alisheherekea siku yake ya 35 ya kuzaliwa siku ya Jumapili alitoa taarifa akisema tamasha hilo halitafanyika mnamo tarehe 7 mwezi Octoba.
Hatahivyo ataendelea na tamasha nyengine katika miji ya Los Angeles,Houston,New Orleans na Atlanta kama ilivyopangwa.
Ziara hiyo ambayo inalenga kuuza albamu yake mpya Lemonade,ilianza mjini Miami mnamo tarehe 27 mwezi Aprili.
Ilitarajiwa kukamilika Nashvile mnamo tarehe 2 mwezi Octoba,lakini sasa inaonekana kwamba New Jersey itaanda tamasha lake la mwisho

No comments:

Post a Comment