Sunday, 2 June 2013

Mauaji ya kutisha yaibuka msituni

 
Na Burhani Yakub,Horohoro  (email the author)

Posted  Juni1  2013  saa 20:14 PM
Kwa ufupi
  • Kwa kipindi kirefu msitu huo umekuwa eneo la kufanyia mauaji kwa watu wasio na hatia, ambapo genge la wahalifu kutoka Kenya limedaiwa kuhusika na mauaji hayo.

Matukio ya mauaji ndani ya msitu wa Mwakijembe yameendelea kutishia usalama wa Watanzania, wanaoishi jirani na eneo la Horohoro linalopakana na nchi jirani ya Kenya.
Kwa kipindi kirefu msitu huo umekuwa eneo la kufanyia mauaji kwa watu wasio na hatia, ambapo genge la wahalifu kutoka Kenya limedaiwa kuhusika na mauaji hayo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini msitu huo wenye rasilimali nyingi unaodaiwa kutumiwa na genge hilo kwa vitendo haramu vya ujangili, uchimbaji madini na uvunaji wa miti, ikiwemo uchomaji mkaa.
Taarifa za uchunguzi ambazo zilithibitishwa na viongozi wa Serikali ya Vijiji vinavyopakana na msitu huo, zilibaini genge hilo limekuwa likiua kila linayemhisi atafichua uhalifu wao.
Inatoka UK 1
Uchapisha wa Hati za Kusafiria (Kwa mujibu wa taarifa za karibuni, kwa mwaka huu pekee, watu wawili tayari wameshauawa kwa kuchinjwa ndani ya msitu huo.
Matukio hayo ya mauaji yalithibitishwa na Diwani wa Kata ya Mwakijembe, Ramadhani Mtiota ambaye alisema kwa sasa katika eneo hilo hali imekuwa ya hofu kutokana na kuongezeka kwa makundi ya vijana wa rika la Morani wa Kimasai, wanaojiandaa kuvishambulia vijiji vya Kenya.
Diwani huyo alisema ametoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza kuhusu hali hiyo pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Andrew Ngoda.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alisema wanafahamu kuhusu mauaji yanayotokea kwenye msitu huo.
Alisema taarifa za mauaji ya hivi karibuni ya watu wawili, Ali Mohamed na msichana wa kabila la Kimasai Kendie Minja yanafahamika na yanafanyiwa uchunguzi na polisi.
”Ninachofahamu ni mauaji yaliyofanyika ya msichana Kendie kuchinjwa na kufichwa msituni upande wa Kenya, lakini upelelezi unafanywa na Jeshi la Polisi la wenzetu wa Kenya kwa hivyo sijui zaidi ya hivyo,” alisema Massawe.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza alisema anaandaa mkutano wa ujirani mwema utakaowahusisha viongozi wa Serikali Mkoa wa Tanga na Jimbo la Mombasa, Kenya.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Mauaji-ya-kutisha-yaibuka-msituni/-/1597296/1869732/-/11tcb6hz/-/index.html 

No comments:

Post a Comment