m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Tuesday, 21 January 2014

Computer Basic Skills-Handout Coming Soon

Dear customer and supporter of KII be prepared to get Computer handout which will save students and the society from Computer Ignorance and join the computer expert family. 
Handout will be available for best price compared to contents.

 

Sunday, 19 January 2014

Serikali yawabeba waliofeli kidato cha pili


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa. Picha na Maktaba 
Na Fidelis Butahe, Mwananchi

Posted  Jumapili,Januari19  2014  saa 2:0 AM
Kwa ufupi
  • Licha ya matokeo hayo kutotangazwa hadi sasa, imebainika kuwa waliofaulu mtihani huo uliofanywa Oktoba 7 hadi 21 mwaka jana ni asilimia 62 tu, asilimia 31 wakitakiwa kukariri (kurudia) kidato cha pili mwaka huu, huku asilimia saba wakishindwa mtihani huo kwa mara ya pili.
Dar es Salaam. Wakati Watanzania wakisubiri matokeo ya kidato cha pili mwaka 2013, imebaini kuwa Serikali imetoa agizo kwamba wanafunzi wote waliofeli mtihani huo kuendelea na masomo ya kidato cha tatu, huku wakisoma mafunzo ya kurudia mtihani wa kidato cha pili.
Licha ya matokeo hayo kutotangazwa hadi sasa, imebainika kuwa waliofaulu mtihani huo uliofanywa Oktoba 7 hadi 21 mwaka jana ni asilimia 62 tu, asilimia 31 wakitakiwa kukariri (kurudia) kidato cha pili mwaka huu, huku asilimia saba wakishindwa mtihani huo kwa mara ya pili.
Jumla ya wanafunzi 531,457 walitajwa na Wizara ya Elimu mwaka jana kuwa watafanya mtihani huo.
Uamuzi huo wa Serikali ni tofauti na ule uliotolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa Novemba 4, mwaka 2012, kwamba kuanzia wakati huo mtihani wa kidato cha pili utakuwa ni wa mchujo na kwamba atakayefeli atatimuliwa.
Dk Kawambwa alisema matokeo ya mtihani wa kidato cha pili yatatumika kama kigezo cha kuchuja na kukariri kidato cha pili kwa watahiniwa watakaoshindwa kufikia wastani wa ufaulu wa alama 30.
Alisema mtahiniwa ataruhusiwa kukariri kidato cha pili mara moja tu na endapo mtahiniwa atashindwa mtihani kwa mara ya pili kwa mwaka utakaofuatia, itabidi aendelee na elimu ya sekondari nje ya mfumo rasmi.
Gazeti hili limeiona barua iliyoandikwa Januari 16 mwaka huu na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kusainiwa na Katibu Mkuu wake, Profesa Sifuni Mchome, kwenda kwa wadau wa elimu nchini, wakiwamo maofisa elimu wa mikoa na Chama cha Wamiliki wa Vyuo na Shule Binafsi (Tamongsco).
Katika barua hiyo, wizara hiyo imewataka wadau hao kuhakikisha kuwa wanafunzi watakaofeli mtihani huo, wanaendelea na masomo ya kidato cha tatu.
“Matokeo ya kidato cha pili yamepokewa na kufanyiwa uchambuzi ili kupata taswira ya taifa. Taarifa ya matokeo hayo imebaini kuwa watahiniwa waliofanya mtihani na kufaulu ni sawa na asilimia 62 tu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo na kuongeza;
“Hali hii inaonyesha kuwa asilimia 31 ya wanafunzi watatakiwa kukariri kidato cha pili, 2014. Wale walioshindwa kwa mara ya pili ambao ni asilimia saba wanatakiwa kuendelea na masomo nje ya mfumo rasmi.”
Barua hiyo inaeleza kuwa wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 na kuendelea waendelee na masomo ya kidato cha tatu mwaka 2014, wakati awali Serikali ilitoa tamko kuwa watakaoshindwa kufikisha alama 30 watatimuliwa.
“Wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 hadi 39 wapewe mafunzo rekebishi ‘Remedial class’ wakiwa kidato cha tatu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo
SOMA ZAIDI http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/2151230/-/utnth5z/-/index.html.

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI LATAJWA

ASHA MIGIRO,NKAMIA NA SAADA WAULA,NCHIMBI,KAGASHEKI NJE, MAGUFULI APETA

Katibu kiongozi wa Serikali ya Tanzania oOmbeni Sefue kwa niaba ya rais Kikwete ametangaa baraza jipya la mawaziri.
                                         
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UHAMISHO NA UTEUZI WA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
______________________________________________
            Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-
1.0              OFISI YA RAIS
Hakuna mabadiliko.
2.0              OFISI YA MAKAMU WA RAIS
2.1  Waziri wa Nchi (Muungano) - Hakuna mabadiliko
2.2   Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb)
            Waziri wa Nchi (Mazingira).
2.3    Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb)
                                                Naibu Waziri                            
3.0              OFISI YA WAZIRI MKUU
Hakuna mabadiliko
            4.0       WIZARA
           
                        4.1  WIZARA YA FEDHA
4.1.1        Mhe. Saada Mkuya SALUM (Mb)
            Waziri wa Fedha
                                    Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA (Mb)           
                        Naibu Waziri wa Fedha
4.1.2        Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Fedha
                       
4.2              WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
Hakuna mabadiliko
           
4.3       WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
4.3.1    Mhe. Dkt. Asha-Rose Mtengeti MIGIRO (Mb)
                        Waziri wa Katiba na Sheria
4.3.2        Naibu Waziri - Hakuna mabadiliko
4.4      WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
Hakuna mabadiliko
            4.5       WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA
           
4.5.1    Waziri - Hakuna mabadiliko
4.5.2    Mhe. Janet Zebedayo MBENE (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
            4.6       WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA
            Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb)
                                                Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
           
4.7        WIZARA YA UJENZI
Hakuna mabadiliko
4.8       WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
4.8.1    Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb)
                        Waziri wa Mambo ya Ndani
                       
4.8.2        Naibu Waziri - Hakuna Mabadiliko
           

4.9       WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
4.9.1        Mhe. Dkt. Seif Seleman RASHIDI (Mb)
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
4.9.2        Mhe. Dkt. Kebwe Stephen KEBWE (Mb)
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
4.10     WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
4.10.1  Waziri:  Hakuna mabadiliko
4.10.2  Mhe. Jenista Joakim MHAGAMA (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
14.11   WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
14.11.1  Waziri: Hakuna mabadiliko
14. 11.2 Mhe. Dkt. Pindi Hazara CHANA (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
14.12  WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
14.12.1 Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Dismas KAMANI (Mb)
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
14.12.2 Mhe. Kaika Saning’o TELELE (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
14.13      WIZARA YA KAZI NA AJIRA
Hakuna mabadiliko
                                                              
14.14      WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Hakuna mabadiliko
14.15   WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
14.15.1  Waziri - Hakuna mabadiliko
14.15.2  Mhe. George Boniface Taguluvala SIMBACHAWENE (Mb)
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
14.16   WIZARA YA MAJI
14.16.1  Waziri - Hakuna mabadiliko
14.16.2  Mhe. Amos Gabriel MAKALLA (Mb)
Naibu Waziri wa Maji
14.17  WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA
14.17.1  Waziri - Hakuna mabadiliko
            14.17.2   Mhe. Godfrey Weston ZAMBI (Mb)
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
            4.18     WIZARA YA UCHUKUZI
            Hakuna mabadiliko
4.19     WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
4.19.1  Waziri -  Hakuna mabadiliko
4.19.2  Mhe. Juma Selemani NKAMIA (Mb)
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
4.20     WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
4.20.1 Mhe. Lazaro Samuel NYALANDU (Mb)
Waziri wa Maliasili na Utalii
                        4.20.2 Mhe. Mahmoud Hassan MGIMWA (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
4.21     WIZARA YA NISHATI NA MADINI
4.21.1    Waziri - Hakuna mabadiliko
4.21.2    Naibu Waziri (Madini) - Hakuna mabadiliko
4.21.3  Mhe. Charles Muhangwa KITWANGA (Mb)
Naibu Waziri (Nishati)
     

Balozi Ombeni Y. Sefue
KATIBU MKUU KIONGOZI
Ikulu
DAR ES SALAAM
19 Januari, 2014

Wednesday, 15 January 2014

Kuhamia teknolojia ya digitali Kenya bado changamoto

Raia wa Kenya bado wana hofu na mchanganyiko wa kuhama kutoka matumizi ya teknolojia ya utangazaji ya analojia na kuhamia teknolojia ya digitali.
Kuingia teknolojia ya digitali Kenya ni kitendawili. Kuingia teknolojia ya digitali Kenya ni kitendawili.
Ifikapo mwaka 2015, muda ambao umepangwa na Umoja wa Mawasiliano ya Kimataifa Duniani kutawsitisha utangazaji wa kutumia analojia. Kuhamia teknolojia ya digitali kunalenga kuwapa huduma bora watumiaji, ingawa kwa nchi za Afrika Mashariki zoezi hilo limekuwa gumu na hivyo serikali husika kulazimika kuahirisha mara kadhaa.
Huku kesi ya kupinga uamuzi wa serikali wa kuvikatalia leseni ya matumizi ya digitali vyombo vya habari nchini Kenya haijamalizika, kesi ambayo ilifunguliwa na wamiliki wa vyombo vikuu vya habari nchini humo bado kuna masuala yaliyoibuka juu ya kuhamia tekenolojia ya digitali, ikiwa ni pamoja na malalamiko juu ya wachina kuchukua fursa kubwa ya kutawala vyombo vya habari, hasa kuelekea teknolojia ya digitali.
Lakini kwa Javas Bigambo, mchambuzi wa masuala ya siasa nchini Kenya, aliyebobea katika masuala ya vyombo vya habari , utawala na sera ameliambia shirika la habari la IPS kuwa halikuwa suala la bahati mbaya kwa serikali kuipa leseni ya digitali kampuni ya Kichina na kuwanyima wazawa, huku miundo mbinu ya kuanza kutumia digitali ikiwa bado haijatengenezwa.
Anasema mchambuzi huyo na hapa namnukuu "ikiwa bado tuna majonzi ya uamuzi wa Bunge kupitisha muswada tata kuhusu vyombo vya habari nchini humo wenye lengo la kudhibiti tasnia ya uandishi habari nchini bado serikali inaendelea kuyumbisha uhuru wa vyombo vya habari kwa hali ya juu", mwisho wa kumnukuu.
Walalamikia kampuni ya Kichina kupewa leseni
Kwa leseni hiyo, kampuni ya Kichina inayomilikiwa na mtandao wa Pan-Afrika –PANG na SIGNET-shirika la kimataifa la utangazaji , watakuwa na jukumu la kuwaunganisha watumiaji wa televisheni na televisheni hizo , ambapo pande zote zitahusika katika kurusha matangazo kwa makubaliano maalum na wamiliki wa vyombo vya habari, ambapo televisheni za ndani zitawajibika katika kutayarisha matangazo pekee.
Kwa upande wake Alex Gakuru ambaye ni mwenyekiti wa chama cha watumiaji wa mawasiliano ya teknolojia nchini Kenya na mjumbe wa kamati ya kusimamia uhamiaji kutoka analojia kwenda digitali amesema kumekuwa na hali ya wasi wasi kuwa kampuni hiyo ya kichina itadhibiti vyombo vya ndani vya habari na hivyo kudharau katiba na sheria za nchi, ingawa anasema hofu hizo zinapata ushawishi mbaya.
Amesema mawasiliano kwa umma ni suala la kisheria kwa mamlaka za mawasiliano na vyombo vya habari na kwamba kampuni hiyo ya kichina itakuwa na mamlaka ya kusambaza ving'amuzi vyenye kuonyesha chaneli zote cha televisheni za ndani na si kupendelea chaneli fulani,ikiwa itafanya hivyo itajiweka katika hatari ya kufungiwa leseni yake.
Grace Githaiga mdau wa mtandao wa mawasiliano ya teknolojia Kenya anasema kuwa ingawa kamisheni ya mawasiliano Kenya na mamlaka inayosimamia mawasiliao wamedai kuwa vyombo vya habari vya ndani hawakupata zabuni ya leseni ya digitali, hata hivyo vyombo hivyo vina kila sababu ya kulalamikia usimamizi wa kampuni ya kigeni wa digitali kwa kuwa wanaona wamevunjiwa haki yao.
Kampuni ya Kichina yalalamikiwa kupewa leseni. Kampuni ya Kichina yalalamikiwa kupewa leseni.
Hata hivyo amasema wasi wasi juu ya kampuni hiyo ya Kichina kupewa leseni limetiwa chumvi kutokana na ukweli kwamba makamupni ya simu yanatumia tekenolojia ya kichina huku mamilioni ya watu wakiendelea kutumia vifaa vya umeme vinavyotengezwa au kununuliwa kutoka China.
Takwimu zilizotolewa na serikali zinaonyesha kuwa, shirika la habari la utangazaji la China, Xinhua husambazwa habari kwa watu milioni 17 wanaotumia simu nchini Kenya.
Lengo la teknolojia ya Digitali inayoendelea kuhimizwa kutumiwa katika ukanda wa Afrika Mashariki ni kutaka kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano kote duniani.
Teknolojia ya digitali kuongeza ubora
Miongoni mwa faida za kutumia teknolojia ya digitali ni kuongezeka kwa ubora wa matangazo, ongezeko la chaneli za televisheni litakalotokana na matumizi bora ya masafa, kuwepo kwa masafa ya ziada yatakayopatikana baada ya kuzimwa kwa mitambo ya analojia inayotumia masafa mengi.
Faida nyingine zilizobainishwa ni kuongezeka kwa watoa huduma wa mawasiliamo ya simu, matangazo ya televisheni kupatikana kwa vifaa vingi zaidi vya mawasilino kama vile simu za mkononi na kompyuta kupitia mtandao wa internet.
Mwandishi: Flora Nzema/IPS
Mhariri: Mohamed Khelef
Chanzo: dw.de

Tuesday, 14 January 2014

Je, unajua Kila unapofungua website au blog unaacha fingerprints? Ina madhara hivyo jifunnze kujihami


Huwezi kutumia internet kwa matumizi ya kawaida bila kutumia Web browser. Hii ni interface inayotuwezesha kufungua blog, websites na progams nyingine za Internet.  Kuna aina sita za Web browser:
·         Internet ExplorerMicrosoft Inc
·         Google ChromeGoogle Inc
·         Mozilla FirefoxMozilla Corporation
·         Safari Apple
·         Opera Opera Software
Ili kurahisisha matumizi yake, Internet browser zote zinahifadhi kumbukumbu ya web sites zote ulizotembelea. Zinafanya hivyo kwa sababu kadhaa. Sababu ya kwanza ni kwamba kwa kuhifadhi kumbukumbu hizo huwa inamrahisishia mtumiaji anapotaka kutembelea website hizo hizo hapo baadaye. Hii inapelekea internet experience kuwa faster kwa sababu baadhi ya information imehifadhiwa kwenye komputa yako na sio kwenye server maili kadhaa kutoka ulipo.
Pamoja na kwamba web browser inaokoa muda wako, kuna mswala kadhaa yanayoweza kuleta madhara kwenye komputa yako.
Kawanza kumbuka kwa kuwa wewe umerahisishiwa  unapotembelea web sites ulizozea, hali hii inamwezesha mtu mwingine kuziona kumbukumbu hizo zinazohifadhiwa na webbrowser. Baadhi ya web site ulizotembelea inawezekana information zilizohifadhiwa ni muhimu au za siri (kama mambo ya kiakazi). Mtu mwingine mwenye nia mbaya anaweza kujua kila website uliyotembelea na nini ulichofanya kwenye website hiyo. Kuepusha watu kuona information zako usiache fingerprint unapotumia internet. Unafanya hivyo kwa kufuta (delete) kumbukumbu zote ambazo web browser imezihifadhi.
Unaweza kufuta kumbukumbu hizo kirahisi kabisa kama ifuatavyo:
·         Google Chrome: Select “Tools” and choose “Clear Browsing History”
·         Safari: Click on the “History” tab in your menu bar. Select “Clear History” located at the bottom of the list.
·         Internet Explorer: Select the “Safety” drop down menu at the top right of the screen. Choose “Delete Browsing History.”
·         Mozilla Firefox: Click on the “Tools” menu, then select “Clear Recent History.”
Pia kuna njia nyingine unayoweza kutumia web browser bila kuacha fingerprint. Web browser zote zina feature inayokuwezesha kufanya hivyo: Kwa watumiaji wa Internet explore hii inaitwa “In Private”; kwa Mozilla Firefox na Safari hii inaitwa “Private Browsing”; na kwa Google Chrome hii inaitwa “incognito”. Njia hii ni nzuri zaidi hasa kwa wale wanaotumia komputa za public kwa mfano café, shuleni, vyuoni, kazini, n.k.
Kila la kheri
CHANZO: http://it4dev.blogspot.com

Monday, 13 January 2014

Shujaa Ariel Sharon azikwa kijeshi Israel

  

Shujaa Ariel Sharon enzi za uhai wake akiwa waziri Mkuu alipohudhuria kikao cha ulinzi Pentagon, Washington
 
Watu wakitoa heshima mbele ya mwili wa Ariel Sharon na Mwili wa Sharon ukiwa umebebwa na majenerali
Military service at Latrun, 13 Jan

Wageni waliofika kwa ibada maalum ya Sharon walimsifu kama kiongozi aliyepigania waisraeli
Aliekuwa waziri mkuu wa Isreal , Ariel Sharon amezikwa kwa heshima za kijeshi katika shamba la familia yake kusini mwa Israel. Kundi la majenerali ndio walibeba jeneza lake.
Ulinzi uliimarishwa wakati waombolezaji walipokuwa wanafika katika shamba hilo ambalo liko karibu na mpaka wa eneo Gaza la waPalestina linalokaliwa na Israel.
Rais Shimon Peres amemtaja Bw Sharon kama mwanajeshi shupavu aliyejua kushinda vita.
Awali ibada maalum ilifanyika nje ya majengo ya bunge la Israel.
Bwana Sharon atakumbukwa kwa kuwa miongoni mwa waanzilishi wa taifa la Israel lakini pia alikuwa mwanajeshi na mwanasiasa jasiri aliyechukiwa na wapalestina wengi.
Waliohutubia umati,wamemtaja Sharon kama mtu aliyejitolea kuhakikisha kuna usalama kwa watu wake.
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu alisema kuwa Sharon alikuwa mmoja wa makamanda wakuu wa wayahudi na ambaye atakumbukwa zaidi ya wote.
Licha ya sifa hizo Bwana Sharon anachukiwa sana na waarabu hasa wapalestina kwa dhuluma alizowatendea chini ya utawala wake.
Kiongozi huyo aliaga dunia siku ya Jumamaosi akiwa na umri wa miaka 85 baada ya kuwa hali mahututi kwa takriban miaka minane.
Atazikwa baadaye leo katika shamba la familia yake jangwani Negev.
Maelfu ya waombolezaji walitoa heshima zao za mwisho kwa Sharon siku ya Jumapili wakati ambapo mwili wake ulikuwa umelazwa nje ya majengo ya bunge mjini Jerusalem.

Sunday, 12 January 2014

JAMANI MANABII NA MITUME KWELI HAYA NDIO MAOMBI KULA MANYASI? MWE

Mdada akila majani ambayo huduma hiyo wanasema ni chakula kutoka mbinguni mwe!
Kuna mengi ambayo yamekuwa yakizungumzwa kuhusu huduma za watumishi mbalimbali, moja wapo ni hii huduma iitwayo Rabboni Centre ministries iliyopo Pretoria nchini Afrika ya kusini, huduma hii iliyochini ya mwanzilishi wake mwalimu ,mchungaji na nabii Daniel Lesego ilianza mwaka 2002. Ni huduma ambayo kwa watu wasioabudu hapo huitilia mashaka kutokana na mwenendo wake.

Kwasasa wapo kwenye mfungo ambao watu hufika kanisani na hatimaye wanaishia kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo akisema kwamba Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote huku ikidaiwa kuwa manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni.

Inaelezwa kwamba mara baada ya maombi waumini wengi huanza kutapika jambo ambalo kanisani hapo huashiria kwamba mtu amejazwa Roho Mtakatifu.

Lakini kama haitoshi nabii Lesego hufanya maombi huku amewakanyaga watu. Huduma hii imekuwa gumzo nchini humo na nchi jirani kwa jinsi mambo yao yanavyokwenda.

Mnasemaje watumishi kuhusu jambo hili? mwe kula manyasi kweli? mma!

Hapa nabii huyo akikanyaga watu kama njia ya mafundisho yake.
Haa!! angalia jamani, sasa ng'ombe watakula nini jamani???
Mungu tufunulie macho ya rohoni kuyajua mambo haya kama ni wewe au sisi kha!
Hajamaliza bado.
Baada ya manyasi ni mwendo wa kutapika sasa







Picha ya juu na hii huyu ndio nabii Lesego Daniel mwenye maono na huduma hii.
Watu wanajaa kwenye huduma.
Mwe! kama uti wa mgongo shida hii dawa 
Maombi yanaendelea.
Waumini wakikaribisha mwaka mpya.
Nabii anafundisha huku skuna yake imekanyaga mtu, sijui 

Tembelea TOVUTI YAO  Picha zote kwa hisani ya ukurasa wao wa Facebook.
Chanzo : gospelkitaa.blogspot.com