m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Saturday, 22 March 2014

UNABII WA TANZANIA KATIKA BIBLIA



Bwana Yesu asifiwe…
Mpendwa leo ninayo furaha kubwa sana kurejea tena ukurasa wetu na kichwa hapo juu.
JE WAJUA KUWA NCHI YETU TANZANIA IMETAJWA KATIKA BIBLIA TAKATIFU?
ISAYA 18:
 Mst 1. Ole wa nchi ya uvumi wa mabawa, Iliyoko mbali kupita mito ya Kushi;
2  Ipelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari, Na katika vyombo vya manyasi juu ya maji.
Nendeni wajumbe wepesi, kwa watu warefu laini, watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu wakanyagao watu, ambao mito inakata nchi yao.
3  Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni.
4  Maana Bwana ameniambia hivi, Mimi nitatulia, na kuangalia katika makazi yangu, kama wakati wa mwangaza mweupe wa jua kali, mfano wa wingu la umande katika hari ya mavuno.
5  Maana kabla ya mavuno, maua yaangukapo, na maua yakawa zabibu zianzazo kuiva, ndipo atakapoyakata matawi kwa miundu, na kuviondoa vitawi vilivyopanuka na kuvikata.
6  Wote pamoja wataachiwa ndege wakali wa milimani, na hayawani wa nchi; ndege wakali watakaa juu yao wakati wa jua, na hayawani wote wa nchi watakaa juu yao wakati wa baridi.
7  Wakati huo Bwana wa majeshi ataletewa hedaya na watu warefu, laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu, wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao;

Mpendwa nilistaajabu mwaka 2011 nilipokutana na Mwl. Brown Mwakibete pale Kijitonyama, kwa kujiamini sana akanidokeza kwamba Tanzania imetajwa kwenye Biblia, imetabiriwa na nabii Isaya. Nami kwa nilivyokuwa namwamini nikaungana naye kutafakari kifungu hicho mara tu aliponitaka nifungue Biblia yangu.

Ndugu yangu ukitazama mstari wa kwanza wa Isaya 18 utaona unataja nchi ya uvumi iliyoko mbali kupita mito ya kushi. Katika Biblia Kushi ni nchi ya Ethiopia ya leo, ukitazama ramani utabaini kuwa nchi zilizo mbali na mito ya Ethiopia ni nchi za Afrika Mashariki na Somalia kidogo. (ukitokea kaskazini ambako ndio inapatikana Israel) TANZANIA ni mojawapo ya nchi hizo.

Mstari wa 2 unataja kuwa nchi hiyo inapeleka wajumbe wake kwa njia ya habari na katika vyombo vya mnyasi. Hapo utabaini kuwa nchi zinazopakana na bahari na kutumia ngalawa ni Kenya, TANZANIA na Somalia.

Sehemu ya pili inazungumzia watu wepesi lani watishao tangu mwanzo wao hata sasa. Hapa utaona kuna mkanganyiko kidogo kwa watu laini tunaweza tafsiri kuwa watu wapole wasio na makuu lakini wakati huohuo watu hao wanatisha tangu mwanzo. TANZANIA ndio nchi inayoongoza Afrika kwa ukarimu (hospitality) lakini pia ndio nchi pekee Afrika iliyoongoza mapambano dhini ya wakoloni kwa nchi zote za kusini mwa jangwa la Sahara, iliwatisha wakoloni ikiwa ina ujinga, maradhi na umaskini wakati wao wana silaha, elimu, utajiri na afya njema. TANZANIA ndio nchi pekee Afrika iliyopigana na nchi nyingine na kuishinda iliipiga Uganda ikakanyaga watu wao hadi kaskazini ikamng’oa Dikteta Idd Amini na kisha kuweka mtawala wao. Kabla ya Amiri Jeshi Mkuu kuruhusu vita alianza kwa kuwatisha waganda na dunia nzima. TANZANIA inatisha kwani wakati huo pia Malawi walitaka kunyang’anya ziwa Nyasa na Kenya wakaumendea mila Kilimanjaro lakini Nyerere akawatisha wakashindwa. Tanzania. Hakuna aisyeijua TANZANIA katika kusuluhisha migogoro, mfano Mauaji ya Kimbari ya Rwanda, Imedhibiti uasi visiwa vya Comorro, imetatua mgogoro wa Kenya 2007 na hatimaye madagascar

Mstari unaomaliza kwa kutaja kuwa mito inakata nchi yao, Afrika Mashariki ni TANZANIA pekee mbayo mito mikubwa inapita katikati, hebu tazama Mito mikubwa ya Ruaha, Pangani, Malagarasi, Ugalla, Rufiji, Wami  bila kusahau mito ya mipakani ambayo ni pamoja na Kagera, Mara, Ruvuma na Songwe. Bila shaka yeyote nchi inayozungumziwa hapa ni TANZANIA kwani Kenya na Somalia hazina mito mikubwa.

Mst wa 3 unazaungumzia kuinuliwa bendera mlimani na kupiga tarumbeta. Tanzania ndio nchi pekee barani Afrika ambayo ilipandisha bendera yake ju ya mlima Kilimanjaro. Na ikapiga tarumbeta kwani baada tu ya uhuru wa Tanzania ndipo nchi nyingi zikafuatia miaka ya 1962 na 1963 zikiwemo Uganda, Kenya na makoloni mengi ya kifaransa. Yote ni kwa kuwa nchi ya Tanzania ilisimama kidete kwa ajili ya ukombozi wa waafrika.

Mst 7 unazungumzia kwamba watu hao warefu laini watamletea Hedaya Bwana wa majeshi, tena unasisitiza kabisa Taifa la wenye nguvu, wakanyagao watu, amabo mito inakata nchi yao.
Ni nchi gani hiyo zaidi ya TANZANIA?

Huwezi kuombea vema kitu usichokujua, natamani unabii huu ukupe nguvu ya kuiombea nchi yetu TANZANIA.

Mpendwa leo nimedokeza kidogo tu unabii wan chi yetu TANZANIA kama ulivyotolewa na nabii Isaya. Nitafurahi kama utakuwa mwanzo tu wa mjadala juu ya nchi yetu katika ulimwengu war oho, wengine husema Tanzania ndiyo Israeli ya Afrika, je ni kweli? Kuna hoja gani?

Kama una masomo au hoja yoyote juu ya Tanzania yetu katika ulimwengu wa roho usisite kuwasilisha kupitia mawasiliano yafuatayo;
Simu: +255 685 306666, +255 764 734620

MUNGU IBARIKI TANZANIA

Wenu katika safari
Mwl Peter Kajolo Kapagi


Sunday, 9 March 2014

HOW TO ACTIVATE WINDOWS NOT GENUINE

A you getting trouble with Windows not genuine notification and black screen?
Worry out, if you get this problem find application software called Window Activation Technology, turnoff Antivirus the install WAT, follow the instruction with aid of COMPUTER doctor the problem will be solved.

Enjoy wallpapers on your PC
Photo












Black screen after windows not genuine notification
Photo

Installation of WAT

HOW TO RECOGNIZE WINDOWS NOT GENUINE

Before getting trouble with windows not genuine notification and black screen you can recognize if you window is not activated soon after window booting.
Go to Computer icon>right click check properties then read all windows properties



Thursday, 6 March 2014

Tips for Entrepreneurship Opportunities in Tanzania



KAPAGI INFORMATION INSTITUTE-KII
Mbeya, Sae Zambia rd/Ituha st

Mob: 0764734620, 0685 306666
Email: kakakapagi@gmail.com
Blog: kapagiii.blogpspot.com

Department of Training and Seminars
Entrepreneurship Training
Tips for Entrepreneurship Opportunities in Tanzania
Course Instructor: Peter K Kapagi (BAED)
Instructor Assistant: Edgar Kajolo
Venue: Seminar room at KII Head Office

Tanzanian are getting trouble when want establish entrepreneurial business, some have capital they didn’t know where to invest. Here are 17 entrepreneurship opportunities.
1.      Printing industry
Printing industry is growing now days due to the Information development as forces much information to be published like advertisements, posters, calendars, banners, books etc.
Analog machines
Printing cards, Brochures, banners, Posters, flayers, Postcards, Books, Exercise Books, Notebooks, Graph papers, Stickers, Tickets, T-shirts printing
Digital machines

2.      Stationeries
Increase of schools and colleges are good indicator that stationery demands increase for learners and education institutions.
·         Selling and supplying of school materials to both individual and institutions

3.      Full/Combined stationary and secretarial services
stationery
 Selling and supplying of school materials to both individual and institutions
secretarial services
Providing secretarial services to individuals and institutions as well: Typing, Printing, Card designing, Scanning, Binding, Copying etc.

4.      Food processing
Food demands are always high because population is increasing. Food processing should be based on take away foods especially bites:
Bakery

Breads, bun(andazi), Donat, Egg chops, Cakes, Meat ball(kababu)

Colored Baobab nuts (Ubuyu), Baobab Powder,

Crips making

Chama/ Tingatinga

Pop corns

5.      Boutique and Saloons
One of the Tanzanian girls and women daily demands is fashions and beauty, so Boutique and saloon services are best business especially in urban areas.
·         Boutique in general
·         Cosmetics
·         Saloon; hair braiding, waving etc

6.      Horticulture
Cultivation of vegetables, onions, tomatoes etc all are consumed daily in families, cafeteria and hotels.

7.      Education
·         Tuition centers and learning centers for private candidates
·         Private laboratories for science tests because government school s lack laboratories and experiment apparatuses.
·         Establishing Private secondary schools as the community lost hope towards government schools performance.
·         Private nursery schools and English medium primary Schools are marketable as government policy which is on swahili medium primary schools. People especially rich people prefer English medium schools.
·         Vocational training centers
·         Polytechnic colleges: Agriculture, computers etc
Investment capital for education depends on the type of institution, some need small capital like nursery school, Tuition centers.
8.      Entrepreneurship seminars
Providing seminars for entrepreneurship skills, teaching opportunities as well as practical activities on Soap making, food processing etc
Payments for seminars nowadays are minimum of 10000Tshs. So to have at least two seminars per month with at least 100 attendances will make 1,000,000Tshs

9.      Soap making industry
Soap is one of the daily needs, so its market is growing as population increase. It’s simple to make soaps. For example Southern Highlands regions are using soups form Dar es Salaam Industries so if you will try to invest in Soap making and make good supply will be a best deals with satisfactory market.

10. Mobile Phones stores
It’s another growing trade; mobile phones are part of life, so people are travelling long distance to find mobile phone stores. Due to the growing communication network Mobile phones should be sold nearby customers.

11. Computer Stores
As mobile phones also Computer market is growing very fast as IT development. PC users are increasing like workers and university students because much information is computerized. Computer stores should be located out of Dar es Salaam city but upcountry.

12. Full commercial Agriculture
Commercial agriculture is very productive but it needs big capital and tolerance because it takes a long time produce. But its market is high for at every agricultural product

13. Candle making machines
Even if you have a single room you can make it as factory because candle making machines are simple and occupy small area. It’s simple to make candles in Tanzania as we have bee keeping industry and machines mix it with simple skills.
0768250347

14. Chalk making Machines
Chalks are in high demand in schools. Chalk materials are available in Mbeya and chalk making machines can be purchased from India South Africa with price less than 8,000,000/=. Effort needed after establishing chalk factory is strong supply, promotion and advertisement so that because in Mbeya region chalks are purchased from Singida and Dar ES Salaam, also Kenya, China and India.


15. Whiteboard making
Whiteboard making will be new innovation since nowadays are used for universities. But whiteboards demand is for all students, teachers and instructors for all levels of education. To establish it is to take risk on promoting the use of whiteboards and influencing government policy on the use of whiteboards. Whiteboard is healthily than blackboards.

16. Cloth processing
As fashion cloth processing is marketable in Tanzania. Batiki, Tshirt printing, Hanger chiefs, etc

17. Hostel investment.
One of the growing demands is accommodation in Urban. Investing in hostel which will be full accommodated would be a big deal. This investment need big capital at least to build house with ten 10 room as starting point.
Hostels can be in into two categories; students’ hostels and Ordinary hostels.
Hostel Distribution table
Category
Rooms
Capacity
C/month
Cost
Total cost
Students Hostel
10rooms
4students @room
40 students total per month
30000@students per moth
30000 X 40 =1,200,000/=
Ordinary Hostels
10rooms
1person @room
10 people per month
3000Tsh@ person/day
90000/=@personmonth
90000 X 10= 900,000
Total cost which would be taken as gross profit is big compared to gross salary of Tutorial Assistant which is estimated to Tsh, 800,000 and Education Officer II =Tsh.590,000
Success is not a miracle its results of desire, preparation, plan, and hard work
People are waiting for Changes, Changes they are waiting is us
PETER KAJOLO KAPAGI                                                       March 2014
CHIEF EXECUTIVE OFFICER                                                 Mbeya. Tanzania

Friday, 28 February 2014

YODAE: MBEBA MAONO NI LAZIMA AWE MTII NA MWENYE KUFUATA MAELEKEZO

Shalom Mpendwa.
Mwanzo: 37
Ninaendelea kujifunza kutoka kwa Mbeba maono Yusufu. Watu wengi tunamtazama Yusufu kam ambeba maono tu, lakini kumbe hatupaswi kuishia hapo tunatakiwa kuangalia namna alivyoyabeba maono na nguvu iliyomwezesha kubeba maono yake.

Maono ni jambo la kwanza, kubeba ni jambo la pili na nguvu ni jambo la tatu. Unaweza ukawa na maono lakini maono yako yakafa kwa sababu umeshindwa kubeba, wakati mwingine unaweza ukayabeba maono lakini ukashindwa kuendelea nayo kwa. Mpenzi kuinua mzigo ni jambo rahisi lakini kuendelea nao ama kupiga hatua nao ni jambo lingine gumu sana kwani inategemea nguvu ya misuli uliyonayo.

Binafsi naamini hakuna kijana aliyekosa maono ikiwa ana imani thabiti kwani Yoeli 2:28 inatamka wazi kuwa vijana wataona maono. Vijana wengi wanalo jambo la kufanya lakini hawajatambua na waliotambua wameshindwa kubeba. Lazima kuwa mwanagalifu unapokuwa na maono.

Kubeba maono ni kama kubeba YAI, yai si kiumbe chenyewe bali kasha lililobeba kiumbe kumbe kulivunja ni kuvunja kiumbe na kulitunza vizuri ni kutunza kiumbe kijacho. Kwa mfano kufikiri kuanzisha shule ni sawa na yai kwani mawazo yamebeba shule lakini si shule yenyewe.

Unapobeba maono kunakuwa na changamoto nyingi ambazo zinaweza kuharibu au kuua kabisa maono yako.

Kwa leo hebu tujifunze kwa Yusufu nguvu iliyomsaidia kubeba maono. YUSUFU ALIKUWA MTII NA MWENYE KUFUATA MAELEKEZO katika safari yake ya maono. Ndugu unapobeba maono umeanza safari ni kama kuku anapoatamamia yai, kutotoa kwa vifaranga kutategemea namna ambavyo atadhamiria kuatamia mayai yake.

AMUA KUATAMIA MAONO YAKO

Yusufu alikuwa mtii kweli kwani tunamtazama akiwa na umri wa miaka 17 tu tayari ameanz kuota ndozo zinazotoa maelekezo ya maono yake...nini atafanya kwa wakati gani na kwa nani.

Utii unaonekana kwa Yusufu kwanza kila alipoota kamsimulia baba yake na familia yake mst. 2, 5 na 9. Pili Yusufu alipotumwa kwenda kuwaona nduguze bado anaendelea na desturi ya utii kwani inaoneka anaenda mahali asipojua vizuri ndio maana anapofika anauliza wapo wapi ndugu zake na hapo tena utaona namna Yusufu anavyopenda kufuata maelekezo kwani anauliza. Hizi ni tabia za kawaida kwa mtu lakini zina maana sana kwa ajili ya kutunza maono. Mst 15

Utii wa Yusufu ndio uliopelekea kuweza kubeba maono yake, Kwani Ysufu unafiak wakati nduguze wanamkamata wanamvua kanzu bao hatuambiwi kama alileta matata bali alitii, wanamtumbukiza kisimani bado hakuleta matata akatii, wanamuuza bado akatulia akatii, Wamidiani wanamchukua hadi Misri bado anatii na tena wamidiani wanamuuza kwa Potifa bado anatii (kama angeleta matata ingeandikwa).

Kumbe kama umebeba maono ni lazima uwe mtii, unaweza kukumbana na mugumu wakati wa maono lakini yakupasa uchukulia kama changamoto tu, Yusufu aliandaliwa kuwa mtawala lakini tunaona natawaliwa na ndugu zake na hata utumwani jambo ambalo ni kinyume na alivyoona. Yeye anaona kutawala lakini yanayotokea ni kutaliwa na hata kutaka kuuawa. mst 23, 24, 27, 28, 36.

Maisha ya ushindi ni pamoja na kuwa na maono, wengine waimngia dhambini kwa sababu hawana maono, hawajui nafasi yao na wanapoelekea.

Ikiwa umebeba maono kubali kuwa mtii kwa Mungu mwenyewe, viongozi wa Imani na wakati mwingine hata watawala kwani hujua ni nani atakayeweza maono yako, maono yatatekelezeka kutia nani. Yusufu ilikuwa kupitia nduguze na hatimaye Farao

Wednesday, 26 February 2014

DOWNLOADS: Windows Free downloads

A PC running Windows 8.1


Click this link to visit downloads

‘Anayeona posho haimtoshi afungashe virago’


Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba.PICHA|MAKTABA 
Na Daniel Mjema, Mwananchi

Posted  Jumanne,Februari25  2014  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Hoja ya kutaka nyongeza ya posho iliibuliwa na wajumbe wawili ambao pia ni wabunge wa CCM, Richard Ndasa (Sumve) na Suleiman Nchambi (Kishapu).


Dodoma. Wizara ya Fedha imepigilia msumari maombi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ya kutaka waongezewe posho na kusema anayeona ameacha kazi inayomlipa zaidi kwenda bungeni afungashe virago na kuondoka.
Msimamo huo umekuja siku moja tu baada ya gazeti hili kudokeza kuwa madai ya wajumbe wa bunge hilo kutaka waongezewe posho kutoka Sh300,000 za sasa kwa siku, yamegonga mwamba baada ya kamati iliyoteuliwa kuchunguza uhalali wake kusema kiwango hicho kinatosha.
Mwenyekiti wa muda wa bunge hilo, Pandu Kificho alisema jana bila kutaja viwango, kuwa ripoti ya kamati hiyo imewasilishwa kwa Rais Jakaya Kikwete kwa uamuzi.
Madai ya wajumbe kutaka waongezewe posho, yamechafua hali ya hewa ndani na nje ya Bunge, huku baadhi ya wananchi wakipaza sauti zao na kumsihi Rais Kikwete alivunje bunge hilo iwapo wajumbe watashikilia msimamo wa kutaka nyongeza ya posho.
Jana, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema wanaoshiriki kutunga Katiba ni Watanzania na siyo wataalamu washauri waliokodiwa kutoka nje.
Alisema kwa msingi huo, Serikali ilitarajia kuwaona watu hao wakitanguliza uzalendo zaidi badala ya kudai malipo manono.
“Katika kutengeneza Katiba hii, hatujakodi consultants (wataalamu washauri) kutoka Uingereza, Marekani, Kenya, Uganda wala nchi nyingine yoyote… Hawa ni Watanzania na kazi wanayoifanya ni yao,” alisema.
“Wangekuwa wataalamu wa kukodi wangeweza kudai malipo hayo, lakini hapa ni tofauti... wanafanya kazi yao na kila mtu anafanya kazi yake na anapaswa kujivunia kushiriki katika tendo hili la kihistoria kwa kutanguliza uzalendo,” alisema.
Nchemba alisema anazielewa hoja za baadhi ya wajumbe walioibua suala la posho, lakini kwa mtazamo wake, hoja hiyo hata kama ingekuwa na mashiko kiasi gani, imewasilishwa wakati usiokuwa mwafaka. Alisema wapo makandarasi na wazabuni waliotoa huduma kwenye taasisi mbalimbali za umma lakini hawajalipwa.
Alisema kwa kawaida, Februari ni mwezi mbaya kwa kuwa baadhi ya wilaya zina historia ya kukumbwa na uhaba wa chakula hivyo kuhitaji fedha nyingi za Serikali ili kuokoa maisha ya watu katika maeneo hayo.
Pia alisema si wakati mwafaka wa kudai nyongeza hiyo hasa ikizingatiwa kuwa kuna walimu wapya 30,000 nchini kote ambao hawajapangiwa vituo kutokana na kukosekana kwa fedha za kulipa stahiki zao.
Nchemba alisema mbali na walimu hao wapya kutokupangiwa vituo, walimu wengine wanadai malimbikizo ya fedha zao na kwamba hawajalipwa kutokana na ufinyu wa bajeti serikalini.
Soma zaidi http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-Anayeona-posho-haimtoshi-afungashe-virago-/-/1597296/2220374/-/item/1/-/tmerhu/-/index.html

Tuesday, 25 February 2014

DOWNLOADS: Get best Antivirus Microsoft Security Essentials

Download free antivirus
Click this link to Download
Microsoft Security Essentials 

Complete guide to using Windows 8 (roundup)


Microsoft's newest operating system has a whole new interface and loads of new features. Of course, learning a whole new operating system always takes a little time. Here are our tips for getting up to speed quickly and getting the most out of Windows 8.

Preparing for Windows 8

Check compatibility
Is the software and hardware on your PC compatible with Windows 8? It's easy to find out with the Windows 8 Upgrade Assistant.
Read: Check your PC for Windows 8 readiness with upgrade assistant
Get your PC ready
If you're planning to upgrade to Microsoft's latest OS, now might be a good time to begin preparing your PC.
Read: How to prepare your PC for Windows 8
Try it out -- sort of
You've probably heard about the new Metro interface in Windows 8, but how to know if you'll like it? Current Windows users can get a sneak peek into the look and feel of Metro with the free metro7 app.
Read: How to try the Windows 8 Metro interface free
Get Windows 8
Microsoft's biggest desire is to get you using Windows 8, and fast. Here's how to use that $40 upgrade to flip older versions of Windows to Windows 8.
Read: How to upgrade to Windows 8

Starting up and shutting down

Skip the log-in
Users who don't need the security of a lock screen and a log-in screen can bypass both through a few simple steps.
Read: How to bypass the Windows 8 log-in screen
Get the start menu back
Three free utilities can replicate the classic Start button and menu in Windows 8.
Read: How to get the classic Start menu back in Windows 8 RTM
Going back to start
Clean and simple, Windows 8's Desktop mode also lacks any apparent ways to get back to Metro. Here's three tips on how to do just that.
Read: How to return to the Windows 8 Start screen
Use a picture as your password
Tablet and PC users alike can create a picture password in Windows 8 as a visual way of signing in. Here's how.
Read: How to create a picture password in Windows 8
Shut down with a tile
Shutting down or rebooting Windows 8 can be as easy as point, then click, if you want it to be.
Read: How to create a shutdown and reboot tile in Windows 8

The basics

Keyboard shortcuts
Windows 8 has some new keyboard shortcuts that will help you get around Microsoft's latest OS.
Read: 23 new keyboard shortcuts for Windows 8
Set default programs
Windows 8 chooses its default players to run your music and video, but what if you want different programs to open your files? Here's how to change them.
Read: How to change default programs in Windows 8
Task Manager
The most neglected feature of Windows since it landed in 1995, Task Manager has finally received some love in Windows 8. Here's what's new.
Read: How to use Windows 8 Task Manager
Automatic backups
The new File History feature in Windows 8 can automatically back up your documents, music, pictures, and other personal files.
Read: How to automatically back up your personal files in Windows 8
Sync your devices
One of the best things about Windows 8 is that you can sync settings, apps, and more across multiple computers and tablets. Here's how you do it.
Read: How to set up sync on Windows 8
Printing
Printing from a Metro app in Windows 8 works differently than printing from a Desktop app. So, how do you print from a Metro app?
Read: How to print from a Metro app in Windows 8
Get Windows Media Center back
Windows Media Center isn't included with Windows 8, but for a limited time, you can get it free of charge.
Read: How to add Windows Media Center to Windows 8 Pro for free

Advanced tips

Run Windows 8 Desktop and Metro side by side
Not sure if you prefer Windows 8 in Desktop or Metro view? With an external monitor you can use both at the same time.
Read: Run Windows 8 desktop on a second monitor
Dual-boot with 7
Dual-booting your Windows 7 PC with Windows 8 can help you ease into using Windows 8.
Read: How to dual-boot Windows 7 with Windows 8
Make it kid-safe
Parental controls in Windows 8 are more configurable and robust than ever before. We'll show you how to use parental controls in Windows 8 to help keep kids safe while using a PC.
Read: How to use parental controls in Windows 8

Source http://howto.cnet.com/8301-11310_39-57529213-285/complete-guide-to-using-windows-8-roundup/

Monday, 24 February 2014

Facebook kununua WhatsApp kwa Sh 30.9 trilioni



Usimamizi wa Facebook ulisema utalipa Dola4 bilioni pesa taslimu na Dola 13 bilioni kupitia ubadilishanaji wa hisa.PICHA|MAKTABA 
Na Mwandishi wetu, Mwananchi

Posted  Ijumaa,Februari21  2014  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
WhatsApp ni maarufu miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma ya kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS).


Marekani. Kampuni ya Mtandao wa Jamii ya Facebook imesema itanunua mtandao wa mawasiliano wa ujumbe mfupi wa WhatsApp kwa Dola 19 bilioni za Marekani (Sh30.9 trilioni), ili kuimarisha umaarufu wake hasa miongoni mwa vijana.
Pia, wasimamizi wa Facebook walitangaza nyongeza zaidi ya Dola 3 bilioni zitalipwa waanzilishi wa Mtandao wa WhatsApp na wafanyakazi wake.
Hiyo ndiyo biashara kubwa zaidi ya ununuzi ambayo iliwahi kutekelezwa na Facebook kufikia sasa.
WhatsApp ni maarufu miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma ya kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS).
WhatsApp iliweza kuwasajili zaidi ya watumiaji milioni 450. Katika taarifa yake, Mwanzilishi wa Facebook, Mark Zuckerberg alisema mtandao huo upo kwenye harakati ya kuwaunganisha watu bilioni moja, jambo litakalofanya Facebook kuwa na thamani kubwa zaidi.
Zuckerberg alisema idadi kubwa ya watumiaji wa Facebook wanatumia simu za mkononi, hivyo mtandao wa WhatsApp ambao hutumiwa kwa simu utasaidia kuimarisha mawasiliano kwa gharama ya chini. Mitandao hiyo imekuwa na watumiaji wengi duniani.
Jan Koum alitangazwa kujiunga na bodi ya usimamizi wa mtandao wa Facebook.
Usimamizi wa Facebook ulisema utalipa Dola4 bilioni pesa taslimu na Dola 13 bilioni kupitia ubadilishanaji wa hisa.
Masharti
Watumiaji wa WhatsApp na Facebook ambao ni wengi katika mataifa ya Amerika na Canada walisifu hatua hiyo.
Mamlaka ya Facebook iliahidi kudumisha masharti ya WhatsApp na kutoa kitita cha 1milioni kulipa iwapo masharti hayo yatakiukwa.
Mapema mwezi huu Facebook ilisherehekea miaka 10 tangu kubuniwa na kufikia sasa ina watumiaji zaidi ya bilioni moja.
Soma zaidi http://www.mwananchi.co.tz/kitaifa/Facebook-kununua-WhatsApp-kwa-Sh1-36-trilioni/-/1597568/2215618/-/item/1/-/fqr6tj/-/index.html