m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Thursday, 30 January 2014

Factors to Consider When Buying a PC



Shopping for a personal computer (PC) can be enjoyable, or it can be frustrating. Unfortunately, some shoppers believe all personal computers are alike so their main objective is to find the cheapest one. Doing so can be a mistake. The old saying "You get what you pay for" is true. Many buyers have later discovered the computer they purchased lacked important components and features. Avoid making this mistake. The following sections provide some useful guidelines to help you in your search for the right PC.
Plan Before You Buy
Before spending your money, prepare a written list of your computing needs and how and where you will be using your new system. Following is a list of questions that will help you identify your needs.
1. How much can I afford to pay for a computer? Prices of personal computers range from a few hundred to thousands of dollars. Faster and more feature-rich PCs are usually more expensive. Also, personal computers soon become obsolete. Within a few years you may want or need one that is faster and more versatile.
2. Where will my new PC be used? If you will be using it only in your home or office, a desktop computer will be suitable. However, if you will need to take it with you, you should consider purchasing a laptop (notebook) computer weighing 4 pounds or less.
3. Which applications will I run on my computer? Make a list of applications for which you plan to use your PC. For example, will you use your PC to prepare letters and reports? Analyze numeric and financial data? Prepare visual presentations? Access the Internet? Listen to music? Create and work with graphics?
4. How long will I keep this computer? Try to estimate the length of time (years) you will use your computer before buying the next one. If you expect use your PC for several years or if you think you may later want to add new applications, consider one that is expandable, so you can add new components, such as a modem, printer, or add-on boards. Make sure the PC has expansion slots so you can connect these devices to your PC.
5. Check out the manufacturer’s and seller’s reputations and warranties and become familiar with various brands and models. Talk with friends, co-workers, classmates, teachers, and others about their PCs. Ask about the performance of their PCs and get recommendations from persons you trust. Eventually you may need to have your PC serviced. Ideally, the vendor has a service department that can repair your PC. If not, you may need to locate a third-party to provide this service.
Select the Hardware Components
Hardware refers to all the equipment that makes up a personal computer system. Hardware includes the system unit, input devices, output devices, secondary storage devices, and all peripheral devices, such as printers. Following are some guidelines for selecting PC hardware components.
1. The System Unit: The system unit is typically a metal cabinet containing the essential components for processing information. Along with other standard components, the system unit contains a microprocessor, main memory (RAM), and slots for installing a graphics board, sound board, modem, or other peripherals.
a. PC architecture. PC architecture refers to the design and construction of the PC and its system unit, and not all architectures are the same. For example, the architecture of an Apple Macintosh differs from that of an IBM or IBM-compatible PC. Therefore, software written for an Apple Macintosh PC may not run on an IBM or IBM-compatible PC. However, newer Macintosh PC models run both types of software. Although some users prefer a Macintosh PC, more software is available for IBM and IBM-compatible PCs.
b. Microprocessor. Selecting the right microprocessor is extremely important. Processing speed, typically measured in gigahertz (GHz), is probably the first consideration. The higher the number of GHz, the faster the processor will access programs and manipulate data. If speed is important, consider choosing a microprocessor with a speed of 2.0 GHz or more. PCs containing microprocessors with speeds up to 3.0 GHz and higher are available.
c. Main memory. Main memory (RAM) is needed for the temporary storage of programs and data while the data is being processed. Some application software requires a considerable amount of RAM to function properly, and newer software versions usually require more RAM than older versions. Typical PCs now come with 512 MB of RAM, or more. Make certain the PC has sufficient RAM to run the software you will be using.
d. Secondary storage. What type(s) and amounts of secondary storage are you likely to need? Typical computers come with a CD drive and a hard disk drive already installed. A standard compact disc can store up to 750 MB of data, and certain DVDs provide even greater storage capacity. A hard disk drive contains one or more rigid storage platters and provides for the permanent storage of considerably more data. However, the disk itself cannot be removed from the drive. The storage capacity of a hard disk is an important consideration because it is used to store all system and application software. Typical hard disk capacities are 80, 160 GB, and up to 500 GB. Be certain the PC you are considering has sufficient secondary capacity for your needs.
Other secondary storage devices and media are available. If you will use your PC to play movies, your purchase should include a DVD (digital video disk) drive. If you will work with large files, consider purchasing a computer that includes a CD-RW drive. A CD-RW disc is a reusable high-capacity disc that allows you to store huge amounts of data and to erase data no longer needed. Flash drives are also easy to use and are portable.
e. Ports. The number of ports (slots) available inside the system unit determines the number of add-on boards that can be installed inside the system unit. External ports allow you to connect peripheral devices such as modems, printers, digital cameras, and mice. The number of available ports determines the number of devices and add-on boards that can be connnected to the system unit.
2. Input Devices. Typical input devices are a keyboard and a mouse, although other kinds of input devices are available. Most keyboards and mice operate similarly. However, there are slight differences in how each "feels" to the user. Before buying a PC, you may want to test the keyboard and mouse for comfort and ease of use. Some sellers will allow you to exchange the keyboard or mouse that comes with the computer for a different one.
3. Output Devices. Output devices produce output in either soft copy or hard copy form. Most PCs come with a monitor (for soft copy output), but you may have to purchase a hard copy device, such as a printer, separately.
a. Monitors. Slim, lightweight, flat-screen liquid crystal display (LCD) monitors have virtually replaced the bulkier cathode ray tube (CRT) displays. The resolution of most LCD monitors is quite good and they take up less desktop space than CRT monitors. There are wide differences among PC monitors, with resolution being perhaps the most important variable. Resolution refers to the clarity of the text and images being displayed. Before making a purchase, carefully evaluate the monitor’s resolution. Many vendors allow you to choose from monitors with varying resolutions. A resolution of 1,024 by 1,024 pixels is considered high-resolution, in which text and images display exceptionally clearly. High-resolution monitors are typically more expensive.
Monitor size is another important consideration. Viewing areas range from 15 diagonal inches to 21 inches and higher. Larger monitors are usually more expensive, but may be worth the extra cost. For example, an individual with weak vision may prefer a larger monitor.
b. Printers. Two popular types of printers are ink-jet and laser, both of which are versatile and capable of producing high-quality output in color. Examine a variety of printers and models and check the price, print speed, and output quality of each.
Most ink-jet printers are quiet, produce high-quality output, and are relatively affordable, although the ink cartridges they use can be expensive. Print resolution is an important factor to consider. Some offer impressive resolution and can produce output of amazing color.
Laser printers are fast and can produce high-quality output in both black and color tones. Color laser printers are more expensive than those using only black toner. The cost of color laser printers ranges from a few hundred to thousands of dollars.
Choose Software to Match Your Needs List
By itself, a computer is merely a collection of electronic components and devices. Every computer must have software, including system software and applications software. System software, such as Microsoft Windows or Mac OS, allows a computer to manage its computing resources, including the system unit and input and output devices. Most PCs come with the system software already installed. If the PC you are considering does not, be sure the system software you choose is will run on the PC of your choice. Recall that both system software and application software are written for a specific architecture.
Before making a final purchasing decision, review your list of the ways in which you will use your computer. Then find out if the necessary application software is available (pre-installed) on the PC you have chosen. Some PCs come equipped with a software suite such as Microsoft Office, which includes word processing, spreadsheet, database management, and other applications.
A Reminder: Be a wise shopper, and learn which PC best satisfies your wants and needs. Even the least expensive personal computer system represents a major purchase. Making the right decisions means you will enjoy using your new PC in the months and years ahead.

KII strengthening Services/ TUNAIMARISHA HUDUMA




Dear esteemed customers of Kapagi Information Institute-KII, we are happy to strength our services in Computer Basic Skills. Now we start offering Computer information through posts of our blog and facebook pages, we ill be publishing IT articles from our center and different sources every week so that to provide basic skills everywhere our customers found. Don’t miss it, its easy just follow/like our blog and facebook page to get updates including IT posts.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Mpendwa mdau muhimu wa Kapagi Information Institute-KII, tunayo furaha kuimarisha huduma zetu za maarifa ya ngamizi (Computer). Sasa tunaanza rasmi kuchapisha habari zihusuzo maarifa ya ngamizi kupitia kurasa zetu za blogu na facebook. Tutakuwa tunachapisha makala na machapisho yahusuyo ngamizi kutoka kituo chetu na vyanzo mbalimbali ili kutoa maarifa kwa wadau wetu popote walipo. Tafadhali usikose fursa hii muhimu, ni rahisi tu fuatisha(Follow) /penda(like) blogu na ukurasa wetu wa facebook ili kupata machapisho yetu.
Mkurugenzi

Wednesday, 22 January 2014

ZZK NA WARAKA WA MAREHEMU CHACHA WANGWE KWA CHADEMA

Ndugu zangu watanzania
Naomba kwanza nikiri kwamba mimi si mwanachama wala shabiki wa chama chochote nchini, niliwahishabikia CCJ kabla hakijauawa katika uchanga wake. Nazungumzia uanachama na ushabiki na tena ushabiki unagawanyika zaidi kwa mtazamo wangu upo ushabiki wa dhati na ule uchwara. Shabiki yupo tayari kutetea timu au chama chake pasipo kujali ukweli wenyewe, shabiki huitaji kushinda kwa maneno, hupenda kuongoza kijiwe na kamwe hakubali kuumizwa moyo wake kwa ushindi wa mpinzani wake. Kama ni mfuatiliaji wa machapisho ya blogu hii utabaini kuwa nimeguswa sana na mnyukano wa kisiasa ulioanza mwishoni mwa mwaka hadi sasa kwenye chama kikiuu cha upinzani nchini. Yalipotokea ya Zitto Zuberi Kabwe maarufu kama ZZK na mkakati wao na Komredi Mwigamba na Dkt Kitila Mkumbo ghafla nikakumbuka yaliyompata Chacha Wangwe. Nilipokumbuka hayo ndipo nikadhamiria kuusaka waraka wa Marehemu Chacha Wangwe ili kujiridhisha ikiwa mawazo yangu ni halisi. Nimebaini mambo kadhaa
1. katika siasa za nchi hii kuhoji ni dhambi iwe kwa upinzani au utawala kwani ndio matokea ya akina Chacha wangwe, Shibuda alipohoji CCM, Dkt Ulimboka na sakata la madaktari na Sasa ZZK na makomredi zake
2. Hoja hutendewa kazi kutokana na nafasi ya anayehoji... si suala la uzito wa hoja.
3. Katika meza ya wapinzani anayehoji ni wa CCM na katika kiti cha CCM anayehoji ni mpinzani.
Mwisho kabla ya kuchapisha waraka huo niseme kwamba nimeuchapisha ili kuwapa nafasi watanzania uwanja wa kufikiri wenye mapana na marefu kwani naipenda nchi yangu na ni ndoto zangu siku moja kuwa na nchi yenye siasa safi. Pia lazima tukubali uzito wa hoja na si uzito wa anayehoji, ikiwa hoja ni nzito itendewe kazi na si kutuhumu aliyehoji.
Nagona

WARAKA WA MAREHEMU CHACHA WANGWE KWA CHADEMA
Jumamosi, June 28 mwaka huu wajumbe kadhaa wa Kamati Kuu ya CHADEMA walidai kuwa wamesitisha Umakau Mwenyekiti wangu katika kikao kilichofanyika mjini Dodoma siku hiyo. Kesho yake Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. FREEMAN MBOWE akaitisha mkutano wa waandishi wa habari na kutaja sababu za kunisimamisha uongozi.

Inatosha tu kusema kuwa sababu zote alizotoa ni za uzushi kama ile inayodai kuwa mimi navujisha siri za chama kwa viongozi wa CCM bila hata kutaja siri hizo, au kusema nimezitoa lini, wapi, na kwa kiongozi yupi?Kikao hicho kinachosemekana kunisimamisha uongozi, kilikuwa na wajumbe 31 ambao takribani nusu hawakuwa na uhalali wa kupiga kura kinyume cha katiba na kanuni za CHADEMA kwa vile walikuwa wameandaliwa kwa kazi hiyo. Wajumbe 7 walikataa kushiriki njama hizo.

Kufuatia jaribio hilo la kunivua uongozi kutokubalika kwa wanachama walio wengi wa CHADEMA , Mwenyekiti MBOWE na wafuasi wake wameendelea kuhaha kwa kuongeza sababu nyingine mbalimbali ili kuhalalisha njama zao. Sasa hivi wameingia hatua ya kuwashawishi wanachama wa Tarime eti wanifukuze uanachama.Kwa kuzingatia katiba, kanuni na taratibu za CHADEMA, nilichokifanya mimi baada ya kubaini njama zao ni kukata rufaa kwa Baraza Kuu la Chama, kupinga upotoshaji unaofanywa chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE anayeonekana kutaka kuendesha chama kinyume na matarajio ya wanachama walio wengi.Hivyo basi zipo habari za uhakika kuwa kikao hicho cha Baraza Kuu hakitaitishwa ama kabisa, au kitacheleweshwa kwa makusudi, kwa visingizio mbalimbali ikiwemo kutokuwa na fedha za kukidhi gharama za kikao hicho.

Naomba nikiri kuwa ninakerwa sana na mtiririko mzima wa sakata hili linalozua mgogoro unaokiyumbisha chama. Ukweli ni kwamba mimi niligombea Umakamu Mwenyekiti nikiwa na agenda ya kufufua uhai wa chama kwa kukaripia vitendo visivyostahili katika kuendesha chama. Agenda yangu haijabadilika. Yote niliyoyasema wakati nagombea nafasi hii yanafahamika kwa wana CHADEMA wote.

Walikuwepo walioyalalamikia na walikuwepo walioyapongeza matamshi yangu hayo.Mwisho wa yote wana CHADEMA waliridhika kuwa ajenda yangu ilikuwa sahihi na hivyo wakanichagua kuwa Makamu Mwenyekiti. Hivyo basi hata kama ni kweli kuwa ulikuwepo mvutano wakati wa kampeni ile, lakini hilo ni jambo la kawaida katika uchaguzi. Nijuavyo mimi hayo yalitakiwa yawe si ndwele nasi tugange yajayo kwani wanachama walikwisha fanya uamuzi halali kupitia kura zao.

Baada ya kuingia kwenye wadhifa wa Makamu Mwenyekiti Taifa, nilifanikiwa kuzungumza na Mhe. MBOWE kuhusu mambo, hususan yale, niliyoyapigania wakati wa kinyang?anyiro kile na kumuomba tukae chini na kutafuta jinsi ya kufanikisha azma hiyo.Ni imani yangu kuwa waraka huu utawasaidia wanaCHADEMA wenzangu na watanzania wote kwa ujumla, kuelewa vizuri ukweli wa mambo niliyoyapigania kabla ya kuwa Makamu Mwenyekiti, na ninayoendelea kuyasimamia hivi sasa nikiwa Makamu Mwenyekiti, na inshallah nitakayoyatekeleza baadae kama Taifa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Kimsingi mambo tunayotofautiana na Mhe. MBOWE ni haya yafuatayo:-

MATUMIZI YA RUZUKU
CHADEMA hupata ruzuku ya Tshs. 66,000,000 kwa mwezi (Milioni sitini na sita). Mimi nasema si haba hasa tukizingatia chama kilikotoka. Naamini kuwa kiasi hiki cha fedha kikisimamiwa vizuri kinaweza kukirahisishia chama kujieneza katika ngazi zote toka Tawi, Wilaya, Mkoa na Taifa.

Si kweli kwamba matatizo yote yatamalizwa na fedha hizi lakini basi hata ofisi za chama zinaweza kuwa hai nchi nzima kitu ambacho kwa sasa hakipo. Mahesabu yanaonesha kuwa mtaji wa laki moja (Tshs.100,000/=) kwa wilaya moja nchini inatosha, hivyo kwa Wilaya 126 kwa mwezi jumla yake ni Tshs. milioni 12 (Tshs. 12,600,000/= ) zinahitajika ( Wilaya 126 x 100,000 kila wilaya = 12,000,000/=)Hata tukisema tupeleke kiasi hicho kwa kila jimbo la uchaguzi jumla yake ni Tshs. Milioni 23 (Tshs. 23,000,000/=) kwa maana ya majimbo 213 x 100,000 = 23,000,000/=.
Mhe. MBOWE anasema hizo ni pesa nyingi sana kwa uimarishaji wa chama. Mimi nasema hapana, kiwango hiki kwa kila Wilaya au Jimbo la uchaguzi ni muafaka kwani haba na haba hujaza kibaba.Chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE na wafuasi wake hawastaajabu kuwa kati ya Tshs. 374,144,000.40 zilizopatikana kama ruzuku katika ya Januari 1 na Juni, 30, 2008, Tshs. 350,000,000/= zilitumika Makao Makuu ya CHADEMA na Tshs. 25,000,000/= tu ndizo zilikwenda Wilayani kuimarisha chama.Mimi naona mgao huu unayatukuza Makao Makuu ya
CHADEMA isivyostahili wakati huo huo ukidhalilisha chama nchi nzima.

MADENI YA UCHAGUZI
Kufuatia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mhe. MBOWE alitufahamisha wanachama kuwa alikuwa anakidai chama US $ 181,949.00 sawa na Tshs. 218,338,546. Mpaka sasa chama kimekwisha mlipa Tshs. 175,000,000/=Baada ya kupata wadhifa wa Makamu Mwenyekiti, na kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha Wilayani na Makao Makuu niliamua kumshauri MBOWE asitishe kujilipa deni kutokana na fedha za ruzuku kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopita kunaendana na utaratibu wa usimamizi wa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa toka serikalini.

Mhe. MBOWE alichachamaa na ndipo nilipomshauri kuwa kama ni hivyo basi atuthibishie pesa hizo anazodai alikikopesha chama ziliingia kwenye akaunti gani ya CHADEMA, kupitia hundi ipi, na lini? Nilimuomba pia kutaja ni kikao gani cha chama kiliidhinisha matumizi ya fedha hizo kwani kama hakuna ushahidi wa maidhinisho, ni dhahiri kuwa matumizi hayo hayakudhibitiwa na chama na kwa mantiki hiyo kuyafanya kuwa matumizi binafsi ya Mhe. MBOWE.Vilevile, nilimueleza kuwa matumizi ya fedha hizo alizodai alikikopesha chama yalikuwa yakinuka harufu ya UFISADI.

Stakabadhi zote kuhusiana na matumizi hayo zilionesha kuwa gharama za aidha ununuzi na / au ukodishaji wa vifaa hivyo, hazikutofautiana na viwango wanavyolipishwa watalii kwa huduma kama hizo, kwa maana ya gharama ya juu sana.Na kwa kuwa hata baada ya kuwa Mhe. MBOWE amekwisha lipwa zaidi ya nusu ya deni alilodai kuikopehsa CHADEMA, vifaa vyote yakiwemo magari, vipaza sauti na kadhalika vimebakia kuwa mali yake binafsi, basi bila kumficha nilimueleza kuwa huko ni kukinyonya chama kwa kukigeuza kitega uchumi cha watu binafsi.Kuhusu suala la kulipa madeni kupitia ruzuku ya serikali, nilimuomba Mhe. MBOWE afuatilie kwa Msajili wa Vyama vya siasa ili tupate ufafanuzi kama kweli fedha za ruzuku ya serikali kwa vyama vya siasa, inaweza kutumika kulipia madeni ya viongozi wa vyama hivyo yatokanayo na uchaguzi ili CHADEMA isiathirike kisheria.

Niseme kweli hapa kwamba, kwa vile wanaCHADEMA wengi walinichagua kuwa Makamu Mwenyekiti, na hata mimi mwenyewe tulikuwa wagombea wa nafasi za ubunge, udiwani n.k katika uchaguzi wa mwaka 2005 ningefarijika sana iwapo na sisi tungerejeshewa angalau chochote cha kufidia gharama zetu, kwa maana kwamba kama chama kimeamua kurudisha gharama hizo kiwalipe wote badala ya kulipa madeni kwa wateule wachache.

UTEUZI WA WABUNGE WA VITI MAALUM
Naamini ukweli wa suala hili hauna mjadala. Kwamba Mhe. MBOWE na wafuasi wake walighushi orodha ya majina ya viti Maalum badala ya kupeleka yaliyopendekezwa na Kamati Kuu sio siri.

Naamini hata Mhe. MBOWE anakubaliana nami kuwa suala hili si moja ya siri anazodai nimevujisha! Yamesemwa mengi juu ya mtafaruku uliojitokeza kuhusu viti maalum hadi baadhi ya waasisi wa chama wakataka kujitoa na hivyo kumlazimisha Mwenyekiti Taifa ( FREEMN MBOWE) na Katibu Mkuu (DR WILBROAD SLAA) kukiomba radhi kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kwa kukiuka katiba, kanuni na maadili ya chama katika suala hili la kugushi viti maalum.

Ni ukweli ulio wazi kuwa kitendo hicho cha upendeleo bado kina iumiza taswira ya CHADEMA. Chama kinaonekana kuendekeza ujanja ujanja kiasi kwamba watu na binti zao, wakwe zao, shemeji zao, waume wenzao, wachumba wa shemeji zao, wake wenza na kwa kiwango kikubwa watu wa kabila moja ndiyo wamekuwa sura ya CHADEMA bungeni.Katika hili nilichoweza kumueleza Mhe. MBOWE ni kuwa chaguzi mbalimbali tangu za Mitaa, Ubunge na Urais zinakaribia ni vizuri tufanye bidii kusambaza nguvu zetu nchi nzima tuwe na mtaji wa kura maeneo mengi ili kashfa kama hii isijirudie. Hii ni kwa msingi kuwa chama kikijitanua kutakuwa hakuna sababu ya kuwaona watu wa eneo fulani tu kuwa ndiyo mhimili wa CHADEMA na hivyo zikitokea fursa itakuwa rahisi chama kuwakilishwa na mtandao wake mpana badala ya koo au kabila fulani.Sasa kwa kuwa kuimarisha chama kitaifa maana yake ni matumizi ya fedha, nalo hili likawa nongwa ingawa kwa mtazamo wa Makao Makuu kulipa madeni kwa wateule wachache si nongwa.

Cha ajabu ni kwamba Mhe. MBOWE hakukana kuwa hili la viti maalum na hata upangaji wa ajira kwa ukabila una leta athari mbaya kwa mustakabali wa CHADEMA

Katika maongezi yangu nae nilikuwa wazi nilipotahadharisha kuwa:

1. Watanzania wakiendelea kuona kwamba CHADEMA inaendeshwa kwa misingi ya kikabila hawatajiunga na chama chetu na tutakosa wafuasi.

2. Watanzania wakiona kuwa sisi tumeweka mbele ukabila kuliko utaifa hawatatupa madaraka na kutawala kwa kuhofia yale yanayotokea nchi jirani kama Rwanda, Burundi, Kenya na kadhalika ambako nafasi za raia wote zimehodhiwa na kabila moja na hatma yake watu wamechinjana kama kuku kwa kupinga hilo.
Pia nilimwambia kwamba, kwa jinsi sura ya uteuzi wa Wakurugenzi na watendaji wengine wa Makao Makuu inavyoonekana, sasa tayari chama chetu kimebatizwa jina la CHAMA CHA WACHAGA, na hii si kuwatendea haki raia wengine na makabila yao ambao wataonekana kama punguani kujihusisha na chama na ukabila.Yote haya ninayosema kuhusu ukabila, upendeleo na kadhalika sio dhana tu. Kufuatia malalamiko mengi yaliyokuwa yakisikika nchi nzima kuhusu masuala haya, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikwisha unda Tume kutafuta ukweli wa mambo hayo. Tume hiyo ya watu watano iliongozwa na Mhe. Merky Lugendo Mziray ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA nayo imekwisha toa taarifa yake kwamba Makao Makuu ya CHADEMA yanatawaliwa na ubaguzi wa kikabila, kidini na kielimu.

UTENDAJI WA KIBABE
CHADEMA ni chama kilicho njia panda kwa sasa kutokana na utendaji wa kibabe wa Mhe. MBOWE. Ninafahamu jinsi vyama vingine vya upinzani hapa nchini kama vile NCCR ? Mageuzi vilivyoporomoka haraka haraka mithili ya nyumba ya mabua. Chama NCCR ? Mageuzi kilifikia mahali pazuri tu hadi watu wakaanza kufikiria kuwa kingekuwa chama mbadala kwa CCM.

kwa bahati mbaya uchu wa madaraka, ulafi wa ruzuku, na tabia za kimangimeza kwa pamoja vikakiathiri hadi kupoteza umaarufu wake.Na hata vyama vingine vya upinzani vina dalili hizo hizo japo kwa viwango vinavyotofautiana. Ila badala ya kujichunguza na kujua kasoro zetu, kila siku vyama vyetu, vimekuwa vikidai kuwa ni chama tawala ndicho kinachoviroga, kama ambavyo Mhe. MBOWE ameanza kuweweseka kupitia vyombo vya habari.Napenda kuthibitisha kuwa katika mgogoro unaopaliliwa sasa na Mhe. MBOWE ndani ya CHADEMA kutokana na ufisadi, ufuska, ulevi wa madaraka na umangimeza chanzo chake ni tabia yake ya kuendesha chama kibabe. Mathalan kumzuia Martin Mung?ong?o Mkurugenzi aliyechaguliwa kwa kura kutofanya kazi zake ndani ya chama, madai ya kupigana na watendaji wa chama ndani ya baa na vitendo vingine vya aina hiyo ni ushahidi tosha wa hulka hii.

Hadi sasa Mhe. MBOWE amefanikiwa kukizuia chama hiki kisifanye kazi ya siasa mkoa wa Dar es salaam kwa miaka minne.Ninavyoongea hivi sasa CHADEMA imekuwa ikikimbia vikao vya Democratic Union of Afrika (DUA), Muungano wa Vyama Vya Upinzani, uliofanikisha CHADEMA kujuana na Conservative Party ya Uingereza na Republican ya Marekani. Vyama dada hivi vyote vinaulalamikia uongozi wa CHADEMA kwa kufuja fedha ya misaada na kuwasilisha kwao risiti za kugushi, kama ilivyofanyiwa Conservative Party baada ya kutoa msaada wa Tshs. 78,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa baiskeli na pikipiki ambazo hazikununuliwa.Katika mkutano wa Kamati Kuu ya CHADEMA huko Dodoma hivi majuzi tu, Mhe. MBOWE kwa kauli yake aliwatisha wajumbe kuwa alikuwa amethibiti uwezekano wowote wa wajumbe kujisikia huru kwa kutoa mawazo ambayo yangepingana na ajenda yake aliyoitoa ghafla kikaoni kunisimamisha Umakamu Mwenyekiti.

Mhe. MBOWE Alikifahamisha kikao kuwa alitoa taarifa kwa IGP, SAID MWEMA kuwa kuna wahuni ambao walitaka kuuchafua mkutano wake, naye IGP akahakikisha kuwa mkutano ule unalindwa kwa kiwango cha kushtua kama ambavyo hata vyombo vya habari vimethibitisha.Hayo ni baadhi tu ya mambo yanayobainisha Mhe. MBOWE ni kiongozi wa aina gani.

HITIMISHO
Kama nilivyokwisha sema hapo awali, sijaacha na sintoacha ajenda yangu ya kufufua uhai wa CHADEMA kwani ndiyo ahadi iliyofanikisha kuchaguliwa kwangu kuwa Makamu Mwenyekiti Taifa. Nilipopata wadhifa huo nilianza kuitekeleza ajenda hiyo kupitia mahojiano na Mwenyekiti MBOWE kuhusu matumizi ya ruzuku, madeni ya uchaguzi, uteuzi wa wabunge wa viti maalum, nafasi za ajira Makao Makuu, na kuhusu mwenendo wa chama Mkoa wa Dar es salaam.

Nilijikuta katika mvutano mkubwa kila nilipogusa eneo lolote katika haya. Nakiri kuwa kwa kiwango kikubwa sikuwa na uwezo wa kubadili mambo hayo yaliyokuwa yakiratibiwa kwa ukaribu na Mhe. MBOWE na wafuasi wake kwani sikupewa ushirikiano wa aina yoyote na chama pale Makao Makuu.

Ni vigumu kuamini, lakini ni kweli kuwa sikuwa na ofisi Makao Makuu, sikupewa vitendea kazi kama magari, vipaza sauti na/au vyombo vya habari, na sikuwahi kupata taarifa yoyote ya kiutendaji toka Makao Makuu.Kwa kuzingatia yote hayo, naomba nichukue fursa hii kuwashukuru kwa dhati wanachama wa CHADEMA mkoa wa Dar es salaam ambao kwa pamoja tulisimama kidete kufufua uhai wa chama hapa jijini. Niseme tu ushirikiano wao wa hali na mali uliniwezesha kushughulikia masuala muhimu ya kitaifa na kimataifa.

Rai yangu kwa wana CHADEMA na wale wote wanaokitakia mema chama chetu na nchi yetu kwa ujumla ni kwamba kazi ya kupigania demokrasia ya kweli ndani na nje ya chama, kukiepusha chama na vitendo vya ukabila, migogoro, ubadhirifu, umangimeza, ufisadi na ubaguzi wa aina yoyote bado inaendelea na nawaombeni mniunge mkono kwa hali na mali katika vita hii.
UTANGULIZI.
Naamini tutashinda.
Mungu Ibariki CHADEMA
Mungu Ibariki TANZANIA
Mungu Ibariki AFRIKA
Chanzo:
 


Tuesday, 21 January 2014

Computer Basic Skills-Handout Coming Soon

Dear customer and supporter of KII be prepared to get Computer handout which will save students and the society from Computer Ignorance and join the computer expert family. 
Handout will be available for best price compared to contents.

 

Sunday, 19 January 2014

Serikali yawabeba waliofeli kidato cha pili


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa. Picha na Maktaba 
Na Fidelis Butahe, Mwananchi

Posted  Jumapili,Januari19  2014  saa 2:0 AM
Kwa ufupi
  • Licha ya matokeo hayo kutotangazwa hadi sasa, imebainika kuwa waliofaulu mtihani huo uliofanywa Oktoba 7 hadi 21 mwaka jana ni asilimia 62 tu, asilimia 31 wakitakiwa kukariri (kurudia) kidato cha pili mwaka huu, huku asilimia saba wakishindwa mtihani huo kwa mara ya pili.
Dar es Salaam. Wakati Watanzania wakisubiri matokeo ya kidato cha pili mwaka 2013, imebaini kuwa Serikali imetoa agizo kwamba wanafunzi wote waliofeli mtihani huo kuendelea na masomo ya kidato cha tatu, huku wakisoma mafunzo ya kurudia mtihani wa kidato cha pili.
Licha ya matokeo hayo kutotangazwa hadi sasa, imebainika kuwa waliofaulu mtihani huo uliofanywa Oktoba 7 hadi 21 mwaka jana ni asilimia 62 tu, asilimia 31 wakitakiwa kukariri (kurudia) kidato cha pili mwaka huu, huku asilimia saba wakishindwa mtihani huo kwa mara ya pili.
Jumla ya wanafunzi 531,457 walitajwa na Wizara ya Elimu mwaka jana kuwa watafanya mtihani huo.
Uamuzi huo wa Serikali ni tofauti na ule uliotolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa Novemba 4, mwaka 2012, kwamba kuanzia wakati huo mtihani wa kidato cha pili utakuwa ni wa mchujo na kwamba atakayefeli atatimuliwa.
Dk Kawambwa alisema matokeo ya mtihani wa kidato cha pili yatatumika kama kigezo cha kuchuja na kukariri kidato cha pili kwa watahiniwa watakaoshindwa kufikia wastani wa ufaulu wa alama 30.
Alisema mtahiniwa ataruhusiwa kukariri kidato cha pili mara moja tu na endapo mtahiniwa atashindwa mtihani kwa mara ya pili kwa mwaka utakaofuatia, itabidi aendelee na elimu ya sekondari nje ya mfumo rasmi.
Gazeti hili limeiona barua iliyoandikwa Januari 16 mwaka huu na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kusainiwa na Katibu Mkuu wake, Profesa Sifuni Mchome, kwenda kwa wadau wa elimu nchini, wakiwamo maofisa elimu wa mikoa na Chama cha Wamiliki wa Vyuo na Shule Binafsi (Tamongsco).
Katika barua hiyo, wizara hiyo imewataka wadau hao kuhakikisha kuwa wanafunzi watakaofeli mtihani huo, wanaendelea na masomo ya kidato cha tatu.
“Matokeo ya kidato cha pili yamepokewa na kufanyiwa uchambuzi ili kupata taswira ya taifa. Taarifa ya matokeo hayo imebaini kuwa watahiniwa waliofanya mtihani na kufaulu ni sawa na asilimia 62 tu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo na kuongeza;
“Hali hii inaonyesha kuwa asilimia 31 ya wanafunzi watatakiwa kukariri kidato cha pili, 2014. Wale walioshindwa kwa mara ya pili ambao ni asilimia saba wanatakiwa kuendelea na masomo nje ya mfumo rasmi.”
Barua hiyo inaeleza kuwa wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 na kuendelea waendelee na masomo ya kidato cha tatu mwaka 2014, wakati awali Serikali ilitoa tamko kuwa watakaoshindwa kufikisha alama 30 watatimuliwa.
“Wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 hadi 39 wapewe mafunzo rekebishi ‘Remedial class’ wakiwa kidato cha tatu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo
SOMA ZAIDI http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/2151230/-/utnth5z/-/index.html.