m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Saturday, 8 June 2013

Roho mtakatifu ni nani?



Swali: "Roho mtakatifu ni nani?"

Jibu:
Kuna utatanishi mwingi juu ya kumtambua Roho mtakatifu. Wengine humchukulia kama nguvu Fulani zisizoonekana. Wengine huamini kwamba ni uwezo wa Mungu ambao Mungu huuachilia maishani mwa wale ambao ni waumini wa kristo. Je, biblia inasemaje juu ya Roho mtakatifu? Kwa kifupi biblia inasema kwamba Roho mtakatifu ni Mungu. Pia biblia inasema kuwa Roho mtakatifu ni mtu, mwenye akili, hisia na mapenzi yake.

Swala la kuwa Roho mtakatifu ni Mungu limo ndani ya aya nyingi za biblia kama vile Matendo 5:3-4. Katika ayah ii petro anapambana na anania aliyemdanganya Roho mtakatifu na nasisitiza yakuwa “hukumdanya mtu bali Mungu.” Hili ni tangazo la wazi kwamba kumdanganya Roho mtakatifu ni kumdanganya Mungu. Tunaweza pia kujua Roho mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana tajwa na hali sawa na za Mungu. Roho mtakatifu yuko kila mahali katika Zaburi 139:7-8, “nitaenda wapi nijifiche na Roho? ama nitakimbilia wapi mbali na uwepo wako? Nikipanda juu mbinguni, huko uko; nikifanya malazi yangu kuzimu, tazama uko huko,” tena katika wakorintho wa Kwanza 2:10 tunaona hali yakuwepo kila mahali kwa Roho mtakatifu “Lakini Mungu ameyajulisha kwetu kupitia Roho wake mtakatifu. Kwa kuwa Roho huyachunguza mambo yote, naam, mambo ya siri ya Mungu. Kwa maana ni nani ayajuaye ya mwanadamu isipokuwa roho ya mwanadamu inayokaa ndani yake? Vivyo hivyo, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.”

Tunaweza kujua kweli kwamba Roho mtakatifu ni Mungu kwa kuwa ana akili, hisia na mapenzi yake. Roho mtakatifu hufikiri na hujua (Wakorintho wa kwanza 2:10). Roho mtakatifu anaweza kuugua (Waefeso 4:30). Roho hutuombea (Warumi 8:26-27). Roho mtakatifu hufanya maamuzi kutokana na mapenzi yake mwenyewe (Wakorintho wa kwanza 12:7-11). Roho mtakatifu ni Mungu, sehemu ya tatu ya utatu wa Mungu. Kama Mungu, Roho mtakatifu anaweza kufanya kazi ya msaidizi na mshauri kama vile Yesu kristo aliyevyoahidi kuwa atakuja kufanya (Yohana 14:16,26; 15:26).
Chanzo; http://www.gotquestions.org/Kiswahili/roho-mtakatifu.html

Tuesday, 4 June 2013

Tanzania mpya na Rasimu ya Katibu

Share bookmark Print Email Rating
 
Na Mwandishi Wetu  (email the author)

Posted  Jumatatu,Juni3  2013  saa 20:50 PM
Kwa ufupi
Miongoni mwa mambo ambayo hayamo kwenye Rasimu ya Katiba ni pamoja na Serikali za majimbo, Mahakama ya Kadhi.
 
Dar es Salaam. Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana ilizindua rasimu ya Katiba Mpya inayopendekeza kuwapo kwa mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa utawala, yakiwamo ya kuwa na Serikali Tatu; Shirikisho la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar.

Mabadiliko mengine yaliyosheheni kwenye rasimu hiyo ni kufutwa kwa viti maalumu vya ubunge, suala la maadili ya viongozi wa taifa, umri wa urais kubaki kama ulivyokuwa na kuruhusiwa kwa wagombea binafsi katika ngazi zote; urais, ubunge, udiwani mpaka ngazi za mitaa.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba alisema Tume pia imependekeza kuingizwa kwenye Katiba Mpya mambo kadhaa kama Tunu, Dira na Misingi ya Taifa.
“Tulitaka kuifanya rasimu hii iwe fupi kadri iwezekanavyo, lakini kutokana na wingi wa maoni tumeifanya iwe na Ibara 240. Katiba ya sasa ina Ibara 152,” alisema Jaji Warioba na kuongeza:
“Tumeendelea kuitambua misingi mikuu minne ya taifa ambayo ni Uhuru, Haki, Udugu na Amani. Lakini pia tukaongeza misingi mingine mitatu ambayo ni Usawa, Umoja na Mshikamano. Tumependekeza Katiba yetu mpya iwe na misingi saba.”
Jaji Warioba alisema Tume pia imetambua mambo kadhaa kuwa ni Tunu za Taifa: “Tunu ya kwanza ni Utu. Tunaamini kuwa watu wote ni sawa, tusiwe na ubaguzi wala tofauti zozote. Tunu nyingine ni Uzalendo, Uadilifu, Umoja, Uwazi Uwajibikaji na Lugha ya Kiswahili.”
Jaji Warioba alisema pia kuwa Tume imebainisha malengo ya Taifa ambayo yatakuwa mwongozo wa Mihimili ya Dola; Serikali, Bunge na Mahakama.
“Malengo hayo yatakuwa ya aina mbalimbali. Kuna malengo ya kisiasa, kiuchumi, kimazingira na mengine mengi yatakayofafanuliwa baadaye,” alisema.
Jaji Warioba alisema Tume pia imependekeza Katiba ijayo ionyeshe wazi maadili ya kijamii, kiutawala na kiuongozi.
“Tumependekeza kuwapo maadili ya viongozi, miiko na kiundwe chombo cha kusimamia maadili. Tunapendekeza sekretarieti ya maadili ya viongozi iliyopo, iwe tume kamili,” alisema.
Muundo wa Serikali Tatu
Jaji Warioba alisema baada ya kupitia maoni mengi, Tume imeridhika kwamba inafaa Tanzania iwe na mfumo wa Serikali tatu, yaani Serikali ya Shirikisho, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
“Tumependekeza Serikali ya Muungano iwe na mawaziri wasiozidi 15 na wabunge 75. Wabunge 50 kutoka Bara, 20 Zanzibar na wabunge watano wa kuteuliwa na Rais,” alisema wabunge wa kuteuliwa watatoka katika kundi la watu wenye ulemavu tu.
Alisema Serikali hiyo ya Muungano itakuwa inaongozwa na Rais Mtendaji. Alitaja mambo yatakayoingia kwenye Muungano kuwa ni Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ulinzi na usalama, uraia na uhamiaji, sarafu na Benki Kuu, mambo ya nje, usajili wa vyama vya siasa na ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.
Mikutano 1,942
Jaji Warioba alisema rasimu hiyo ya Katiba imekamilika baada ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba kufanya mikutano 1,942 ambayo ilihudhuriwa na watu 1,306,500.
“Watu 395,000 walitoa maoni ya ana kwa ana na makundi 160 maalumu yalitoa maoni yao. Pia tulizungumza na viongozi wa kitaifa; walioko madarakani na wastaafu. Viongozi 43 walitoa maoni,” alisema.
Jaji Warioba alisema baada ya maoni hayo, walikuwa na miezi mitatu kuyachambua na kuandaa rasimu ya Katiba, lakini wakalazimika kuongeza muda huo hadi Mei mwaka huu.
“Kutokana Sheria, Rasimu hii itachapishwa kwenye Gazeti la Serikali na baadaye kwenye magazeti kabla ya Mabaraza ya Katiba kuanza kazi,” alisema Jaji Warioba .
Alisema mchakato huo wa Mabadiliko ya Katiba ulioanza kwa Sheria iliyotungwa Novemba 2011 na baadaye kufanyiwa mabadiliko Februari 2012, umepangwa kumalizika ndani ya miezi 18... “Hivyo Tume imekusudia kumaliza mchakato huo Novemba Mosi mwaka huu,” alisema.
Chanzo; mwananchi.co.tz

Sunday, 2 June 2013

Mauaji ya kutisha yaibuka msituni

 
Na Burhani Yakub,Horohoro  (email the author)

Posted  Juni1  2013  saa 20:14 PM
Kwa ufupi
  • Kwa kipindi kirefu msitu huo umekuwa eneo la kufanyia mauaji kwa watu wasio na hatia, ambapo genge la wahalifu kutoka Kenya limedaiwa kuhusika na mauaji hayo.

Matukio ya mauaji ndani ya msitu wa Mwakijembe yameendelea kutishia usalama wa Watanzania, wanaoishi jirani na eneo la Horohoro linalopakana na nchi jirani ya Kenya.
Kwa kipindi kirefu msitu huo umekuwa eneo la kufanyia mauaji kwa watu wasio na hatia, ambapo genge la wahalifu kutoka Kenya limedaiwa kuhusika na mauaji hayo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini msitu huo wenye rasilimali nyingi unaodaiwa kutumiwa na genge hilo kwa vitendo haramu vya ujangili, uchimbaji madini na uvunaji wa miti, ikiwemo uchomaji mkaa.
Taarifa za uchunguzi ambazo zilithibitishwa na viongozi wa Serikali ya Vijiji vinavyopakana na msitu huo, zilibaini genge hilo limekuwa likiua kila linayemhisi atafichua uhalifu wao.
Inatoka UK 1
Uchapisha wa Hati za Kusafiria (Kwa mujibu wa taarifa za karibuni, kwa mwaka huu pekee, watu wawili tayari wameshauawa kwa kuchinjwa ndani ya msitu huo.
Matukio hayo ya mauaji yalithibitishwa na Diwani wa Kata ya Mwakijembe, Ramadhani Mtiota ambaye alisema kwa sasa katika eneo hilo hali imekuwa ya hofu kutokana na kuongezeka kwa makundi ya vijana wa rika la Morani wa Kimasai, wanaojiandaa kuvishambulia vijiji vya Kenya.
Diwani huyo alisema ametoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza kuhusu hali hiyo pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Andrew Ngoda.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alisema wanafahamu kuhusu mauaji yanayotokea kwenye msitu huo.
Alisema taarifa za mauaji ya hivi karibuni ya watu wawili, Ali Mohamed na msichana wa kabila la Kimasai Kendie Minja yanafahamika na yanafanyiwa uchunguzi na polisi.
”Ninachofahamu ni mauaji yaliyofanyika ya msichana Kendie kuchinjwa na kufichwa msituni upande wa Kenya, lakini upelelezi unafanywa na Jeshi la Polisi la wenzetu wa Kenya kwa hivyo sijui zaidi ya hivyo,” alisema Massawe.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza alisema anaandaa mkutano wa ujirani mwema utakaowahusisha viongozi wa Serikali Mkoa wa Tanga na Jimbo la Mombasa, Kenya.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Mauaji-ya-kutisha-yaibuka-msituni/-/1597296/1869732/-/11tcb6hz/-/index.html 

Membe: Tanzania haiwezi kuomba radhi Rwanda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akipongezwa na Mawaziri na wabunge mara baada ya kusoma makadirio ya bajeti ya wizara yake Bungeni. ameelezea  kuwa Tanzania haitaiomba Rwanda msamaha kutokana na kauli ya Rais Jakaya Kikwete 
Na Fidelis Butahe, Mwananchi  (email the author)

Posted  Juni1  2013  saa 20:22 PM
Kwa ufupi
  • Serikali ya Rwanda iliitaka Tanzania iombe radhi kwa madai kuwa kauli ya Rais Kikwete ni kama tusi kwao na kwamba wao hawawezi kukaa na kuzungumza wapinzani ambao ni wauaji

Dodoma. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amesema kamwe Tanzania haitaiomba radhi Rwanda, baada ya Rais Jakaya Kikwete kuishauri nchi hiyo kufanya mazungumzo na upinzani ili kumaliza vita katika eneo hilo la Maziwa Makuu.
Serikali ya Rwanda iliitaka Tanzania iombe radhi kwa madai kuwa kauli ya Rais Kikwete ni kama tusi kwao na kwamba wao hawawezi kukaa na kuzungumza wapinzani ambao ni wauaji.
“Kama Rwanda haitaki kufuata ushauri wa Rais Kikwete inatakiwa kuuacha na siyo kumtaka aombe radhi,” alisema.
Membe alitoa ufafanuzi huo bungeni jana wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika mjadala wa makadirio ya matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka 2013/2014.
Tamko hilo la Serikali limekuja ikiwa zimepita takriban siku sita tangu Serikali ya Rwanda kutoa tamko la kupinga ushauri huo uliotolewa na Rais Kikwete wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Akijibu pendekezo hilo la Rais Kikwete, Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Louise Mushikiwabo alisema kuwa Rwanda haiko tayari kufanya mazungumzo na watu ambao walishiriki kwenye mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, dhidi ya Watutsi na kwamba kufanya hivyo ni sawa na kuhalalisha mauaji kwa wananchi wake.
“ Wale wote wanaodhani kuwa Rwanda itaanzisha majadiliano na waasi wa FDLR nadhani kwa ukweli hawajui kile wanachozungumza. Rwanda haiwezi kujadiliana na wauaji,” alisema waziri huyo wakati akizungumza na Idhaa ya Kimataifa ya Radio Ufaransa.
Alisema kuwa wakati serikali ya Rwanda imefaulu kuzika mienendo inayopalilia mauaji ya halaiki, lakini bahati mbaya kumesalia makundi ya watu ambayo bado yanahubiri itikadi zinazokumbusha uchungu na kutonesha kidonda kilicholeta maafa makubwa kwa wananchi.
“ Kumbe kuna wasemaji wengi wa kundi la FDLR. Wengine wao wanaendelea kufungamana na itikadi za kundi hili. Rwanda ilifaulu kutokomeza mauaji ya halaiki lakini hatukutokomeza itikadi za kundi hili,” alisema waziri huyo.
Kauli ya waziri huyo imeungwa mkono na baadhi ya wasomi pamoja na wanaharakati waliosema kuwa kuiomba Rwanda ianzishe majadiliano na kundi hilo, wanapaswa kufikiri mara mbili.
Katika ufafanuzi wake Membe alimnukuu Waziri Mkuu wa zamani wa Israel, Isaack Rabin kwamba mwaka 1995 aliwahi kutoa tamko lililosema, ‘Tunajenga amani na tunajadiliana na maadui zetu na si marafiki’.
Alisema kama Serikali ya Rwanda itakuwa imesikia kauli hiyo inatakiwa kufanya mazungumzo ya amani na maadui, na wasingoje kufanya mazungumzo ya amani na Tanzania, ambayo wana uhusiano mzuri na ni nchi rafiki kwa muda mrefu.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Tanzania-haiwezi-kuomba-radhi-Rwanda/-/1597296/1869740/-/11cm237z/-/index.html 

Saturday, 1 June 2013

Zana za Hizbollah zapatikana Nigeria

  31 Mei, 2013 - Saa 08:30 GMT


Jeshi lilisema kuwa silaha hizo zilikuwa zimefichwa chini ya vumbi la mbao
Karakana ya silaha inayoaminika kumilikiwa na kundi la Hezbollah, nchini Lebanon imapatikana Kaskazini mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa za jeshi na shirika la ujasusi la Nigeria raia watatu wa Lebanon wamekamatwa. Msemaji wa jeshi, Brigedia Gen Ilyasu Isa Abba, pia amethibitisha hilo.
Silaha hizo ikiwemo, risasi, zana za kukinga magari ya kivita dhidi ya mashambulizi na RPG, zilipatikana ktika karakana mjini Kano.
Maafisa wa usalama walisema kuwa silaha hizo zilinuiwa kutumiwa dhidi ya maslahi ya Israel na nchi za Magharibi.
Hii ni kazi ya Hezbollah," katibu mkuu wa usalama mjini Kano Bassey Ettang alisema.Na unaweza hata kuwa na uhakika kuwa ikiwa hili linafanyika, inawezekana wanasaidia makundi ya kigaidi wanaoendesha harakati zao nchini humu,'' alidokeza bwana Bassey.
Brig Gen Ilyasu Isa Abba alisema kuwa zana 11 za magari ya kivita, guruneti na makombora 21 bunduki 17 aina ya Ak-47 na maguruneti 76 ni baadhi ya silaha zilizopatikana.
Mmiliki wa karakana hiyo, ambako silaha zilipatikana, zikiwa zimefichwa chini ya vumbi la mbao, hakuwa nchini humo.
Kuna jamii kubwa ya walebanese wanaofanya kazi mjini Kano, mji wa kibiashara wa Nigeria Kaskazini.
Mji wa Kano eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zimekubwa na mashambulizi ya mara kwa mara katika miaka mitatu iliyopita, tangu wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram walipoanzisha harakati zao.
Bwana Ettang aliongeza kuwa "unaweza pia kuwa na uhakika kundi kama hili likiwa lipo, inaweza hata kuwasaidia wapiganaji wengine walioko nchini humo.''
Hezbollah ni kundi la Kishia pamoja na kuwa vuguvugu la kisiasa lenye makao yake nchini Lebanon. Linatambulika na Marekani kama kundi la kigaidi.
Boko Haram, ambalo jina lake lina maanisha tamaduni za kimagharibi zinapingwa, linasema, nia yake ni kuipindua serikali sasa na kubuni serikali ya kiisilamu.
Kuna wasiwasi mkubwa kuwa kundi la Boko Haram huenda linasaidiwa na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda katika nchi zengine
bbcswahili.com

Japani kuipa Afrika msaada wa dola bilioni 32




Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe Jumamosi (01.06.2013) ameahidi kutowa msaada wa dola bilioni 32 kwa Afrika katika kipindi cha miaka mitano kusaidia ukuaji wa uchumi wa bara hilo kupitia sekta za serikali na binafsi.
Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe ametoa ahadi ya masaada huo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa siku tatu kuhusu maendeleo ya Afrika unaofanyika katika mji wa Yokohama nchini Japani.
Msaada huo unajumuisha utowaji wa yeni bilioni 650 kwa ajili ya mikopo katika ujenzi wa miundo mbinu na mpango wa mafunzo kwa ajili ya vijana wa Afrika.Mpango huo utawapa fursa vijana 1,000 wa Kiafrika kujifunza katika vyuo vikuu vya Japani na kujifunza kazi katika makampuni ya Kijapani.
Abe amesema kuendeleza rasilmali ya nguvu kazi, huduma muhimu za matibabu na kukuza sekta ya kilimo ni mambo muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa Afrika.Amesema kile inachokihitaji Afrika ni uwekezaji katika sekta ya binafsi ambapo ushirikiano kati ya sekta za umma na binafsi utatoa fursa ya kufaidikia na uwekezaji huo. #
Shauku ya Japani kuwekeza Afrika
Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Maendeleo ya Afrika (TICAD) mjini Yokohama Japani. Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Maendeleo ya Afrika (TICAD) mjini Yokohama Japani.
Tangazo lake hilo linaonyesha shauku ya Japani kuchuana na China katika masuala ya kuipatia msaada na kuwekeza Afrika bara lenye utajiri wa mali asili.
Licha ya uhusiano wa muda mrefu uliopo kati ya Japani na Afrika,umuhimu wa Japani kwa bara hilo umekuwa ukipunguwa kulinganishwa na ule wa China ambapo kiwango chake cha biashara na Afrika ikilinganishwa na Japani ni mara tano zaidi na mara nane zaidi katika uwekezaji wa moja kwa moja.
China huwa haitangazi kiwango cha msaada wake wa maendeleo lakini repoti zinadokeza kwamba hutoa hadi dola bilioni mbili kila mwaka.Kiwango ilichotangaza Japani Jumamosi kimepita sana kiwango hicho cha China.Uhusiano wa Japani kwa Afrika unatofautiana na mataifa mengine kwa bara hilo amesema Abe katika kauli inayoonekana kuikusudia China.
Serikali ya China imekuwa ikishutumiwa na baadhi ya nchi kwa kile mara nyengine kinachoonekana kuwa inachofanya barani humo ni kunyakua ardhi na kutohusisha uwekezaji na masharti ya kuboresha haki za binaadamu au kuzitaka nchi zinazopokea misaada kuwa wazi zaidi.
Waziri Mkuu huyo wa Japani amesema mali asili ya Afrika inasababisha kuwepo kwa fursa muhimu za biashara kwa nchi yenye uhaba mkubwa wa mali ghafi kama Japani lakini nchi hiyo haitotafuta na kuchimba rasilmali hizo kwa sababu tu ya kuzileta Japani.
Msaada ukuze uchumi
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn na Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa mkutano wa TICAD mjini Yokohama Japani. Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn na Waziri Mkuu wa Japani Shinzo Abe wakati wa ufunguzi wa mkutano wa TICAD mjini Yokohama Japani.
Amesema wataisaidia Afrika ili kwamba mali asili za Afrika zisababishe ukuaji wa kiuchumi wa bara hilo.Abe pia ametoa wito wa kuanzishwa kwa kanuni za uwazi katika biashara na kuimarisha usalama kwa Wajapani wanaoishi na kufanya kazi barani Afrika.Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn ameitaka Japani kuimarisha uwepo wake barani Afrika.
Akizungumza katika kikao cha ufunguzi wa mkutano huo wa Kimataita wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD), amesema ni jambo la kushangaza kwamba kuhusika kwa Japani katika fani ya uwekezaji barani humo kuko nyuma kabisa kuliko vile ingelipaswa iwe kwa hivi sasa kulinganisha na nchi mpya ambazo hivi sasa zimekuwa zikijihusisha katika harakati nyingi.
Afrika lazima ibadilike
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini. Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
Suala la uwekezaji katika sekta ya binafsi limekaribishwa na wajumbe ambapo Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amesema uchumi wa bara hilo hauna budi kuendelezwa. Amesema Afrika lazima ibadilike kutoka kuwa na uchumi unaotegemea usafirishaji nje wa bidhaa na kuwa na uchumi wenye kuongozwa na viwanda pamoja na kutanuwa njia mbali mbali za kiuchumi.Zuma amesema mambo matatu ni muhimu kufikia maendeleo nayo ni : kuunganisha masoko, kuendeleza viwanda na kuendeleza miundo mbinu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon pia amehudhuria mkutano huo ambapo amesema malengo ya mkutano huo ni malengo ya Umoja wa Mataifa.Amesema wamejizatiti kuisaidia Afrika itimize Malengo ya Maendeleo ya Milenia yakiwemo kutokomeza umaskini na njaa ifikapo mwaka 2015.
Mkutano huo wa TICAD utaendelea kufanyika hadi Jumatatu ambapo wajumbe kutoka zaidi ya nchi 50 za Afrika watakuwa wanajadili na Japani jinsi ya kuhakikisha ukuaji wa uchumi endelevu barani Afrika.Mkutano huo unaandaliwa kwa ushirikiano wa mashirika ya kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa,Benki ya Dunia na kwa mara ya kwanza Umoja wa Afrika.Mkutano huo umekuwa ukifanyika kila baada ya miaka mitano nchini Japani tokea ulipoanzishwa hapo mwaka 1993.
Mwandishi : Mohamed Dahman/AFP,dpa
Mhariri :Caro Robdw
dw.de

Ziara ya Obama nchini yazua malumbano

ZIARA ya Rais Barrack Obama wa Marekani imewagawa Watanzania huku wengi wao wakionyesha hofu kubwa ya viongozi wa mataifa makubwa kuwa wanakuja kwa nia ya kupora rasilimali za nchi. Wakati Watanzania wakiwa na hofu, Wakenya wamelalamika kupitia mitandao ya jamii kitendo cha Rais Obama kuwatenga wakati chimbuko la baba yake ni kutoka Kenya.
Wakizungumza na MTANZANIA kwa nyakati tofauti jana baadhi ya wananchi walisema wanashangazwa na ziara ya Rais Obama ikiwa ni miezi michache baada ya ziara ya Rais Xi Jimping wa China ambaye alitia saini mikataba 17 ya maendeleo.

Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro alisema kitendo cha nchi kupokea wageni wakubwa wa mataifa makubwa ni heshima kwa nchi lakini inategemea kiongozi huo amebeba ajenda gani.

Naye Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), Deogratus Munishi alisema Tanzania ni uwanja wa mapambano kwa mataifa makubwa kutokana na rasilimali zake.

Munishi alisema uchumi wa mataifa makubwa unategemea soko na rasilimali za mataifa madogo na akisisitiza kwamba madini ya uranium ndiyo chanzo cha viongozi wakubwa kukimbilia Tanzania.

Katika ziara yake ya kwanza katika Afrika, Rais Obama aliitembelea Ghana.

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YAPAA

Baraza la mitihani limetangaza matokeo ya kidato cha sita mwaka 2013. Matokeo hayo ni mazuri kulinganisha na matokeo ya kidato cha nne yalileta mtikisiko mkubwa. Kwa mujibu wa baraza la mitihani

Asilimia 93 ya waliofanya mtihani huo wa kidato cha 6 wamefaulu.

Shule ya kwanza iliyoongoza ni Marian Girls ya mkoani Pwani na ya pili ni Mzumbe ya Morogoro.

Mwanafunzi wa 1 wa kiume kwa sayansi ni Erasmi Inyase kutoka Ilboru, na kwa wasichana ni Lucylight wa Marian girls.

Upande wa masomo ya Biashara mwanafunzi wa 1 ametoka shule ya Tusiime anaitwa Erick Robert.

Wanafunzi 89 matokeo yao yamezuiliwa kwa sababu mbalimbali.

Wanafunzi watakaothibitika kuwa walikuwa na matatizo ya kiafya, watapewa nafasi ya kurudia mtihani.

Bofya hapa chini ujionee matokeo

http://www.necta.go.tz/matangazo2013/tangazo-usajili-ACSEE2014.pdf 


Thursday, 30 May 2013

ICC tayari kushauriana na Kenya kisheria


 30 Mei, 2013 - Saa 16:25 GMT

ICC inashikizwa iweze kuhamishia Kenya kesi za washukiwa William Ruto na Rais Uhuru Kenyatta
Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya jinai ya kimataifa- ICC, Fatou Bensouda leo amesema kwamba mahakama hiyo iko tayari kushauriana na Kenya kisheria kuhusu ombi la kutaka kesi inayowakabili rais wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto kuhamishiwa nyumbani.
Tamko hilo linatolewa wiki moja tu baada ya viongozi wa Umoja wa Afrika kutoa wito kwa ICC irejeshe kesi za Uhuru na Ruto zishughulikiwe nchini Kenya.
Akijibu maswali ya waandishi kutoka radio moja ya kibinafsi ya Nairobi, mwendesha mashtaka huyo mkuu amenukuliwa akisema hatua ya ICC kufanya mazungmzo na Kenya kuhusu kesi za Uhuru na Ruto kurejeshwa nchini Kenya ni utaratibu wa kisheria utakao amuliwa na majaji wa ICC.
Alisema kwa mujibu wa mkataba wa Roma ambao ndio msingi wa mahakama ya ICC, nchi yoyote inayotaka kesi irejeshwe yafaa itosheleze kwa majaji wa ICC kwamba itaendeleza mashtaka hayo hayo kwa watuhumiwa.
Bi Bensouda alisema ICC ni mahakama huru ambayo haiegemei misingi ya kisiasa na majaji wake hutoa uamuzi bila kushurutishwa na yeyote.Alisema ICC itaendelea kushirikiana na mataifa 34 yaliyosaini mkataba wa kujiunga na mahakama hiyo.
Wiki jana, viongozi na serikali wanachama wa Umoja wa Afrika waliafikiana mjini Addis Ababa Ethiopia kwenye kongamano lao kwamba yafaa kesi zinazowakabili rais Uhuru Kenyatta, naibu wake, William Ruto pamoja na mwanahabari Joshua arap Sang zirejeshwe na kushughulikiwa nchini Kenya.
Uhuru na Ruto wameshtakiwa kwa kupanga na kufadhili mapigano ya baada ya uchaguzi mkuu wa Kenya wa 2007, yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu na kuwaacha wengine takriban nusu milioni bila makao.
bbcswahili

Israel yapanga kujenga makaazi mapya Jerusalem

Mjumbe wa kimataifa wa Wapalestina Saeb Erakat amesema mpango wa Israel wa kujenga makaazi mengine 1000 mashariki mwa Jerusalem utazikwamisha juhudi za kuyafufua mazungumzo ya kuutatua mgogoro wa Mashariki ya Kati.
Erakat aliitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya asasi moja kuarifu kwamba Israel inapanga kujenga makaazi zaidi ya walowezi.
Erakat amesema mpango wa Israel wa kujenga makaazi zaidi katika Jerusalem ya Mashariki utazivuruga kabisa juhudi zinazofanywa na Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry za kuufufua mchakato wa kuleta amani katika Mashariki ya Kati.
Erakat ameliambia shirika la habari la AFP kwamba Israel ina mpango wa makusudi wa kuzivuruga juhudi za Waziri Kerry. Amesema inapohusu kuchagua biana ya makaazi mapya na amani, Israel wakati wote imechagua kuendelea na ujenzi wa makaazi mapya katika maeneo ya Wapalestina.
Kandarasi za ujenzi zatiwa saini:
U.S. Secretary of State John Kerry (L) meets with Israeli Prime Minster Benjamin Netanyahu in Jerusalem May 23, 2013. REUTERS/Jim Young (ISRAEL - Tags: POLITICS) Jonh Kerry und Benjamin Netanjahu wakiwa Jerusalem
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali nchini Israel bwana Danny Seidemann aliliambia shirika la habari la AFP kwamba kandarasi kwa ajili ya nyumba 300 katika kitongoji cha Ramot kaskazini mashariki mwa Jerusalem tayari zimeshatiwa saini na viwanja 797 vitauzwa kusini mwa Jerusalem katika kitongojo cha Golo kilichopo karibu na Ukingo wa Magharibi.
Vitongoji hivyo viwili vipo katika maeneo ambayo hasa ni ya Waarabu katika mji huo wa Jerusalem. Vitongoji hivyo vilitekwa na Israel katika vita vya siku sita vyamwaka wa 1967 na baadae kuwekwa chini ya himaya ya Israel, hatua ambayo mpaka leo haijatambuliwa na jumuiya ya kimataifa.
Mkurugenzi wa asasi iliyotoa taarifa juu ya ujenzi wa makaazi mapya bwana Seidemann amesema mipango ya ujenzi ilishapitishwa mwaka uliopita kabla ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuagiza kimya kimya kusimamisha kwa muda ujenzi wa makaazi. Lakini habari juu ya mipango ya ujenzi wa makaazi hayo 1000 zimepenya kwa vyombo vya habari.
Netanyahu ajaribu kuepuka lawama:
Ingawa hatua ya kusimamisha ujenzi kwa muda ,haikuthibitishwa rasmi, mashirika yasiyo ya kiserikali nchini Israel yamesema, Netanyahu hakutaka kuonekana kuwa ni pingamizi la juhudi za Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry za kuyafufua mazungumzo baina ya Israel na Wapalestina
Wapalestina wanaitaka Israel iache kabisa shughuli za ujenzi wa maakazi mapya katika maeneo yao ili mazungumzo yaweze kuanza tena.
Mwandishi:Mtullya Abdu.Aptn,afp,
Mhariri:Mohammed Abdul-rahman

Matokeo Mapya ya Kidato cha nne haya hapa!!!

MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE YAMETOKA!

Baraza la mitihani linapenda kuwataarifu kuwa matokeo mapya ya kidato cha nne yaliyopangwa upya yametoka.

Unaweza kuangalia matokeo hayo hupitia:

LINK 1: http://196.44.162.25/csee2012/Olevel.htm

LINK 2: http://196.44.162.33/csee2012/Olevel.htm

LINK 3: http://www.matokeo.necta.go.tz/matokeo_html_2013/CSEE_2012/olevel.htm

LINK 4:http://www.necta.go.tz/matokeo_html_2013/CSEE_2012/olevel.htm

Wednesday, 29 May 2013

IBADA YA MASWALI NA MAJIBU YA KIROHO CASFETA SJUT-DSM

Bwana asifiwe wapendwa.
Siku ya Ijumaa tar 24.05.2013 ilikuwa njema sana hasa pale ilipotimu muda wa kawaida wa ibada wa saa 6:00 CASFETA TAYOMI tawi la Chuo Kikuu St. John's. Siku ilikuwa ya pekee kwa kuwa ilikuwa ibada ya kwanza kuruhusu maswali na majibu ya kiroho.
Maswali makuu yaliyoulizwa na kujadiliwa ni;
1. Nini maana ya Mkristo, anapatikanaje na nini uthibitisho wake?
2. Ni kwanini tunakataza kunywa pombe wakati yesu alitengeneza divai? Na je nimsaidiaje mtu anayeohoji uhalali wa kukataza pombe kwa mkristo?
3. Kijana wa kiume anapotaka mchumba afanyaje? Makanisa mengine yana hatua tatu za urafiki, uchumba mpaka ndoa, Je nini msimamo wa kipentekoste?
4. Nini tofauti ya divai na mvinyo?
5. Fafanua tofauti ya Sala, Maombezi, Shukrani na Dua?
 Spika wa mjadala Peter kapagi  ndo anaruhusu maswali
 Mwenyekiti Hamphrey Mhuville akiongoza shangwe za ibada hiyo
 Mwl Luka akitoa ufafanuzi
 Katibu mkuu mstaafu akiulizwa Swali
 Aquilina Charles akikoleza kipindi kwa swali mwanana
 Jacob Msokwa akiulizwa swali nini maana ya mkristo?
 Majibu ya kiroho ni Biblia bwana, ona Mwenyekiti wa wakaka mstaafu akijibu kwa ufafanuzi makini

Ibada ilikuwa tulivu wakati wa maswali japo ilikuwa na shangwe kuu ilipoanza
 Usajili pia ulikuwepo ili kubaini wangapi wamehudhuria