m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Monday, 20 May 2013

Uvamizi kwa "kumfichua" Museveni


 20 Mei, 2013 - Saa 16:37 GMT

Ofisi za Gaeti la Daily Monitor zilizovamiwa na polisi wa Uganda
Polisi nchini Ugandan wamevamia ofisi za magazeti kufuatia taarifa kwamba Rais Yeweri Museveni anamuandaa mwanawe wa kiume kumrithi urais.
Vituo viwili vya Redio pia vamiwa na kuzimwa , hii ni kwa muujibu wa gazeti la serikali la New Vision.
Wiki iliyopita magazeti ya Uganda yalidai kuwa kuna njama za kuwaua wale watakao pinga mpango wa Rais Museveni kumuandaa mwanawe kuchukua madaraka ya Uganda.
Magazeti hayo yalidai kuwa mipango hiyo ya mauaji yalitolewa na Mkuu fulani wa jeshi la Uganda.
Bwana Museveni, ambaye amekuwa madarakani tangu 1986, anatarajiwa kung'atuka uongozini mwaka 2016.
Kwa muda mrefu kumekuwa na madai kwamba Museveni anamuandaa mwanawe Muhoozi Kainerugaba,ambaye ni brigadier jeshini kushikilia uongozi wa Uganda.
Lakini serikali ya Museveni imekanusha kwamba kuna mipango kama hiyo.

Mwanawe Museveni Brig. Kainerugaba.

Wiki iliyopita gazeti la, the Daily Monitor,na jengine la , Red Pepper, lilichapisha barua ya siri ikidai ilikuwa imeandikwa na Jeneral David Sejusa, ikitaka uchunguzi ufanywe kuthibitisha madai kwamba kuna mipango ya kuwauwa wote watakao piga mipango ya Rais Museveni kumpachika mwanawe uongozini.
Uvamizi huo wa polisi umeidhinishwa na mahakama ya Uganda na ulikuwa unalengo la kutafuta barua hiyo inayodaiwa kuandikwa na mkuu huyo wa Jeshi akifichua njama za mauaji.
Vituo viwili vya Redio vinavyohusiana na Daily Monitor, Dembe FM na KFM, pia vilivamiwa na kuzimwa.
Rais Yoweri Museveni
Mkurugenzi Mkuu wa Daily Monitor Bwana Alex Assimwe aliambia BBC kwamba Chumba chao cha Habari kilivamiwa na polisi wapatao 50 waliojihami kwa silaha.
Lakini wachanganuzi wa maswala ya kisiasa wanadai kuwa ikiwa barua ya Jenerali Sejusa ni ya kweli basi ni dalili kuwa kuna hali mvutano ndani ya jeshi huku ikidhaniwa kuwa wanajeshi wakongwe huenda wanapoteza uwezo kwa wanajeshi chipukizi wanaoongozwa na mwanawe Museveni Brigadia Kainerugaba.
Jenerali Sejusa ni mwanajeshi mkongwe aliyekuwa katika vita vya ukombozi uliyomuweka Rais Museveni madarakani mwaka1986.
Kwa muujibu wa taarifa za AP kamanda mmoja wa jeshi Jenerali Aronda Nyakairima amenukiliwa akisema kuwa Jenerali Sejusa kwa wakati huu anachunguzwa kutokana na barua anayodaiwa kuiandika.

Thursday, 16 May 2013

Tume ya Kidato cha IV yatoa mapendekezo 130

 
Profesa Sifuni Mchome 
Na Fredy Azzah, Mwananchi  (email the author)

Posted  Jumanne,Mei14  2013  saa 20:25 PM
Kwa ufupi
  • Pendekezo la kufutwa kwa matokeo na kisha kupangwa upya ni moja tu kati ya mengi. Mpaka sasa tumeandaa zaidi ya mapendekezo 130 na kazi bado inaendelea

Dar es Salaam. Tume ya Kuchunguza Kushuka kwa Kiwango cha Ufaulu wa Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012, imetoa mapendekezo 130, mojawapo ikitaka kupitiwa upya kwa mitalaa ya elimu nchini.
Akizungumza na Mwananchi jana, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Profesa Sifuni Mchome alisema likitaka mitalaa ya shule za msingi hadi vyuo vya ualimu itazamwe upya.
Tume hiyo iliundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda Februari 23, mwaka huu kuchunguza chanzo cha asilimia 65.5 ya wanafunzi kupata daraja la sifuri kwenye mtihani wa mwaka 2012.
Alisema mapendekezo hayo yatawasilishwa kwa Waziri Mkuu baada ya Tume kumaliza kazi yake Juni 15 mwaka huu.
“Pendekezo la kufutwa kwa matokeo na kisha kupangwa upya ni moja tu kati ya mengi. Mpaka sasa tumeandaa zaidi ya mapendekezo 130 na kazi bado inaendelea,” alisema Profesa Mchome.
Alisema kwa kawaida mtalaa unabadilishwa baada ya kumaliza mzunguko wake mmoja, hivyo tume hiyo imependekeza kupitiwa upya kwa mitalaa yote ambayo imemaliza mzunguko. Mzunguko huu ni miaka saba kwa elimu ya msingi, minne kwa sekondari na miwili kwa kidato cha tano na sita.
“Mtalaa wa sekondari unaweza kupitiwa upya baada ya miaka minne tangu kuanza kutumika kwake, huu wa Sekondari wa ‘based competence’ (kuangalia ubora) ulianza kutumika 2006, mpaka sasa tayari umemaliza mzunguko wake na haya matokeo yametokana na mtalaa huu.
Tume imependekeza mitalaa yote itazamwe upya kuanzia ile ya shule za msingi mpaka vyuo vya ualimu,” alisema.
Kuhusu vitabu, Tume imependekeza kuangaliwa kwa njia rahisi ya kutumia teknolojia kuhakikisha vinapatikana badala ya kusubiri mpaka vichapishwe na kisha kupelekwa kwa wanafunzi.
“Unaweza ukaongea na makampuni ya simu kuwa waweke vitabu kwenye system (mfumo) yao na wakaanza mashindano kuwa mwanafunzi atakayesoma sana atapata zawadi,” alisema na kuongeza.
“Unaweza pia kuongea na kampuni ya magazeti kama Mwananchi ukawaambia watoe ukurasa wachapishe kitabu fulani kwa mwezi mzima na shule ziambiwe zinunue nakala moja ambayo kwa mwezi itakuwa Sh30,000 kwa kila shule na tatizo la vitabu litakwisha.”
Pendekezo jingine alisema ni kuangaliwa upya kwa sheria mbalimbali za elimu jinsi zilivyo na utekelezwaji wake pamoja na kuhakikisha madaraka yanapelekwa kwenye ngazi za Serikali za Mitaa.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Tume-ya-Kidato-cha-IV-yatoa-mapendekezo-130/-/1597296/1852852/-/12p5ogez/-/index.html

Hayati Patrice Lumumba atunukiwa mji


Lumumba alichaguliwa kama waziri mkuu wa DRC mwaka 1960
Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo inatarejiwa kujenga mji ambao utakuwa kumbukumbu na kwa mpiganiaji uhuru wa nchi hiyo Patrice Lumumba . Hii ni kwa mujibu wa msemaji wa serikali Lambert Mende.
Lumumba aliongeza kuwa, mji huo utakaojulikana kama Lumumbaville utazileta pamoja jamii mbili zilizoko katika eneo hilo.
Lumumba aliyekuwa mshirika wa nchi za muungano wa Kisovieti, alichaguliwa kama waziri mkuu mwaka 1960, baada ya zaidi ya karne moja ya utawala wa kikoloni.
Mauaji yake, yalitokea miezi minne baadaye alipokuwa na umri wa miaka 35 na Marekani na Uingereza ndizo zililaumiwa kwa kifo chake.
Mwezi Aprili, mmoja wa wabunge wa bunge la malodi nchini Uingereza alisema kuwa afisaa mmoja wa MI6, alimwambia kuwa Uingereza ilihusika na kifo cha Lumumba.
Mwandishi wa BBC mjini Kishansa anasema kuwa habari hii bila shaka itapokelewa vyema na wananchi wa DRC kwani Lumumba anasalia kuwa mtu mashuhuri.
Mji wa Lumumbaville utajengwa katika mkoa wa Kassai-Oriental ambako alizaliwa hayati Lumumba.
Ujenzi wa mji huo unatarajiwa kuanza mwaka 2014, aliongeza kusema bwana Mende.
Serikali inatumai kuwa wahisani watasaidia katika ujenzi wa mji huo na kuwa utakuwa kivutio kwa watalii.
Mwanawe Lumumba, Raymond, aliambia BBC kuwa babake angefurahia sana uamuzi wa serikali kujenga mji huo.
"alitaka Congo kuwa kitovu cha maendeleo barani Afrika," alisema Raymond Lumumba.
"kwa hivyo, angetaka uwe mji wa kisasa.''
DR Congo ina utajiri wa madini ingawa watu wengi wanaishi katika umaskini.
Nchi hiyo imekumbwa sana na mizozo kadha wa kadha tangu ijipatie uhuru kutoka kwa Ubelgiji mwaka 1960.
Mzozo wa hivi sasa ambao umesababishwa na kundi la M23, ulianza mwaka jana Mashariki mwa nchi na kusababisha takriban watu 800,000 kutoroka makwao.
chanzo; bbcswahili.com

Tuesday, 7 May 2013

DRC: Nchi hatari zaidi kwa mama

Shirika la kimataifa la kuhudumia watoto - Save the Children limeitaja Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kuwa eneo baya zaidi ulimwenguni kuishi ukiwa mama, wakati Finland ikiibuka eneo bora zaidi.
Shirika la kimataifa la kuhudumia watoto - Save the Children limeitaja Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kuwa eneo baya zaidi ulimwenguni kuishi ukiwa mama.
Ripoti ya shirika hilo lenye makao yake jijini London Uingereza iliyotolewa leo inaonyesha kuwa mataifa ya kiafrika yemechukua nafasi zote kumi za chini kabisaa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 14 wakati Finland na nchi nyengine za Skandinavia zikiongoza  katika kumi bora.
Nembo ya shirika la Save the Children Nembo ya shirika la Save the Children
Ripoti hiyo iliyopewa kichwa cha 'Hali ya kina mama wa dunia' inalinganisha mataifa 176 kwa kuizingatia vitu kama afya ya uzazi, vifo vya watoto, elimu na viwango vya mapato ya wanawake na hadhi zao za kisiasa. Save the Children ilitoa wito wa kupunguza tofauti kubwa katika upatikanaji wa huduma za afya ya uzazi kati ya mataifa yaliyoendelea na yale yanayoendelea, na kuwepo na juhudi za maksudi kupambana dhidi ya ukosefu wa usawa na utapiamlo.
Ripoti hiyo imegundua kuwa mwanamke au msichana yuko katika hatari zaidi ya kufariki kutokana sababu zinazohusiana na uzazi katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwa nafasi moja katika 30, hii ikiwa ni pamoja na wakati wa kujifungua, ikilinganishwa na nchini Finland, ambako hatari hiyo ni nfasi moja katika 12,200.  Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Save the Children Jasmine Whitehead, alisema kwa kuwekeza kwa kina mama na watoto, mataifa yatakuwa yanawekeza katika mafanikio yao ya baadae.
Elimu kwa wanawake itasaidia ustawi wao na wa watoto
Amesema kama wanawake wanaelimishwa, wanawakilishwa kisiasa, na wanapata huduma nzuri za afya ya uzazi na huduma za watoto, basi kuna uwezekano mkubwa kwa wao na watoto wao kuishi vizuri na kustawi , na hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa jamii wanamoishi. Alisema kumekuwepo na maendeleo makubwa katika mataifa yanaoyoendelea, lakini kazi bado kuna kazi kubwa inayotakiwa kufanywa ili kuokoa na kuboresha mamilioni ya maisha ya kina mama maskini zaidi na ya watoto wanaozaliwa.
Wanawake nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo wakisubiri maji mjini Kinshasa.  
Wanawake nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo wakisubiri maji mjini Kinshasa.
Baada ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, mataifa yanayofuatia kwa kuwa hatari zaidi kwa kina mama yaliorodheshwa kuwa ni Somalia, Sierra Leon, Mali na Niger. Ripoti hiyo inasema viwango vikubwa vya vifo vya watoto katika bara la Afrika chini ya jangwa la Sahara, vinatokana na afya duni ya kina mama -- ikionyesha tarakimu zinazoonyesha kuwa asilimia kati ya 10 na 20 wako chini ya uzito unaotakiwa.
Ripoti hiyo pia ilitoa umuhimu kwa idadi ya kina mama wanaojifungua kabla watoto wao hawajakua, matumizi madogo ya vizuia mimba, upatikanaji mdogo wa huduma za afya ya uzazi na uhaba wa wafanyakazi wa afya. Mataifa ya juu baada ya Finland ni Sweden, Norway, Iceland na Uholanzi, wakati Marekani ikishika nafasi ya 30 nyuma ya Slovenia na Lithuania.
Mwandishi: Iddi Ismail Ssessanga/afpe
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman

FBI watua Arusha kusaka magaidi

 7 Mei, 2013 - Saa 11:24 GMT

Makachero wa FBI wawasili Mjini Arusha kusaidia Polisi Tanzania kusaka magaidi
kachero wa FBI kutoka Marekani wamewasili nchini Tanzania kusaidia katika upelelezi wa shambulizi la bomu lililotekelezwa katika kanisa katoliki mjini Arusha siku ya jumapili.
Mwandishi wa BBC Baruan Muhuza akiwa mjini Arusha anasema makachero hao wa FBI wako Tanzania kusaidiana na Jeshi la wananchi wa Tanzania na Polisi kutafuta undani wa tukio hili ambalo limeishtua na kuiweka serikali ya Tanzania katika wakati mgumu.
Baruan Muhuza anaongezea hali inaonekana kuwa ngumu zaidi hasa kutokana na aina ya matukio ambayo yamekuwa yakitokea katika siku za hivi karibuni yakihusisha viongozi wa dini ambapo wengi ya wanaodhurika huwa ni wa imani ya kikristo.
Wakati huo huo wakuu wa serikali wakishirikiana na viongozi wa kidini wameandaa mkutano utakaojumuisha viongozi wapatao 200.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq amewaambia wanahabari kuwa wamelazimika kuandaa mkutano huo wa siku mbili kufuatia agizo la Rais Jakaya Kikwete.
Mkutano huo utajadili uhusiano bora baina ya wakrito na waislamu.
bbcswahili.com

Monday, 6 May 2013

MFANYA BIASHARA ALIYEJIRUSHA TOKA GOROFA YA TISA AFARIKI DUNIA

TAARIFA za awali zina arifu kuwa Mfanya Biashara, Costa Shirima anaedaiwa kujirusha kutoka gorofa ya tisa ya Hoteli ya Concord iliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam inaelezwa kuwa alikuwa asafiri na ndege ya saa 10 jioni kuelekea China kufuata bidhaa za maduka yake.
Shirima (47), ambaye amefikwa na umauti muda mfupi baada ya kudondoka chini ni mfanyabiashara aliyekuwa akimiliki maduka kadhaa ya urembo wa akina mama yaliyopo jirani na Hoteli hiyo ya Concord.
Aidha taarifa hizo za awali kutoka kwa mmoja wa wanafamilia ambaye alidai kuwa si msemaji wa familia ya Shirima ya Mwika Moshi mkoani Kilimanjaro, nikuwa Marehemu mara kwamara alikuwa akipendelea kula katika hoteli hiyo na siku ya tukio inadaiwa kuwa aliwaeleza watu kuwa anapanda juu ya Hoteli hiyo kupunga upepo baada ya kuhisi hewa nzito mahali alipokuwa.
Inadaiwa kuwa baada ya kupanda huko juu ghafla alianguka chini na kudondokea gari dogo aina ya Toyota Corola linalofanya biashara ya Taxi na kupoteza maisha yake na gari hilo kuharibika vibaya kutokana na kishindo hicho.
Marehemu Shirima mbali na kuwa Mfanya Biashara wa muda mrefu Kariakoo pia alikuwa akiendelea na Ujenzi wa Jengo la Gorofa maeneo ya Kariakoo.
Marehemu ameacha Mjane na watoto 5.
Uchunguzi wa Kipolisi bado unaendelea kuhusiana na tukio hilo na taarifa kamili zitatolewa pindi zitakapo kamilika

Mfanya biashara huyu mkazi wa Dar es salaam mzaliwa wa Moshi kilimanjaro alikutwa na mauti hayo baada ya kujirusha kutoka gorofa ya tisa ya hoteli hiyo ambayo alienda kwa lengo la kuuona ukumbi wa tukio hilo ambao uko gorofa ya tisa ya hoteli hiyo.
Chanzo Cha Mfanyabiashara huyu kujirusha bado hakijafahamika mpaka sasa.
Taratibu za Mazishi ya Marehemu Zinapangwa jijini dar es salaam  na tukizipata tutakuhabarisha mapema. 
Ndugu Costa shirima ameacha mke na watoto.
Mungu ailaze roho ya marehemu Mahali Pema Peponi 
Amina
chanzo;jambotz
 

Sunday, 5 May 2013

MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA KATOLIKI HUKO ARUSHA

Ni habari ya kusikitisha baada ya kutokea mlipuko wa bomu wakati wa ibada ya kanisa katoliki Arusha. Bomu hilo limetupwa na watu wasiojulikana na muda mfupi kabla balozi wa papa hajaanza ibada ya kunyunyiza. Katika mlupuko huo amefariki mtu mmoja na watu zaidi ya 40 kujeruhiwa. Huu ni mfululizao mashambulizi kwa kanisa nchini Tanzania hasa ikizingatiwa bado kuna kumbukumbu ya mashambulizi kwa mapadri visiwani Zanzibar. Kanisa tuombe kwa ajili ya nchi kwani matukio haya yanaichafua Tanzanzia nchi Takatifu.





DSCN2227Hali ya eneo mlipuko ulipotokea
DSCN2220Waumini na wananchi wengine wakiwa na shauku ya kujua kilichotokea
DSCN2228Ulinzi umeimarishwa
DSCN2252Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi.

Tuesday, 30 April 2013

Maajabu ya Mnali kuwachapa walimu viboko


Leo nimekumbushwa mbali kwa maajabu aliyofanya kanali Mnali aliyewachapa walimu viboko. hakika ni tukio baya kuwahi kutokea hasa kwa mtu mkubwa kama yeye, alituongoza kutokuwa na heshima na maadili. Walimu wote waungane kulaani uonevu

 Kama uliwahi kusikia mkuu wa  wilaya ya Bukoba, Bwana Albert Mnali aliyewachapa walimu viboko ni huyo mwenye miwani na koti jeusi (aliyezungushiwa duara jeusi) aliweka historia Tanzania,kipindi hicho alikuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba na
 taarifa ni kwamba aliwachapa viboko walimu wa shule tatu za Katerero, Kanazi na Kasenene katika mkoa wa Kagera.

Israeli PM admits airstrike against Gaza

04-30-2013 18:45 BJT
JERUSALEM, April 30 (Xinhua) -- Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu admitted that the Israeli Air Force launched a raid on the Gaza Strip on Tuesday morning, leaving a Salafist militiaman dead.
"Today we struck at one of those involved in the criminal firing of rockets at Eilat," Netanyahu said at the start of his meeting with Serbian President Tomislav Nikolic.
"I said that we will not ignore this. Our action is in continuation of our police. We will not accept sporadic firing of rockets from the Gaza Strip or Sinai," Netanyahu added.
"We will act, and are acting, to defend Israeli citizen," Netanyahu said.
He further offered condolences to the Israeli victim, who was stabbed by a Palestinian in the Tapuch junction in the West Bank on Tuesday morning.
"I would like to extend my condolences to his family. The terrorist who perpetrated the murder has been captured and we will continue to act on this front as well in order to defend our citizens," he added.
Earlier, the Israeli Air Force raided the Gaza enclave and killed one person, who is allegedly connected to missile launches towards southern Israel.
The target of the raid was Hitam al-Mashal, 29, who was said to be responsible for 17 missiles launches towards southern Israel in April.
Hitam al-Mashal, 29, was killed as he was riding his motorcycle near a Hamas military base.
This is the first time Israel had targeted a specific person at an air raid since operation Pillar of Defense took place in November, 2012.
The IAF attacked targets at the strip on Saturday night following a rocket launch from the strip towards an Israeli community.
According to a statement released by the Israeli Defense Forces (IDF) spokesperson unit, an Israeli aircraft shelled a terror facility and weapons cache in the southern strip.
This comes after a ceasefire agreement inked between Hamas and Israel after the November military campaign.
cctv.cn

Monday, 29 April 2013

Wafu wanavyofukuliwa, kisha kuzikwa wapya

Makaburi yaliyopo jijini Dar es Salaam 
Na Florence Majani  (email the author)

Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.

Siku zote tunaamini kuwa mtu anapofariki hupumzika kwa amani, lakini siku hizi wafu hao hawapumziki tena kwa amani, bali huamshwa, kisha, wafu wengine kushika nafasi zao.
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.
Maeneo mengi ya kuzikia katika Jiji la Dar es Salaam, hasa yale maarufu kama Kinondoni, Sinza, Temeke na Kisutu yanapendwa zaidi na watu na sasa yamefurika.
Kujaa kwa maeneo haya ya kuzikia kumesababisha makaburi ya watu wengine, kufukuliwa kisha kutumika kuzikia miili mingine.
Hata hivyo, makaburi ambayo hufukuliwa ni yale ambayo hayajajengewa, yametelekezwa, hayana kitu chochote cha kuonyesha kuwa kuna kaburi pale au mengine hayana alama kama misalaba au imeondolewa.
Msemaji wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian Kaiohela anasema kuwa anafahamu kwamba makaburi hayo yamejaa, lakini hakutaka kuzungumza zaidi akitoa ahadi kuwa siku ya Jumatatu atalifikisha suala hilo kwa wahusika wakuu.
Katika makaburi ya Temeke Chang’ombe, Mwananchi Jumapili lilishuhudia makaburi yakiwa yamesongamana kiasi ambacho ni vigumu mtu kupata nafasi ya kuweka mguu.
Mlinzi wa makaburi hayo, Athuman Mtembwe anasema kutokana na ufinyu wa nafasi katika makaburi hayo, makaburi ambayo hayana alama yoyote ni rahisi kufukuliwa na kuzikiwa kwa mara nyingine.
“Mimi kama mlinzi wa eneo hili ninaweza kukutafutia sehemu ambayo unaweza kuchimba kaburi, lakini kama hufahamu utafukua tu maiti nyingine,” anasema
Anasema kuwa mara kwa mara watu wanaokuja kuchimba makaburi ili kuzika ndugu zao, wamekuwa wakifukua miili ya watu wengine ambayo makaburi yao hayakuwa na alama yoyote.
“Ni kawaida, mchimba kaburi anafukua, anakuta mifupa, anaiweka pembeni au anaizika katika shimo dogo…kisha anaendelea na taratibu za kuzika mwili mwingine,” anaeleza.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760490/-/12b2t5y/-/index.html 

Kiongozi wa Kanisa azikwa akiwa hai mkoani Mbeya

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani 


Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Mbeya. Msaidizi wa zamani wa Padri (Katekisita) katika Kigango cha Kanisa Katoliki Kijiji cha Mkwajuni, Florian Mwamosi (70) amekufa baada ya kuzikwa akiwa hai katika kaburi moja na mtu anayedaiwa kumuua kwa njia ya kishirikina.
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani  alikiri kutokea  kwa tukio hilo akieleza kuwa lilitokea  saa 9:00 mchana katika kijiji hicho cha Maweni Mkwajuni wilayani Chunya.
“Marehemu aliuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na mawe kwa tuhuma za kuhusika na uchawi na kusababisha kifo cha Peter Robert,” alisema.
Kamanda Athumani alisema kuwa uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea na kwamba wahusika wote wa tukio hilo wamekimbia na kuzihama nyumba zao, hivyo polisi wanaendelea na msako wa kuwatia mbaroni watuhumiwa na kwamba tayari  kaburi hilo limefukuliwa jana kutenganisha maiti hizo.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa  marehemu huyo ambaye alikuwa akituhumiwa kwa ushirikina aliwahi kuwa Katekista wa kigango hicho hadi mwaka 2007.
Wameeleza kuwa Mwamosi alikwenda kuhudhuria mazishi ya Peter  Robert (28) katika kitongoji hicho cha Maweni, baada ya kufuatwa nyumbani kwake na watu wakitaka aende kwa sababu yeye ni mmoja wa wazee wa mila katika kitongoji hicho.
“Bwana Mwamosi alikuwa akituhumiwa kwa uchawi kwa muda mrefu na wenzie wawili, hivyo alipofika makaburini ilianza minong`ono ya watu na huku wengine wakiguna na ndipo alipoombwa aingie kaburini kwa ajili ya kupokea jeneza lililobeba mwili wa marehemu Peter Robert,” alisema mkazi mmoja wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Joseph.
Alisema kuwa baada ya kuingia kaburini akiwa na watu wengine watatu wenzake walitoka kwa haraka na kumwacha Mwamosi peke yake ndipo kundi la watu waliokuwa eneo hilo la makaburi walianza kumshambulia kwa kumpiga mawe huku wakimwamuru akae chini.
Shuhuda huyo alisema kuwa baada ya kukubali kukaa chini akiwa ndani ya kaburi hilo, walianza kumfukia na alipofukiwa nusu ya mwili wake waliingiza jeneza la marehemu Peter na kuliweka juu yake na kuanza kulifukia kaburi hilo.
“Baada ya kukaa chini ndani ya kaburi hilo ndipo walianza kumfukia kwa udongo na baadaye wakachukua jeneza la marehemu na kuliweka juu yake, kisha kumfukia na udongo na taratibu za mazishi ziliendelea kwa ajili ya marehemu  Peter,”alisema.
 http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760482/-/12b2t55/-/index.html