m
"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "
-- Dale Carnegie, motivational expert
Sunday, 5 May 2013
MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA KATOLIKI HUKO ARUSHA
Ni habari ya kusikitisha baada ya kutokea mlipuko wa bomu wakati wa ibada ya kanisa katoliki Arusha. Bomu hilo limetupwa na watu wasiojulikana na muda mfupi kabla balozi wa papa hajaanza ibada ya kunyunyiza. Katika mlupuko huo amefariki mtu mmoja na watu zaidi ya 40 kujeruhiwa. Huu ni mfululizao mashambulizi kwa kanisa nchini Tanzania hasa ikizingatiwa bado kuna kumbukumbu ya mashambulizi kwa mapadri visiwani Zanzibar. Kanisa tuombe kwa ajili ya nchi kwani matukio haya yanaichafua Tanzanzia nchi Takatifu.
Tuesday, 30 April 2013
Maajabu ya Mnali kuwachapa walimu viboko
Leo nimekumbushwa mbali kwa maajabu aliyofanya kanali Mnali aliyewachapa walimu viboko. hakika ni tukio baya kuwahi kutokea hasa kwa mtu mkubwa kama yeye, alituongoza kutokuwa na heshima na maadili. Walimu wote waungane kulaani uonevu
Kama uliwahi kusikia mkuu wa
wilaya ya Bukoba, Bwana Albert Mnali aliyewachapa walimu viboko ni huyo mwenye miwani na koti jeusi (aliyezungushiwa duara jeusi) aliweka
historia Tanzania,kipindi hicho alikuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba na
taarifa ni kwamba aliwachapa
viboko walimu wa shule tatu za Katerero, Kanazi na Kasenene katika mkoa
wa Kagera.
Israeli PM admits airstrike against Gaza
04-30-2013 18:45 BJT
"Today we struck at one of those involved in the criminal firing of rockets at Eilat," Netanyahu said at the start of his meeting with Serbian President Tomislav Nikolic.
"I said that we will not ignore this. Our action is in continuation of our police. We will not accept sporadic firing of rockets from the Gaza Strip or Sinai," Netanyahu added.
"We will act, and are acting, to defend Israeli citizen," Netanyahu said.
He further offered condolences to the Israeli victim, who was stabbed by a Palestinian in the Tapuch junction in the West Bank on Tuesday morning.
"I would like to extend my condolences to his family. The terrorist who perpetrated the murder has been captured and we will continue to act on this front as well in order to defend our citizens," he added.
Earlier, the Israeli Air Force raided the Gaza enclave and killed one person, who is allegedly connected to missile launches towards southern Israel.
The target of the raid was Hitam al-Mashal, 29, who was said to be responsible for 17 missiles launches towards southern Israel in April.
Hitam al-Mashal, 29, was killed as he was riding his motorcycle near a Hamas military base.
This is the first time Israel had targeted a specific person at an air raid since operation Pillar of Defense took place in November, 2012.
The IAF attacked targets at the strip on Saturday night following a rocket launch from the strip towards an Israeli community.
According to a statement released by the Israeli Defense Forces (IDF) spokesperson unit, an Israeli aircraft shelled a terror facility and weapons cache in the southern strip.
This comes after a ceasefire agreement inked between Hamas and Israel after the November military campaign.
cctv.cn
Monday, 29 April 2013
Wafu wanavyofukuliwa, kisha kuzikwa wapya
Makaburi yaliyopo jijini Dar es Salaam
Kwa ufupi
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini
umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na
uhaba wa maeneo ya kuzikia.
Siku zote tunaamini kuwa mtu anapofariki
hupumzika kwa amani, lakini siku hizi wafu hao hawapumziki tena kwa
amani, bali huamshwa, kisha, wafu wengine kushika nafasi zao.
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini
umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na
uhaba wa maeneo ya kuzikia.
Maeneo mengi ya kuzikia katika Jiji la Dar es
Salaam, hasa yale maarufu kama Kinondoni, Sinza, Temeke na Kisutu
yanapendwa zaidi na watu na sasa yamefurika.
Kujaa kwa maeneo haya ya kuzikia kumesababisha makaburi ya watu wengine, kufukuliwa kisha kutumika kuzikia miili mingine.
Hata hivyo, makaburi ambayo hufukuliwa ni yale
ambayo hayajajengewa, yametelekezwa, hayana kitu chochote cha kuonyesha
kuwa kuna kaburi pale au mengine hayana alama kama misalaba au
imeondolewa.
Msemaji wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian
Kaiohela anasema kuwa anafahamu kwamba makaburi hayo yamejaa, lakini
hakutaka kuzungumza zaidi akitoa ahadi kuwa siku ya Jumatatu
atalifikisha suala hilo kwa wahusika wakuu.
Katika makaburi ya Temeke Chang’ombe, Mwananchi
Jumapili lilishuhudia makaburi yakiwa yamesongamana kiasi ambacho ni
vigumu mtu kupata nafasi ya kuweka mguu.
Mlinzi wa makaburi hayo, Athuman Mtembwe anasema
kutokana na ufinyu wa nafasi katika makaburi hayo, makaburi ambayo
hayana alama yoyote ni rahisi kufukuliwa na kuzikiwa kwa mara nyingine.
“Mimi kama mlinzi wa eneo hili ninaweza
kukutafutia sehemu ambayo unaweza kuchimba kaburi, lakini kama hufahamu
utafukua tu maiti nyingine,” anasema
Anasema kuwa mara kwa mara watu wanaokuja kuchimba
makaburi ili kuzika ndugu zao, wamekuwa wakifukua miili ya watu wengine
ambayo makaburi yao hayakuwa na alama yoyote.
“Ni kawaida, mchimba kaburi anafukua, anakuta
mifupa, anaiweka pembeni au anaizika katika shimo dogo…kisha anaendelea
na taratibu za kuzika mwili mwingine,” anaeleza.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760490/-/12b2t5y/-/index.html
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760490/-/12b2t5y/-/index.html
Kiongozi wa Kanisa azikwa akiwa hai mkoani Mbeya
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani
Posted Jumapili,Aprili28 2013 saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Mbeya. Msaidizi wa zamani wa Padri (Katekisita)
katika Kigango cha Kanisa Katoliki Kijiji cha Mkwajuni, Florian
Mwamosi (70) amekufa baada ya kuzikwa akiwa hai katika kaburi moja na
mtu anayedaiwa kumuua kwa njia ya kishirikina.
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani
alikiri kutokea kwa tukio hilo akieleza kuwa lilitokea saa 9:00
mchana katika kijiji hicho cha Maweni Mkwajuni wilayani Chunya.
“Marehemu aliuawa na wananchi wenye hasira kali
kwa kupigwa na mawe kwa tuhuma za kuhusika na uchawi na kusababisha kifo
cha Peter Robert,” alisema.
Kamanda Athumani alisema kuwa uchunguzi kuhusiana
na tukio hilo unaendelea na kwamba wahusika wote wa tukio hilo
wamekimbia na kuzihama nyumba zao, hivyo polisi wanaendelea na msako wa
kuwatia mbaroni watuhumiwa na kwamba tayari kaburi hilo limefukuliwa
jana kutenganisha maiti hizo.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa marehemu
huyo ambaye alikuwa akituhumiwa kwa ushirikina aliwahi kuwa Katekista wa
kigango hicho hadi mwaka 2007.
Wameeleza kuwa Mwamosi alikwenda kuhudhuria
mazishi ya Peter Robert (28) katika kitongoji hicho cha Maweni, baada
ya kufuatwa nyumbani kwake na watu wakitaka aende kwa sababu yeye ni
mmoja wa wazee wa mila katika kitongoji hicho.
“Bwana Mwamosi alikuwa akituhumiwa kwa uchawi kwa
muda mrefu na wenzie wawili, hivyo alipofika makaburini ilianza
minong`ono ya watu na huku wengine wakiguna na ndipo alipoombwa aingie
kaburini kwa ajili ya kupokea jeneza lililobeba mwili wa marehemu Peter
Robert,” alisema mkazi mmoja wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina
moja la Joseph.
Alisema kuwa baada ya kuingia kaburini akiwa na
watu wengine watatu wenzake walitoka kwa haraka na kumwacha Mwamosi peke
yake ndipo kundi la watu waliokuwa eneo hilo la makaburi walianza
kumshambulia kwa kumpiga mawe huku wakimwamuru akae chini.
Shuhuda huyo alisema kuwa baada ya kukubali kukaa
chini akiwa ndani ya kaburi hilo, walianza kumfukia na alipofukiwa nusu
ya mwili wake waliingiza jeneza la marehemu Peter na kuliweka juu yake
na kuanza kulifukia kaburi hilo.
“Baada ya kukaa chini ndani ya kaburi hilo ndipo
walianza kumfukia kwa udongo na baadaye wakachukua jeneza la marehemu na
kuliweka juu yake, kisha kumfukia na udongo na taratibu za mazishi
ziliendelea kwa ajili ya marehemu Peter,”alisema.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760482/-/12b2t55/-/index.html
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760482/-/12b2t55/-/index.html
Thursday, 25 April 2013
Saturday, 20 April 2013
Darasa la saba sasa kujiunga vyuo vikuu
Jengo la Chuo Kikuu Dodoma(Udom) moja ya vyuo vitakavyo tumika katika utaratibu huo mpya
Kwa ufupi
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14,
utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na
kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo
kikuu.
Dar es Salaam. Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU),
imepanga kuanza kuwadahili wanafunzi wa kujiunga na masomo ya vyuo vikuu
kwa kutumia uzoefu wao.
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo
2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la
saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi
ya chuo kikuu.
Kupitia utaratibu huo mpya, mtahiniwa atajiunga na
Chuo Kikuu kulingana na fani atakayoiomba na atatakiwa kufanya mitihani
mitatu na kufaulu kwa wastani wa daraja B.
Mkurugenzi wa Ithibati na Ubora wa Elimu ya Juu
kutoka TCU, Dk Savinus Maronga aliliambia gazeti hili kuwa baada ya
kuona kuna watu wengi wanaopenda kuendelea na masomo ya elimu ya juu,
lakini wameshindwa kutokana na kutokuwa na vigezo, TCU imeamua kuanzisha
mitihani hiyo maalumu.
Alisema kuwa mfumo huo unaojulikana kama
‘Recognition of Prior Learning’ (RPL), utamwezesha mwombaji kudahiliwa
vyuoni kupitia tume hiyo kama wanavyofanya watahiniwa wengine.
Sifa zinazotakiwa
Kuhusu sifa za kujiunga, Dk Maronga alisema kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba.
Kuhusu sifa za kujiunga, Dk Maronga alisema kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba.
“Mwombaji anatakiwa kuwa na nia ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu na uzoefu wa kile ambacho anakusudia kukisoma.
Awe na uwezo wa kuandika na kusoma Lugha ya
Kiingereza, ambayo ndiyo inayotumika kufundishia vyuoni,”alisema Dk
Maronga na kuongeza:
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1753450/-/12aid4m/-/index.html
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1753450/-/12aid4m/-/index.html
Monday, 15 April 2013
Dar yarejea enzi za ujima
Abiria wakigombea basi dogo katika kituo cha mabasi ya daladala Ubungo jijini Dar es Salaam jana.
Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE umebaini kuwa maeneo ambayo
yamekumbwa zaidi na tatizo la usafiri ni kutoka Mwenge kwenda Tegeta,
Mwenge-Kibaoni, Ubungo-Mbezi, Ubungo-Mbagala, Gongolamboto-Mwenge na
Ubungo kwenda Mlandizi.
Kutokana na ukosefu wa daladala kwenye maeneo hayo, kwa takribani
wiki moja sasa wananchi wamekuwa wakitumia malori, Toyota Noah, Bajaj,
Pick Up, teksi pamoja na Toyota Coaster ambazo hazijasajiliwa kuchukua
abiria jijini hapa.
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa kutokana na ukosefu wa daladala, hali
hiyo imetoa fursa kwa magari yaliyoanza kutoa huduma ya usafiri kwenye
maeneo hayo kutoza abiria nauli kubwa ambayo haipo katika viwango vya
nauli vilivyopangwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Usafiri wa
Majini na Nchi kavu (Sumatra). Nauli inayotozwa na wamiliki magari hayo
mfano kutoka Mwenge hadi Tegeta, Mwenge-Bunju, Mwenge-Kibaoni ni
Sh.1,000 hadi 2,000 kwa mtu mmoja badala ya Sh. 300 au 400 ya sasa.
Kutoka Ubungo kwenda Mbezi, Ubungo-Mbagala, nauli zinazotozwa ni
kati ya Sh. 500 hadi 1,000 badala ya Sh.300 wakati kutoka
Ubungo-Mlandazi ni Sh.1,000 hadi 2,500.
Magari yaliyobainika kutoza nauli kubwa ni yale ambayo
hayajasajiliwa na Sumatra kutoa huduma ya usafiri katika Jiji la Dar es
Salaam na yaliyoiba njia.
Aidha, daladala ambazo zimesajiliwa kutoa huduma jijini hapa,
zinaongoza kukatisha ruti (kuiba njia) na zinafanya hivyo ziweze kurejea
mapema vituoni kuchukua abiria wengine hali ambayo inakuwa ni faida
kwao.
Mathalani, katika kituo cha Mwenge inapofika jioni, gari za ruti ya
Tandika-Mwenge kupitia barabara ya Ali Hassan zimekuwa zikipakia Ubungo
na kisha kushusha abiria wote na kupakia tena kwenda Bugurudi na
zinapofika hapo hupakia kwenda Tandika.
Wakati mwingine, gari hizo zinapofika Ubungo hurudi tena Mwenge kupakia abiria.
Wakizunguma na NIPASHE kituo cha Ubungo, abiria waliokuwa
wakisafiri kwenda Mbezi Luis, walisema tatizo la usafiri limekuwa sugu
na kwamba wakati mwingine wanachukua zaidi ya saa tano kupata gari.
Amon Kisimbo mkazi wa Mbezi Luis alisema tatizo la usafiri katika
jiji la Dar es Salaam linasababishwa na msongamano wa malori na kwamba
serikali inatakiwa kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyowahi kutolewa mwaka
2009.
Kisimbo ambaye alidai alikuwa miongoni mwa watu walioshiriki
kuandaa mapendekezo hayo katika tume iliyoundwa na serikali, alisema
pendekezo walilotoa ni kutaka Bandari ya Dar es Salaam ihamishwe kutoka
ilipo sababu inasababisha malori kupita katikati ya jiji na hivyo
kusababisha msongano usiokuwa wa lazima. Ofisa Mfawidhi wa Sumatra,
Kanda ya Mashariki, Conrad Shio, akizunguza na NIPASHE jana alisema
kutokana na ukiukwaji wa sheria za barabara unaofanywa na wenye magari
hayo, magari 74 yamekamatwa kutokana na makosa mbalimbali.
Shio alisema magari 36 yamekamatwa kwa kukatisha ruti, 18 kwa kuiba ruti na magari 20 yamekamatwa kwa kutoza nauli kubwa.
Alisema magari ambayo yamekamatwa kwa kosa la kukatisha ruti
wamiliki wake watatakiwa kwenda Sumatra na mkataba wa madereva wengine
na hao waliosababisha kosa hilo hawataruhusiwa kufaya kazi ya udereva
mahali popote nchini.
Alisema tatizo la ukosefu wa magari katika baadhi ya maeneo
linatokana na kwamba Sumatra imesimamisha usajili katika ruti ya
barabara ya Ali Hasani Mwinyi-Kilwa kwa sababu kuanzia Julai mwaka huu
wamiliki wa daladala watatakiwa kujiunga katika kampuni ili kutoa huduma
ya usafiri kwenye ruti hiyo.
Alisema siyo kweli kwamba daladala zimeadimika na kwamba baadhi ya
wamiliki wanakwepa kusajili magari yao kwenye njia zenye foleni kubwa
kama Mbezi-Kimara hadi Kivukoni au Kariakoo.
MWAKYEMBE ABARIKI NAULI
Serikali imebariki ongezeko jipya la nauli za mabasi yanayotoa
huduma mijini, ya masafa marefu na treni hivyo kuziruhusu kuanza
kutumika rasmi leo.
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, aliwaambia wanahabari
jana mjini Dodoma kuwa nauli mpya imeongeza Sh. 50 kwa mwanafunzi na Sh.
100 kwa watu wazima; hivyo daladala zitatoza Sh. 400 badala ya 300 na
wanafunzi Sh. 200 badala ya Sh. 150.
Alisema serikali imeridhia ongezeko la nauli lililotangazwa na
Sumatra, baada ya kuhakiki na kujiridhisha kuwa ongezeko hilo
lilizingatia mchakato wa kupandisha nauli na viwango viliridhiwa na
wadau wanaowakilisha maslahi ya wanaotoa na wale wanaotumia huduma hiyo.
“Mimi kama Waziri wa Uchukuzi sina tatizo na ongezeko hili dogo la
nauli za daladala tatizo langu ni tabia ya Watanzania kukacha vikao
halali vinavyojadili mambo yanayotuhusu na kusubiri kuja kulalamika
baadaye,” alisema Dk. Mwakyembe.
Alisema hayo akiwakosoa wananchi na asasi nyingine kulalamikia
nauli nje ya utaratibu licha ya vikao vya kuwataka kutoa maoni kupitia
Sumatra kutangazwa na kuwataka wananchi wajitokeze wakati maombi ya
wamiliki wa vyombo vya usafiri ya kupandisha nauli yalipokuwa
yanajadiliwa.
Waziri Mwakyembe alisema maombi ya kuongezwa nauli hiyo mpya
yalitolewa baada ya wadau wakiwamo Baraza la Taifa la Walaji wa Huduma
zinazodhibitiwa na Sumatra, Chuo cha Usafirishaji, vikiwamo vyama vya
watoa huduma vya madereva vya kutetea abiria na wanahabari, kuridhia.
“Kulikuwa na mvutano mkubwa wamiliki wakitaka nauli iongezeke na
wawakilishi wa abiria wakitaka nauli ibakie ile ile iliyotangazwa mwaka
2011. Ndipo maamuzi ya nyongeza ya nyongeza ndogo yakawa Sh. 100 na Sh.
50 kwa mwanafunzi yakaafikiwa,” alisema.
Aliongeza kuwa wawakilishi wa abiria na wamiliki wa vyombo vya
usafirishaji waliamriwa kuwa iwapo kuna upande usioridhia ukate rufaa
kwenye Baraza la Ushindani, lakini hakuna aliyefanya hivyo.
Wiki iliyopita Waziri Mwakyembe alisema wizara hiyo itapitia nauli
hizo kutokana na malalamiko mengi kutolewa na wananchi wakipinga
nyongeza hiyo.
Imeandikwa na Gaudensia Mngumi, Dodoma na Thobias Mwanakatwe, Dar
CHANZO:
NIPASHE
Gesi ni hatari, Zimamoto wawahi kuokoa.
Gari la zimamoto likiwasili eneo la tukio
Leo
asubuhi muda wa saa 3:30 kumetokea mlipuko mkubwa kwenye Glosary ya Kipingu
eneo Mtaa wa Sae karibu kabisa na kituo cha Sae. Mlipuko huo wa moto umetokana
na jiko la gesi lililokuwa likiwashwa ili kupasha supu na ndipo likalipuka na
kuanza kuwaka moto mkali. Moto umezua balaa kubwa kwani kutokana na ukosefu wa
vifaa vya tahadhari vya zima moto na
elimu ya majanga watu wakaanza kuzima kwa maji na mchaka lakini ikawa ni kama
kuuchochea zaidi. Baada ya kushindika kuzima moto uliokuwa ukiwaka kwenye
mtungu wa gesi na kuendelea kusambaa kwenye vyombo vingine ndipo kijana mmoja
jasiri maarufu kama KP akajitosa na kuuburuzia nje mtungi uliokuwa ukiwaka moto
mkali. Hapo ndipo akawa ameokoa nyumba hiyo yenye maduka manne isiwake moto.
Zimamoto
wawahi kuokoa, kinyume na desturi ya zimamoto ya kuchelewa mara wanapoitwa kwenye
majanga ya moto kwani waliwasiri mara moja baada ya kupigiwa simu. Zimamoto
wamewapongeza wananchi kwa kuweza kuokoka jingo kuwaka moto kwa kuutoa nje
mtungi unaowaka moto. Askari wa zimamoto wakauzima moto uliokuwa unaendelea
kuwaka kwenye mtungi wa Gesi.
Wasisitiza
kutoa taarifa mapema kila mara janga linapotokea kuwakumbusha wananchi kuw ana
namba za simu ya kiganjani mbali ya ile ya mezani ili kutoa taaarifa kwa haraka
zaidi. Ikumbukwe kuwa mara nyingi zima moto wamekuwa wakilalamikia baadhi ya
watu wasio waaminifu wamekuwa waktoa taarifa za uongo kupitia simu ya bure ya
111.
Ushauri
wa bure kwa wote wenye majiko ya gesi ni bora wakanunua kifaa cha kuzima moto
(Fire Extinguisher) ili watumie kuzima moto mara moto unapolipuka.
Namba za kiganjani za Zimamoto jiji la Mbeya ni
0755 651923
Tazama
Picha kutoka eneo la tukio
watu wakushuhudia uzimaji wa mtungi
mtungi umezima
Askari akizima mtungi uliolipuka
Hata boda boda walikuwepo kujionea wenyewe
Moto umezimwa tayari kwa safari.
Picha zote na KII
Kwisha! UFARANSA YAPITISHA MUSWADA NDOA ZA JINSIA MOJA, SWEDEN NAKO KIMBILIO LAO
Vuta nikuvute imetokea katika bunge la senate nchini Ufaransa, ambapo
mwisho wa siku iliamuliwa kupitisha kwa muswada wa sheria ya kuruhusu
ndoa za jinsia moja nchini humo, licha ya upinzani mkali kutoka kwa
wabunge wenye msimamo mkali, ikiwamo viongozi wa dini.
Uamuzi huu ambao umepitishwa Ijumaa taehe 12 Aprili 2013 na Ufaransa ,
taifa lenye asili ya katoliki, umekuja baada ya muda mrefu wa
majadiliano, kama ambavyo Rais François Hollande alivyoahidi kwenye
uchaguzi mkuu mnamo Aprili mwaka 2012, sera ambayo ilimfanya avune kura
nyingi za wafuasi wa ndoa hizo.
| Waziri wa Haki, Bi Christian Taubira. © Gouvernement |
Mtetezi mkubwa wa muswada huo, waziri wa haki nchini huko, Bi Christian
Taubira, amesemema kuwa muswada huo unakuja kutokana na umuhimu wake,
hasahasa kwa watoto wanaoishi na wazazi wa jinsia moja, ili wapate haki
zao sawa na watoto wa wazazi wa kawaida. na kwa mujibu wa muswada huu,
basi wenye ndoa za jinsia moja, watarushusiwa kuasili watoto kwa ajili
ya kuwalea.
Tumefanya hivi kwa sababu kuna watoto hawali chakula cha afya, wanakula
pipi kwa wingi, na kadha wa kadha, hao pia tunawalinda - wanahitaji
hilo. Christian aliwaambia maseneta mara baada ya kupitisha muswada huo,
ambao utapitiwa tena February 2014 kwa ajili ya marekebisho.
Kwa upande wake, seneta wa chama cha UMP, Jean-Pierre Raffarin, amesema
kuwa bado wataendeleza mpambano kwa kuwa bunge bado lipo, na kilichopo
ni kwamba watakuwa wakiongea na wananchi wataobadili mawazo ili
kuhakikisha muswada huu unaondolewa na kurejea katika hali ya mwanzo,
yaani mume na mke na si vinginevyo.
Mpaka sasa ufaransa imegawanyika kuhusiana na ndoa za jinsia moja,
ambapo mnamo January mwaka huu, takriban watu 340,000 waliandamana
kupinga ndoa za aina hii, wakisisitiza Baba na Mama kwa familia. Ambapo
wiki mbili baadae, kundi la watu takriban 125,000 walijitokeza mtaani
kuunga mkono ndoa za namna hiyo.
| Nchi ambazo zimeridhia ndoa za jinsia moja mpaka hivi sasa. © CBC |
Ulaya ni bara ambalo nchi zake kadhaa zimeruhusu ndoa za namna hii,
ambapo kwa watu ambao nchi zao haziruhusu, wamekuwa wakikimbilia huko
ili kuonana na kuishi kwa sheria za huko. mfano mmojawapo ni mashoga
wawili Waganda, ambao walikimbia nchi yao na kuelekea Sweden ili kuonana
kutokana na nchi yao kukataza vitendo vya ushoga na usagaji.
Wadau wa Gospel Kitaa walio nchini Sweden, walifanikiwa kupata tukio
hilo kama lilivyofanyika mwezi wa kwanza kwa kamera, na hatimaye mdau
Nahshon Kamugisha kuzirusha kwa GK.
Jimmy na Lawrence wakiwa na mashoga wenzao wakati wa sherehe ya 'kuonana'.
Gospelkitaa.com
Maajabu Geita:Aliyefariki miaka mitano iliyopita afufuka
mwanamke anayedaiwa kufariki miaka mitano iliyopita
Posted Jumapili,Aprili14 2013 saa 24:51 AM
Kwa ufupi
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari
28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji
cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi
nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.inShare
Geita: Mji wa Geita na maeneo ya jirani
juzi ulikumbwa na taharuki ya aina yake, pale mwanamke ambaye anadaiwa
kwamba alifariki miaka mitano iliyopita alipoonekana akiwa hai katika
eneo la Kasamwa.
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki
Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika
Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa
ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi
Kasamwa.
Aliyekuwa wa kwanza kumwona Flora ni mdogo wake
aitwaye Monica Onesmo ambaye baada ya kuamka saa 11:00 alfajiri nyumbani
kwa dada yake, alimwona mwanamke aliyekuwa ameketi nje ya nyumba hiyo,
lakini alimfananisha mwanamama huyo na marehemu dada yake.
“Baada ya kumwona nilimwita mtoto wake tunayekaa
naye na nikampigia simu dada (Monica) ambaye alikuwa amelala chumba
kingine nikamwambia kwamba nimeamka na kumkuta mwanamke amekaa hapa nje,
lakini kila nikimwangalia anafanana na marehemu dada yetu,”alisema
Jubili na kuongeza kwamba alipowaita wote walitoka nje.
Alisema mtoto wa Flora (marehemu anayedaiwa
kufufuka) anaitwa Rebeka Elisha (16) na kwamba walimchukua tangu 2008
wakati mama yake huyo alipofariki dunia katika Hospitali ya Geita ambako
alikuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.
Rebeka ambaye ni mtoto wa nne wa Flora alisema:
“Mama mdogo alituita sisi tulikuwa tumelala akasema kwamba nje kuna
mwanamke ambaye anafanana na marehemu mama yetu, ndipo na sisi tukatoka
na kweli kumwangalia alikuwa ni yeye kabisa.”
Alisema walipomuhoji mama yake huyo kwamba
ametokea wapi, aliwaeleza kuwa ametoka eneo la Katoro kwa mganga na
aliletwa na watu ambao hakuwatambua Alhamisi saa 1:30 usiku ndani ya
gari na watu hao walimshusha kwa mtu aitwaye Juma Luchunga ambaye ni
jirani na dada zake hao.
Kauli ya Flora
Akizungumza na waandishi wa habari, Flora alisema
yeye ni mkazi wa Katoro na kwamba alitokea Katoro nyumbani kwa mganga wa
jadi ambaye hata hivyo hakumtaja kwa maelezo kwamba wataalamu wake
(majini) wamemkataza.
“Nilikuwa naishi kwa mganga wa kienyeji ila
alikuja mwanaume wakati nikiwa pale akaninywesha dawa kisha tukapakizwa
kwenye gari na watu wawili ambao sikuwatambua, mmoja mwanamke na
mwingine mwanaume mpaka hapa Kasamwa tukashushwa saa 1:00 jioni,”alisema
Flora.
Alisema alipofika Kasamwa alikwenda kunywa uji kwa
mama mmoja ambaye pia hakumtaja na kwamba baadaye alipelekwa nyumbani
kwa mtu mwingine saa nne usiku, lakini watu wa nyumba hiyo walipomwona
walimwambia: “Hapa si kwako twende tukupeleke kwa ndugu yako” na ndipo
wakampeleka kwa dada yake ambako aliketi nje hadi alfajiri.
Flora alisema kabla ya kuishi kwa mganga alikuwa
akiishi porini ambako alitupwa na watu asiowafahamu na baadaye aliokotwa
na wasamaria wema ambao ndiyo walimpeleka kwa mganga ambako alikuwa
akiishi muda wote.
Endeleahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1747968/-/129ypge/-/index.html
Endeleahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1747968/-/129ypge/-/index.html
Subscribe to:
Posts (Atom)












