m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Sunday, 5 May 2013

MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA KATOLIKI HUKO ARUSHA

Ni habari ya kusikitisha baada ya kutokea mlipuko wa bomu wakati wa ibada ya kanisa katoliki Arusha. Bomu hilo limetupwa na watu wasiojulikana na muda mfupi kabla balozi wa papa hajaanza ibada ya kunyunyiza. Katika mlupuko huo amefariki mtu mmoja na watu zaidi ya 40 kujeruhiwa. Huu ni mfululizao mashambulizi kwa kanisa nchini Tanzania hasa ikizingatiwa bado kuna kumbukumbu ya mashambulizi kwa mapadri visiwani Zanzibar. Kanisa tuombe kwa ajili ya nchi kwani matukio haya yanaichafua Tanzanzia nchi Takatifu.





DSCN2227Hali ya eneo mlipuko ulipotokea
DSCN2220Waumini na wananchi wengine wakiwa na shauku ya kujua kilichotokea
DSCN2228Ulinzi umeimarishwa
DSCN2252Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi.

Tuesday, 30 April 2013

Maajabu ya Mnali kuwachapa walimu viboko


Leo nimekumbushwa mbali kwa maajabu aliyofanya kanali Mnali aliyewachapa walimu viboko. hakika ni tukio baya kuwahi kutokea hasa kwa mtu mkubwa kama yeye, alituongoza kutokuwa na heshima na maadili. Walimu wote waungane kulaani uonevu

 Kama uliwahi kusikia mkuu wa  wilaya ya Bukoba, Bwana Albert Mnali aliyewachapa walimu viboko ni huyo mwenye miwani na koti jeusi (aliyezungushiwa duara jeusi) aliweka historia Tanzania,kipindi hicho alikuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba na
 taarifa ni kwamba aliwachapa viboko walimu wa shule tatu za Katerero, Kanazi na Kasenene katika mkoa wa Kagera.

Israeli PM admits airstrike against Gaza

04-30-2013 18:45 BJT
JERUSALEM, April 30 (Xinhua) -- Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu admitted that the Israeli Air Force launched a raid on the Gaza Strip on Tuesday morning, leaving a Salafist militiaman dead.
"Today we struck at one of those involved in the criminal firing of rockets at Eilat," Netanyahu said at the start of his meeting with Serbian President Tomislav Nikolic.
"I said that we will not ignore this. Our action is in continuation of our police. We will not accept sporadic firing of rockets from the Gaza Strip or Sinai," Netanyahu added.
"We will act, and are acting, to defend Israeli citizen," Netanyahu said.
He further offered condolences to the Israeli victim, who was stabbed by a Palestinian in the Tapuch junction in the West Bank on Tuesday morning.
"I would like to extend my condolences to his family. The terrorist who perpetrated the murder has been captured and we will continue to act on this front as well in order to defend our citizens," he added.
Earlier, the Israeli Air Force raided the Gaza enclave and killed one person, who is allegedly connected to missile launches towards southern Israel.
The target of the raid was Hitam al-Mashal, 29, who was said to be responsible for 17 missiles launches towards southern Israel in April.
Hitam al-Mashal, 29, was killed as he was riding his motorcycle near a Hamas military base.
This is the first time Israel had targeted a specific person at an air raid since operation Pillar of Defense took place in November, 2012.
The IAF attacked targets at the strip on Saturday night following a rocket launch from the strip towards an Israeli community.
According to a statement released by the Israeli Defense Forces (IDF) spokesperson unit, an Israeli aircraft shelled a terror facility and weapons cache in the southern strip.
This comes after a ceasefire agreement inked between Hamas and Israel after the November military campaign.
cctv.cn

Monday, 29 April 2013

Wafu wanavyofukuliwa, kisha kuzikwa wapya

Makaburi yaliyopo jijini Dar es Salaam 
Na Florence Majani  (email the author)

Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.

Siku zote tunaamini kuwa mtu anapofariki hupumzika kwa amani, lakini siku hizi wafu hao hawapumziki tena kwa amani, bali huamshwa, kisha, wafu wengine kushika nafasi zao.
Ni kama vile muda wa marehemu hao kukaa kaburini umekwisha hivyo, nafasi zao zinatakiwa kutumiwa na wengine kutokana na uhaba wa maeneo ya kuzikia.
Maeneo mengi ya kuzikia katika Jiji la Dar es Salaam, hasa yale maarufu kama Kinondoni, Sinza, Temeke na Kisutu yanapendwa zaidi na watu na sasa yamefurika.
Kujaa kwa maeneo haya ya kuzikia kumesababisha makaburi ya watu wengine, kufukuliwa kisha kutumika kuzikia miili mingine.
Hata hivyo, makaburi ambayo hufukuliwa ni yale ambayo hayajajengewa, yametelekezwa, hayana kitu chochote cha kuonyesha kuwa kuna kaburi pale au mengine hayana alama kama misalaba au imeondolewa.
Msemaji wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian Kaiohela anasema kuwa anafahamu kwamba makaburi hayo yamejaa, lakini hakutaka kuzungumza zaidi akitoa ahadi kuwa siku ya Jumatatu atalifikisha suala hilo kwa wahusika wakuu.
Katika makaburi ya Temeke Chang’ombe, Mwananchi Jumapili lilishuhudia makaburi yakiwa yamesongamana kiasi ambacho ni vigumu mtu kupata nafasi ya kuweka mguu.
Mlinzi wa makaburi hayo, Athuman Mtembwe anasema kutokana na ufinyu wa nafasi katika makaburi hayo, makaburi ambayo hayana alama yoyote ni rahisi kufukuliwa na kuzikiwa kwa mara nyingine.
“Mimi kama mlinzi wa eneo hili ninaweza kukutafutia sehemu ambayo unaweza kuchimba kaburi, lakini kama hufahamu utafukua tu maiti nyingine,” anasema
Anasema kuwa mara kwa mara watu wanaokuja kuchimba makaburi ili kuzika ndugu zao, wamekuwa wakifukua miili ya watu wengine ambayo makaburi yao hayakuwa na alama yoyote.
“Ni kawaida, mchimba kaburi anafukua, anakuta mifupa, anaiweka pembeni au anaizika katika shimo dogo…kisha anaendelea na taratibu za kuzika mwili mwingine,” anaeleza.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760490/-/12b2t5y/-/index.html 

Kiongozi wa Kanisa azikwa akiwa hai mkoani Mbeya

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani 


Posted  Jumapili,Aprili28  2013  saa 24:3 AM
Kwa ufupi
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Mbeya. Msaidizi wa zamani wa Padri (Katekisita) katika Kigango cha Kanisa Katoliki Kijiji cha Mkwajuni, Florian Mwamosi (70) amekufa baada ya kuzikwa akiwa hai katika kaburi moja na mtu anayedaiwa kumuua kwa njia ya kishirikina.
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani  alikiri kutokea  kwa tukio hilo akieleza kuwa lilitokea  saa 9:00 mchana katika kijiji hicho cha Maweni Mkwajuni wilayani Chunya.
“Marehemu aliuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na mawe kwa tuhuma za kuhusika na uchawi na kusababisha kifo cha Peter Robert,” alisema.
Kamanda Athumani alisema kuwa uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea na kwamba wahusika wote wa tukio hilo wamekimbia na kuzihama nyumba zao, hivyo polisi wanaendelea na msako wa kuwatia mbaroni watuhumiwa na kwamba tayari  kaburi hilo limefukuliwa jana kutenganisha maiti hizo.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa  marehemu huyo ambaye alikuwa akituhumiwa kwa ushirikina aliwahi kuwa Katekista wa kigango hicho hadi mwaka 2007.
Wameeleza kuwa Mwamosi alikwenda kuhudhuria mazishi ya Peter  Robert (28) katika kitongoji hicho cha Maweni, baada ya kufuatwa nyumbani kwake na watu wakitaka aende kwa sababu yeye ni mmoja wa wazee wa mila katika kitongoji hicho.
“Bwana Mwamosi alikuwa akituhumiwa kwa uchawi kwa muda mrefu na wenzie wawili, hivyo alipofika makaburini ilianza minong`ono ya watu na huku wengine wakiguna na ndipo alipoombwa aingie kaburini kwa ajili ya kupokea jeneza lililobeba mwili wa marehemu Peter Robert,” alisema mkazi mmoja wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Joseph.
Alisema kuwa baada ya kuingia kaburini akiwa na watu wengine watatu wenzake walitoka kwa haraka na kumwacha Mwamosi peke yake ndipo kundi la watu waliokuwa eneo hilo la makaburi walianza kumshambulia kwa kumpiga mawe huku wakimwamuru akae chini.
Shuhuda huyo alisema kuwa baada ya kukubali kukaa chini akiwa ndani ya kaburi hilo, walianza kumfukia na alipofukiwa nusu ya mwili wake waliingiza jeneza la marehemu Peter na kuliweka juu yake na kuanza kulifukia kaburi hilo.
“Baada ya kukaa chini ndani ya kaburi hilo ndipo walianza kumfukia kwa udongo na baadaye wakachukua jeneza la marehemu na kuliweka juu yake, kisha kumfukia na udongo na taratibu za mazishi ziliendelea kwa ajili ya marehemu  Peter,”alisema.
 http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760482/-/12b2t55/-/index.html

Saturday, 20 April 2013

Darasa la saba sasa kujiunga vyuo vikuu

Jengo la Chuo Kikuu Dodoma(Udom) moja ya vyuo vitakavyo tumika katika utaratibu huo mpya 
Na Ibrahim Yamola, Mwananchi  (email the author)

Posted  Aprili20  2013  saa 24:48 AM
Kwa ufupi
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.

Dar es Salaam. Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), imepanga kuanza kuwadahili wanafunzi wa kujiunga na masomo ya vyuo vikuu kwa kutumia uzoefu wao.
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.
Kupitia utaratibu huo mpya, mtahiniwa atajiunga na Chuo Kikuu kulingana na fani atakayoiomba na atatakiwa kufanya mitihani mitatu na kufaulu kwa wastani wa daraja B.
Mkurugenzi wa Ithibati na Ubora wa Elimu ya Juu kutoka TCU, Dk Savinus Maronga aliliambia gazeti hili kuwa baada ya kuona kuna watu wengi wanaopenda kuendelea na masomo ya elimu ya juu, lakini wameshindwa kutokana na kutokuwa na vigezo, TCU imeamua kuanzisha mitihani hiyo maalumu.
Alisema kuwa mfumo huo unaojulikana kama ‘Recognition of Prior Learning’ (RPL), utamwezesha mwombaji kudahiliwa vyuoni kupitia tume hiyo kama wanavyofanya watahiniwa wengine.
Sifa zinazotakiwa
Kuhusu sifa za kujiunga, Dk Maronga alisema kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba.
“Mwombaji anatakiwa kuwa na nia ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu na uzoefu wa kile ambacho anakusudia kukisoma.
Awe na uwezo wa kuandika na kusoma Lugha ya Kiingereza, ambayo ndiyo inayotumika kufundishia vyuoni,”alisema Dk Maronga na kuongeza:
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1753450/-/12aid4m/-/index.html 

Monday, 15 April 2013

Dar yarejea enzi za ujima

Abiria wakigombea basi dogo katika kituo cha mabasi ya daladala Ubungo jijini Dar es Salaam jana.
Wakati nauli mpya za daladala, mabasi na treni zikianza kutumika rasmi leo, hali ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam imezidi kuwa mbaya kutokana na mabasi kuwa machache na hivyo kusababisha abiria kulazimika kusafiri kwa malori na magari mengi madogo huku wakitozwa nauli kubwa.
 
Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE umebaini kuwa maeneo ambayo yamekumbwa zaidi na tatizo la usafiri ni kutoka Mwenge kwenda Tegeta, Mwenge-Kibaoni, Ubungo-Mbezi, Ubungo-Mbagala, Gongolamboto-Mwenge na Ubungo kwenda Mlandizi.
 
Kutokana na ukosefu wa daladala kwenye maeneo hayo, kwa takribani wiki moja sasa wananchi wamekuwa wakitumia malori, Toyota Noah, Bajaj, Pick Up, teksi pamoja na Toyota Coaster ambazo hazijasajiliwa kuchukua abiria jijini hapa.
 
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa kutokana na ukosefu wa daladala, hali hiyo imetoa fursa kwa magari yaliyoanza kutoa huduma ya usafiri kwenye maeneo hayo kutoza abiria nauli kubwa ambayo haipo katika viwango vya nauli vilivyopangwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Usafiri wa Majini na Nchi kavu (Sumatra). Nauli inayotozwa na wamiliki magari hayo mfano kutoka Mwenge hadi Tegeta, Mwenge-Bunju, Mwenge-Kibaoni ni Sh.1,000 hadi 2,000 kwa mtu mmoja badala ya Sh. 300 au 400 ya sasa.
 
Kutoka Ubungo kwenda Mbezi, Ubungo-Mbagala, nauli zinazotozwa ni kati ya Sh. 500 hadi 1,000 badala ya Sh.300 wakati kutoka Ubungo-Mlandazi ni Sh.1,000 hadi 2,500.
Magari yaliyobainika kutoza nauli kubwa ni yale ambayo hayajasajiliwa na Sumatra kutoa huduma ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam na yaliyoiba njia.
 
Aidha, daladala ambazo zimesajiliwa kutoa huduma jijini hapa, zinaongoza kukatisha ruti (kuiba njia) na zinafanya hivyo ziweze kurejea mapema vituoni kuchukua abiria wengine hali ambayo inakuwa ni faida kwao. 
 
Mathalani, katika kituo cha Mwenge inapofika jioni, gari za ruti ya Tandika-Mwenge kupitia barabara ya Ali Hassan zimekuwa zikipakia Ubungo na kisha kushusha abiria wote na kupakia tena kwenda Bugurudi na zinapofika hapo hupakia kwenda Tandika.
 
Wakati mwingine, gari hizo zinapofika Ubungo hurudi tena Mwenge kupakia abiria.
 
Wakizunguma na NIPASHE kituo cha Ubungo, abiria waliokuwa wakisafiri kwenda Mbezi Luis, walisema tatizo la usafiri limekuwa sugu na kwamba wakati mwingine wanachukua zaidi ya saa tano kupata gari.
 
Amon Kisimbo mkazi wa Mbezi Luis alisema tatizo la usafiri katika jiji la Dar es Salaam linasababishwa na msongamano wa malori na kwamba serikali inatakiwa kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyowahi kutolewa mwaka 2009.
 
Kisimbo ambaye alidai alikuwa miongoni mwa watu walioshiriki kuandaa mapendekezo hayo katika tume iliyoundwa na serikali, alisema pendekezo walilotoa ni kutaka Bandari ya Dar es Salaam ihamishwe kutoka ilipo sababu inasababisha malori kupita katikati ya jiji na hivyo kusababisha msongano usiokuwa wa lazima. Ofisa Mfawidhi wa Sumatra, Kanda ya Mashariki, Conrad Shio, akizunguza na NIPASHE jana alisema kutokana na ukiukwaji wa sheria za barabara unaofanywa na wenye magari hayo, magari 74 yamekamatwa kutokana na makosa mbalimbali.
 
Shio alisema magari 36 yamekamatwa kwa kukatisha ruti, 18 kwa kuiba ruti na magari 20 yamekamatwa kwa kutoza nauli kubwa.
 
Alisema magari ambayo yamekamatwa kwa kosa la kukatisha ruti wamiliki wake watatakiwa kwenda Sumatra na mkataba wa madereva wengine na hao waliosababisha kosa hilo hawataruhusiwa kufaya kazi ya udereva mahali popote nchini.
 
Alisema tatizo la ukosefu wa magari katika baadhi ya maeneo linatokana na kwamba Sumatra imesimamisha usajili katika ruti ya barabara ya Ali Hasani Mwinyi-Kilwa kwa sababu kuanzia Julai mwaka huu wamiliki wa daladala watatakiwa kujiunga katika kampuni ili kutoa huduma ya usafiri kwenye ruti hiyo.
 
Alisema siyo kweli kwamba daladala zimeadimika na kwamba baadhi ya wamiliki wanakwepa kusajili magari yao kwenye njia zenye foleni kubwa kama Mbezi-Kimara hadi Kivukoni au Kariakoo.
 
MWAKYEMBE ABARIKI NAULI
Serikali imebariki ongezeko jipya la nauli za mabasi yanayotoa huduma mijini, ya masafa marefu na treni hivyo kuziruhusu kuanza kutumika rasmi leo.
 
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, aliwaambia wanahabari jana mjini Dodoma kuwa nauli mpya imeongeza Sh. 50 kwa mwanafunzi na Sh. 100 kwa watu wazima; hivyo daladala zitatoza Sh. 400 badala ya 300 na wanafunzi Sh. 200 badala ya Sh. 150.
 
Alisema  serikali imeridhia ongezeko la nauli lililotangazwa na Sumatra, baada ya kuhakiki na kujiridhisha kuwa ongezeko hilo lilizingatia mchakato wa kupandisha nauli na viwango viliridhiwa na wadau wanaowakilisha maslahi ya wanaotoa na wale wanaotumia huduma hiyo.
 
“Mimi kama Waziri wa Uchukuzi sina tatizo na ongezeko hili dogo la nauli za daladala tatizo langu ni tabia ya Watanzania kukacha vikao halali vinavyojadili mambo yanayotuhusu na kusubiri kuja kulalamika baadaye,” alisema Dk. Mwakyembe.
 
Alisema hayo akiwakosoa wananchi na asasi nyingine kulalamikia nauli nje ya utaratibu licha ya vikao vya kuwataka kutoa maoni kupitia Sumatra kutangazwa na kuwataka wananchi wajitokeze wakati maombi ya wamiliki wa vyombo vya usafiri ya kupandisha nauli yalipokuwa yanajadiliwa.
 
Waziri Mwakyembe alisema maombi ya kuongezwa nauli hiyo mpya yalitolewa baada ya wadau wakiwamo Baraza la Taifa la Walaji wa Huduma zinazodhibitiwa na Sumatra, Chuo cha Usafirishaji, vikiwamo vyama vya watoa huduma vya madereva vya kutetea abiria na wanahabari, kuridhia.
 
“Kulikuwa na mvutano mkubwa wamiliki wakitaka nauli iongezeke na wawakilishi wa abiria wakitaka nauli ibakie ile ile iliyotangazwa mwaka 2011. Ndipo maamuzi  ya nyongeza ya nyongeza ndogo yakawa Sh. 100 na Sh. 50 kwa mwanafunzi yakaafikiwa,” alisema.
 
Aliongeza kuwa wawakilishi wa abiria na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji waliamriwa kuwa iwapo kuna upande usioridhia ukate rufaa kwenye Baraza la  Ushindani, lakini hakuna aliyefanya hivyo.
 
Wiki iliyopita Waziri Mwakyembe alisema wizara hiyo itapitia nauli hizo kutokana na malalamiko mengi kutolewa na wananchi wakipinga nyongeza hiyo.
Imeandikwa na Gaudensia Mngumi, Dodoma na Thobias Mwanakatwe, Dar
CHANZO: NIPASHE

Baadhi ya wadaiwa wa Bodi ya Mikopo wako taabani

http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/10881-baadhi-ya-wadaiwa-bodi-ya-mikopo-wako-taabani

Gesi ni hatari, Zimamoto wawahi kuokoa.



Gari la zimamoto likiwasili eneo la tukio
Leo asubuhi muda wa saa 3:30 kumetokea mlipuko mkubwa kwenye Glosary ya Kipingu eneo Mtaa wa Sae karibu kabisa na kituo cha Sae. Mlipuko huo wa moto umetokana na jiko la gesi lililokuwa likiwashwa ili kupasha supu na ndipo likalipuka na kuanza kuwaka moto mkali. Moto umezua balaa kubwa kwani kutokana na ukosefu wa vifaa vya tahadhari  vya zima moto na elimu ya majanga watu wakaanza kuzima kwa maji na mchaka lakini ikawa ni kama kuuchochea zaidi. Baada ya kushindika kuzima moto uliokuwa ukiwaka kwenye mtungu wa gesi na kuendelea kusambaa kwenye vyombo vingine ndipo kijana mmoja jasiri maarufu kama KP akajitosa na kuuburuzia nje mtungi uliokuwa ukiwaka moto mkali. Hapo ndipo akawa ameokoa nyumba hiyo yenye maduka manne isiwake moto.
Zimamoto wawahi kuokoa, kinyume na desturi ya zimamoto ya kuchelewa mara wanapoitwa kwenye majanga ya moto kwani waliwasiri mara moja baada ya kupigiwa simu. Zimamoto wamewapongeza wananchi kwa kuweza kuokoka jingo kuwaka moto kwa kuutoa nje mtungi unaowaka moto. Askari wa zimamoto wakauzima moto uliokuwa unaendelea kuwaka kwenye mtungi wa Gesi.
Wasisitiza kutoa taarifa mapema kila mara janga linapotokea kuwakumbusha wananchi kuw ana namba za simu ya kiganjani mbali ya ile ya mezani ili kutoa taaarifa kwa haraka zaidi. Ikumbukwe kuwa mara nyingi zima moto wamekuwa wakilalamikia baadhi ya watu wasio waaminifu wamekuwa waktoa taarifa za uongo kupitia simu ya bure ya 111.
Ushauri wa bure kwa wote wenye majiko ya gesi ni bora wakanunua kifaa cha kuzima moto (Fire Extinguisher) ili watumie kuzima moto mara moto unapolipuka.
Namba za kiganjani za Zimamoto jiji la Mbeya ni
0755 651923
Tazama Picha kutoka eneo la tukio
watu wakushuhudia uzimaji wa mtungi

mtungi umezima

Askari akizima mtungi uliolipuka

 Hata boda boda walikuwepo kujionea wenyewe




 Moto umezimwa tayari kwa safari.
Picha zote na KII

Kwisha! UFARANSA YAPITISHA MUSWADA NDOA ZA JINSIA MOJA, SWEDEN NAKO KIMBILIO LAO

Vuta nikuvute imetokea katika bunge la senate nchini Ufaransa, ambapo mwisho wa siku iliamuliwa kupitisha kwa muswada wa sheria ya kuruhusu ndoa za jinsia moja nchini humo, licha ya upinzani mkali kutoka kwa wabunge wenye msimamo mkali, ikiwamo viongozi wa dini.
Uamuzi huu ambao umepitishwa Ijumaa taehe 12 Aprili 2013 na Ufaransa , taifa lenye asili ya katoliki, umekuja baada ya muda mrefu wa majadiliano, kama ambavyo Rais François Hollande alivyoahidi kwenye uchaguzi mkuu mnamo Aprili mwaka 2012, sera ambayo ilimfanya avune kura nyingi za wafuasi wa ndoa hizo.
Waziri wa Haki, Bi Christian Taubira. © Gouvernement
Mtetezi mkubwa wa muswada huo, waziri wa haki nchini huko, Bi Christian Taubira, amesemema kuwa muswada huo unakuja kutokana na umuhimu wake, hasahasa kwa watoto wanaoishi na wazazi wa jinsia moja, ili wapate haki zao sawa na watoto wa wazazi wa kawaida. na kwa mujibu wa muswada huu, basi wenye ndoa za jinsia moja, watarushusiwa kuasili watoto kwa ajili ya kuwalea.
Tumefanya hivi kwa sababu kuna watoto hawali chakula cha afya, wanakula pipi kwa wingi, na kadha wa kadha, hao pia tunawalinda - wanahitaji hilo. Christian aliwaambia maseneta mara baada ya kupitisha muswada huo, ambao utapitiwa tena February 2014 kwa ajili ya marekebisho.
Kwa upande wake, seneta wa chama cha UMP, Jean-Pierre Raffarin, amesema kuwa bado wataendeleza mpambano kwa kuwa bunge bado lipo, na kilichopo ni kwamba watakuwa wakiongea na wananchi wataobadili mawazo ili kuhakikisha muswada huu unaondolewa na kurejea katika hali ya mwanzo, yaani mume na mke na si vinginevyo.
Mpaka sasa ufaransa imegawanyika kuhusiana na ndoa za jinsia moja, ambapo mnamo January mwaka huu, takriban watu 340,000 waliandamana kupinga ndoa za aina hii, wakisisitiza Baba na Mama kwa familia. Ambapo wiki mbili baadae, kundi la watu takriban 125,000 walijitokeza mtaani kuunga mkono ndoa za namna hiyo.
Nchi ambazo zimeridhia ndoa za jinsia moja mpaka hivi sasa. © CBC
Ulaya ni bara ambalo nchi zake kadhaa zimeruhusu ndoa za namna hii, ambapo kwa watu ambao nchi zao haziruhusu, wamekuwa wakikimbilia huko ili kuonana na kuishi kwa sheria za huko. mfano mmojawapo ni mashoga wawili Waganda, ambao walikimbia nchi yao na kuelekea Sweden ili kuonana kutokana na nchi yao kukataza vitendo vya ushoga na usagaji.
Wadau wa Gospel Kitaa walio nchini Sweden, walifanikiwa kupata tukio hilo kama lilivyofanyika mwezi wa kwanza kwa kamera, na hatimaye mdau Nahshon Kamugisha kuzirusha kwa GK.


Jimmy na Lawrence wakiwa na mashoga wenzao wakati wa sherehe ya 'kuonana'.
Gospelkitaa.com

Maajabu Geita:Aliyefariki miaka mitano iliyopita afufuka

mwanamke anayedaiwa kufariki miaka mitano iliyopita 


Posted  Jumapili,Aprili14  2013  saa 24:51 AM
Kwa ufupi
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.Share

Geita: Mji wa Geita na maeneo ya jirani juzi ulikumbwa na taharuki ya aina yake, pale mwanamke ambaye anadaiwa kwamba alifariki miaka mitano iliyopita alipoonekana akiwa hai katika eneo la Kasamwa.
Inadaiwa kwamba Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.
Aliyekuwa wa kwanza kumwona Flora ni mdogo wake aitwaye Monica Onesmo ambaye baada ya kuamka saa 11:00 alfajiri nyumbani kwa dada yake, alimwona mwanamke aliyekuwa ameketi nje ya nyumba hiyo, lakini alimfananisha mwanamama huyo na marehemu dada yake.
“Baada ya kumwona nilimwita mtoto wake tunayekaa naye na nikampigia simu dada (Monica) ambaye alikuwa amelala chumba kingine nikamwambia kwamba nimeamka na kumkuta mwanamke amekaa hapa nje, lakini kila nikimwangalia anafanana na marehemu dada yetu,”alisema Jubili na kuongeza kwamba alipowaita wote walitoka nje.
Alisema mtoto wa Flora (marehemu anayedaiwa kufufuka) anaitwa Rebeka Elisha (16) na kwamba walimchukua tangu 2008 wakati mama yake huyo alipofariki dunia katika Hospitali ya Geita ambako alikuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.
Rebeka ambaye ni mtoto wa nne wa Flora alisema: “Mama mdogo alituita sisi tulikuwa tumelala akasema kwamba nje kuna mwanamke ambaye anafanana na marehemu mama yetu, ndipo na sisi tukatoka na kweli kumwangalia alikuwa ni yeye kabisa.”
Alisema walipomuhoji mama yake huyo kwamba ametokea wapi, aliwaeleza kuwa ametoka eneo la Katoro kwa mganga na aliletwa na watu ambao hakuwatambua Alhamisi saa 1:30 usiku ndani ya gari na watu hao walimshusha kwa mtu aitwaye Juma Luchunga ambaye ni jirani na dada zake hao.
Kauli ya Flora
Akizungumza na waandishi wa habari, Flora alisema yeye ni mkazi wa Katoro na kwamba alitokea Katoro nyumbani kwa mganga wa jadi ambaye hata hivyo hakumtaja kwa maelezo kwamba wataalamu wake (majini) wamemkataza.
“Nilikuwa naishi kwa mganga wa kienyeji ila alikuja mwanaume wakati nikiwa pale akaninywesha dawa kisha tukapakizwa kwenye gari na watu wawili ambao sikuwatambua, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume mpaka hapa Kasamwa tukashushwa saa 1:00 jioni,”alisema Flora.
Alisema alipofika Kasamwa alikwenda kunywa uji kwa mama mmoja ambaye pia hakumtaja na kwamba baadaye alipelekwa nyumbani kwa mtu mwingine saa nne usiku, lakini watu wa nyumba hiyo walipomwona walimwambia: “Hapa si kwako twende tukupeleke kwa ndugu yako” na ndipo wakampeleka kwa dada yake ambako aliketi nje hadi alfajiri.
Flora alisema kabla ya kuishi kwa mganga alikuwa akiishi porini ambako alitupwa na watu asiowafahamu na baadaye aliokotwa na wasamaria wema ambao ndiyo walimpeleka kwa mganga ambako alikuwa akiishi muda wote.
Endeleahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1747968/-/129ypge/-/index.html