m

"If you want to conquer fear, don't sit at home and think about it. Go out and get busy. "

-- Dale Carnegie, motivational expert

Wednesday, 12 October 2016

Rais Magufuli aagiza viongozi walioalikwa kuhudhuria sherehe za mwenge kutohudhuria, awataka warudishe posho.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza viongozi wote wa Serikali walioalikwa kuhudhuria sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa zitakazofanyika tarehe 14 Oktoba, 2016 katika Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu kutohudhuria sherehe hizo na wale ambao walishalipwa fedha ya posho na safari kwa ajili hiyo wazirejeshe
Taarifa iliyotolewa leo tarehe 12 Oktoba, 2016 Ikulu Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Rais Magufuli ametoa maagizo hayo ikiwa ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kubana matumizi yasiyo ya lazima na kuelekeza rasilimali nyingi katika shughuli za maendeleo ya nchi.
Viongozi waliotajwa kutakiwa kufuta safari zao za kwenda Bariadi ni pamoja na Wakuu wote wa Mikoa, Wakuu wote wa Wilaya, Wakurugenzi wote wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Mameya na Wenyeviti wote wa Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya pamoja na watumishi ambao huambatana nao wakiwemo madereva na wasaidizi wao ambao kwa idadi hufikia takribani 1,500.
Kwa kuwa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru huambatana na Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Muasisi wa Taifa na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyefariki dunia miaka 17 iliyopita, agizo hilo limewataka Viongozi wote wa Mikoa na Wilaya kubaki katika maeneo yao ya kazi na kujiwekea utaratibu wa jinsi ya kuienzi siku hiyo.
Aidha, Rais Magufuli ameagiza Wilaya zote ambazo zimefanya vizuri katika shughuli za maendeleo wakati Mwenge ulipokuwa katika maeneo yao, zitambuliwe kwa kutangazwa rasmi katika siku ya kilele cha Mbio za Mwenge na kwamba zawadi zilizoandaliwa zitapelekwa kwa wahusika kwa utaratibu utakaoelekezwa na Mamlaka inayohusika kutoa zawadi hizo.
Hata hivyo Dkt. Magufuli ameelekeza kuwa kutokana na umuhimu wa Mwenge wa Uhuru kwa Taifa, Viongozi wote wa Serikali ya Mkoa wa Simiyu na Wilaya zake pamoja na wananchi wote wa mkoa huo wajitokeze kwa wingi na kushiriki katika sherehe za kuzima Mwenge wa Uhuru siku hiyo ya tarehe 14 Oktoba, 2016.
Mgeni Rasmi katika sherehe za kuzima Mwenge wa Uhuru atakuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Tuesday, 11 October 2016

Angela Merkel azindua Jumba la makao makuu ya AU lililopewa Jina la Julius Nyerere, Addis Ababa.

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amezindua jumba jipya makao makuu ya Umoja wa Afrika ambalo limepewa jina la rais mwanzilishi wa taifa la Tanzania, Julius Nyerere.
Jumba hilo ambalo jina lake kamili ni Jumba la Amani na Usalama la Julius Nyerere limejengwa kwa ufadhili kutoka Ujerumani.
Litakuwa makao ya idara ya Amani na Usalama ya AU na litatumiwa pia na maafisa wa kutoa tahadhari ya mapema kuhusu mizozo barani pamoja na kuratibu juhudi za kulinda amani za AU.
Ujenzi wa jumba hilo, ambalo ukubwa wake wa sakafu ni mita 13,500 mraba na linaweza kutumiwa na wafanyakazi 360, uligharimu euro 27 milioni.
Jumba hilo afisi za kufanyia kazi, vyumba vya mikutano vya kutumiwa na Baraza la Amani na Usalama, chumba cha kuratibia shughuli, maktaba na vyumba vya shughuli za pembeni.
Mwalimu Nyerere, ambaye alikuwa rais wa Tanzania hadi 1985, alikuwa mmoja wa viongozi waanzilishi wa Muungano wa Nchi za Afrika (OAU) ambao sasa ni Umoja wa Afrika (AU).


Bi Merkel amezuru nchi kadha za Afrika zikiwemo Mali na Niger. Hapa anaonekana na Rais Mahamadou Issoufou wa Niger.
Alishiriki sana katika jitihada za kuendeleza bara la Afrika na kusaidia mataifa ambayo hayakuwa yamepata uhuru kujipatia uhuru wake.
Mwalimu Nyerere alipigania sana kumalizwa kwa ubabe wa Wazungu katika nchi za Rhodesia (sasa Zimbabwe), Afrika Kusini, na taifa la Kusini Magharibi mwa Afrika/Namibia (sasa Namibia).

Source:BBCSwahili

Wednesday, 7 September 2016

Wakonta Kapunda, binti aliyeandika kwa ulimi, apata kifaa


Wakonta Kapunda
Unamkumbuka Wakonta Kapunda? Binti Mtanzania mwandishi wa miswada ya filamu anayeandika kwa kutumia ulimi wake?
Wakonta alipata ajali siku ya mahafali yake ya kidato cha sita miaka minne iliyopita. Ajali hiyo ilimuacha akiwa amepooza kwanzia shingoni kushuka chini na kumfanya kutoweza kutumia mkono yake kuandika.
Wakonta Kapunda
Wiki kadhaa zilizopita, BBC iliporusha habari yake Msamaria Mwema mmoja aliguswa kumsaidia
Kupitia kipindi cha televisheni cha Focus on Africa katika BBC World Service, mwanadada Olivia Soko kutoka Afrika ya Kusini aliguswa kufanya kitu kumsaidia Wakonta.
Wakonta Kapunda, msichana anayeandika kwa ulimi
Akiwa mkurugenzi wa kampuni ya Whirlmarket Technologies, Olivia alijitolea kutoa msaada wa programu ya kompyuta iitwayo Nuance Dragon Naturally Speaking.
Jinsi Program hii inavyofanya kazi ni kwamba mtumiaji yeye anazungumza anachotaka kukiandika kupitia kipaza sauti chake halafu programu hii inaandika yenyewe katika kompyuta ya mtumiaji
Wakonta alijaribu kuitumia jana, akaifurahia, lakini bila shaka atahitaji muda zaidi ili aizoee vizuri.
Familia yake pia imefurahishwa sana na msaada huu.
Chanzo; bbcswahili.com

Trump aungwa mkono na wanajeshi wastaafu 88

Tofauti na watu wanavyobeza nguvu ya Mgombea urais wa Republican Bw. Trump BBC inaripoti kwamba anaungwa mkono na wanajeshi wastaafu 88.
Donald Trump
Image captionDonald Trump
Mgombea wa chama cha Republican Donald Trump ameungwa mkono na viongozi 88 wa zamani wa jeshi katika barua ya wazi kulingana na kampeni yake.
Kundi hilo lenye majenerali wastaafu pamoja na admirali waliamua kuwa kiongozi huyo ana uwezo wa kuwa kamanda mkuu wa jeshi.
Bwana Trump ambaye ameangazia maswala ya wazee wakati wa kampeni yake alitaja uungwaji mkono huo kuwa heshima kubwa.
Hatahivyo amepinga madai ya utumizi mbaya kuhusu ufadhili wa kisiasa kwa afisa mmoja wa Florida.
Gazeti la The Washington liliripoti siku ya Jumatatu kwamba mwaka 2013,mwanasheria mkuu wa Florida Pam Bondi alipendekeza mashtaka ya udanganyifu dhidi ya chuo kikuu cha Trump.
Lakini alisitisha uchunguzi huo baada ya mchango wa dola 25,000 kutolewa na wakfu wa Donald Trump kusaidia kampeni yake ya kisiasa.
Bwana Trump alipigwa faini kwa kuwa hakutangaza mchango wake kwa halmashauri ya ushuru nchini Marekani.

Kimungu mke (Goddess) achoka sauti

Hakika Mungu mkuu atabaki kuwa Mungu kwani mwimbaji Beyonce yule aliyejiita kimungu mke( goddess) kule marekani na kuanzisha kitabu chake alichofananisha na biblia kiitwacho beyble achoka sauti na kushauriwa na madaktari kupumzisha sauti. Je ni Mungu gani anayeshauriwa na wanadamu juu ya Afya yake akakubali?Habari kamili na bbcswahili;-

 

Beyonce ashauriwa kupumzisha sauti yake


Beyonce ashauriwa kupumzisha sauti yakeImage copyrightV
Image captionBeyonce ashauriwa kupumzisha sauti yake
Mwanamuziki Beyonce ameahirisha tamasha lake la New Jersey kwa jina World Tour baada ya madaktari kumshauri kupumzisha sauti yake.
Msanii huyo ambaye alisheherekea siku yake ya 35 ya kuzaliwa siku ya Jumapili alitoa taarifa akisema tamasha hilo halitafanyika mnamo tarehe 7 mwezi Octoba.
Hatahivyo ataendelea na tamasha nyengine katika miji ya Los Angeles,Houston,New Orleans na Atlanta kama ilivyopangwa.
Ziara hiyo ambayo inalenga kuuza albamu yake mpya Lemonade,ilianza mjini Miami mnamo tarehe 27 mwezi Aprili.
Ilitarajiwa kukamilika Nashvile mnamo tarehe 2 mwezi Octoba,lakini sasa inaonekana kwamba New Jersey itaanda tamasha lake la mwisho

Binadamu mzee Zaidi duniani huyu hapa


Mungu wa ajabu, wakati wengi wakifikiri wazee zaidi ni wale wenye miaka 80 na 90 shirika la habari la uingereza(bbc) linaripoti juu ya mzee wa miaka 145 aliyepo Indonesia

Mbah Gotho
Mzee huyu kwa jina Mbah Ghoto kutoka Indonesia anaamini ndiye binadamu mzee zaidi kuwahi kuishi duniani.
Anasema ameishi muda zaidi kushinda wake zake wanne, ndugu zake 10 na wanawe wote.
Anatokea kisiwa cha Java ya Kati.
"Huwa najaribu kuwa mvumilivu na kuamini kuwa kuna watu watakaonitunza," ameambia BBC.
"Nimeishi muda mrefu kwa sababu nina watu wanaonipenda na kunitunza."
Yeye bado huvuta sigara.
Mjukuu wake Suryanto anasema kwa mujibu wa stakabadhi rasmi za serikali, Mbah Gotho ana miaka 145. Alizaliwa 31 Desemba 1870.
"Tunaamini stakabadhi hizi ni halali, kwa mujibu wa nyaraka rasmi za serikali. Tunaamini tarehe yake ya kuzaliwa ni sahihi," anasema afisa wa serikali Wahyu Wiyanto.
Indonesia ilianza kunakili rasmi kuzaliwa kwa watu 1900 hivyo ni vigumu kuthibitisha tarehe kamili ya watu waliozaliwa kabla ya hapo.
Na kumewahi kutokea makosa awali.
Lakini Mbah Gotho anachukuliwa kama shujaa eneo analotoka.
"Siku ya Uhuru alikuwa akialikwa kusimulia yaliyotokea wakati wa vita. Anaweza kusimulia kuhusu vita dhidi ya wakoloni kutoka Japan na Uholanzi," anasema Wahyu Wiyanto.
Mjukuu wake anasema mzee huyo huwa hana masharti mengi na huwa haitishi chakula maalum.
"Kitu pekee alitutaka tufanye ni kununua jiwe la kaburi lake," anasema.
Mzee huyo anasema kwa sasa anaishiwa na nguvu na hawezi kutarajia aishi muda mrefu zaidi.
"Sina nguvu kama zamani. Hata kutembea ni shida. Nilikuwa mkulima na nilivua samaki mtoni. Sitaki kuendelea kuishi sana, ndio maana nimeandaa kaburi. "Ili nikifariki, kila kitu kiwe tayari," anasema.
"Kwa sasa nataka tu kufariki, lakini wakati wangu haujafika bado."
Mtu ambaye aliishi miaka mingi zaidi duniani kulingana na Guinness ni Jeanne Calment kutoka ufaransa ambaye aliishi miaka 122 na siku 164 . Aliaga dunia mwezi Agosti mwaka 1997.

Sherehe za kufungwa kwa Olimpiki Rio

Mashindano ya Olimpiki ya Rio yamemalizika rasmi, yakihitimisha siku 16 za matukio ya raha na karaha . Wakazi wa Rio walivumilia mvua na upepo mkali kushuhudia sherehe za mwisho za kufungwa kwa mashindano hayo.

Brasilien Olympische Spiele Rio 2016 21 08 Abschlussfeier
Sherehe za kufunga michezo ya Olimipiki ya Rio uwanjani -Maracana - Rio de Janeiro, Brazil -
Wakicheza densi aina ya Samba katika mitindo ya Ki-Brazil, wanamichezo mbali mbali pamoja na mashabiki waliaga mashindano hayo kwa mbwembwe za aina yake.
Wanariadha walimiminika katika uwanja huo wakipeperusha bendera za nchi zao katika msafara wa kuvutia huku wanariadha wa Brazil wakivalia viatu vilivyokuwa na nyayo zilizokuwa zikiwaka rangi tofauti kama vile nyekundu, nyeupe na samawati na mwanamiereka wa Tongan Pita Taufatofua akicheza jukwaani akiwa amevalia skati huku disco joka akicheza muziki na kuleta kumbukumbu ya wakati alipovutia umati mkubwa wakati alipopeperusha bendera ya nchi yake wakati wa sherehe za ufunguzi.
Kulingana na Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki, Thomas Bach, mashindano hayo yalikuwa ya kuvutia katika mji wa kupendeza:
Kumbukumbu za michezo hiyo
Hata hivyo, michezo hiyo pia ilikuwa na kumbukumbu kwa wanariadha kutoka Brazil na wale wa nchi nyingine kote ulimwenguni. Timu ya kandanda ya Brazil iliicharagaza Ujerumani na kujishindia nishani ya dhahabu miaka miwili baada ya kushindwa kwa mabao 7-1 katika fainali ya kombe la dunia na kuwahuzunisha mashambiki wengi katika taifa hilo.
Brasilien Olympische Spiele Rio 2016 21 08 Abschlussfeier Thomas Bach
Rais wa kamati ya kimataifa ya Olimpiki Thomas Bach akitoa hotuba wakati wa sherehe za kufungwa kwa michezo hiyo katika uwanja wa Maracana huko Rio de Janeiro
Mwanasakarasi wa Marekani, Simone Biles, alijishindia dhahabu 4, mwogeleaji Michael Phelps akaongeza nishani nyingine 5 na Usain Bolt akiwa ni mkimbiaji bora zaidi duniani akijishindia nishani 3 za dhahabu siku chache kabla ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa atakapohitimu miaka 30.
Baadhi ya changamoto
Lakini pia kulikuwa na matukio ambayo hayakuridhisha kama vile tukio la kutunga la mwogeleaji wa Marekani, Ryan Lochte, la kuvamiwa na maswala kama vile vidimbi vya maji katika mashindano hayo ya olimpiki kugeuka rangi kutoka samawati hadi kijani kibichi.
Sherehe hizo za kufunga mashindano hayo katika uwanja wa Maracana pia zilimaanisha kutimiza jukumu rasmi la kutia saini hatua ya kupokeza bendera kwa Japan itakayoandaa mashindano yajao ya Olimpiki katika majira ya kiangazi ya mwaka 2020.
Kuna matumaini kwamba mashindano ya Japan yatakuwa bora zaidi kuliko yalivyokuwa nchini Brazil lakini pia kuna wasiwasi kwenye nchini Japan iwapo mashindano hayo yatazidi kusambaratisha uchumi wa nchi hiyo ambao umekuwa ukijikokota kwa miaka mingi.
Gavana wa Japan alipokea bendera hiyo kutoka kwa Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki, Thomas Bach, na meya wa Rio Eduardo na kuashiria kukubalika Japan kuandaa mashindano hayo mwaka 2020.
Mwandishi: Tatu Karema/AP
Mhariri: Mohammed Khelef

Merkel asema Ujerumani ya sasa ni bora zaidi

Licha ya chama cha CDU kuangushwa vibaya kwenye uchaguzi la kwao la Mecklenburg-Vorpommern kutokana na sera yake ya wahamiaji, Kansela Angela Merkel anasema sera yake ni sahihi na kamwe hatarudi nyuma.

Kansela Angela Merkel akihutubia bungeni siku ya Jumatano (7 Septemba 2016).
Kansela Angela Merkel akihutubia bungeni siku ya Jumatano (7 Septemba 2016).
Vichwa vya habari katika magazeti na ripoti za televisheni na redio mara tu baada ya CDU kushindwa uchaguzi huo wa Jumapili, zilitazamiwa kumrejesha Kansela Merkel nyuma, na hotuba ya leo ilidhaniwa kuwa ingekuwa nyepesi na laini. Lakini hivyo sivyo ilivyokuwa, kwani kwenye hotuba ya bungeni ya leo Jumatano (7 Septemba 2016), ambapo alionekana kusimama imara.
"Hali yetu leo ni bora zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka mmoja uliopita kwetu sote. Hapana shaka, bado kuna mambo ya kufanywa. Changamoto kubwa ikiwa kuwarejesha nyumbani wahamiaji ambao hawawezi kubakia hapa na sisi. Na kwa uadilifu kuwahudumia raia wetu, huku tukiwafahamisha kuwa tunapaswa kuwasiaidia wale wenye haki ya kusaidiwa," aliwaambia wabunge.
Katika hotuba hii, ambayo tayari imeshaonesha kuzua mjadala mkali, Kansela Merkel amesema si kweli kuwa mmiminiko wa mamia kwa maelfu ya wakimbizi nchini Ujerumani utapunguza mafao wanayopata raia wazawa wa Ujerumani, hoja ambayo imekuwa ikitumiwa na wapinzani wake wa kisiasa.
Chama chake, CDU, kiliangushwa kwenye uchaguzi wa mwishoni mwa wiki na chama kinachopinga wahamiaji nchini Ujerumani, AfD, katika jimbo la Mecklenburg-Vorpommern, kwa hoja hiyo hiyo dhidi ya wakimbizi.
Wapigakura kwenye jimbo hilo walitumia nafasi hiyo kumuonesha kutokubaliana na sera yake ya kufungua milango kwa wakimbizi na wahamiaji kutoka mataifa yenye Waislamu wengi, hasa baada ya matukio kadhaa ya mashambulizi kwenye miji ya kusini mwa Ujerumani, lakini kwenye hotuba yake ya leo bungeni, Kansela Merkel amesema ugaidi si jambo linalohusiana moja kwa moja na wakimbizi.
Kansela Angela Merkel wa Ujerumani na Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki wakiwa kwenye mkutano wa kilele wa mataifa ya G20, mjini Hangzhou, China.
Kansela Angela Merkel wa Ujerumani na Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki wakiwa kwenye mkutano wa kilele wa mataifa ya G20, mjini Hangzhou, China.
"Licha ya kuwa tulikumbwa na mashambulizi mabaya ya Ansbach na Wurzburg, ugaidi si jambo jipya lililokuja na wakimbizi kwetu. Hata kama si kila mkimbizi anakuja na dhamira njema, hatupaswi kuwahukumu kijumla-jamala. Kuifanya Ujerumani kuwa salama, ni pamoja na kuwaonesha wengine kwamba wanaadamu wenzetu wanaweza kututegemea sisi wanapokuwa na matatizo," alisema Kansela Merkel.
Makubaliano na Uturuki ni sahihi
Sambamba na hilo, alitetea pia namna anavyoliendea suala la mahusiano kati ya nchi yake na Uturuki, akiwakosoa wale wanaomwambia ameshinda kulaani hatua kali za ukandamizaji zinazochukuliwa na utawala wa Rais Tayyip Erdogan baada ya jaribio la mapinduzi yaliyoshindwa mwezi Julai.
Merkel amesema makubaliano kati ya Umoja wa Ulaya na serikali ya Uturuki yaliyolenga kuzuia mmimiko wa wahamiaji yalikuwa hatua muhimu na inayoweza baadaye kuigizwa kama msingi wa makubaliano na mataifa mengine.
Mdahalo wa jioni ya leo kuhusiana na hotuba hii iliyoshadidia msimamo na muelekeo wa Kansela Merkel kwa masuala ya wakimbizi, usalama, na sera yake ya nje unatazamiwa kuwa mkali sana.
Tayari msuguano ndani ya serikali yake ya muungano umeshadhihirika, huku mshirika wake mkuu, chama cha SPD kikionekana kujipanga kumpiku.
Upinzani mkali pia umo ndani ya chake mwenyewe cha CDU, huku chama ndugu cha CSU kikiwa tangu mwanzoni mbali sana na sera ya wakimbizi ya Kansela Merkel.
Chanzo: dw.de
Mwandishi: Mohammed Khelef/dpa/Reuters
Mhariri: Saumu Yussuf


Sababu ya wanawake marafiki kupata hedhi pamoja


Picha ya mwanamke aliye kwenye hedhi
Image captionPicha ya mwanamke aliye kwenye hedhi
Inaaminiwa kwamba wanawake wanaoishi pamoja hatimaye huwa na mizunguko inayofanana ya kila mwezi ya hedhi. Lakini je hili ni kweli ama ni jambo linalotokea kwa bahati tu?
Dhana kuhusu mizunguko hiyo ya hedhi ni kwamba vichocheo vya mwili vya mwanamke ama homoni vinavyosababisha hedhi kwa lugha ya kitaalamu-pheromones- hufanya kazi kwa wakati mmoja wanapokuwa na uhusiano wa karibu, na hivyo kuwasababisha kupata hedhi kwa wakati mmoja. Wanawake wengi wamejikuta katika hali hii.
"Nadhani suala hili ni kweli ," anasema Emma. "Tukisema ni suala linalojitokeza kwa bahati basi zitakuwa ni bahati nyingi sana ."
Emma, mwenye umri wa miaka 24, anaishi na wasichana wenzake watano katika chuo kikuu. Anasema kwamba katika kipindi cha miezi michache wote walipata hedhi zao kwa wakati mmoja.
"Ni suala linaloaminiwa na wengi," anasema Alexandra Alvergne, profesa wa masuala ya kibiolojia na maumbile ya binadamu katika chuo kikuu cha Oxford.
chati ya hedhi ya mwanamkeImage copyrightISTOCK
Image captionTafiti nyingine, kuhusu binadamu na watu waliowahi kuishi pamoja zinathibitisha kuwa wanawake wanaoishi pamoja hupata hedhi wakati mmoja
Kuna nadharia mbali mbali kuhusu sababu inayoweza kusababisha wanawake wanaoishi pamoja kupata hedhi wakati mmoja.
Utafiti wa Dkt Martha McClintock mwaka 1971 ulidokeza hili huenda lilikuwa ni kwa sababu wanawake waliokuwa wanaishi pamoja walikuwa na uwezekano kwamba homoni za kila mmoja ziliweza kuathiri za mwenzake miongoni mwa marafiki wa karibu.
Na kwa nini basi hili likawezekana? Nadharia ambayo inakubaliwa na wengi ilikuwa ni uwezo wa ushirikiano uliopo baina ya wanawake katika mambo na kwamba huenda walikata kushirikiana kuzuia kugeuzwa kuwa maharimu na mwanamume mmoja.
Kwa kuoanisha mizunguko yao ya hedhi, hii ina maana kwamba mwanamume mmoja aliye karibu nao hangeweza kuwatungisha mimba kwa pamoja kwani wakati mmoja angelikuwa anamwangazia mmoja na kabla amwangazie yule mwingine, kipindi chake cha kuweza kushika mimba kitakuwa kimepita.
Baadhi ya wasomi hivi karibuni waliamua kuchunguza kwa kina iwapo matokeo ya mzunguko wa hedhi kwa wanawake wanaoishi pamoja yanaweza kuwa ni ya kubahatisha.
Waliangalia taarifa za mizunguko ya hedhi walizokusanya katika kipindi cha miaka sita wakiangazia nyani, ambao wanakaribiana sana na binadamu.
" Walipendekeza nadharia mbili," anasema Alvergne. " Moja ni ya kutumia "msisimuko " ambayo pia ilifahamika kama "mpango wa mabadiliko," ambapo wanawake hubadilisha mzunguko ili kuungana na kushirikiana kama kinga dhidi ya mwanamume mbabe.
"Nadharia nyingine ni ya mtu anayeudhi. Ambapo mienendo yake inaweza kuelezwa kwamba inatokana tu na bahati."
WanawakeImage copyrightISTOCK
Watafiti walilinganisha nadharia hizo mbili kulingana na taarifa zinazochunguzwa.
Walibaini kwamba nadharia kwamba kulingana kwa mzunguko wa hedhi unaweza kuelezwa vyema kwa 'mtu wa kuudhi' ambapo ulinganifu ulitokea kibahati tu ndiyo iliyofaa zaidi.
Utafiti zaidi unaweza kufanyika siku zijazo ambao utafichua zaidi ushahidi kuhusu mizunguko ya hedhi ya wanawake. Lakini kwa sasa watafiti wana shaka kuhusu kuwepo utaratibu au sababu inayosababisha hili.
"Labda kusema ukweli, kile tulichokiona ni jambo la kibahati tu," anasema Alvergne.
Tafiti nyengine, kuhusu binadamu na watu waliowahi kuishi pamoja zilionyesha majibu yanayofanana na hayo.
Lakini kulikuwa na tafiti nyingine ambazo hazikupata ushahidi wa wanawake wanaoishi pamoja na kuwa na urafiki kupata hedhi kwa wakati mmoja.
chanzo: bbcswahili.com

Business and Blog Changes

Its time for Change from Kapagi Infomation Institute- KII to Kapagi Enterprise-Ke and our blog/pages to Kapagi pages-Kp

our motto from Habari ni Maisha to Open the new pages/ Fungua kurasa mpya

what we do is to extend more services from education and consulting to IT, Consultancy, news/media and business/sales/products.

Its a matter of time

We are moving to Great and best times ever.

Tuesday, 17 March 2015

Get the best IT websites

Dear IT expert, here are list of the best IT websites; Software Downloads , IT discussions , IT Articles etc.. 
 http://www.techrepublic.com
http://slashdot.org
https://isc.sans.edu//diary.html
http://arstechnica.com
http://computer-news.nettop20.com
http://www.gpanswers.com/
http://www.practicallynetworked.com/
https://www.techsupportalert.com/
https://technet.microsoft.com/en-us/scriptcenter/default.aspx
http://it.toolbox.com/
http://www.informationweek.com/

WARAKA WA ELIMU NA 3 WA MWAKA 2015 KUHUSU VIGEZO VYA UDAHILI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO


| Print |
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inatoa Waraka kuhusu vigezo vya kudahili wanafunzi wa Kidato cha Tano ili kuwaongoza wamiliki wa Shule za Sekondari zenye Kidato cha Tano katika kudahili wanafunzi wa Kidato cha Tano, mwaka 2015. Waraka huu utatumika kwa shule zote, yaani za Serikali na zile zisizokuwa za Serikali.

ISOME KATIBA INAYOPENDEKEZWA USIKIMBIE KUPIGA KURA

Mtanzania ninayo shauku kukuchochea kushiriki kupiga kura ya NDIYO/HAPANA kwa ajili ya katiba inayopendekezwa. Tafadhali usikimbie kupiga kura kwani ni haki yako ili kuzuia kuwapa nafasi wachache kwa ajili ya maamuzi muhimu ya nchi. Isome katiba kisha ushiriki kupiga kura kwa kuepuka unafiki, ikiwa hujaridhika nayo utapiga kura ya HAPANA maana yake utakuwa umezuia kupitisha katiba inayopendekezwa na ikiwa umeipenda utapiga kura ya ndiyo. 

IKIWA HUJAPATA NAKALA YA KATIBA MFUATE MWENYEKITI WA KIJIJI/MTAA AU KITONGOJI


JE SERA MPYA YA ELIMU NDIO SULUHISHO LA MATATIZO YA ELIMU NA AJIRA TANZANIA?

Hivi karibuni kumezinduliwa sera mpya ya elimu na mheshimiwa rais Dkt. J.Kikwete. Kumekuwa na kilio juu ya elimu yetu na changamoto ya ajira. Je sera hii mpya ndio mwarobaini?

BOFYA HAPA UPAKUE SERA MPYA YA ELIMU UJISOMEE MWENYEWE

Friday, 4 July 2014

DW moja kwa moja kwenye simu yako kupitia WhatsApp

Mpenzi msikilizaji, msomaji na shabiki wa DW popote pale ulipo, unasemaje kuhusu kupokea habari, picha, vidio na sauti zenye ujumbe wa kukuchangamsha moja kwa moja kwenye simu yako ya mkononi?
Sasa Idhaa ya Kiswahili ya DW inawasiliana nawe moja kwa moja kupitia WhatsApp. Sasa Idhaa ya Kiswahili ya DW inawasiliana nawe moja kwa moja kupitia WhatsApp.
DW inakupa huduma hii mpya bila malipo kupitia mtandao wa WhatsApp. Unachohitaji ni simu yako tu yenye huduma ya intaneti na pia WhatsApp. Baada ya hapo fuata hatua zifuatazo kupokea taarifa kutoka kwetu:
1. Hifadhi namba ya WhatsApp ya Idhaa ya Kiswahili ya DW ambayo ni +4915752862185 kwenye simu yako
2. Tuma ujumbe kwa kutumia WhatsApp kwenye namba hiyo ukiwa na neno “Niunge.” Ukipenda, tuambie jina na pia nchi yako.
Baada ya hapo, tutakuweka kwenye orodha ya watu wanaopokea ujumbe kutoka kwetu kila tunapotuma taarifa mpya. Usihofu, hatutakutumia zaidi ya taarifa mbili kwa siku.
Kuwa mmoja wa wanachama wetu wa mwanzo kabisa kwenye jamii ya DW WhatsApp, uwe karibu kabisa na habari mpya na ujumbe wa moja kwa moja kwenye simu yako. DW iko nawe popote ulipo.
Mueleze na rafiki yako kwa kumtumia namba yetu ya simu. Unaweza pia kutufahamisha vile ambavyo ungelipenda kutumia WhatsApp kupokea habari na kututumia ujumbe wa moja kwa moja.
Ikiwa bado wewe hujaanza kutumia WhatsApp na ikiwa simu yako inaweza kutumia huduma hiyo, tafadhali weka sasa kwa simu zinazotumia mifumo ya Android, BlackBerry, Windows, ingia kwenye http://www.whatsapp.com/download/.
Usalama wa Taarifa: Namba yako ya simu itatumiwa na DW tu. Usalama wako wakati tunapotumia taarifa zako ni muhimu kwetu. Tunazitumia tu kwa mujibu wa matakwa ya kisheria. Kwa taarifa zaidi juu ya usalama wa taarifa za WhatsApp, tembelea http://www.whatsapp.com/legal/.

Chanzo: Dw.de

Monday, 30 June 2014

Zip file format; advantage and disadvantage of zip file

Ans: The Zip file format is a data compression and archive format. It is used to reduce the size of original data. It contains one or more than one files that have been compressed to reduce the size of the file. Zipping a file means that you are reducing the size of your original data into small size. The zipped version of the file has a .zip extension. Suppose you have a doc file of approx 12MB (Megabytes) and you want to send it to your friend through e-mail. But the problem is that this file is taking too much time to upload. Then you can use ZIP to reduce the file size. Your original file will be reduced to 4-5MB. Microsoft has included built-in ZIP support for all the users (under the name "Compressed folder"). It is available in all the products of Microsoft since 1998. But sometimes these .zip file corrupted due to some virus attacks, power failures or incorrect operations made by applications. It may cause severe data loss to the individual or a corporate. In these situations of losing data we can use third party tools which solved our problem by applying sophisticated recovery algorithms.

Advantages of .ZIP file:

  • You save storage space. Zipping large files can save up to 80 percent or more in hard disk space.
  • Smaller file size drastically reduces e-mail transmission time.
  • The smaller file size of e-mail messages that you want to keep is useful when your mailbox has a space limit.
  • Zipping allows you to encrypt private data, helpful when sending such data over internet.

Disadvantages of .ZIP file:

It may not be possible to extract all of the files from the Zip file correctly. Damaged data can affect the entire Zip file, multiple files, or just one file.

Following errors are encountered when ZIP is corrupt:

  • "Unexpected end of archive" error while opening ZIP file.
  • WinZip Self-Extractor Header Corrupt. Possible Cause: Bad Disk or File Transfer Error.
  • Zip file corrupt -- Cannot open file: it does not appear to be a valid zip archive.
  • CRC (cyclic redundancy check) error.
  • Compressed (ZIP folders error) -- Compressed (ZIP) folder is invalid or corrupted.

Advantages of email -or electronic mail

Some people refuse to embrace new technology... and I suppose this is fine. Imagine what a wonderful place the world would have been if many countries wouldn't have taken up nuclear energy and developed it into bombs. Anyway, I have no problems with such people as long as they don't throw foolish criticism without knowing details.
For instance, I met a not-so-old gentleman a few days back who kept on haranguing me on how the internet and email has changed the "social landscape" and is responsible for most of the problems faced by youngsters. I found this a little far-fetched because email for all the 'risks' involved has some great advantages as a communication tool.

Almost instantaneous

Email messages are transferred instantly - well almost. They move as fast as current in copper wires or light in optical cables, which is pretty darn quick. When you send an email is leaves your computer and arrives at the recipient's inbox immediately. You can potentially have a conversation with a person over email - hence, the conversation view in Gmail.

Cost of sending an email is zero or negligible

If you have a 24 hour internet such as a through cable / broadband connection, the cost of sending an email is zero or very very small. For dialup users, the maximum cost of sending an email will be that of a phone call or a few (depending on the size of the message and the files attached).

Emails can be sent in bulk

One email message can be sent to multiple recipients almost at the cost of a single email. When compared to conventional postal service this is indeed a huge saving.

Email attachments - any digital document can be sent over email

As long as a document can be converted into digital format, it can be sent over email. Again, the cost aspect comes into picture. Imagine the money you will save by sending a 500 page document attached to an email instead of the same as hard copy printout - not only is the postage more expensive but there is also the cost of printing and paper to consider.
And the story doesn't end with text documents. Photographs, music and audio files and even video from a camcorder can be attached along with an email message. To learn more, refer how to send photographs taken from your digital camera through email.
Though many email services put a limit to the email attachment size, there are workarounds; refer sending large files over email.

Delivery is almost guaranteed

The delivery of email messages in almost guaranteed. Why do I say "almost"? Because sometimes for reasons that are beyond the scope of this article, email can get lost in cyberspace but this is very rare.

Request return receipt

Just like with postal and courier services, you can request a return receipt which simply involves a click of a mouse button by the recipient. But even if the recipient doesn't get back, you know your email has been delivered - refer point above.

Email is accessible

OK, this is one of the greatest advantages of using email - its accessible anywhere, anytime and through a multitude of devices - computers, laptops, palmtops and even cell phones.
One can check email from any location as long as an active internet connection is available.
Also email can be sent from any place with the same requirement of an active net connection.

Built in spell checking

Most email programs (or email clients) have built in spell check dictionaries - so you have no excuse of sending badly written messages. Spell checkers are also found in online email services such as Hotmail and Yahoo.

Notification of new arrivals

Email programs or devices can also be set up so you get a notification through sound or a flash of light when new messages arrive at your inbox.

Can be formal as well as informal

Email messages do not signify informality. Just because email is easy to compose and send does not mean it cannot be used in formal and official correspondences.

Automation

Several, if not all, steps in the emailing process can be automated.
A good example is sending birthday greetings to people. An email program checks the birthday and the name of the recipient from a list. A message (from a template) is then formulated and sent on the specified date.

Email storage and management

Storing and managing emails you receive is very easy if you use an email program or a good email service. Segregating messages into folders and organizing them properly is just like cleaning your desk and filing your work. However, with email there is no usage of physical space excepting that on your hard disk, of course. Also, any email client worth its salt has an inbuilt search utility that hunts out the elusive email in a jiffy.

Email security

The best way to secure your email messages is to use the PGP (Pretty Good Privacy) technology. However, most people are unaware of it but it's very much there!
These were some advantages I could think of. If you come up with others, write to me using the form below.
It's now time to look at some disadvantages of using email.

Disadvantages of email

Email creates more work

In contrast to the popular notion, email actually creates more work. The easy of sending and receiving email has transformed businesses throughout the world and we know that the stress levels are increase, right?

People expect immediate replies

Most people know that emails are delivered instantaneously and hence expect replies immediately. I agree that the "human" element is kind of lost with email.

Most email messages are not secure

As I mentioned above, though a good secure technology exists for email, the masses seldom bother to use it... or even know about it. Hence transferring sensitive information over email such as credit card numbers or bank details (password?) is not advisable.

Source: http://www.webdevelopersnotes.com/basics/advantages-of-email.php

Advantages And Disadvantages Of Using Online File Storage

by Pedro Pacheco published 2 years ago

1. Google Online Storage.
Google wants to take care of your entire life with their online storage systems, and now with Google Drive, Google wants to become your virtual hard disk on the internet. The combination of Google Drive and Gmail makes it possible to have a real office that runs only using the internet without even needing the desktop for anything. Such system has advantages and disadvantages. The first advantage is the files are available from anywhere whether you use a computer or a mobile phone. However if you are running a business chances are you will always use the same computer.  Mobile phones will never be good enough for written business despite how fast they become.
Google Drive has the advantage of allowing the installation of applications but despite you having a fast internet connection, these applications are just too slow and not enough powerful for professional use. Google Drive allows you to upload your entire hard disk (provided you have enough storage online, it starts with just 5 GB) and allows to view and edit some files if you install the right application. However the desktop is still much faster and reliable than the Google Drive.
Gmail on the other hand is not the best place to store your documents and images either if you need to edit them later. Gmail should be used only for communications and nothing more. Google Drive and only Google Drive should be in charge of file storage.
With Google Drive you have
2. Zoho.
This company offers an all in one office solution for any serious business that needs documents, spreadsheets and databases. Their system is powerful enough for basic edition, however for serious matters it cannot beat Microsoft Office.  With Zoho you can have all your business online, but you cannot for example to make files work with each other like you can with Microsoft Office. Zoho is still a good solution for basic business and for university students who cannot afford Microsoft Office. With Zoho you have enough services to power an entire business. You have recruit, meetings, chat, notes, almost everything a desktop computer has. The only problem is some of these tools are paid and you need to upgrade, but still more cost effective than using desktop tools to do the same.
3. Microsoft Skydrive and Hotmail and Office 365
Microsoft is desperate to make their own true online solution to save files online and to make it work properly. First it started with Live Storage which was nothing but a pre-historic way to save files online. After some years upgraded to Mesh that failed miserably. After a while it upgraded to Office 365 and now Skydrive. The confusion is amazing, you have no idea where to work with Microsoft because all products are in Beta and some of them disappear while in beta as well.
I do not recommend that you use any Microsoft service for online business. Google Drive is much more competent in all areas and if the trend continues, it will continue that way for many years to come. Since the beginning of the internet that Microsoft has done absolutely nothing brilliant about the internet.
4. Yahoo Mail
Yahoo has no solution to online file storage such as documents or images or video. All Yahoo as is Yahoo Mail with unlimited space so you can upload files to your email and then save them using your inbox. This is the only thing you can do with Yahoo Mail and it is not recommended that you use it for serious file storage. The files are not encrypted in the server nor when you send them via email so you never know if there is someone sniffing the traffic. Another disadvantage, Yahoo Mail does not have free POP3 so if you ever need to mass download files using Outlook or Thunderbird, you can forget about it, or pay for POP3. Yahoo Mail is not a smart option to store files online considering the speed, lack of instant search and reliability of file access. You need to download them all one by one to access them and that takes much longer than having the files in the desktop.
5. Dropbox.
This service is amazing to share and sync files between computers however for online file edition it is simply impossible to work with. To make matters even worse, if you edit one document and your friend edits the very same document, when you upload them all to the Dropbox again, it will have trouble and could overwrite the document using the automatic sync. Google Drive is much better for this matter as it allows people to work on the same document in real time.
Working with online tools only has some advantages and disadvantages. However, based on my experience of online freelancing and university student, the desktop beats the online storage any day of the week in terms of security, speed and search. The cloud has yet to become faster and until everyone uses optic fiber the desktop will continue to beat the cloud. Mobile phones may trigger the development t of new web applications to manage a business but like DVDs never managed to be better than hard disks despite the faster development, desktop solutions will improve much faster than online solutions. One strong reason is the lack of success of the Google Notebook, it clearly shows that people need more powerful solutions than relying on online storage for everything. All it takes is a hacker to find out how to crack the system or the password and everything is gone forever.

Source: http://www.thepencentral.com/view/articles/online-file-storage-advantages-and-disadvantages-of-using-online-file-storage-258